Uislamu haujakataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani, siungi mkono wasio waislamu kuzuiwa kula mchana

Uislamu haujakataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani, siungi mkono wasio waislamu kuzuiwa kula mchana

safuher

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2019
Posts
11,837
Reaction score
17,412
Habarini za kutwa nyote.

Naomba niseme kwamba katika dini yetu ya uislamu hakuna pahala mtume kamkataza asiyekuwa muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna pahala qurani imekataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna sehemu wakati wa mtume imeonesha kwamba walikatazwa wasiokuwa waislamu wasile mchana wa ramadhani.

Katika masharti ya mtu kulazimika kufunga kwanza awe muislamu.

Kwa maana asiyekuwa muislamu hailazimiki kufunga,kama halazimiki kufunga maana yake ana uhalali wa kula mchana wa ramadhani kwa sababu sio muislamu.

Mtu anaweza akasema kwamba wamekatazwa wasile hadharani ?

Hadharani kwanza ni wapi kwa mujibu wa sheria ya dini ?

Watu wanakula kwenye migahawa hakuna anayekunywa chai na chapati anatembea pale kariakoo.

Hivyo kuhusu kula hadharani uislamu pia haujakataza kwa sababu neno hadharani ni pana katika muktadhwa huu.

Uislamu umekataza kwa muislamu ambaye hana udhuru wowote alafu akala mchana wa ramadhani,huyu anapata dhambi.

Lakini kuwakataza watu wasile mchana na kuwashambulia sio katika adabu za kiislamu kwa sababu

Kuna wagonjwa hawatakiwi kufunga.
Kuna wanawake wako kwenye siku
Kuna watoto
Kuna wazee
Kuna wasafiri
Kuna wasiokuwa waislamu

Hawa wote ruhusa kula mchana kwa mujibu wa ssheri ya uislamu wetu.

Sasa kama wanaruhusiwa kula mchana vipi wasiruhusiwe kula hadharani wakati hakuna katazo lolote la kula hadharani katika uislamu.

Allah anasema, "Hakuna kulazimishana katika dini".

Asiye muislamu kumkataza asile mchana maana yake unamlazimisha akae na njaa jambo ambalo sheria ya dini imekataza.

Tutaheshimu sheria itakayowekwa na serikali lakini tunaomba sheria hizo zisinasibishwe na uislamu.

Ni bora uislamu ulaumiwe kwa sheria ambayo kweli imeiweka kama vile viboko kwa wazinifu n.k.

Kuliko uislamu kulaumiwa kwa sheria ambayo haijaiweka kama hizi kukataza kula mchana wa ramadhani.

Nakaribisha maswali.

Naomba kuwasilisha.

===

Kwa mijadala zaidi kuhusu suala hili na marufuku nyingine Zanzibar soma:

Yanayoendelea Zanzibar tusubiri majibu ya Wahanga na kuzaa gharika
 
werevu tumekuelew.. akili lazme itumike ktk baadhi y tartbu znaz husianisha imani!
Sahihi mkuu.

Bila akili tutachukua mawazo ya wasomi wa zamani kana kwamba sisi hatuishi kabisa na hatuna mawazo kabisa.
 
Binadamu ni changamoto sana unapata wapi ujasiri wa kumuhukumu mwenzako kwa vile wewe umefunga.
Yohane 8:7, Yesu alikutana na wahifadhi desturi kama hao (wanafiki) akawaambie Yeye asiye na dhambi na aanze kumtupa mawe.
 
Binadamu ni changamoto sana unapata wapi ujasiri wa kumuhukumu mwenzako kwa vile wewe umefunga.
Yohane 8:7, Yesu alikutana na wahifadhi desturi kama hao (wanafiki) akawaambie Yeye asiye na dhambi na aanze kumtupa mawe.
Mkuu kuna watu wana tamaduni zao fulani ambazo wanazibatiza jina hizo tamaduni na kufanya kana kwwmba ndio sheria ya kiislamu.

Imagine mtu anauza chakula stendi ya mabasi halafu unampiga marufuku wakati unajua kabisa kuna wasafiri wanataka kula.

Hii sio poa kabisa.
 
Mkuu kuna watu wana tamaduni zao fulani ambazo wqnazibatiza jina hizo tamaduni na kufanya kana kwwmba ndio sheria ya kiislamu.

Imagine mtu anauza chakulabstendi ya mabasi alafu unampiga marufuku wakati unajua kabisa kuna wasafiri wanataka kula.

Hii sio poa kabisa.
Nimeona barua fulani Zanzibar nikacheka sana maana binadamu tunaangamia kwa kukosa maarifa na ufahamu wa nini tunaabudu. Kweli binadamu ambaye maisha yake ni kama upepo muda wowote yanapeperuka anajigeuza Mungu kuwahukumu wengine dhambi eti kisa amekula maajabu kabisa
 
Nimeona barua fulani Zanzibar nikacheka sana maana binadamu tunaangamia kwa kukosa maarifa na ufahamu wa nini tunaabudu. Kweli binadamu ambaye maisha yake ni kama upepo muda wowote yanapeperuka anajigeuza Mungu kuwahukumu wengine dhambi eti kisa amekula maajabu kabisa
Haha hatari aise
 
Kwa nini mnaita watu wengine wasio waislamu ni makafir?
Mkuu kafiri maana yake ni kila asiyekuwa muislamu.

Kwa maana ni jina la jumla kwa kila asiyekuwa muislamu, badala ya uislamu kutamka dini zote ikaona iweke kwa ufupi tu kuwa wasiokuwa waislamu ni makafiri.

Hili jina linaonekana baya kwa sababu ya mindset zetu zimejengeka na tunalisikia likitajwa katika maeneo hatarishi.

Kama vile katika mambo ya kuuana utaskia anatajwa kaafiriii, mtu ataona hee kumbe kafiri hii ni jitu la kuuawa kabisa kumbe sivyo kabisa.

Hivyo kafiri ni jina la utambulisho kwa wasiokuwa waislamu mkuu.

Ni kama ukienda kwenye fani ya afya mgonjwa ataitwa mteja, utajiuliza kwamba mimi naumwa alafu naitwa mteja?


Kumbe Maana yake mteja ni mtu ambaye anakuja pale kutaka huduma.

Hivyo neno mteja ni jina la jumla kama ambavyo neno kafiri ni la jumla
 
Habarini za kutwa nyote.

Naomba niseme kwamba katika dini yetu ya uislamu hakuna pahala mtume kamkataza asiyekuwa muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna pahala qurani imekataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna sehemu wakati wa mtume imeonesha kwamba walikatazwa wasiokuwa waislamu wasile mchana wa ramadhani.

Katika masharti ya mtu kulazimika kufunga kwanza awe muislamu.

Kwa maana asiyekuwa muislamu hailazimiki kufunga,kama halazimiki kufunga maana yake ana uhalali wa kula mchana wa ramadhani kwa sababu sio muislamu.

Mtu anaweza akasema kwamba wamekatazwa wasile hadharani ?

Hadharani kwanza ni wapi kwa mujibu wa sheria ya dini ?

Watu wanakula kwenye migahawa hakuna anayekunywa chai na chapati anatembea pale kariakoo.

Hivyo kuhusu kula hadharani uislamu pia haujakataza kwa sababu neno hadharani ni pana katika muktadhwa huu.

Uislamu umekataza kwa muislamu ambaye hana udhuru wowote alafu akala mchana wa ramadhani,huyu anapata dhambi.

Lakini kuwakataza watu wasile mchana na kuwashambulia sio katika adabu za kiislamu kwa sababu

Kuna wagonjwa hawatakiwi kufunga.
Kuna wanawake wako kwenye siku
Kuna watoto
Kuna wazee
Kuna wasafiri
Kuna wasiokuwa waislamu

Hawa wote ruhusa kula mchana kwa mujibu wa ssheri ya uislamu wetu.

Sasa kama wanaruhusiwa kula mchana vipi wasiruhusiwe kula hadharani wakati hakuna katazo lolote la kula hadharani katika uislamu.

Allah anasema..

"Hakuna kulazimishana katika dini"

Asiye muislamu kumkataza asile mchana maana yake unamlazimisha akae na njaa jambo ambalo sheria ya dini imekataza.

Tutaheshimu sheria itakayowekwa na serikali lakini tunaomba sheria hizo zisinasibishwe na uislamu.

Ni bora uislamu ulaumiwe kwa sheria ambayo kweli imeiweka kama vile viboko kwa wazinifu n.k

Kuliko uislamu kulaumiwa kwa sheria ambayo haijaiweka kama hizi kukataza kula mchana wa ramadhani

Nakaribisha maswali.

Naomba kuwasilisha.
Tangazo sijaliona, kwani katiba ya Zenji ndio imekataza wasile mchana au ni kutaka Kuchafua maana hawashindwi.!!!! Wakristo huko zenji kama mtu anataka kula wali wake na samaki ale bana
 
Mkuu kafiri maana yake ni kila asiyekuwa muislamu.

Kwa maana ni jina la jumla kwa kila asiyekuwa muislamu,badala ya uislamu kutamka dini zote ikaona iweke kwa ufupi tu kuwa waaiokuwa waislamu ni makafiri.

Hili jina linaonekana baya kwa sababu ya mindset zetu zimejengeka na tunalisikia likitajwa katika maeneo hatarishi.

Kama vile katika mambo ya kuuwana utaskia anatajwa kaafiriii,mtu ataona hee kumbe kafiri hii ni jitu la kuuwawa kabisa kumbe sivyo kabisa.

hvyo kafiri ni jina la utambulisho kwa wasiokuwa waislamu mkuu.
Natafakari jibu lako. Naongeza swali. Kwa nini huwa mnajiita "watukufu waislamu"?
 
Natafakari jibu lako.Naongeza swali.Kwa nini huwa mnajiita "watukufu waislamu"?
Utukufu ni kuwapa thamani watu.

Nikisema uraisi ni cheo kitukufu maana yake nakusudia ni cheo chenye thamani.

Nikisema mitume ni watukufu maana yake wana au wenye thamani.

Hivyo mtu akisema watukufu waislamu anakusudia "wenye thamani waislamu".

Na neno utukufu mpaka Mungu ni mtukufu lakini utukufu wa Mungu ni mpana kuliko wetu sisi.

Utukufu kwa binadamu tukiitana tunakusudia ni thamani tu.
 
Tangazo sijaliona.kwani katiba ya zenji ndio imekataza wasile mchanA au ni kutak Kuchafua mana hawashindwi.!!!! Wakiristo huko zenji kama mtu anataka kula wali wake na samaki ale bana
Sijaitaja Zanzibar katika andiko langu.

Nimezungumzia kwa ujumla wake mkuu
 
Utukufu ni kuwapa thamani watu.

Nikisema uraisi ni cheo kitukufu maana yake nakusudia ni cheo chenye thamani.

Nikisema mitume ni watukufu maana yake wana au wenye thamani.

Hivyo mtu akisema watukufu waislamu anakusudia "wenye thamani waislamu".

Na neno utukufu mpaka Mungu ni mtukufu lakini utukufu wa amungu ni mpana kuliko wetu sisi.

Utukufu kwa binadamu tukiitana tunakusudia ni thamani tu.
Kuna tofauti ya kimaana kati ya mtukufu na mtakatifu?
 
Back
Top Bottom