Uislamu haujakataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani, siungi mkono wasio waislamu kuzuiwa kula mchana

Uislamu haujakataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani, siungi mkono wasio waislamu kuzuiwa kula mchana

Habarini za kutwa nyote.

Naomba niseme kwamba katika dini yetu ya uislamu hakuna pahala mtume kamkataza asiyekuwa muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna pahala qurani imekataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna sehemu wakati wa mtume imeonesha kwamba walikatazwa wasiokuwa waislamu wasile mchana wa ramadhani.

Katika masharti ya mtu kulazimika kufunga kwanza awe muislamu.

Kwa maana asiyekuwa muislamu hailazimiki kufunga,kama halazimiki kufunga maana yake ana uhalali wa kula mchana wa ramadhani kwa sababu sio muislamu.

Mtu anaweza akasema kwamba wamekatazwa wasile hadharani ?

Hadharani kwanza ni wapi kwa mujibu wa sheria ya dini ?

Watu wanakula kwenye migahawa hakuna anayekunywa chai na chapati anatembea pale kariakoo.

Hivyo kuhusu kula hadharani uislamu pia haujakataza kwa sababu neno hadharani ni pana katika muktadhwa huu.

Uislamu umekataza kwa muislamu ambaye hana udhuru wowote alafu akala mchana wa ramadhani,huyu anapata dhambi.

Lakini kuwakataza watu wasile mchana na kuwashambulia sio katika adabu za kiislamu kwa sababu

Kuna wagonjwa hawatakiwi kufunga.
Kuna wanawake wako kwenye siku
Kuna watoto
Kuna wazee
Kuna wasafiri
Kuna wasiokuwa waislamu

Hawa wote ruhusa kula mchana kwa mujibu wa ssheri ya uislamu wetu.

Sasa kama wanaruhusiwa kula mchana vipi wasiruhusiwe kula hadharani wakati hakuna katazo lolote la kula hadharani katika uislamu.

Allah anasema..

"Hakuna kulazimishana katika dini"

Asiye muislamu kumkataza asile mchana maana yake unamlazimisha akae na njaa jambo ambalo sheria ya dini imekataza.

Tutaheshimu sheria itakayowekwa na serikali lakini tunaomba sheria hizo zisinasibishwe na uislamu.

Ni bora uislamu ulaumiwe kwa sheria ambayo kweli imeiweka kama vile viboko kwa wazinifu n.k

Kuliko uislamu kulaumiwa kwa sheria ambayo haijaiweka kama hizi kukataza kula mchana wa ramadhani

Nakaribisha maswali.

Naomba kuwasilisha.
Tatizo wale waliojifunza uislam vichochoroni ndo wanaona ni makosa wengine kula mchana.

Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
 
Kwani walio waislam na wasio waislamu wakila shida iko wapi?,na kama mtu ni muislamu na akaamua kula mchana dhambi si anapata mwenyewe shida iko wapi,na je kama ni wagonjwa?, wewe kama umefunga na una imani kwelikweli unatakiwa ushindane na matamanio sio kuingilia uhuru wa watu wengine,mi nadhani mambo ya kulazimishana kwenye dini hayana maana yoyote,imani inatoka moyoni sio kuigiza, kila mtu afanye kile moyo wake unataka bila kuingilia uhuru wa mwingine.
Serikali itabeba dhimma ndio. Bora mtu ale huko kwa kujificha atajijua mwenyewe na Mola wake. Kuna wtt tunawakuza wakiona mambo km hayo watajifunza nini?

Nyumbani tunawafundisha kufunga wakitoka nje waone watu wanajilia ovyo tu na kuvuta sigara na kufanya uesherati wao hadharani.

Kazini tunafanya kazi na wakristo na wanakula kwa staha tu. Hamna anaowakataza wala kuwalazimisha kufunga. Kwa sababu inajulikana haijawalizimikia. Lkn hawatoki nje wakala hadharani.

Kuhusu Wagonjwa, vikongwe, wajawazito, wanaonyonyesha, wasafiri na wenye dharura hio imeshatolewa maeleze kwenye Qur'an.
IMG-20220403-WA0047.jpg
 
Unafunga ili ujitakase na kujiweka karibu na muumba wako ama unafunga kwa sababu hamna namna utafanyaje ni lazma iwe hvyo?
Nafunga ili nipate kumcha Allah.

Kama hamna namna si ningekula tu kuna shida gani
 
Hivi ni wapi kuna watu wamezuiwa kula? Kama ni kuhusu Zanzibar hiyo ni ishu nyengine kabisa mana Zanzibar ni nchi ya Kiislamu, 99% ya watu wao ni waislamau. So wana haki ya kujipangia wanavyotaka wao, Unapokua mgeni nchi za watu heshimu sheria za watu.
Kwahyo leo hii wakristo wa Italia wakiweka sheria hakuna kula hadharani wakati wa kwaresma utaona wametenda haki ?
 
Serikali itabeba dhimma ndio. Bora mtu ale huko kwa kujificha atajijua mwenyewe na Mola wake. Kuna wtt tunawakuza wakiona mambo km hayo watajifunza nini?

Nyumbani tunawafundisha kufunga wakitoka nje waone watu wanajilia ovyo tu na kuvuta sigara na kufanya uesherati wao hadharani.

Kazini tunafanya kazi na wakristo na wanakula kwa staha tu. Hamna anaowakataza wala kuwalazimisha kufunga. Kwa sababu inajulikana haijawalizimikia. Lkn hawatoki nje wakala hadharani.

Kuhusu Wagonjwa, vikongwe, wajawazito, wanaonyonyesha, wasafiri na wenye dharura hio imeshatolewa maeleze kwenye Qur'an. View attachment 2174435
Swali ni moja tu.

Utaratibu wa kukataza watu kula hadharani mmeutoa kwenye Quran, hadith au muongozo upi wa kiislamu ?
 
Misikitini hatuna nafasi ya kusema.

Acha tuseme huku ambako tunayo nafasi na ujumbe utafika tu
Km wewe unaijua kweli na unaogopa kuisema hadharani halafu unachimba shimo unaingiza shingo humo ndo unapaza sauti, basi wewe unaingia kwenye kundi la wanafiki.

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
Habarini za kutwa nyote.

Naomba niseme kwamba katika dini yetu ya uislamu hakuna pahala mtume kamkataza asiyekuwa muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna pahala qurani imekataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna sehemu wakati wa mtume imeonesha kwamba walikatazwa wasiokuwa waislamu wasile mchana wa ramadhani.

Katika masharti ya mtu kulazimika kufunga kwanza awe muislamu.

Kwa maana asiyekuwa muislamu hailazimiki kufunga,kama halazimiki kufunga maana yake ana uhalali wa kula mchana wa ramadhani kwa sababu sio muislamu.

Mtu anaweza akasema kwamba wamekatazwa wasile hadharani ?

Hadharani kwanza ni wapi kwa mujibu wa sheria ya dini ?

Watu wanakula kwenye migahawa hakuna anayekunywa chai na chapati anatembea pale kariakoo.

Hivyo kuhusu kula hadharani uislamu pia haujakataza kwa sababu neno hadharani ni pana katika muktadhwa huu.

Uislamu umekataza kwa muislamu ambaye hana udhuru wowote alafu akala mchana wa ramadhani,huyu anapata dhambi.

Lakini kuwakataza watu wasile mchana na kuwashambulia sio katika adabu za kiislamu kwa sababu

Kuna wagonjwa hawatakiwi kufunga.
Kuna wanawake wako kwenye siku
Kuna watoto
Kuna wazee
Kuna wasafiri
Kuna wasiokuwa waislamu

Hawa wote ruhusa kula mchana kwa mujibu wa ssheri ya uislamu wetu.

Sasa kama wanaruhusiwa kula mchana vipi wasiruhusiwe kula hadharani wakati hakuna katazo lolote la kula hadharani katika uislamu.

Allah anasema..

"Hakuna kulazimishana katika dini"

Asiye muislamu kumkataza asile mchana maana yake unamlazimisha akae na njaa jambo ambalo sheria ya dini imekataza.

Tutaheshimu sheria itakayowekwa na serikali lakini tunaomba sheria hizo zisinasibishwe na uislamu.

Ni bora uislamu ulaumiwe kwa sheria ambayo kweli imeiweka kama vile viboko kwa wazinifu n.k

Kuliko uislamu kulaumiwa kwa sheria ambayo haijaiweka kama hizi kukataza kula mchana wa ramadhani

Nakaribisha maswali.

Naomba kuwasilisha.
wewe sio muislam kaa kimyaaa
 
Sawa,
Ila sisi ambao hatufungi basi ni vyema kutafuta sehemu ambayo haipo hadharani

Ni ustaarabu tu

Funga yako wewe inamzuia nini mtu mwingi kula, kwanza kufunga ni ibada ambayo inapaswa kuwa siri baina yako wewe na Mungu, sasa iweje ukifunga unataka kila mtu ajue umefunga na kuzuia watu wengine kula wakati wa mfungo? Huu upuuzi na ubinafsi wa hali ya juu.
 
HONGERA KAMA UNALIJUA HILO

KABALISHE HIYO TITTLE YAKO ULOIANDIKA KWENYE HABARI/NYUZI HII
Nikupe pole sana kwa sababu mpaka leo hujui kwamba kuna kauli za waislamu zinaharamisha wasio waislamu kula mchana wa ramadhani hata kama sio hadharani.

Pole sana ndugu.
 
Habarini za kutwa nyote.

Naomba niseme kwamba katika dini yetu ya uislamu hakuna pahala mtume kamkataza asiyekuwa muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna pahala qurani imekataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna sehemu wakati wa mtume imeonesha kwamba walikatazwa wasiokuwa waislamu wasile mchana wa ramadhani.

Katika masharti ya mtu kulazimika kufunga kwanza awe muislamu.

Kwa maana asiyekuwa muislamu hailazimiki kufunga,kama halazimiki kufunga maana yake ana uhalali wa kula mchana wa ramadhani kwa sababu sio muislamu.

Mtu anaweza akasema kwamba wamekatazwa wasile hadharani ?

Hadharani kwanza ni wapi kwa mujibu wa sheria ya dini ?

Watu wanakula kwenye migahawa hakuna anayekunywa chai na chapati anatembea pale kariakoo.

Hivyo kuhusu kula hadharani uislamu pia haujakataza kwa sababu neno hadharani ni pana katika muktadhwa huu.

Uislamu umekataza kwa muislamu ambaye hana udhuru wowote alafu akala mchana wa ramadhani,huyu anapata dhambi.

Lakini kuwakataza watu wasile mchana na kuwashambulia sio katika adabu za kiislamu kwa sababu

Kuna wagonjwa hawatakiwi kufunga.
Kuna wanawake wako kwenye siku
Kuna watoto
Kuna wazee
Kuna wasafiri
Kuna wasiokuwa waislamu

Hawa wote ruhusa kula mchana kwa mujibu wa ssheri ya uislamu wetu.

Sasa kama wanaruhusiwa kula mchana vipi wasiruhusiwe kula hadharani wakati hakuna katazo lolote la kula hadharani katika uislamu.

Allah anasema..

"Hakuna kulazimishana katika dini"

Asiye muislamu kumkataza asile mchana maana yake unamlazimisha akae na njaa jambo ambalo sheria ya dini imekataza.

Tutaheshimu sheria itakayowekwa na serikali lakini tunaomba sheria hizo zisinasibishwe na uislamu.

Ni bora uislamu ulaumiwe kwa sheria ambayo kweli imeiweka kama vile viboko kwa wazinifu n.k

Kuliko uislamu kulaumiwa kwa sheria ambayo haijaiweka kama hizi kukataza kula mchana wa ramadhani

Nakaribisha maswali.

Naomba kuwasilisha.
naungana na wewe mkuu
 
Bora mtu ale huko kwa kujificha atajijua mwenyewe na Mola wake.
Hapa unakusudia mtu ale nyumbani kwake asile hadharani akaonekana na watu.
Kuna wtt tunawakuza wakiona mambo km hayo watajifunza nini?
Hii hoja inanipa shida mno kwa sababu hao Wasiofunga wakila majumbani mwao si wanaishi na watoto wa kiislamu ambao wqtakuwa wanaona hao watu wakila chakula.

Au pia wajifungie mavyumbani huko wachungulie kama hakuna watoto wanaoona wakati wanakula ?

Hiyo itakuwa ni tashaddudi ambayo hata kwenye dini haijaelezwa ni matashi ya watu.
Nyumbani tunawafundisha kufunga wakitoka nje waone watu wanajilia ovyo tu na kuvuta sigara na kufanya uesherati wao hadharani.
Mkuu nyumbani mnawafundisha watoto kusali lakini wakitoka nje wanaona watu kibao hawaendi kusali muda wa sala mbona hili haliwapotoshi watoto wa kiislamu badala yake wanasali ?

Mnachotakiwa kuwwfundisha watoto ni kuwa kuna ambao hawafungi mtawaona wanakula msiwashangae wana nyudhuru na wengine sio waislamu.

Ila nadhani mafundisho mnayowapa watoto mnawadanganya kwamba huko nje hakuna mtu ambaye anakula katika mwezi wa ramadhani ndio maana mnahofia wasije watoto wakaona watu wanakula.
Imani haifundishwi hivyo.
Lkn hawatoki nje wakala hadharani.
Migahawa inafungwa.

Je ukila ndani ya mgahawa ni hadharani mpaka ifungwe migahawa ?
Au mkuu unaelewa nini maana ya neno hadharani ?
hio imeshatolewa maeleze kwenye Qur'an.
Na kuhusu wasio waislamu kula mchana katika miji hilo halijatolewa maelekezo bali ni maelekezo ya wqtu.

Why yanasibishwe na uislamu wakati Qurani haijasema mambo hayo aisee
 
Kafiri ni mtu yoyote yule asiye amini uwepo wa MUNGU au yule anae amini uwepo wa Miungu mingine zaidi ya MUNGU mmoja alieumba mbingu na nchi.
Hata kama anajiita ni muislamu ila kama anaamini na kuiomba/kuitegemea miungu mingine imtatulie shida zake zaidi ya MUNGU mmoja mfano mizimu, nyoka, majini n.k huyo pia anahesabika ni kafiri vile pia.
Swali: kwa nini waislamu wanawaita wakristo ni makafiri?
Jibu: sio matakwa yetu kuwaita hivyo ila Qur'ani tayari imeshaelezea ukafiri wa wakristo na imewetaja wakristo ni makafiri.
Swali: Ni upi haswa ukafiri wa Wakristo?
Jibu:
“Kwa hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni wa tatu wa Utatu. Hali hakuna mungu ila Mungu Mmoja.” (al-Maida, 5/73).

“Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu. Sema: Ni nani mwenye kumiliki cho chote mbele ya Mwenyezi Mungu ikiwa Yeye angetaka kumuangamiza Masihi mwana wa Maryamu, na mama yake, na wote waliomo katika ardhi? Na mamlaka ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ni vya Mwenyezi Mungu. Huumba apendavyo. Na Mwenyezi Mungu anao uweza juu ya kila kitu.” (al-Maida, 5/17)

“Hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu! Na hali Masihi mwenyewe alisema: Enyi Wana wa Israili! Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio dhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru.” (al-Maida, 5/72).

Kama bado una swali lolote kuhusu ukafiri unaruhusiwa kuuliza.
Ina maana Quran ilikuja kutengua injili?
 
Hivi ni wapi kuna watu wamezuiwa kula?
Screenshot_20220403-192854_Samsung Internet.jpg

Kuna hiyo fatwa hapo ambayo inakataza kabisa asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na pia zipo sehemu migahawa imefungwa kabisa kwa kusema kwamba mchana wa ramadhani hairuhusiwi kula hadharani.

Je mgahawani ni hadharani ?
Kama ni kuhusu Zanzibar hiyo ni ishu nyengine kabisa mana Zanzibar ni nchi ya Kiislamu, 99% ya watu wao ni waislamau.
Mbona zanzibar haihimizi kila mtu atakayekutwa nje muda wa sala apigwe au apewe adhabu kwa sababu huoo ni muda wa sala ?

Unaposema 99 ni waislamu hiyo 1% hawana haki ya kula mchana wakati ilikuwa waachwe tu kwa sababu hiyo 1% haina madhara yoyote hata wakila mchana itaonekana kana kwwmba wote wamefunga tu ?

Unapokua mgeni nchi za watu heshimu sheria za watu.
Sheria lazima ziheshimiwe.

Hata tunachokisema ni kwaba uislamu haujakataza popote watu kula mchana wa ramadhani kwa wale ambao hawalazimiki kufunga.
 
Back
Top Bottom