Ujenzi: Je, hii nyumba ya TAKUKURU Dodoma inafikia thamani tajwa ya Tsh. 143 milioni?

Inategemea yafuatayo kama yapo :-
-msingi wake umesanifiwa kwa namna gani?
-partitions zake zikoje, Je kuna kumbi ndani?
-finishing /umaliziaji wake ukoje na umetumia malighafi zipi?
-Je ni kweli muonekano wake ndivyo ilivyo au kuna cha ziada /undeground/basement?
-bati,dali,kenchi ni za ubora upi?
-mfumo upi wa majitaka?
-Je gharama hizo ni pamoja na umeme, Maji, ICT,ditector za moto, CCTV camera na nk
Ikumbukwe kuwa kujua gharama sio kuangalia picha, details nyingi zinahitajika.
 
Naona watu wanaosema kupaua mil 10 finishing mil 15 hawajui maana yake. Labda wanazungumzia za uswahilini
 
Wewe hiyo finishing ya mil 10 ni finishing ya aina gani? Mbona mnaunderestimate sana? Ni finishing ya nyumba ya tandale kwa mfuga mbwa au?
Finishing ya nje, namaanisha vitu kama paving,na walkways e.t.c,acha kukurupuka,soma vizuri hapo utaelewa.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
ficha upumbavu wako
 
Umezingatia matumizi ya force account?
 
yaliyomo yamo katka receipt au ndioyale yale-ukiongeza na ile mbili ya jana zinakuwa 8[emoji3][emoji23][emoji23]

maana mnaanzaga hivi,wazee wa viwango wakija tunakuta madudu.kuweni watulivu kwanza.

hapa nilipo mimi taasisi nyeti ya serikali nyumba zimekataliwa kupokelewa kisa,hesabu za kila nyumba ghorofa moja moja ni mill 800,watu wanajalibu kuangalia millioni 800 imeishaje kwenye vijumba kama vidungu ngorofa moja moja.
 
😀 😀 😀 😀 😀 Tumechoka malalamiko si wana mikono na macho kila pahala
 


Acha uongo
Siku zte B.O.Q za ki-tz nizauchakajuaji, ukitaka jua hilo fatilia mkandarasi wa hyi nyumba alikuwa nani.
Kuna hosptali nyingi nchini tumejenga kwa 70ml.
Niliwahi chukua tender ya kufanya finishing ya majengo ya sekondary madarasa4 na nyumba 3 za walimu two in one tyepe kwa 16ml. Nanilipata nafaida.
 
Hii nyumba Ni kubwa mno,
Tena inatakiwa kua mil 150+ Kama ukiamua kuitendea haki upande wa material

HEBU TUPIGE HESABU SASA[emoji116]

1. MSINGI
(Kusafisha kiwanja, Kuchimba msingi,KIFUSI, tofali,cement, mchanga, maji,kumwaga jamvi,ufundi,mengineyo)
Almost 10mil imekata.

2. Kuinua kuta
(Tofali, mchanga, maji, ufundi,mengineyo)
Almost 15 mil imekata

3. Kumwaga beam nondo 4 nyumba nzima
(Nondo,kokoto,mbao, misumari, maji,mchanga,cement,ufundi, mengineyo)
Almost 10 mil imekata

4. Kupinga kenchi(KUPAUA)
(Mbao,misumari,binding wire, ufundi,fisha bodi ,mengineyo)
Almost 5mil imekata

5. Kupiga bati (kuezeka)
(Bati geji 28 au 26, misumari, gundi, ufundi, mengineyo)
Almost 15mil imekata

BOMA LIMEISHA, ALMOST 45Mil IMESHAKATA

Finishing[emoji116]

6. Hizo dirisha (alminium+ Gril+rangi+mengineyo) zilizotandazwa apo usichukulie poa.
Kwa haraka haraka Ziko sio chini ya 15 apo@500,000.
Mpaka zinavoonekana apo Almost 8mil imekata

7.Bado milango (frem+Top+vitasa+rangi+ufundi, mengineyo)
Kwa haraka haraka haipungui milango 10 ilo jengo. Each 400,000.
Mpaka inavoonekana apo Almost 5mil imekata

8.Hizo tiles bila shaka Ni first grade (TAASISI),
zimetandazwa sakafuni mpaka ukutani.
Mpaka zinavoonekana (tiles,grout,strips,skating,ufundi,mengineyo) apo Almost 15mil imekata

9.Hujaja gharama ya lipu, (mchanga, cement, ufundi,maji,mengineyo)
almost 10 mil nje ndani imekata

10.skimming ya nyumba nzima nje ndani kwa white cement(Rangi, white cement,ufundi, mengineyo)
Almost 7mil imekata

11. Kupiga BANDARINGI kwa ajili ya gypsum bodi.
(Mbao,misumari,ufundi,mengineyo)
Almost 7mil imekata

12. Kupiga GYPSUM BOARD
(Gypsum bodi,skruu, faiba tepu,ufundi,mengineyo)
Almost 7 mil imekata

13. Kupiga RANGI NYUMBA NZIMA nje ndani
(Rangi,ufundi,mengineyo)
Almost 5 mil imekata

14. MFUMO WA UMEME (wayaringi)
Hapo lazima nyaya SINGLE CORE first grade zimetembea za kutosha, TRONIC switch,socket,m/switch,breaker,cutout, earthrod,conduit,boxes, process za KUOMBA MITA TANESCO,ufundi n.k.
Apo almost 10mil imekata

15. MFUMO WA MAJI
Nazungumzia vyooni,jikoni,bafuni na kwingineko.
(MaSink, tanki, mabomba, ufundi, mengineyo)
Almost 5mil lazima ikate.

16. SHIMO LA CHOO
(Kuchimba,tofali,cement,mchanga,nondo,kokoto, ufundi,waya meshi, mengineyo)
Almost 2mil imekata

FINISHING tu MPAKA HAPO, jumla 81mil IMESHAKATA.

Sasa ukijumlisha
Kujenga boma 45mil + finishing 81mil= jumla 126mil.

Unaweza kuongezea na 10 mil ya kupiga FINAL TOUCHES ili kunogesha zaidi nyumba.

Kama urembo kwenye nguzo, vibaraza mbalimbali, bustani, taa za urembo, mfumo wa CCTV camera, bango, n.k

ALMOST 136MILLION inakamilisha Ilo jengo.


My take:
SIDHANI KAMA Kuna upigaji hapa.
Na Kama upo Basi ni kwa kiwango kidogo Sana.

Tena inaweza kua kwa kwa vitu vidogo vidogoKama kulipana posho, overtime,chakula Cha saiti,usafiri n.k.

Vinaweza kukava icho kiwango kinachopelea (yaani 7million) kufikia icho kiwango halisi walichotaja Cha 143million.

Shukran [emoji120]
 
Watanzania tuache kukurupuka. M 143 sio nyingi kabisa . japo nyumba zetu tunajenga kimaskini tunahamia hata kwa kuweka mashuka ila ukichukua diary upige hesabu unakuta M 70 imeisha hata aluminium dirisha hujaweka. Mm binafsi naushuhuda zilinunuliwa tiles za M 17 zikawekwa kwenye ghetto la kawaida tu.
 
Kama kuna finishing touches nzuri huko ndani, na structure ilijengwa kwa viwango stahiki, no way hiyo nyumba ni less than 100m.. mnaosema milioni sijui 60, 70 mnaongelea very low qualoty houses...
Huwajui lumumba ww, hapo wanaongelea ushabiki tu..hiyo nyumba hata Kama wamepiga cha juu bc ni kdg sana ...si chini ya M 120
 
Asante umemaliza kila kitu
 
Hebu Nisaidie huo mchanganuo wa kumwaga linta la million 5 kwenye hiyo nyumba?

Nondo kiasi gani?
Zinafungwa ngapi ngapi?
Cement kiasi gani na kwa resho gani?
Kokoto kiasi gani na za Aina gani?
Mchanga tripu ngapi?
Fundi utamlipa kiasi gani?
Mbao utakodi/utanunua kwa kiasi gani?
 
Mi naomba kuuliza kwanini majengo yote ya serikali yasiwe yanafanana? Kama ni ofisi ya TAKUKURU yafanane nchi nzima. Kama ni la hamlashauri hivyi hivyo. Kwa nini kila wilaya/mji majengi ya ofisi ya taasisi moja hayafanani?
Kwa sababu ofisi sio kambi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…