Ujana haudumu, kuchora tattoo kunaweza kukugharimu sana maisha yako ukubwani

Ujana haudumu, kuchora tattoo kunaweza kukugharimu sana maisha yako ukubwani

Namfahamu kijana, babu na babake wote walikuwa jeda waheshima!
Yeye bright akapelekwa China kusoma, karudi na degree Kali!
Finance & Chinese. Anajua lugha 4, Kiswahili, English, French na Chinese.

Kumuingiza jeshi CV ikagoma, kisa tattoo!
Wakajaribu aende sijui wanyama Pori, nako kukabuma! Kisa tattoo!
Sikuwahi kuwaza kibongobongo, mtu aweza kosa kazi!

He is frustrated, anakunywa mipombe na mabangi, anashinda na bodaboda Tu vijiweni!
Wamemfanyia counseling, haamini hawezi kuitwa GENERAL!

He is lost, kwa sababu aliamini yeye kazi ni moja tu, jeshi!
Kazi za ukalimani wapo masela wengi mitaani wanajua lugha.
 
labda kwa tanzania na africa.ila kwa wenzetu hakuna hayo kuna wanajeshi,mahakimu,wacheza mpira,wasanii,madaktari wanatattoo na maisha yana kwenda
 
Huwa nawaonea huruma sana vijana wadogo wanaochora tattoo kuona ni ujanja ama kufuata mkumbo... majuto huanza baada ya kuzochora.

hio tattoo itakushushia sana heshima kwenye jamii, jamii hasa kundi la watu wazima watakuona ni muhuni wa mtaa.

itakufanya uonekane ni mhalifu mbele ya vyombo vya usalama, utaonekana ni muhalifu mbele ya polisi hata kama haujafanya kosa. hata mahakamani inakuwa kazi sana kujitetea maana hakimu nae anakuona mhalifu kirahisi.

inakuwa shida zaidi ukiwa ni binti, itakuharibia sana kwenye swala la kupata mume, hata utapoenda kutambulishwa kwa familia ya mwanaume basi tegemea wakuone huna maadili na humfai mtoto wao.

kama unatafuta kazi serikalini na umechora tattoo, hapo watakupiga panga wazi wazi na watakupa makavu .... labda uende kampuni binafsi ama ngo za wazungu

kadiri miaka inavyoenda mambo hubadilika, umechora tattoo ya mpenzi wako mkaja kuachana inakuwa vp ? umechora tattoo ya msanii flani kaja kuwa teja huko mbele itakuwaje ?

Pia jua ya kwamba ukichora tattoo hurusiwi kuchangia damu, vuta picha mtoto wako kapata majanga na kapungukiwa damu ila wewe huwezi kumchangia damu kwasababu uliamua kuchora tattoo !! kwa wenzetu marekani wanaruhusu kuchangia naada ya miezi kadhaa kwa vibali maalum na baada ya uchunguzi wa kina, kibongo bongo ni shida
Usipangiane maisha watu..hivyo vizazi vya kuona tatoo uhuni vimeanza kutoweka..soon wazazi nao watakua na tatoo.

Halafu mbona wamakonde, wanyaturu n.k walikua wanajichora zamani..hao mbona huwaongelei.

#MaendeleoHayanaChama
 
Hapo kwenye kuajiriwa ni serikalini tu ndiyo shida ila ofisi za private hawana tatizo.

Nimekutana na dada ana tattoo na bleach anafanya kazi USAID. Nimekutana na dada ana tattoo Soft Net, nimekutana na dada ana tattoo Jubilee Insurance, nimekutana na mdada ana bleach JICA.

Nimekutana na dada ana tattoo IOM.
Bado ni changamoto sana hakika, kama mtu hakuna ulazima sana achana na tatoo ni mbaya sana haswa baadaye kama alivyo eleza mtoa mada
 
Ebu toa madhara ya Tatoo na usitageti katika .... Kuajiriwa tu.
Achana na kuajiriwa athari kubwa ni mitazamo ya jamii zetu....mtu akisha chora tatoo basi kwa kaisi fulani heshima yake inapungua pakubwa mno kwenye jamii zetu, hata kuaminika hawezi kuaminika sana
 
Miaka ijayo itakuwa kitu cha kawaida na hii Taboo itaondoka tu.
Itachukua muda mrefu sana labda huko mijini lakini huku kwetu vijijini itachukua muda mrefu sana, pia unapaswa ukumbuke uwepo wa tatoo umeanza miaka mingi sana imepita lakini hadi sasa bado ni changamoto
 
Muwe mnaweka na picha mazejooo hili kuchangamsha uzi
 

Attachments

  • FB_IMG_1650807588706.jpg
    FB_IMG_1650807588706.jpg
    43.4 KB · Views: 28
Usipangiane maisha watu..hivyo vizazi vya kuona tatoo uhuni vimeanza kutoweka..soon wazazi nao watakua na tatoo.

Halafu mbona wamakonde, wanyaturu n.k walikua wanajichora zamani..hao mbona huwaongelei.

#MaendeleoHayanaChama
Ndonya za wamakonde ndiyo kwa upande mwingine ni kweli ndizo tatoo zenyewe lakini hiki ni kitu tofauti sana na hizi za kisasa haswa katika mitazamo na fikra za watu...hebu jaribu kufikiria wanaume wa Kimasai wanasuka nywele na jamii haina shida na hilo...lakini hebu niambie mwanaume wa Kichaga/Kihaya akisuka jamii itamtazamaje?
 
Sio kweli mimi nina tattoo kadhaa mwilini kwa zaidi ya miaka kumi na ni mchangiaji wa damu kila baada ya miezi minne hadi bank ya damu wamenipa tuzo, huwa wanakataza kwa mtu aliyechora tattoo ndani ya miezi mitatu kwa kuhofia magonjwa yanayoambukizwa kwa damu
Sawa mkuu
 
Acha kutisha watu..kwa illusion zako.

#MaendeleoHayanaChama
Haman mtu anamtiaha mtu mzima. Tunaandika kutokana na uhalisia kama unadhan natisha na iwe hivyo. Binadamu tunapenda kusikia tunachokiamini
 
Ndonya za wamakonde ndiyo kwa upande mwingine ni kweli ndizo tatoo zenyewe lakini hiki ni kitu tofauti sana na hizi za kisasa haswa katika mitazamo na fikra za watu...hebu jaribu kufikiria wanaume wa Kimasai wanasuka nywele na jamii haina shida na hilo...lakini hebu niambie mwanaume wa Kichaga/Kihaya akisuka jamii itamtazamaje?
Familia lazima ilie na kujua kijana wao tayarii kashaisha
 
Back
Top Bottom