Ujana haudumu, kuchora tattoo kunaweza kukugharimu sana maisha yako ukubwani

Ujana haudumu, kuchora tattoo kunaweza kukugharimu sana maisha yako ukubwani

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
2725d79e591cf1241d8fbae8ab49ab5e.jpg


EZrYzJkWsAAILu- (1).jfif.jpg


Huwa nawaonea huruma sana vijana wadogo wanaochora tattoo kuona ni ujanja ama kufuata mkumbo... kwa nchi kama ulaya na marekani tattoo sio shida hata kidogo, ila kwa hapa bongo hali ni tofauti kabisa.


kwa mitazamo ya jamii zetu, mtu akisha chora tatoo basi heshima yake inapungua pakubwa mno kwenye jamii zetu, jamii itamuweka kundi moja na wavuta bangi ambao huonekana ni wahuni, yes! ndivyo jamii zetu zilivyo, kuna vitu ukivifanya hata kama havina madhara utaonekana ni muhuni tu.

itakufanya uonekane ni mhalifu mbele ya vyombo vya usalama, upo hatarini kuwa mtuhumiwa namba moja endapo kuna uhalifu umetokea kwa sababu tu jamii imejenga dhana kwamba mtu mwente tatoo ni muhalifu. ni rahisi sana hata kusingiziwa wewe ni jambazi, muuza madawa, n.k.

inakuwa shida zaidi ukiwa ni binti, itakuharibia sana kwenye swala la kupata mume, wanaume wengi tuna dhana ya kwamba mwanamke aliechora tattoo ni malaya aliekubuhu. hata utapoenda kutambulishwa kwa familia ya mwanaume basi tegemea wakuone huna maadili na humfai mtoto wao.

kwa ulaya na marekani kuna wanajeshi, mahakimu, madaktari wana tattoo na maisha yana kwenda ila kwa hapa bongo ukiwa na tattoo hupati kazi serikalini hata kama una connection ama una vyeti vizuri. ponea yako labda utafte kazi makampuni binafsi au N.G.O za wazungu hapa bongo.

kadiri miaka inavyoenda mambo hubadilika, umechora tattoo ya mpenzi wako mkaja kuachana inakuwa vp ? umechora tattoo ya msanii flani havumi tena huko mbele itakuwaje ? ulichora tatoo ya nyota shingoni kuendana na fasheni za miaka ya 2010, leo hii unajisikiaje hii fashen imeshachuja ?

Pia jua ya kwamba kwa hapa bongo ukichora tattoo hurusiwi kuchangia damu kwasababu tattoo huwa inachorwa na sindano inayoingiza wino kwenye ngozi ila huwa inafika kwenye damu, huu wino ukishaingia kwenye damu ni hatari kiafya kuchangia damu.
 
Huwa nawaonea huruma wanaochora tats kwa kufuata mkumbo, i got mine almost 3years now and it was purposely, sitokuja kujuta coz ilinichukua zaidi ya miaka minne kutafakari juu ya uamuzi wa kuchora ama kutokuchora.
 
Hapo kwenye kuajiriwa ni serikalini tu ndiyo shida ila ofisi za private hawana tatizo.

Nimekutana na dada ana tattoo na bleach anafanya kazi USAID. Nimekutana na dada ana tattoo Soft Net, nimekutana na dada ana tattoo Jubilee Insurance, nimekutana na mdada ana bleach JICA.

Nimekutana na dada ana tattoo IOM.
 
Huwa nawaonea huruma sana vijana wadogo wanaochora tattoo kuona ni ujanja ama kufuata mkumbo... majuto huanza baada ya kuzochora.

hio tattoo itakushushia sana heshima kwenye jamii, jamii hasa kundi la watu wazima watakuona ni muhuni wa mtaa.

itakufanya uonekane ni mhalifu mbele ya vyombo vya usalama, utaonekana ni muhalifu mbele ya polisi hata kama haujafanya kosa. hata mahakamani inakuwa kazi sana kujitetea maana hakimu nae anakuona mhalifu kirahisi.

inakuwa shida zaidi ukiwa ni binti, itakuharibia sana kwenye swala la kupata mume, hata utapoenda kutambulishwa kwa familia ya mwanaume basi tegemea wakuone huna maadili na humfai mtoto wao.

kama unatafuta kazi na tattoo yako inaonekana kabisa, hapo hata uwe na division 1 ya form 4 na 6 ukiongezea degree na masters, watakukwepa na watakuchana live.

kadiri miaka inavyoenda mambo hubadilika, umechora tattoo ya mpenzi wako mkaja kuachana inakuwa vp ? umechora tattoo ya msanii flani kaja kuwa teja huko mbele itakuwaje ?

Pia jua ya kwamba ukichora tattoo hurusiwi kuchangia damu, vuta picha mtoto wako kapata majanga na kapungukiwa damu ila wewe huwezi kumchangia damu kwasababu uliamua kuchora tattoo !! huyo mtoto akifariki kwa kukosa damu suluhisho ni kuchora upya tattoo ya kumkumbuka?
Mzee baba.....hivi Kuna uhusiano gani Kati ya kuchangia damu vs mtu aliechora tatoo........coz hili Jambo nalisikia sana
 
Mzee baba.....hivi Kuna uhusiano gani Kati ya kuchangia damu vs mtu aliechora tatoo........coz hili Jambo nalisikia sana
Zile Athari za kuchora tatoo zinakua zimeshaingia kwenye damu kwaio damu yko inakua imechanganyika na hizo chemicals sasa ww utakua huna damu safi that is you are not allowed to do blood donation
 
Kuna nchi mfano kama China mchezaji haruhusiwi kuwa na tatoo kama anazo azi cover zisionekane
 
Zile Athari za kuchora tatoo zinakua zimeshaingia kwenye damu kwaio damu yko inakua imechanganyika na hizo chemicals sasa ww utakua huna damu safi that is you are not allowed to do blood donation
Sio kweli mimi nina tattoo kadhaa mwilini kwa zaidi ya miaka kumi na ni mchangiaji wa damu kila baada ya miezi minne hadi bank ya damu wamenipa tuzo, huwa wanakataza kwa mtu aliyechora tattoo ndani ya miezi mitatu kwa kuhofia magonjwa yanayoambukizwa kwa damu
 
Watu wachore kwa wingi na wachore sanaaa but one day watakuwa wanatafuta nama ya kuzifuta
 
Back
Top Bottom