Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 6,067
- 10,938
Habari wakuu,
Hii barabara kuanzia Segerea-Bonyokwa mpaka Kimara kwa sisi wakazi wa maeneo hayo ilikuwa kero kubwa sana sababu kutokana na ubovu wake hasa kipindi cha mvua. Hii barabara imekuwa ikilalamikiwa miaka na miaka lakini serikali ilikuwa imeziba masikio lakini sasa kilio kimewafikia. Hii barabara ni muhimu sana kutokana na kwamba inaunganisha Tabata Segerea na Kimara.
Juzi nimepita Bonyokwa nikakuta mkandarasi yupo site pale mwisho wa lami, nilifarijika sana. Eneo lile kuanzia kibao cha Shule ya Msingi Macedonia mpaka stendi ya Bonyokwa ilikuwa korofi sana kutokana na kukosa mifereji hivyo maji yalikuwa yakijitafutia njia. Nakumbuka kijana wangu aliachwa pale na school bus kisa ubovu wa barabara akaambiwa atembee kwenda nyumbani umbali kama kilometa 2.
Ujenzi huo utachochea sana maendeleo ya eneo lile na hatimaye tutaachwa kuchekwa watu wa Bonyokwa.
Pia soma
Hii barabara kuanzia Segerea-Bonyokwa mpaka Kimara kwa sisi wakazi wa maeneo hayo ilikuwa kero kubwa sana sababu kutokana na ubovu wake hasa kipindi cha mvua. Hii barabara imekuwa ikilalamikiwa miaka na miaka lakini serikali ilikuwa imeziba masikio lakini sasa kilio kimewafikia. Hii barabara ni muhimu sana kutokana na kwamba inaunganisha Tabata Segerea na Kimara.
Juzi nimepita Bonyokwa nikakuta mkandarasi yupo site pale mwisho wa lami, nilifarijika sana. Eneo lile kuanzia kibao cha Shule ya Msingi Macedonia mpaka stendi ya Bonyokwa ilikuwa korofi sana kutokana na kukosa mifereji hivyo maji yalikuwa yakijitafutia njia. Nakumbuka kijana wangu aliachwa pale na school bus kisa ubovu wa barabara akaambiwa atembee kwenda nyumbani umbali kama kilometa 2.
Ujenzi huo utachochea sana maendeleo ya eneo lile na hatimaye tutaachwa kuchekwa watu wa Bonyokwa.
Pia soma
- DOKEZO - Ni mkandarasi gani anajenga barabara ya Kimara - Bonyokwa - Segerea?
- TANROADS mna mpango gani juu ya barabara ya kimkakati inayotoka Kimara Mwisho kuelekea Tabata (Bonyokwa-Segerea-Kinyerezi)?
- Kero kifusi barabara ya Bunyokwa