Uislamu haujakataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani, siungi mkono wasio waislamu kuzuiwa kula mchana

Wacha tu wakatazwe kula hadharani. Wakiachiwa mpk walio waislam watakula mchana wa Ramadhan tena hadharani kabisa. Halafu nani atabeba hio dhimma!?
Kwani walio waislam na wasio waislamu wakila shida iko wapi?,na kama mtu ni muislamu na akaamua kula mchana dhambi si anapata mwenyewe shida iko wapi,na je kama ni wagonjwa?, wewe kama umefunga na una imani kwelikweli unatakiwa ushindane na matamanio sio kuingilia uhuru wa watu wengine,mi nadhani mambo ya kulazimishana kwenye dini hayana maana yoyote,imani inatoka moyoni sio kuigiza, kila mtu afanye kile moyo wake unataka bila kuingilia uhuru wa mwingine.
 
Hiyo dini watu wake ni watu wa mihemko sana tena umkute Mwafrika amesoma soma basi anakuwa ndio kiranja wa kubagua wenzake kwa misingi ya kuita watu makafiri
Kafiri si tusi bali ni yeyote yule anayepinga uwepo wa Allah pekee asiye na mshirika, Anayepinga

maamrisho ya Allah, pamoja na anayekana siku ya Kufufuliwa na kulipwa kwa yale aliyoyatenda hapa duniani.
 
Zichangamane na imani yao
Kuchangamana unakusudia nini ?

Waislamu waingize ibada za dini zingine kwenye misikiti ?

Au washirikiane katika mambo ya kijamii yasiyohusisha ibada ?

Au unakusudia nini hasa ukisema neno kuchangamana mkuu ?
 
Halafu nani atabeba hio dhimma!?
أَمْ لَمْ يُنَبَّأْ بِمَا فِي صُحُفِ مُوسَىٰ

(ANNAJM - 36)
Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?

وَإِبْرَاهِيمَ الَّذِي وَفَّىٰ

(ANNAJM - 37)
Na vya Ibrahimu aliye timiza ahadi?

ألا تزر وازرة وزر أخرى

[ ANNAJM - 38 ]
Ya kwamba hakika nafsi iliyo beba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?

Kila nafsi itabeba madhambi yake yenyewe.
 
Kuchangamana unakusudia nini ?

Waislamu waingize ibada za dini zingine kwenye misikiti ?

Au washirikiane katika mambo ya kijamii yasiyohusisha ibada ?

Au unakusudia nini hasa ukisema neno kuchangamana mkuu ?
Dini zingine zifanye shughuli zao maeneo/ nchi zenye uislamu bila kubughudhiwa
 
Wasabato kwa Imani yao hawafanyikazi siku ya j'mosi lakini watu wengine wasio na mlengo huo, wanapigakazi kama Kawa!
 
Wacha tu wakatazwe kula hadharani. Wakiachiwa mpk walio waislam watakula mchana wa Ramadhan tena hadharani kabisa. Halafu nani atabeba hio dhimma!?
Unafunga ili ujitakase na kujiweka karibu na muumba wako ama unafunga kwa sababu hamna namna utafanyaje ni lazma iwe hvyo?
 
Hivi ni wapi kuna watu wamezuiwa kula? Kama ni kuhusu Zanzibar hiyo ni ishu nyengine kabisa mana Zanzibar ni nchi ya Kiislamu, 99% ya watu wao ni waislamau. So wana haki ya kujipangia wanavyotaka wao, Unapokua mgeni nchi za watu heshimu sheria za watu.
 
Msaada wandugu; hivi dhambi unapambana nayo uishinde au unaipiga marufuku isiwepo?.

Na utaonekana vipi mshindi endapo hakuna kitu unachotakiwa kukishinda?.
Point yako ni ipi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…