Ujenzi: Je, hii nyumba ya TAKUKURU Dodoma inafikia thamani tajwa ya Tsh. 143 milioni?

Ujenzi: Je, hii nyumba ya TAKUKURU Dodoma inafikia thamani tajwa ya Tsh. 143 milioni?

kwa dodoma hiyo si nyumba ya thamani hiyo??, wana dodoma wanajua. Ujinga wa dar wanataka kuuleta dodoma haiwezekani. Rais anatambua ujinga huu, hiyo nyumba kwa dodoma inajengwa kwa thamani ya chini ya milioni 50 yaani hapo hata uuziwe material kwa bei ya juu sana...utaishia kujenga kwa gharama ya chini ya milioni 50.

Utakuta mkurugenzi alipokea milioni 10 kutoka kwa mkandarasi, ndio maana mkandarasi ka balance mambo imetoka hivyo. Mlolongo wa wapigaji upo kwenye wateule wake hadi kwa mkandarasi
Ninyi hata rais anye barabarani mtaona ni sawa tu... lumumba tumeshawazoea
 
Karibuni waumini wa majadiliano katika mjadala huu ambao mh Rais amesema angeweza kujenga nyumba hii kwa mill 43.

Kwa mtazamo wangu, licha ya kutoiona nyumba hii kwa ndani huwezi jenga chini ya million 90 na kama gharama za vifaa, mchanga na cement eneo husika zipo juu kufika mill 100 sioni ajabu kwa upande wangu.

Karibuni mafundi kwa majadiliano. View attachment 1514090
Million 70 safi kila kitu, tuache unafiki
 
kama ina underground bunker inaweza kuzidi hiyo M143..

lakini kama ndio hiyo niionayo...jenerali amekulwa cha juu

simple like that.
Ofisi nyeti Kama hii haiwezi kukosa Underground bunker au STRONG vault.

Hizi gharama naona Ni halisi.
 
Hii nyumba Ni kubwa mno,
Tena inatakiwa kua mil 150+ Kama ukiamua kuitendea haki upande wa material

HEBU TUPIGE HESABU SASA[emoji116]

1. MSINGI
(Kusafisha kiwanja, Kuchimba msingi,KIFUSI, tofali,cement, mchanga, maji,ufundi,mengineyo)
Almost 10mil imekata.

2. Kuinua kuta
(Tofali, mchanga, maji, ufundi,mengineyo)
Almost 15 mil imekata

3. Kumwaga beam nondo 4 nyumba nzima
(Nondo,kokoto,mbao, misumari, maji,mchanga,cement,ufundi, mengineyo)
Almost 10 mil imekata

4. Kupinga kenchi(KUPAUA)
(Mbao,misumari,binding wire, ufundi,fisha bodi ,mengineyo)
Almost 5mil imekata

5. Kupiga bati (kuezeka)
(Bati geji 28 au 26, misumari, gundi, ufundi, mengineyo)
Almost 15mil imekata

BOMA LIMEISHA, ALMOST 45Mil IMESHAKATA

Finishing[emoji116]

6. Hizo dirisha (alminium+ Gril+rangi+mengineyo) zilizotandazwa apo usichukulie poa.
Kwa haraka haraka Ziko sio chini ya 15 apo@500,000.
Mpaka zinavoonekana apo Almost 8mil imekata

7.Bado milango (frem+Top+vitasa+rangi+ufundi, mengineyo)
Kwa haraka haraka haipungui milango 10 ilo jengo. Each 400,000.
Mpaka inavoonekana apo Almost 5mil imekata

8.Hizo tiles bila shaka Ni first grade (TAASISI),
zimetandazwa sakafuni mpaka ukutani.
Mpaka zinavoonekana (tiles,grout,strips,skating,ufundi,mengineyo) apo Almost 15mil imekata

9.Hujaja gharama ya lipu, (mchanga, cement, ufundi,maji,mengineyo)
almost 10 mil nje ndani imekata

10.skimming ya nyumba nzima nje ndani kwa white cement(Rangi, white cement,ufundi, mengineyo)
Almost 7mil imekata

11. Kupiga BANDARINGI kwa ajili ya gypsum bodi.
(Mbao,misumari,ufundi,mengineyo)
Almost 7mil imekata

12. Kupiga GYPSUM BOARD
(Gypsum bodi,skruu, faiba tepu,ufundi,mengineyo)
Almost 7 mil imekata

13. Kupiga RANGI NYUMBA NZIMA nje ndani
(Rangi,ufundi,mengineyo)
Almost 5 mil imekata

14. MFUMO WA UMEME (wayaringi)
Hapo lazima nyaya SINGLE CORE first grade zimetembea za kutosha, TRONIC switch,socket,m/switch,breaker,cutout, earthrod,conduit,boxes, process za KUOMBA MITA TANESCO,ufundi n.k.
Apo almost 10mil imekata

15. MFUMO WA MAJI
Nazungumzia vyooni,jikoni,bafuni na kwingineko.
(MaSink, tanki, mabomba, ufundi, mengineyo)
Almost 5mil lazima ikate.

16. SHIMO LA CHOO
(Kuchimba,tofali,cement,mchanga,nondo,kokoto, ufundi,waya meshi, mengineyo)
Almost 2mil imekata

FINISHING tu MPAKA HAPO, jumla 81mil IMESHAKATA.

Sasa ukijumlisha
Kujenga boma 45mil + finishing 81mil= jumla 126mil.

Unaweza kuongezea na 10 mil ya kupiga FINAL TOUCHES ili kunogesha zaidi nyumba.

Kama urembo kwenye nguzo, vibaraza mbalimbali, bustani, taa za urembo, mfumo wa CCTV camera, bango, n.k

ALMOST 136MILLION inakamilisha Ilo jengo.


My take:
SIDHANI KAMA Kuna upigaji hapa.
Na Kama upo Basi ni kwa kiwango kidogo Sana.

Tena inaweza kua kwa kwa vitu vidogo vidogoKama kulipana posho, overtime,chakula Cha saiti,usafiri n.k.

Vinaweza kukava icho kiwango kinachopelea (yaani 7million) kufikia icho kiwango halisi walichotaja Cha 143million.

Shukran [emoji120]
Tatizo wengi wetu hatuna utaratibu wa ku record gharama za ujenzi kwa kuogopa tutaumia zaidi.
 
Hiyo nyumba tuseme kupaua ni milioni 10
Msingi na jamvi milion 10.
Kupandisha tofali juu milion 10
Finishing milion 15
Ziada milini 10.

Jumla milioni 55!

Magu yupo sahihi hapo pana upigaji!

Kwa hiyo hela milioni 143 ilitakiwa zitoke nyumba kama hizo 3
Finishing million 15 tu?? Bro hauko serious
 
Hiyo nyumba huwezi kupaua kwa 10 million mkuu labda utumie makuti.
Kuna watu humu hawajawahi kujenga, au huwa wanajenga mtandaoni.

Hii nyumba imekula bati nyingi mno. Asilete masihara kabisa
 
Milioni 143, zinatoka nyumba kama hizo tatu [emoji38][emoji38][emoji38][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji2445][emoji2445][emoji2445][emoji377][emoji377][emoji377]
 
Million 40 ujenge labda utumie tofali za kuchoma na ndipo ujenge Nyumba yenye ukubwa huu.
Ujenzi uko juu waungwana

kuna jamaa hapo kaongelea gharama ki serikali ndio kidogo amenishawishi kuamini,lakini ki raia ningekuonesha picha ya nyumba kama hiyo na ina ukuta,na nyumba za nje bila kusahau maduka kama matatu na haijafikia gharama hizo
 
Hii nyumba Ni kubwa mno,
Tena inatakiwa kua mil 150+ Kama ukiamua kuitendea haki upande wa material

HEBU TUPIGE HESABU SASA[emoji116]

1. MSINGI
(Kusafisha kiwanja, Kuchimba msingi,KIFUSI, tofali,cement, mchanga, maji,ufundi,mengineyo)
Almost 10mil imekata.

2. Kuinua kuta
(Tofali, mchanga, maji, ufundi,mengineyo)
Almost 15 mil imekata

3. Kumwaga beam nondo 4 nyumba nzima
(Nondo,kokoto,mbao, misumari, maji,mchanga,cement,ufundi, mengineyo)
Almost 10 mil imekata

4. Kupinga kenchi(KUPAUA)
(Mbao,misumari,binding wire, ufundi,fisha bodi ,mengineyo)
Almost 5mil imekata

5. Kupiga bati (kuezeka)
(Bati geji 28 au 26, misumari, gundi, ufundi, mengineyo)
Almost 15mil imekata

BOMA LIMEISHA, ALMOST 45Mil IMESHAKATA

Finishing[emoji116]

6. Hizo dirisha (alminium+ Gril+rangi+mengineyo) zilizotandazwa apo usichukulie poa.
Kwa haraka haraka Ziko sio chini ya 15 apo@500,000.
Mpaka zinavoonekana apo Almost 8mil imekata

7.Bado milango (frem+Top+vitasa+rangi+ufundi, mengineyo)
Kwa haraka haraka haipungui milango 10 ilo jengo. Each 400,000.
Mpaka inavoonekana apo Almost 5mil imekata

8.Hizo tiles bila shaka Ni first grade (TAASISI),
zimetandazwa sakafuni mpaka ukutani.
Mpaka zinavoonekana (tiles,grout,strips,skating,ufundi,mengineyo) apo Almost 15mil imekata

9.Hujaja gharama ya lipu, (mchanga, cement, ufundi,maji,mengineyo)
almost 10 mil nje ndani imekata

10.skimming ya nyumba nzima nje ndani kwa white cement(Rangi, white cement,ufundi, mengineyo)
Almost 7mil imekata

11. Kupiga BANDARINGI kwa ajili ya gypsum bodi.
(Mbao,misumari,ufundi,mengineyo)
Almost 7mil imekata

12. Kupiga GYPSUM BOARD
(Gypsum bodi,skruu, faiba tepu,ufundi,mengineyo)
Almost 7 mil imekata

13. Kupiga RANGI NYUMBA NZIMA nje ndani
(Rangi,ufundi,mengineyo)
Almost 5 mil imekata

14. MFUMO WA UMEME (wayaringi)
Hapo lazima nyaya SINGLE CORE first grade zimetembea za kutosha, TRONIC switch,socket,m/switch,breaker,cutout, earthrod,conduit,boxes, process za KUOMBA MITA TANESCO,ufundi n.k.
Apo almost 10mil imekata

15. MFUMO WA MAJI
Nazungumzia vyooni,jikoni,bafuni na kwingineko.
(MaSink, tanki, mabomba, ufundi, mengineyo)
Almost 5mil lazima ikate.

16. SHIMO LA CHOO
(Kuchimba,tofali,cement,mchanga,nondo,kokoto, ufundi,waya meshi, mengineyo)
Almost 2mil imekata

FINISHING tu MPAKA HAPO, jumla 81mil IMESHAKATA.

Sasa ukijumlisha
Kujenga boma 45mil + finishing 81mil= jumla 126mil.

Unaweza kuongezea na 10 mil ya kupiga FINAL TOUCHES ili kunogesha zaidi nyumba.

Kama urembo kwenye nguzo, vibaraza mbalimbali, bustani, taa za urembo, mfumo wa CCTV camera, bango, n.k

ALMOST 136MILLION inakamilisha Ilo jengo.


My take:
SIDHANI KAMA Kuna upigaji hapa.
Na Kama upo Basi ni kwa kiwango kidogo Sana.

Tena inaweza kua kwa kwa vitu vidogo vidogoKama kulipana posho, overtime,chakula Cha saiti,usafiri n.k.

Vinaweza kukava icho kiwango kinachopelea (yaani 7million) kufikia icho kiwango halisi walichotaja Cha 143million.

Shukran [emoji120]
Vyumba vingapi kwani
 
Karibuni waumini wa majadiliano katika mjadala huu ambao mh Rais amesema angeweza kujenga nyumba hii kwa mill 43.

Kwa mtazamo wangu, licha ya kutoiona nyumba hii kwa ndani huwezi jenga chini ya million 90 na kama gharama za vifaa, mchanga na cement eneo husika zipo juu kufika mill 100 sioni ajabu kwa upande wangu.

Karibuni mafundi kwa majadiliano. View attachment 1514090
Kwani kamjengo kana vyumba vingapi? Tuanze hapo[emoji38][emoji38], million 143 iwe na reason basi
 
Tatizo wengi wetu hatuna utaratibu wa ku record gharama za ujenzi kwa kuogopa tutaumia zaidi.
Ni kweli mkuu,
Wengi wanalichukulia jengo Kama Ni kupanga tofali na kufunika na cement.

Ila Kuna vitu vidogo vidogo vinapukuta Ela Sana.

Hasa hasa wakati wa FINISHING.
 
Kwa standard ya majengo ya serikali hata wakisema wamejengea 200M wala sishangai.

Kwangu binafsi hata 30M najenga kama hiyo.

*Ramani yakugongea.
*Hakuna jamvi.
*Tofali za kuchoma.
*Concrete beam "Lenta" nondo moja inalala
*Mbao siyo treated (zinapakwa oil chafu) tena mix na mirunda.
*Bati brand za kichina tena 30g
*Mafundi wote wa mitaani tu.
*Nasimamia mwenyewe A to Z.
*Napiga Ceiling boards.
*Tiles mchina (Goodone)
*Milango siyo mbao ngumu.
 
Gharama iliyotumika ni sahihi kabisa ,sababu kuna vitu vya ndani kama vile mtandao wa simu,internet na CCTV camera hapo sio chinii ya milion 40,Bado kuna viyoyozi na umeme.watu wanaongea tu ,mfano sisi tunaojenga kijengo kidogo tu cha tawi la benki ina kugharimu zaidi ya ml 350 hadi 400 ila watu wasiojua masuala ya ujenzi watajua kwamba pesa imepigwa hapo,mzee wetu tunajua kipindi hiki cha kampeni anataka kukosoa tu ila ukweli anaujua
 
Back
Top Bottom