Ujamaa ni sababu mojawapo kubwa ya umasikini na uharibifu wa nchi nyingi za Afrika

Ujamaa ni sababu mojawapo kubwa ya umasikini na uharibifu wa nchi nyingi za Afrika

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Wanahistoria, wachambuzi na watu wengine wengi mnaopenda kufuatilia maendeleo katika bara la Africa mnapaswa kutilia maanani madhara, hasara na legacy ya ujamaa katika kufifisha maendeleo ya nchi za Africa zilizofuatisha mfumo huo wa uchumi.

Nchi nyingi za Africa wakati zinapata uhuru miaka ya 1960 zilipata uhuru na zikarithi uchumi wa wakoloni uliokuwa ukikua.Viwanda vilivyokuwepo vilikuwa vikifanya kazi kwa ufanisi, hali ya biashara ilikuwa nzuri, sekta ya kilimo ilikuwa nzuri inayokua huku ikiweza kulisha raia wote bila kuagiza chakula nje, hifadhi ya fedha za kigeni ilikuwepo, huduma za kijamii nazo zilikuwa zikisonga mbele n.k

Punde tu baada ya kupata Uhuru miaka ya 60 baadhi ya viongozi kama Nkuramah, Leopold Senghor, Sekou Toure, Julius Nyerere, Kaunda, Milton Obote, Mengistu Haile Mariam(Ethiopia haikuwahi kuwa koloni)na wengine wakaja na sera zao za ujamaa. Japo zilitofautiana lakini zilifanana katika mambo muhimu kama "nationalization", vijiji vya ujamaa, chama kimoja, na kutoruhusu uwekezaji kutoka nje.

Kitu walichosahau au ambacho hawakuzingatia viongozi hawa ni kwamba Africa kwa asili yake ilikuwa ni bara la soko huria au la kibepari tangu karne na karne. Kabla ya ukoloni na hata baada ya wakoloni kuja. Ujamaa ulioletwa miaka ya 1960 hadi 70 ulikuwa kitu kigeni sana kwa raia wa bara hili. Uliharibu na kuvuruga mfumo mzima wa soko huria uliojengeka kwa karne nyingi.

Ujamaa ulileta rushwa, uzembe, matumizi mabaya ya rasilimali na kodi za wananchi. Uliondoa hata uhuru wa ukosoaji ambao ulikuwepo wakati wa ukoloni! Matokeo yake kadri miaka ilivyosonga mbele uchumi wa hizi nchi na nyingine nyingi za Africa ukadorora sana, ukawa mbovu, viwanda vikafa na vingine vikawa havianzishwi, biashara ikasinyaa, uhuru wa raia ukaminywa, migogoro ikachachamaa, umaskini ukazidi kutapakaa.

Ujamaa ni mfumo ovu sana uliochangia pa kubwa kuliharibu bara hili zuri. Unapaswa kulaaniwa na mtu yeyote anayetazamia siku nzuri za usoni katika bara hili.

Hii ni kwa ufupi sana.
 
Magufuli ndio alitaka kuturudisha huko, mambo ya serikali kufanya kila kitu, sekta binafsi kuonyeshwa kuwa ni wanyonyaji na wimbo wa mkombozi wa wanyonge ukatamalaki

Ndio maana hata serikali ya sasa waseme ina upigaji namna gani, attitude yake kwa sekta binafsi na uwekezaji ni nzuri na ndipo ninapoona unafuu

hakuna cancer kubwa inayoua uchumi na ubunifu wa nchi kama ujamaa
 
Mkoloni mweusi ameliharibu sana hili bara, na jambo baya zaidi ni kwamba yeye aliaminiwa, akapewa support na ndugu zake awavushe hadi kuelekea nchi ya maziwa na asali tofauti na mkoloni mweupe aliyetawala kwa mabavu.
Africa chini ya mkoloni mweupe ilikuwa salama zaidi kuliko mkoloni mweusi.
 
Wanahistoria, wachambuzi na watu wengine wengi mnaopenda kufuatilia maendeleo katika bara la Africa mnapaswa kutilia maanani madhara, hasara na legacy ya ujamaa katika kufifisha maendeleo ya nchi za Africa zilizofuatisha mfumo huo wa uchumi.

Nchi nyingi za Africa wakati zinapata uhuru miaka ya 1960 zilipata uhuru na zikarithi uchumi wa wakoloni uliokuwa ukikua.Viwanda vilivyokuwepo vilikuwa vikifanya kazi kwa ufanisi, hali ya biashara ilikuwa nzuri, sekta ya kilimo ilikuwa nzuri inayokua huku ikiweza kulisha raia wote bila kuagiza chakula nje, hifadhi ya fedha za kigeni ilikuwepo, huduma za kijamii nazo zilikuwa zikisonga mbele n.k

Punde tu baada ya kupata Uhuru miaka ya 60 baadhi ya viongozi kama Nkuramah, Leopold Senghor, Sekou Toure, Julius Nyerere, Kaunda, Milton Obote, Mengistu Haile Mariam(Ethiopia haikuwahi kuwa koloni)na wengine wakaja na sera zao za ujamaa. Japo zilitofautiana lakini zilifanana katika mambo muhimu kama "nationalization", vijiji vya ujamaa, chama kimoja, na kutoruhusu uwekezaji kutoka nje.

Kitu walichosahau au ambacho hawakuzingatia viongozi hawa ni kwamba Africa kwa asili yake ilikuwa ni bara la soko huria au la kibepari tangu karne na karne. Kabla ya ukoloni na hata baada ya wakoloni kuja. Ujamaa ulioletwa miaka ya 1960 hadi 70 ulikuwa kitu kigeni sana kwa raia wa bara hili. Uliharibu na kuvuruga mfumo mzima wa soko huria uliojengeka kwa karne nyingi.

Ujamaa ulileta rushwa, uzembe, matumizi mabaya ya rasilimali na kodi za wananchi. Uliondoa hata uhuru wa ukosoaji ambao ulikuwepo wakati wa ukoloni! Matokeo yake kadri miaka ilivyosonga mbele uchumi wa hizi nchi na nyingine nyingi za Africa ukadorora sana, ukawa mbovu, viwanda vikafa na vingine vikawa havianzishwi, biashara ikasinyaa, uhuru wa raia ukaminywa, migogoro ikachachamaa, umaskini ukazidi kutapakaa.

Ujamaa ni mfumo ovu sana uliochangia pa kubwa kuliharibu bara hili zuri. Unapaswa kulaaniwa na mtu yeyote anayetazamia siku nzuri za usoni katika bara hili.

Hii ni kwa ufupi sana.
Umetoa ubaya wa ujamaa..wala hujaja na suluhisho..wewe mwenyewe unalalamika tu.

Toa suluhisho.

#MaendeleoHayanaChama
 
"MAKUWADI WA MABEBERU"

Wala hamuongelei jinsi UJAMAA ulivyovikwa "umbuzi wa kafara" ili uonekane haufai!!! Wala hamuongelei jinsi WAJAMAA WANAVYOKANDAMIZWA KWA VIKWAZO na mbinu nyingi chafu kuonekana si lolote si chochote....!

Na katika katika mifano yenu wala na kamwe hamtaitaja nchi ya kijamaa kama LIBYA na CUBA ambazo pamoja na kubanwa hazikupigia goti UBEPARI

Vilevile mnasahau UJAMAA sio STATIC, una aina zake, una hatua zake na mikakati yake...! CHINA ni nchi ya kijamaa ambayo imesonga mbele kwa style yake ambayo MEREKANI anaduwaa mpaka leo .... ukiuliza MAKUWADI WA MABEBERU wanakwambia China inafata UBEBARI na si ujamaa!!!!! (WAMEPIGWA NA CHINA BILA KUJUA WAKIDHANI NI MWENZAO) Huo sasa ndo ujamaa!!!

UJAMAA HAUBWABWAJI.......... RUSSIA ANAENDELEA KUTOA SOMO ZURI ... UJAMAA NI IMANI
#
 
Kuna aina za ujamaa. So inabidi uwe makini sana. Mfano china ni nchi ya kijamaa na uchumi wao wanafanya kutumia mbinu za kisasa za kijamaa kusurvive. Pia mataifa ya kiarabu wahindi wengi ni wajamaa ila shida tuna elimu ndogo sana ya ujamaa na namna unatakiwa kufanya kazi.

Ujamaa una hasara kama kuna idadi kubwa ya wazembe wanategemea wachache wapate wao watumie.

Mfano Tanzania kuna idadi kubwa ya raia wanataka serikali ifanye mambo yote wao wakiwa na mchango mdogo sana wa kodi au mapato kwa serikali. Matokeo yake pesa zinakuswanywa Dar zinakwenda kuzikwa huko vijijini ujenzi wa miradi ambayo haina mapato na inaishia kuligharimu taifa mabilioni ya Pesa yanayopotea bila kurudi.


Nenda kausome tena uchumi wa china namna una operate halafu utaelewa wao wanadeal na aina gani ya uchumi na kwann wanaipitia marekani.

Urusi pamoja na kuanguka miaka yote tokea miaka ya 90 mbona bado yupo juu na hatikisiki kiuchumi.

Mtazame marekani, nje anaongea sana propaganda nyingi ila ndani huko changamoto alizonazo afrika ikifunga nae mipaka jamaa atakuwa katika hali mbaya sana maana anategemea kuishi kwa kusumbua wengine ndipo yeye apate.

So kwa kumalizia acheni hizi propaganda za magharibi. Kitu chochote ni kizuri ukikifanya kwa balance nzuri. Huwezi ukawa 100% mjamaa au 100% bepari. Kunahitajika balance. Jambo ambalo China ndio analifanya kwa sasa anatumia mifumo yote ya communists na ubepari.
 
Magufuli ndio alitaka kuturudisha huko, mambo ya serikali kufanya kila kitu, sekta binafsi kuonyeshwa kuwa ni wanyonyaji na wimbo wa mkombozi wa wanyonge ukatamalaki

Ndio maana hata serikali ya sasa waseme ina upigaji namna gani, attitude yake kwa sekta binafsi na uwekezaji ni nzuri na ndipo ninapoona unafuu

hakuna cancer kubwa inayoua uchumi na ubunifu wa nchi kama ujamaa

Kabisa boss, yaani hakuna siasa ya kijinga kama ujamaa. Siasa hizi huzaa viongozi miungu watu, na mambo yake mengi hufanyika kwa shuruti hata kama umma haukubaliani na maamuzi hayo.
 
Urusi iliachana na ujamaa mwaka kati ya mwaka 1990-95. Uchumi wa Russia kwa sasa ni ubepari kwa 95%.

China chini ya ujamaa halisi lilikuwa ni taifa lilichoka sana kiuchumi, miaka 1980 lilifungua uchumi wake kutoka na kuanza kutekeleza sera nyingi za kibepari ndipo likaanza kupiga hatua kubwa za kiuchumi kwa haraka. Sasa hivi ni taifa la pili duniani kuwa na mabilionea wa dola za kimarekani.
Kuna aina za ujamaa. So inabidi uwe makini sana. Mfano china ni nchi ya kijamaa na uchumi wao wanafanya kutumia mbinu za kisasa za kijamaa kusurvive. Pia mataifa ya kiarabu wahindi wengi ni wajamaa ila shida tuna elimu ndogo sana ya ujamaa na namna unatakiwa kufanya kazi.

Ujamaa una hasara kama kuna idadi kubwa ya wazembe wanategemea wachache wapate wao watumie.

Mfano Tanzania kuna idadi kubwa ya raia wanataka serikali ifanye mambo yote wao wakiwa na mchango mdogo sana wa kodi au mapato kwa serikali. Matokeo yake pesa zinakuswanywa Dar zinakwenda kuzikwa huko vijijini ujenzi wa miradi ambayo haina mapato na inaishia kuligharimu taifa mabilioni ya Pesa yanayopotea bila kurudi.


Nenda kausome tena uchumi wa china namna una operate halafu utaelewa wao wanadeal na aina gani ya uchumi na kwann wanaipitia marekani.

Urusi pamoja na kuanguka miaka yote tokea miaka ya 90 mbona bado yupo juu na hatikisiki kiuchumi.

Mtazame marekani, nje anaongea sana propaganda nyingi ila ndani huko changamoto alizonazo afrika ikifunga nae mipaka jamaa atakuwa katika hali mbaya sana maana anategemea kuishi kwa kusumbua wengine ndipo yeye apate.

So kwa kumalizia acheni hizi propaganda za magharibi. Kitu chochote ni kizuri ukikifanya kwa balance nzuri. Huwezi ukawa 100% mjamaa au 100% bepari. Kunahitajika balance. Jambo ambalo China ndio analifanya kwa sasa anatumia mifumo yote ya communists na ubepari.
 
Jikite kuizungumzia Africa. Huenda ujamaa ni mfumo unaoifaa Asia kwa sababu mbalimbali, huo ni mjadala mwingine. Hapa naizungumzia Africa ambayo upo wa ushaidi wa kutosha kwamba ilikuwa ni bara la biashara huria kwa muda mrefu raia wake wakistawi kwa kufanya biashara katika mfumo uliokuwa ukitegemea nguvu za soko zaidi badala ya kupangiwa na watwala nini cha kuzalisha na kuuza.
Kuna aina za ujamaa. So inabidi uwe makini sana. Mfano china ni nchi ya kijamaa na uchumi wao wanafanya kutumia mbinu za kisasa za kijamaa kusurvive. Pia mataifa ya kiarabu wahindi wengi ni wajamaa ila shida tuna elimu ndogo sana ya ujamaa na namna unatakiwa kufanya kazi.

Ujamaa una hasara kama kuna idadi kubwa ya wazembe wanategemea wachache wapate wao watumie.

Mfano Tanzania kuna idadi kubwa ya raia wanataka serikali ifanye mambo yote wao wakiwa na mchango mdogo sana wa kodi au mapato kwa serikali. Matokeo yake pesa zinakuswanywa Dar zinakwenda kuzikwa huko vijijini ujenzi wa miradi ambayo haina mapato na inaishia kuligharimu taifa mabilioni ya Pesa yanayopotea bila kurudi.


Nenda kausome tena uchumi wa china namna una operate halafu utaelewa wao wanadeal na aina gani ya uchumi na kwann wanaipitia marekani.

Urusi pamoja na kuanguka miaka yote tokea miaka ya 90 mbona bado yupo juu na hatikisiki kiuchumi.

Mtazame marekani, nje anaongea sana propaganda nyingi ila ndani huko changamoto alizonazo afrika ikifunga nae mipaka jamaa atakuwa katika hali mbaya sana maana anategemea kuishi kwa kusumbua wengine ndipo yeye apate.

So kwa kumalizia acheni hizi propaganda za magharibi. Kitu chochote ni kizuri ukikifanya kwa balance nzuri. Huwezi ukawa 100% mjamaa au 100% bepari. Kunahitajika balance. Jambo ambalo China ndio analifanya kwa sasa anatumia mifumo yote ya communists na ubepari.
 
Hata hapa Tanzania,ujamaa umeleta undezi na ulalamishi na lawama visivyo na msingi.
Kabisa kabisa. Halafu tatizo lingine la ujamaa ni watu kuwa wavivu sana kifikra, no ndependent mind. Yaani hata Yale anayotakiwa ayapambanie mwenyewe kwa survival yake yeye ataanza kuilaumu Serikali. Pia ni mfumo unaowafanya watu kuwa Manyumbu yaani waoga muda wote hata hawawezi kusimama na kutetea haki zao.

Kwenye faida ni kweli ni mfumo unaowaleta watu kuwa pamoja sana, lakini binafsi nimeuchukia sababu kwa kiasi kikubwa ni mfumo unaowafanya watu waone ni favor au hisani wanapopatiwa huduma na Serikali ambazo kimsingi ni wajibu kuzipata.

Mfano leo ijengwe barabara au hospital utaona wananchi wa sehemu husika wanavyoishukuru Serikali, ndio maana hata baadhi ya viongozi unakuta anawaambia wananchi waishukuru Serikali.

Nimeishi Australia sikuwahi ona huduma za jamii zikitolewa halafu wananchi kusema tunamshukuru sijui nani/ serikali, bali kulipokuwa na hitaji la huduma halafu likachelewa ndipo utakuta wananchi wanaishangaa mamlaka husika.

Kwetu sisi Suala la Maji na Barabara za Mpiji Magohe yaani ni Kuiomba Serikali kwa huruma sana na kubembeleza tusaidiwe(Msaada). Na Mamlaka waaaaalah haiguswi wala kushituka. UJAMAA KWAKWELI !!!!!
 
"MAKUWADI WA MABEBERU"

Wala hamuongelei jinsi UJAMAA ulivyovikwa "umbuzi wa kafara" ili uonekane haufai!!! Wala hamuongelei jinsi WAJAMAA WANAVYOKANDAMIZWA KWA VIKWAZO na mbinu nyingi chafu kuonekana si lolote si chochote....!

Na katika katika mifano yenu wala na kamwe hamtaitaja nchi ya kijamaa kama LIBYA na CUBA ambazo pamoja na kubanwa hazikupigia goti UBEPARI

Vilevile mnasahau UJAMAA sio STATIC, una aina zake, una hatua zake na mikakati yake...! CHINA ni nchi ya kijamaa ambayo imesonga mbele kwa style yake ambayo MEREKANI anaduwaa mpaka leo .... ukiuliza MAKUWADI WA MABEBERU wanakwambia China inafata UBEBARI na si ujamaa!!!!! (WAMEPIGWA NA CHINA BILA KUJUA WAKIDHANI NI MWENZAO) Huo sasa ndo ujamaa!!!

UJAMAA HAUBWABWAJI.......... RUSSIA ANAENDELEA KUTOA SOMO ZURI ... UJAMAA NI IMANI
#
Ngoja tuone hatima ya vita huko Ukraine.
 
Back
Top Bottom