Uislamu haujakataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani, siungi mkono wasio waislamu kuzuiwa kula mchana

Nimeingia Kula Ice Cream kwenye Moja ya Canteen za Bakhressa zinazouza ICE Cream TU.

kama kawaida nimeingia naenda nachukua vitu kwa Fridge, naambiwa HAPANA BOSS hairuhusiwi.

nikauliza hairuhisiwi kwa maana ipi? Nikaambiwa Ice Cream zote mpaka Saa 12 ndio zinaanza kuuzwa.

Wameniboa sana wakati nipo pale niliukumbuka huu uzi nikasema kweli, Waislam ni watu kwa kuwatazama Tu.
 
Usishangae hapo akija mtalii akauziwa
 
Reactions: K11
Ulichojibu sicho nilichouliza ndugu, ni wapi kwenye maelezo yangu nimegusia suala la kuwaadhibu watu 'waislamu au wasiokuwa waislamu' wasiofunga mchana wa Ramadhani? naomba yanukuu kisha nionyeshe
Nimejibu kwanza hoja zako ambazo umeweka nadhani umeona.

Unapojenga hoja maana yake ni dalili zamg
Hatari sana.
 

Ndugu, mbona maswali yangu yalikuwa mepesi sana, au nilikosea kuyauliza kiasi cha kushindwa kunielewa nilichokusudia? hadi dakika hii nimepigwa na butwaa: umenifafanulia mambo ambayo nilikuwa siyahitaji na mbaya zaidi mengine umefafanua kwa ufahamu mbovu ...

Kipengele cha kwanza cha swali langu: ulichojibu sicho, na badala yake ukanivisha swali linaloashiria naunga mkono vitendo ambavyo hata sikufikiri wala kuviashiria kuvigusia wala kuvielezea kwenye maelezo yangu

Kipengele cha pili cha swali langu: ungejibu moja kwa moja tu kwamba "sina fatawa ya mwanazuoni yeyote inayo-support maoni 'mada' yangu, au ninazo fatwa: lakini hazina dalili za kisharia, au dalili zake ni shaz au dhwaif, au ungenijibu kwa dalili ya kudhania: kwamba huenda zikawepo lakini hazijakudiriki". Hivyo tu ingejitosheleza. Kwenye hichi kipengele cha pili kwa haraka kasome MAJMOO AL FATAWA juzuu ya 8 ukurasa wa 75 - 80 cha SHAYKH AL UTHAYMEEN

WALLAH nikisema nikosoe kila ufahamu mbovu ulioeleza kwenye ufafanuzi wako hii mada itatoka nje ya mstari, kwa heshima naomba niishie hapa
 
Kwa ufupi ndugu hakuna dalili katika uislamu inayokataza watu kula hadharani mchana wa ramadhani maadamu watu hao hawajalazimishwa na sheria.

Hiyo ndio point yangu mkuu.

Uliza maswali kutoka katika point hiyo.
kasome Majmoo Al Fatawa juzuu ya 8 ukurasa wa 75 - 80 cha mwanazuoni Shaykh Muhammad Ibn Salih Al Uthaymeen
Kwa bahati mbaya sifanyii kazi mambo kama haya.

Kama una hoja ya hadithi ama Qurani unaweza kuweka lakini sio maneno ya mwanachuoni.


mbaya zaidi mengine umefafanua kwa
Ni jukwaa huru unaruhusiwa kuweka uovu pale unapopenda.
Wallah nikisema nikosoe kila ufahamu mbovu ulioeleza kwenye ufafanuzi wako hii mada itatoka nje ya mstari,
Lazima tutoke nje ya maudhui kwa sababu utategemea hpja zingine kutetea hoja yako

Sina tatizo na hilo na mimi nitatoa hoja zingine kutetea hoja yangu,na mimi kwa wema tu niko tayari kwa hilo ikiwa utakuwa na muda.
 

Sawa, mimi naomba kwa hayo machache tuliyojadiliana niishie hapo [emoji4]

الله أعلم
 
Unataka uniambie mpaka leo waislamu bado tunatumia ngamia na farasi kama chombo cha usafiri na tunawasiliana kwa njia ya barua zilizoandikwa kwenye ngozi?

Au nini maana ya kuishi kama Karne ya saba?
Kwa sababu hujitambui bado, si kosa lako. Chunguza jamii inayokuzunguka inaishije.
 
Kimsingi uislamu unakwaza sana sometimes basi tu tunawavumilia. Imagine lile sakata la kuchinja wakati wa kikwete. Yani mwislam analazimisha akuchinjie kisa ni ibada kwake sasa mimi ibada yako inanihusu nini?
 
Kunani huko china mkuu....

Sijapata habari za china zinazohusiana na waislamu..
 
Kunani huko china mkuu....

Sijapata habari za china zinazohusiana na waislamu..
Serikali ya CHINA iliweka marufuku kwa waislamu kufunga mwezi wa RAMADHANI, nguvu zilielekezwa zaidi kwa waislamu wanaoishi UYGHUR, wanaokiuka wanaadhibiwa kwa kufungulishwa kwa nguvu, kupigwa, kifungo na mengine mengi
 
Serikali ya China iliweka marufuku kwa waislamu kufunga mwezi wa Ramadhani, nguvu zilielekezwa zaidi kwa waislamu wanaoishi UYGHUR, wanaokiuka wanaadhibiwa kwa kufungulishwa kwa nguvu, kupigwa, kifungo na mengine mengi
Huo ni mtihani kwa waislamu wa china.

Kama ambavyo mtume alipata shida pale makka wakati anaanzisha daawah na wachina wanapitia katika hali flani ngumu kwa kweli.

Ila katika hilo kama ni kweli basi serikali ya china wanafanya upuuzi mkubwa.
 
Tusipoangalia tutaishia kama nchi za Afrika Magharibi kuwa wanafiki kupigania dini isiyo na mantiki kwetu. Kula ni muhimu kwa kila mwanadamu na Mungu hajakataza Waafrika tusile. Tunakula ili kuimarisha miili yetu ijengeke vizuri.....asiyetaka kula ni juu yake na Mungu wake. HAKUNA siku Mungu alinishukia na kunikataza nisile, kwanini niwasikilize watu na kufuata utashi wao? Nakula kwa sababu nataka nijenge mwili wangu, shida iko wapi? Kwa kweli serikali ingilieni undani ujinga huu wa watu kuingia mitaani kutafuta watu wanaokula mchana. Ukiondoa vijana wanaotumiwa na masheikh/walimu wa dini kusaka walaji mchana huko Zanzibar ila pia kuna wapuuzi wengine wana hasira zao tu kwa sababu hawawezi kula mara tatu au nne kwa siku hivyo wanajifanya wakareketwa wa dini na kutafuta watu wanaokula kuwashikisha adabu kumbe wana hasira zao kuwa hawana vipato vya kula kama wao. This is beyond stupidity, yaani sijuwi waafrika tutaelimika lini?
 
So mkuu tunatofautitishaje kipindi hiki cha ramadhan kwamba huyu ni muislam na yule ni mkiristo..?
 
So mkuu tunatofautitishaje kipindi hiki cha ramadhan kwamba huyu ni muislam na yule ni mkiristo..?
Mkuu unataka kusemaje hapo kabla sijakujibu ?

Au unakusudia kwamba ramadhani inasaidia kuwajua waislamu wepi na wasiokuwa waislamu wepi ?
 
Kwa sababu hujitambui bado, si kosa lako. Chunguza jamii inayokuzunguka inaishije.
Kama kuna mtu ajitambui hapa ni wewe maana huwezi kunyoosha maelezo?

Nimekuuliza nini maana ya kuishi karne ya saba?
 
Yaani chakula changu mwenyewe nipangiwe na mtu nisile kwa masuala yake binafsi kheeee.
Tatizo kila kilichofanywa na mwarabu kwao ni cha allah hakuna kuhoji.Zanzibar wanaiga arabuni na hata uafrika hawapendi basi tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…