Uingereza yasikitishwa na yaliyotokea kwenye Uchaguzi wa Serikali za mitaa nchini Tanzania

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426


Kitendo cha Watendaji kuamriwa kujificha kwa gharama yoyote ile ili kuhakikisha Wagombea wa vyama vya upinzani hawachukui ama kurudisha fomu za uchaguzi wa serikali za mitaa kwa lengo la kuwabeba wagombea wa CCM kwa mbeleko ya chuma, kimeusikitisha mno ubalozi wa Uingereza.

My take: Nchi inazidi kudhalilika kwenye jumuiya ya Kimataifa
 
Nchi yangu isidharau haya matamko ya hawa watu wakati tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu 2020. Hawa watu huenda kuna kitu, wanatuandaa kisaikolojia. Siamini tu kwamba wanaongea hivyo alafu wanaishia hapo, anyway muda ni mwalimu mzuri. Maadam 2020 haipo mbali tutajua tu haya matamko yalikuwa yanatuandaa kuelekea wapi.
 
Watanzania mkiwa nafkira kwamba mapambano ya demokurasia nchini yatafanywa na nchi za Ulaya na Marikani naona kama hiyo ni dhana potofu......kabla ya uingereza kusikitika nyie mmefanya nini kupambana na hiyo hali?
 
Hawajielewi!
Wana hali mbaya!
Hawawashwi!
Haya sawa, basi tusubiri siku wakiwa wamejielewa, wana hali nzuri na wanawashwa ndiyo tutawajuwa wao ni nani!
Wao ni nani kivipi? Kila mtu na nchi yake.
Kama asilimia kubwa ya Watanzania wameridhika wao ndo waje kutudanganya tuna shida?
Wajishughulikie kwanza huko wasiwashwe na yasiyowahusu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…