Ujenzi Mkubwa unaoendelea Kigamboni(Dege Eco Village), ni mradi wa nani?

Ujenzi Mkubwa unaoendelea Kigamboni(Dege Eco Village), ni mradi wa nani?

Binafsi nimeshatembelea miradi yote miwili yaani DEGE na AVIC.
AVIC unaeleweka zaidi na nyumba zao zimekaa vizuri ni bungalows na villas, DEGE naona kama wanajenga hostels. Anyway, take your time utembelee ufanye uamuzi mwenyewe.
zitakuwa ni sehemu za kuishi watz au kutakutakuwa wageni wawekezaji...........nakumbuka mradi huu ulianza enz za jk..sijawahi kupata maelezo ya kina kuhusu hii miradi
 
Wana jamvi,

Kuna mradi mkubwa wa ujenzi wa magorofa unaendelea Kigamboni. Ni Kigamboni ndandani mbele Zoo na naambiwa unaitwa "Dege Eco Village".

View attachment 419269

Wengi wa wafanyakazi ni wazungu wenye asili ya Kituruki. Kazi inafanyika usiku na mchana.

Wenye ukweli kuhusu mradi huo mtujuze.

Karibuni wanajamvi.

=====
BAADHI YA MAJIBU:
MBUNGE:


====
MDAU:



CAG ashitukia ulaji mil.775/- kila eka NSSF
www.ippmedia.com/sw/habari/cag-ashitukia-ulaji-mil775-kila-eka-nssf

Kufuatia taarifa hiyo, wabunge kupitia Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) walikuja juu na kuubana uongozi wa NSSF, wakitaka maelezo ya kina kuhusiana na suala hilo walilodai lina harufu ya ufisadi.

Wakati ikipitia taarifa ya CAG, kamati hiyo, chini ya Mwenyekiti wake, Naghenjwa Kaboyoka, ilibaini kuwa katika mradi wa NSSF kuendeleza mji wa kisasa wa Kigamboni jijini Dar es Salaam ambao shirika hilo limeingia ubia na taasisi nyingine, thamani ya kiwanja kimoja iliyowekwa ni Sh. milioni 800 wakati thamani halisi ni Sh. milioni 25, hivyo kuwapo na malipo ya ziada ya Sh. milioni 775 kwa kila kiwanja.

PAC ilifichua ulaji huo wakati ikiibana NSSF kwa kutaka ufafanuzi kuhusu hoja mbalimbali za ukaguzi zilizoainishwa na CAG katika mwaka wa fedha 2014/15.

Mwenyekiti wa PAC, Kaboyoka, alisema kuwa watalieleza Bunge kuhusu harufu ya ufisadi katika mradi huo wa NSSF katika kuendeleza mji wa Kigamboni.

Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige (CCM), alidai mradi huo umegubikwa na 'uchafu' kutokana na kile kilichofanyika .

Mbunge wa Magomeni, Jamal Kassim Ali (CCM), alisema kuna taarifa kwamba mbia, ambaye ni kampuni ya Azimio Housing Estates, kuwa anataka kukopa tena wakati kuna fedha za uwekezaji hazijaingizwa kwenye mradi.

Ali alidai pia kuwa, kuna mgongano wa maslahi kutokana na kampuni hiyo kuonekana ikipewa kazi nyingi na NSSF.

Makamu Mwenyekiti wa PAC, Aeshi Hilaly, alisema taarifa zao zinaonyesha mbia huyo yupo tayari kuingiza fedha kwenye uwekezaji huo lakini anataka akope, hivyo kuna uwezekano wa NSSF kupoteza Sh. bilioni 270 ambazo zimeingizwa kwenye uwekezaji huo kama isipokuwa makini kuangalia namna ya kuzirudisha.

Katika ripoti ya CAG ya 2014/15, inaelezwa kuwa NSSF iliingia ubia na kampuni hiyo na kuanzisha kampuni maalumu kwa jina la Hifadhi Builders Limited.

Ilielezwa kuwa katika mkataba huo wa mradi wa Kigamboni, Azimio Housing Estates inatakiwa kuendeleza ekari 20,000 za ardhi zilizopo Kigamboni lakini baada ya tathmini, PAC imebaini zipo ekari 3,503 tu.

Katika ubia huo, NSSF inamiliki asilimia 45 ya hisa wakati Azimio Housing Estates inamiliki asilimia 55 ya hisa na jumla ya gharama za mradi ni dola za Marekani milioni 653.44.

Aidha, inaelezwa kuwa utaratibu wa uchangiaji mtaji ni NSSF kutoa fedha kwa asilimia 45 ya gharama za mradi na Azimio kutoa fedha zenye thamani ya asilimia 35 ya gharama za mradi pamoja na ardhi ambayo itathaminishwa kuwa asilimia 20 ya gharama za mradi.

Hata hivyo, wajumbe wa PAC walishangazwa na uthamini uliofanywa kwenye ardhi wakieleza kuwa gharama imeonekana ni kubwa kuliko gharama halisi.

Ripoti ya CAG inaeleza kuwa katika makubaliano ya usitishwaji, kiasi cha Sh. bilioni 43.9 ilicholipwa Azimio na shirika ni sehemu ya ada ya ushauri ambayo inabadilishwa kuwa mkopo utakaorejeshwa na kampuni kupitia sehemu ya mauzo ya nyumba katika mradi wa Dege ndani ya miaka mitatu, kwa riba ya asilimia tatu kwa mwaka.

Akijibu hoja za wabunge, Mkurugenzi wa NSSF, Prof. Godius Kahyarara, alisema utekelezaji wa mradi wa Dege ulisimama tangu Februari mwaka huu kutokana na mwekezaji kutokuwa na fedha huku NSSF tayari ikiwa imeshaingiza Sh. bilioni 270.

Hata hivyo, alisema kuna ukaguzi maalumu unafanyika kwenye miradi yote ya NSSF ukiwamo huo wa Kigamboni.

“Tukitoka kwenye ubia huu, tunaweza kupoteza fedha hizo… tupo makini kuhakikisha mwekezaji huyo (Azimio) anarejesha fedha hizo,” alisema Mkurugenzi huyo.

Prof. Kahyarara alikiri Azimio kupeleka barua kwa NSSF ikitaka kukopa na ilikataliwa kupewa mkopo huo kwa sababu inadaiwa na haiwezi kukopeshwa tena.

Alisema sehemu kubwa ya ardhi imenunuliwa na NSSF kwa bei kubwa tofauti na uhalisia na kuna uchunguzi unafanywa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato (TRA) huku akisema hatua mbalimbali zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kuwasimamisha kazi wale wote waliohusika na mkataba wa mradi huo.

UTATA MIKOPO SACCOS
Katika hatua nyingine, PAC imemuagiza CAG kufanya ukaguzi maalumu wa mikopo yote iliyotolewa na NSSF baada ya kubaini kuwa Saccos ya Bumbuli Development Corporation imepatiwa mkopo usio wa kawaida wa Sh. bilioni 2.4 ndani ya mwaka mmoja.

Mwenyekiti wa PAC, Kaboyoka, alisema juzi kuwa kamati yake ilishtushwa na kumuagiza CAG kufanya ukaguzi maalumu wa fedha za Saccos ya Bumbuli.

Alisema suala la Saccos ya Bumbuli kupatiwa kiasi hicho kikubwa cha fedha, limewashtua wajumbe wa kamati hiyo na kujiuliza imekuwaje ipate fedha nyingi katika kipindi hicho kifupi huku ikipewa tena fedha nyingine na kufanya deni kufikia Sh. bilioni 2.4 ndani ya mwaka mmoja.

“CAG afanye ukaguzi kwenye Saccos maana haijulikani kama fedha walizopewa awali zimerudishwa au la,” alisema Mwenyekiti huyo.

Kaboyoka aliongeza kuwa maelekezo mengine yatatolewa bungeni kwa mujibu wa Kanuni ya 117(10) katika kanuni za Kudumu za Bunge toleo la Januari 2016, inayoipa mamlaka kamati hiyo kuwasilisha taarifa bungeni kuhusu hesabu za serikali.

Awali, wakati wakichangia mapitio ya hesabu za NSSF, wajumbe wa kamati hiyo walionyesha kushtushwa na jinsi Saccos hiyo ilivyopewa mabilioni ya shilingi kwa zaidi ya mara moja ndani ya muda huo mfupi.

Mbunge wa Viti maalumu, Tunza Malapo (Chadema), alihoji kama NSSF imefanya uhakiki na kujiridhisha juu ya uwapo wa Saccos hiyo ya Bumbuli.

Mbunge wa Kilindi, Omar Kigua (CCM), alihoji vigezo vilivyotumika mpaka Saccos moja kupewa mkopo mara tatu ndani ya mwaka mmoja.

Alisema NSSF imetoa mikopo kwa Saccos tisa, kwa kiasi kinachozidi asilimia 50 ya thamani ya mali za Saccoss, husika kinyume cha sera ya kukopesha ya shirika na limeomba kiasi ambacho hakikustahili kutolewa.

Katika ripoti ya CAG, mbali na Bumbuli, Saccos zingine zilizopatiwa fedha nyingi kinyume cha utaratibu ni Korongo Amcos Saccos, UMMA Saccos, SBC Saccos Ltd, Hekima Saccos, Ukombozi Saccos Ltd, Uzinza Saccos Ltd, Harbour Saccos na Umoja Saccos.

Akizungumzia suala hilo la Saccos, Mkurugenzi wa NSSF, Prof. Kahyarara, alisema ukaguzi wa awali uliofanywa, umebaini ni kweli kuna Saccos zilikuwa hazionekani huku kwenye vitabu zikiorodheshwa kuwa zimekopeshwa.

Aidha, alisema kuna wadaiwa wengine wamejitokeza na kupeleka fedha wenyewe, na ambao awali walikuwa hawajulikani.

Mwenyekiti wa Bodi ya NSSF, Prof. Samwel Wangwe, alisema hivi sasa bodi imesimamisha mikopo kwa Saccos hadi uchunguzi ukamilike na baada ya hapo utawekwa utaratibu mpya wa utoaji mikopo.
 
Land for Equity (Ardhi Kwa Hisa) na Mradi wa NSSF Dege Beach Kigamboni

Jana Magazeti mengi yameandika kuwa kuna ufisadi mkubwa kwenye miradi ya Shirika la Hifadhi ya Jamii(NSSF), Hasa Mradi wa Dege Beach Huko Kigamboni ambapo imeelezwa Kuwa Katika Kila Kiwanja Kimoja kati ya Viwanja 300 vilivyoko Katika hatua ya kwanza ya Mradi thamani ya Kiwanja imezidishwa Kwa zaidi ya Shilingi Milioni 775. Ikielezwa Kuwa thamani ya Kila Kiwanja Ni Shilingi Milioni 25 Tofauti na Milioni 800 ambazo NSSF imenunua Kwa Kila Kiwanja Kimoja Kwa Mujibu wa Mkataba kati yake Na Kampuni ya Azimio.

Taarifa Hizi ni za Uongo. Ukweli ni Kuwa NSSF haikununua Ardhi eneo la Dege Beach, Kigamboni Kwa thamani ya Milioni 800 Kwa Kiwanja, imepewa Ardhi Bure Ili iwekeze Kwa kuingia Ushirika wa Mradi Katika Ardhi ya Mtu Binafsi (Kampuni ya Azimio).

Aina hiyo ya Ushirika hujulikana Kwa wataalam wa Sekta ya Majengo (Real Estate) Kama Utaratibu wa "Land for Equity" (Yaani Ardhi Kwa Hisa). Ambapo Katika Makubaliano ya Mradi, Mbia Mmoja wa Mradi anatoa Ardhi Na Mbia mwengine anatoa Fedha za Uwekezaji. Na kisha Hisa za Mradi hugawanywa kulingana Na mtaji wa Kila Mmoja (Ardhi Kwa Mbia wa kwanza, Na Fedha Kwa Mbia mwengine).

Na hili si Jambo jipya nchini. Uchunguzi unathibitisha kuwa kilichofanywa na NSSF (Katika Mradi wa Dege Beach Kigamboni) ndicho kinachofanywa na taasisi mbalimbali nchini (wakiwemo NSSF wenyewe), katika Miradi mbalimbali ya Uwekezaji wa Ushirikiano kati sekta ya Majengo.

Baadhi ya mifano ya Miradi ya namna hiyo ni kama ifuatavyo:

• Miaka ya 90 Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) liliingia makubaliano na Shirika la Mafuta la Taifa (TPDC) kujenga Jengo la Mafuta House kwenye ardhi inayomilikiwa na NHC katika eneo ambalo sasa pamejengwa Jengo la Banjamin Mkapa Towers. Katika Ujenzi Huo NHC walipewa asilimia 25 ya thamani ya mradi kwa kutoa ardhi (Land for Equity) ambayo mwaka 1995 ilikuwa ni Shilingi bilioni 19 bilioni. Kwa mujibu wa mkataba huo thamani ya ardhi ile mwaka huo ilikuwa shs 4.75 bilioni.

Mwaka 1995 thamani ya ardhi katikati ya jiji la Dar es salaam ilikuwa ni shilingi 62,500 kwa kila mita ya mraba na kiwanja kile kina mita za mraba 6,221 sawa na ekari moja na nusu. Kwa kutumia mahesabu ya kawaida thamani ya ardhi ya NHC ingekuwa shilingi 388 milioni Na si hiyo 4.75 Bilioni ambayo inaonyesha bei kukuzwa Kwa nyongeza ya shilingi 4.35 bilioni.

• NSSF ni mfaidika wa Utaratibu wa "Land for Equity" Katika mradi Mpya wa Umeme Mkuranga. Mwaka 2014 NSSF ilinunua ardhi kwa thamani ya shilingi 100 milioni, ardhi hiyo ilikuwa Ni jumla ya ekari 100.

Mwaka 2015 Wawekezaji waliingia ubia na Shirika la NSSF Ili kujenga Mtambo wa Umeme Katika ardhi Husika. Mchango wa NSSF Katika Mradi Huo ulikuwa ni ardhi yake ya Ekari 100 ambayo iliinunua Kwa Shilingi Milioni 100 Tu Mwaka Mmoja nyuma. Lakini Katika Mkataba wa Mradi Huo NSSF imepata asilimia 10 ya thamani ya Mradi Mzima wa Uwekezaji ambayo ni Dola za Kimarekani 450 Milioni Sawa na zaidi ya Shilingi 900 Bilioni.

Katika Mradi huu wa Mkuranga NSSF ndani ya mwaka mmoja iliweza kupandisha thamani ya ardhi ile kutoka shilingi 100 milioni mpaka shilingi 90 Bilioni ambayo ni Asilimia 10 ya thamani ya Mradi Wote. Kama zingetumika Hesabu Za kawaida Tu thamani ya Uwekezaji wa NSSF kwenye Mradi Husika ilipaswa Kuwa Asilia 0.06 Tu Na Sio Asilimia 10 walizopewa.

• Mradi mwengine uliofuata Utaratibu wa "Land for Equity" (Ardhi Kwa Hisa) ni Taarifa Juu ya makubaliano kati ya NHC na PPF Katika Ujenzi wa Jengo la PPF Tower Mwanza, ambapo NHC walitoa ardhi na kupewa Aslimia 25 ya hisa za mradi husika. Mradi huo una thamani ya Shilingi bilioni 258, Lakini Ukubwa wa ardhi waliyotoa NHC ni Kiwanja cha ekari moja tu.

Kamwe huwezi kusikia ikisemwa kuwa PPF wamenunua Kiwanja Cha Ekari Moja Kwa thamani ya Shilingi Bilioni 64 Kwa Kuwa Ni Ushirika wa Pamoja.

• NSSF imejenga jengo RITA, eneo la Posta jirani Kabisa na Jengo la Klabu ya Billicanas Jijini Dar es salaam. Katika Mradi Huo RITA iliyojengewa Jengo Husika, Na Kwa Kutoa ardhi hiyo wamepata hisa Asilimia 25 ya thamani ya mradi mzima wa Jengo Hilo, ambayo ni hilingi Bilioni 198.

Lakini Ukubwa wa Kiwanja cha RITA ni nusu ekari tu. Kamwe huwezi kusikia NSSF wamenunua nusu ekari kwa Shilingi bilioni 49 Katika Mradi wa Jengo la RITA.

• Miradi mengine iliyofuata Utaratibu huu wa "Land for Equity"
* Mradi kati ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) na Fida-Hussein Katika Jengo lililoko Maeneo ya Jirani Na Hospitali ya Ocean Road.
* Mradi wa Jengo la UVCCM eneo la Fire Jijini Dar es salaam.
* Mradi wa Jengo la Mwalimu Nyerere Foundation eneo la Posta.
* Mradi wa Jengo la UWT (Makao makuu ya Airtel) eneo la Morocco nk.

• Hitimisho:

NSSF iliingia ubia na kampuni ya Azimio Kwaajili ya Uendelezwaji wa Ardhi Katika Mradi wa Dege Beach Kule Kigamboni. Kampuni ya Azimio Kwa Kutoa Ardhi ya Mradi Husika ilipewa asilimia 20 ya thamani ya mradi wa Dege Eco Village.

Lakini Pia kwenye Mkataba wa Mradi Azimio wanapaswa Kutoa 35% ya Fedha za thamani ya Mradi, Hivyo kuwafanya wawe na 55% ya Mradi Husika Huku NSSF wakiwa na 45 ya Mradi Kwa Fedha watakazotoa.

La kushangaza this time wameenda kwenye kamati ya bunge juzi . CAG presented his report na amesema amewapa NSSF clean report and everything is ok.

NSSF wenyewe wanasema hapaana things are not ok. Past management imeharibu mambo.

Kamati ikaamua kuwa the report is ADOPTED na Mradi wa Dege uendelee. Management Ikae na the JV partner waangalie modalities za kuendelea na mradi.

Out of desperation Huyu Mkurugenzi mpya wa NSSF fed the reporters with all lies (Tariff za uwongo). Na maya zaidi hakuna gazeti hata moja ambalo lilifanya investigative journalism na kuuliza basic questions kama vile:


1. Kama kuna ufisadi wa mabilioni why did CAG give clean report?

2. Kama kilichofanyika Dege ni ufisadi then why PPF NHC TBA TPDC etc are not taken to task? Why NSSF?

I'm sure wenye vichwa vilivyotulia Hapa Jamiiforums wataweza kulitazama hili kuala kwa jicho la tatu

Hii inanifanya niacin kuwa huko NSSF kuna CIVIL WAR au VITA VYA WENYEWE KWA WENYEWE. Theory yangu ni kuwa wale wanaokaimu wanawafanyia fitna wakiosimamishwa ili wafukuzwe then wao wawe confirmed. Hiyo ndio vita inayoendelea kwa sasa na maya zaidi huyu mkurugenzi mpya naye amejiingiza kwenye hiii michezo michafu na kutoa taarifa za uwongo kwa vyombo vya habari

Pia tusisahau kuwa huyu Mkurugenzi mpya aliwahi kutoa taarifa kwa vyombo vya habari kuwa Mradi wa Daraja la Kigamboni ni mradi wa anasa na haunt tija kwa shirika. Lakini wiki tatu zilizopita huyu huyu Mkurugenzi anawaambia waandishi wa habari kuwa Mradi wa Daraja la kigamboni ni mzuri sana kwa taifa na unaingizia Shirika Mabilioni
 
Land for Equity (Ardhi Kwa Hisa) na Mradi wa NSSF Dege Beach Kigamboni

Jana Magazeti mengi yameandika kuwa kuna ufisadi mkubwa kwenye miradi ya Shirika la Hifadhi ya Jamii(NSSF), Hasa Mradi wa Dege Beach Huko Kigamboni ambapo imeelezwa Kuwa Katika Kila Kiwanja Kimoja kati ya Viwanja 300 vilivyoko Katika hatua ya kwanza ya Mradi thamani ya Kiwanja imezidishwa Kwa zaidi ya Shilingi Milioni 775. Ikielezwa Kuwa thamani ya Kila Kiwanja Ni Shilingi Milioni 25 Tofauti na Milioni 800 ambazo NSSF imenunua Kwa Kila Kiwanja Kimoja Kwa Mujibu wa Mkataba kati yake Na Kampuni ya Azimio.

Taarifa Hizi ni za Uongo. Ukweli ni Kuwa NSSF haikununua Ardhi eneo la Dege Beach, Kigamboni Kwa thamani ya Milioni 800 Kwa Kiwanja, imepewa Ardhi Bure Ili iwekeze Kwa kuingia Ushirika wa Mradi Katika Ardhi ya Mtu Binafsi (Kampuni ya Azimio).

Aina hiyo ya Ushirika hujulikana Kwa wataalam wa Sekta ya Majengo (Real Estate) Kama Utaratibu wa "Land for Equity" (Yaani Ardhi Kwa Hisa). Ambapo Katika Makubaliano ya Mradi, Mbia Mmoja wa Mradi anatoa Ardhi Na Mbia mwengine anatoa Fedha za Uwekezaji. Na kisha Hisa za Mradi hugawanywa kulingana Na mtaji wa Kila Mmoja (Ardhi Kwa Mbia wa kwanza, Na Fedha Kwa Mbia mwengine).

Na hili si Jambo jipya nchini. Uchunguzi unathibitisha kuwa kilichofanywa na NSSF (Katika Mradi wa Dege Beach Kigamboni) ndicho kinachofanywa na taasisi mbalimbali nchini (wakiwemo NSSF wenyewe), katika Miradi mbalimbali ya Uwekezaji wa Ushirikiano kati sekta ya Majengo.

Baadhi ya mifano ya Miradi ya namna hiyo ni kama ifuatavyo:

• Miaka ya 90 Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) liliingia makubaliano na Shirika la Mafuta la Taifa (TPDC) kujenga Jengo la Mafuta House kwenye ardhi inayomilikiwa na NHC katika eneo ambalo sasa pamejengwa Jengo la Banjamin Mkapa Towers. Katika Ujenzi Huo NHC walipewa asilimia 25 ya thamani ya mradi kwa kutoa ardhi (Land for Equity) ambayo mwaka 1995 ilikuwa ni Shilingi bilioni 19 bilioni. Kwa mujibu wa mkataba huo thamani ya ardhi ile mwaka huo ilikuwa shs 4.75 bilioni.

Mwaka 1995 thamani ya ardhi katikati ya jiji la Dar es salaam ilikuwa ni shilingi 62,500 kwa kila mita ya mraba na kiwanja kile kina mita za mraba 6,221 sawa na ekari moja na nusu. Kwa kutumia mahesabu ya kawaida thamani ya ardhi ya NHC ingekuwa shilingi 388 milioni Na si hiyo 4.75 Bilioni ambayo inaonyesha bei kukuzwa Kwa nyongeza ya shilingi 4.35 bilioni.

• NSSF ni mfaidika wa Utaratibu wa "Land for Equity" Katika mradi Mpya wa Umeme Mkuranga. Mwaka 2014 NSSF ilinunua ardhi kwa thamani ya shilingi 100 milioni, ardhi hiyo ilikuwa Ni jumla ya ekari 100.

Mwaka 2015 Wawekezaji waliingia ubia na Shirika la NSSF Ili kujenga Mtambo wa Umeme Katika ardhi Husika. Mchango wa NSSF Katika Mradi Huo ulikuwa ni ardhi yake ya Ekari 100 ambayo iliinunua Kwa Shilingi Milioni 100 Tu Mwaka Mmoja nyuma. Lakini Katika Mkataba wa Mradi Huo NSSF imepata asilimia 10 ya thamani ya Mradi Mzima wa Uwekezaji ambayo ni Dola za Kimarekani 450 Milioni Sawa na zaidi ya Shilingi 900 Bilioni.

Katika Mradi huu wa Mkuranga NSSF ndani ya mwaka mmoja iliweza kupandisha thamani ya ardhi ile kutoka shilingi 100 milioni mpaka shilingi 90 Bilioni ambayo ni Asilimia 10 ya thamani ya Mradi Wote. Kama zingetumika Hesabu Za kawaida Tu thamani ya Uwekezaji wa NSSF kwenye Mradi Husika ilipaswa Kuwa Asilia 0.06 Tu Na Sio Asilimia 10 walizopewa.

• Mradi mwengine uliofuata Utaratibu wa "Land for Equity" (Ardhi Kwa Hisa) ni Taarifa Juu ya makubaliano kati ya NHC na PPF Katika Ujenzi wa Jengo la PPF Tower Mwanza, ambapo NHC walitoa ardhi na kupewa Aslimia 25 ya hisa za mradi husika. Mradi huo una thamani ya Shilingi bilioni 258, Lakini Ukubwa wa ardhi waliyotoa NHC ni Kiwanja cha ekari moja tu.

Kamwe huwezi kusikia ikisemwa kuwa PPF wamenunua Kiwanja Cha Ekari Moja Kwa thamani ya Shilingi Bilioni 64 Kwa Kuwa Ni Ushirika wa Pamoja.

• NSSF imejenga jengo RITA, eneo la Posta jirani Kabisa na Jengo la Klabu ya Billicanas Jijini Dar es salaam. Katika Mradi Huo RITA iliyojengewa Jengo Husika, Na Kwa Kutoa ardhi hiyo wamepata hisa Asilimia 25 ya thamani ya mradi mzima wa Jengo Hilo, ambayo ni hilingi Bilioni 198.

Lakini Ukubwa wa Kiwanja cha RITA ni nusu ekari tu. Kamwe huwezi kusikia NSSF wamenunua nusu ekari kwa Shilingi bilioni 49 Katika Mradi wa Jengo la RITA.

• Miradi mengine iliyofuata Utaratibu huu wa "Land for Equity"
* Mradi kati ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) na Fida-Hussein Katika Jengo lililoko Maeneo ya Jirani Na Hospitali ya Ocean Road.
* Mradi wa Jengo la UVCCM eneo la Fire Jijini Dar es salaam.
* Mradi wa Jengo la Mwalimu Nyerere Foundation eneo la Posta.
* Mradi wa Jengo la UWT (Makao makuu ya Airtel) eneo la Morocco nk.

• Hitimisho:

NSSF iliingia ubia na kampuni ya Azimio Kwaajili ya Uendelezwaji wa Ardhi Katika Mradi wa Dege Beach Kule Kigamboni. Kampuni ya Azimio Kwa Kutoa Ardhi ya Mradi Husika ilipewa asilimia 20 ya thamani ya mradi wa Dege Eco Village.

Lakini Pia kwenye Mkataba wa Mradi Azimio wanapaswa Kutoa 35% ya Fedha za thamani ya Mradi, Hivyo kuwafanya wawe na 55% ya Mradi Husika Huku NSSF wakiwa na 45 ya Mradi Kwa Fedha watakazotoa.

La kushangaza this time wameenda kwenye kamati ya bunge juzi . CAG presented his report na amesema amewapa NSSF clean report and everything is ok.

NSSF wenyewe wanasema hapaana things are not ok. Past management imeharibu mambo.

Kamati ikaamua kuwa the report is ADOPTED na Mradi wa Dege uendelee. Management Ikae na the JV partner waangalie modalities za kuendelea na mradi.

Out of desperation Huyu Mkurugenzi mpya wa NSSF fed the reporters with all lies (Tariff za uwongo). Na maya zaidi hakuna gazeti hata moja ambalo lilifanya investigative journalism na kuuliza basic questions kama vile:


1. Kama kuna ufisadi wa mabilioni why did CAG give clean report?

2. Kama kilichofanyika Dege ni ufisadi then why PPF NHC TBA TPDC etc are not taken to task? Why NSSF?

I'm sure wenye vichwa vilivyotulia Hapa Jamiiforums wataweza kulitazama hili kuala kwa jicho la tatu

Hii inanifanya niacin kuwa huko NSSF kuna CIVIL WAR au VITA VYA WENYEWE KWA WENYEWE. Theory yangu ni kuwa wale wanaokaimu wanawafanyia fitna wakiosimamishwa ili wafukuzwe then wao wawe confirmed. Hiyo ndio vita inayoendelea kwa sasa na maya zaidi huyu mkurugenzi mpya naye amejiingiza kwenye hiii michezo michafu na kutoa taarifa za uwongo kwa vyombo vya habari

Pia tusisahau kuwa huyu Mkurugenzi mpya aliwahi kutoa taarifa kwa vyombo vya habari kuwa Mradi wa Daraja la Kigamboni ni mradi wa anasa na haunt tija kwa shirika. Lakini wiki tatu zilizopita huyu huyu Mkurugenzi anawaambia waandishi wa habari kuwa Mradi wa Daraja la kigamboni ni mzuri sana kwa taifa na unaingizia Shirika Mabilioni
Kimya hakuna asemaye
 
Ina maana huu mradi ndio hauendelei tena au inakuwaje hasaaa??na serikali imeamua nini kuhusu huu mradi??
 
Dr F. Ndugulile tunaomba marejesho kuhusu huu mladi kiongizi ingekuwa vizuri sanaaa tukajuwa je hayo maeneno hayaendelei tena au nini kinaendelea...
 
Sio mchezo maana huu mradi watu tuli target mambo mengi sanaaaa tena sanaa na tukajenga apartments zetu wenyewe maana hili eneo lilikuwa hot cake vibaya sanaa sijui imekuwaje kwa kweli....kila kitu kimesimama...
pole boss naona unajiuma na kujipiliza mwenyewe..tumekosa sera ya Taifa tunaendeshwa na maamuzi ya watu binafsi anaweza kuja kiongozi mwengine akasema mradi wa reli haufai na kuanza upya
 
pole boss naona unajiuma na kujipiliza mwenyewe..tumekosa sera ya Taifa tunaendeshwa na maamuzi ya watu binafsi anaweza kuja kiongozi mwengine akasema mradi wa reli haufai na kuanza upya

Na ule mradi ulikuwa unaenda vizuri sanaaa toka bwana mkubwa aingie tu ukawa umesimama kabisaaa sasa je jwa lile eneo walipofikia je itakuwaje pale??sema wacha tusubirie kwanza tuone itakuwaje after miaka kadhaa ila kwa sasa pale pamekwama nadhani..
 
Back
Top Bottom