Uislamu haujakataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani, siungi mkono wasio waislamu kuzuiwa kula mchana

Uislamu haujakataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani, siungi mkono wasio waislamu kuzuiwa kula mchana

Samahan mtoa post, nauliza kati ya Mtume na Allah nani ambaye ana mamlaka ya kukataza? Maana umesema hakuna mahali mtume amekataza…
Wote wanayo mamlaka ya kukataza ndugu
 
Mkuu kafiri maana yake ni kila asiyekuwa muislamu.

Kwa maana ni jina la jumla kwa kila asiyekuwa muislamu, badala ya uislamu kutamka dini zote ikaona iweke kwa ufupi tu kuwa wasiokuwa waislamu ni makafiri.

Hili jina linaonekana baya kwa sababu ya mindset zetu zimejengeka na tunalisikia likitajwa katika maeneo hatarishi.

Kama vile katika mambo ya kuuana utaskia anatajwa kaafiriii, mtu ataona hee kumbe kafiri hii ni jitu la kuuawa kabisa kumbe sivyo kabisa.

Hivyo kafiri ni jina la utambulisho kwa wasiokuwa waislamu mkuu.

Ni kama ukienda kwenye fani ya afya mgonjwa ataitwa mteja, utajiuliza kwamba mimi naumwa alafu naitwa mteja?


Kumbe Maana yake mteja ni mtu ambaye anakuja pale kutaka huduma.

Hivyo neno mteja ni jina la jumla kama ambavyo neno kafiri ni la jumla

Moderators nao wajue hili neno na maana yake, na sio kukurupuka kupiga watu ban kisa eti flani kaambiwa kafiri.
 
Habarini za kutwa nyote.

Naomba niseme kwamba katika dini yetu ya uislamu hakuna pahala mtume kamkataza asiyekuwa muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna pahala qurani imekataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna sehemu wakati wa mtume imeonesha kwamba walikatazwa wasiokuwa waislamu wasile mchana wa ramadhani.

Katika masharti ya mtu kulazimika kufunga kwanza awe muislamu.

Kwa maana asiyekuwa muislamu hailazimiki kufunga,kama halazimiki kufunga maana yake ana uhalali wa kula mchana wa ramadhani kwa sababu sio muislamu.

Mtu anaweza akasema kwamba wamekatazwa wasile hadharani ?

Hadharani kwanza ni wapi kwa mujibu wa sheria ya dini ?

Watu wanakula kwenye migahawa hakuna anayekunywa chai na chapati anatembea pale kariakoo.

Hivyo kuhusu kula hadharani uislamu pia haujakataza kwa sababu neno hadharani ni pana katika muktadhwa huu.

Uislamu umekataza kwa muislamu ambaye hana udhuru wowote alafu akala mchana wa ramadhani,huyu anapata dhambi.

Lakini kuwakataza watu wasile mchana na kuwashambulia sio katika adabu za kiislamu kwa sababu

Kuna wagonjwa hawatakiwi kufunga.
Kuna wanawake wako kwenye siku
Kuna watoto
Kuna wazee
Kuna wasafiri
Kuna wasiokuwa waislamu

Hawa wote ruhusa kula mchana kwa mujibu wa ssheri ya uislamu wetu.

Sasa kama wanaruhusiwa kula mchana vipi wasiruhusiwe kula hadharani wakati hakuna katazo lolote la kula hadharani katika uislamu.

Allah anasema..

"Hakuna kulazimishana katika dini"

Asiye muislamu kumkataza asile mchana maana yake unamlazimisha akae na njaa jambo ambalo sheria ya dini imekataza.

Tutaheshimu sheria itakayowekwa na serikali lakini tunaomba sheria hizo zisinasibishwe na uislamu.

Ni bora uislamu ulaumiwe kwa sheria ambayo kweli imeiweka kama vile viboko kwa wazinifu n.k

Kuliko uislamu kulaumiwa kwa sheria ambayo haijaiweka kama hizi kukataza kula mchana wa ramadhani

Nakaribisha maswali.

Naomba kuwasilisha.
Uko vizuri Maalim. Nimekusoma
 
Na kwann uislamu uogope competition kutoka imani zingine
 
Kafiri ni mtu yoyote yule asiye amini uwepo wa MUNGU au yule anae amini uwepo wa Miungu mingine zaidi ya MUNGU mmoja alieumba mbingu na nchi.
Hata kama anajiita ni muislamu ila kama anaamini na kuiomba/kuitegemea miungu mingine imtatulie shida zake zaidi ya MUNGU mmoja mfano mizimu, nyoka, majini n.k huyo pia anahesabika ni kafiri vile pia.
Swali: kwa nini waislamu wanawaita wakristo ni makafiri?
Jibu: sio matakwa yetu kuwaita hivyo ila Qur'ani tayari imeshaelezea ukafiri wa wakristo na imewetaja wakristo ni makafiri.
Swali: Ni upi haswa ukafiri wa Wakristo?
Jibu:
“Kwa hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni wa tatu wa Utatu. Hali hakuna mungu ila Mungu Mmoja.” (al-Maida, 5/73).

“Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu. Sema: Ni nani mwenye kumiliki cho chote mbele ya Mwenyezi Mungu ikiwa Yeye angetaka kumuangamiza Masihi mwana wa Maryamu, na mama yake, na wote waliomo katika ardhi? Na mamlaka ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ni vya Mwenyezi Mungu. Huumba apendavyo. Na Mwenyezi Mungu anao uweza juu ya kila kitu.” (al-Maida, 5/17)

“Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu! Na hali Masihi mwenyewe alisema: Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio dhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru.” (al-Maida, 5/72).

Kama bado una swali lolote kuhusu ukafiri unaruhusiwa kuuliza.
Kwa hiyo Wana wa Israel ambao ni wayahudi hawakuwa waarabu sio?
 
Msaada wandugu; hivi dhambi unapambana nayo uishinde au unaipiga marufuku isiwepo?.

Na utaonekana vipi mshindi endapo hakuna kitu unachotakiwa kukishinda?.
 
Habarini za kutwa nyote.

Naomba niseme kwamba katika dini yetu ya uislamu hakuna pahala mtume kamkataza asiyekuwa muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna pahala qurani imekataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna sehemu wakati wa mtume imeonesha kwamba walikatazwa wasiokuwa waislamu wasile mchana wa ramadhani.

Katika masharti ya mtu kulazimika kufunga kwanza awe muislamu.

Kwa maana asiyekuwa muislamu hailazimiki kufunga,kama halazimiki kufunga maana yake ana uhalali wa kula mchana wa ramadhani kwa sababu sio muislamu.

Mtu anaweza akasema kwamba wamekatazwa wasile hadharani ?

Hadharani kwanza ni wapi kwa mujibu wa sheria ya dini ?

Watu wanakula kwenye migahawa hakuna anayekunywa chai na chapati anatembea pale kariakoo.

Hivyo kuhusu kula hadharani uislamu pia haujakataza kwa sababu neno hadharani ni pana katika muktadhwa huu.

Uislamu umekataza kwa muislamu ambaye hana udhuru wowote alafu akala mchana wa ramadhani,huyu anapata dhambi.

Lakini kuwakataza watu wasile mchana na kuwashambulia sio katika adabu za kiislamu kwa sababu

Kuna wagonjwa hawatakiwi kufunga.
Kuna wanawake wako kwenye siku
Kuna watoto
Kuna wazee
Kuna wasafiri
Kuna wasiokuwa waislamu

Hawa wote ruhusa kula mchana kwa mujibu wa ssheri ya uislamu wetu.

Sasa kama wanaruhusiwa kula mchana vipi wasiruhusiwe kula hadharani wakati hakuna katazo lolote la kula hadharani katika uislamu.

Allah anasema..

"Hakuna kulazimishana katika dini"

Asiye muislamu kumkataza asile mchana maana yake unamlazimisha akae na njaa jambo ambalo sheria ya dini imekataza.

Tutaheshimu sheria itakayowekwa na serikali lakini tunaomba sheria hizo zisinasibishwe na uislamu.

Ni bora uislamu ulaumiwe kwa sheria ambayo kweli imeiweka kama vile viboko kwa wazinifu n.k

Kuliko uislamu kulaumiwa kwa sheria ambayo haijaiweka kama hizi kukataza kula mchana wa ramadhani

Nakaribisha maswali.

Naomba kuwasilisha.
Kama hakuna wa kupaza sauti juu ya kugomeana huko, kuna siku watakuja kutuambia TUSISHEHEREKEE PASAKA kama imo ndani ya mfungo..!!!
 
Hiyo dini watu wake ni watu wa mihemko sana tena umkute Mwafrika amesoma soma basi anakuwa ndio kiranja wa kubagua wenzake kwa misingi ya kuita watu makafiri
 
Hiyo dini watu wake ni watu wa mihemko sana tena umkute Mwafrika amesoma soma basi anakuwa ndio kiranja wa kubagua wenzake kwa misingi ya kuita watu makafiri
Mungu atuepushe
 
Nimeona barua fulani Zanzibar nikacheka sana maana binadamu tunaangamia kwa kukosa maarifa na ufahamu wa nini tunaabudu. Kweli binadamu ambaye maisha yake ni kama upepo muda wowote yanapeperuka anajigeuza Mungu kuwahukumu wengine dhambi eti kisa amekula maajabu kabisa
Tatizo wamenyimwa vichogo! Hivyo akili zao zote zimegeuka na kuwa urojo. Yaani usiku mzimu ni kusindilia tu! Sijui futari, wali maharage, chai, soda, vitafuno mbalimbali! Mpaka saa 11 alfajiri!

Halafu mchana wanajifanya eti wamefunga! Wizi mtupu. Huko ni kubadilisha tu ratiba ya chakula.
 
Back
Top Bottom