Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Rais Museveni ametembelea tanzania Kikazi
===
Rais John Magufuli wa Tanzania na Rais Yoweri Museveni wa Uganda wamesaini makubaliano ya kuanza ujenzi wa Bomba la Mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga, Tanzania
Rais Magufuli: Tumeshuhudia uwekaji wa saini wa ujenzi wa Bomba hili la Mafuta lenye km 1,445. Hii ni hatua muhimu sana kuelekea utekelezaji wa mradi huu. Ni mradi wa takribani USD 3.5 Billion
Rais Magufuli: Km 330 za bomba hili zipo Uganda. Kwa Tanzania, bomba litapita kwenye mikoa 8, wilaya 24 na kata 132. Tathmini kwa Tanzania, watu zaidi ya 90,000 watalipwa fidia; ni takribani bilioni 21
Rais Magufuli: Nampongeza Rais Museveni, amefanya mambo yasiyowezekana! Haya mafuta yasingepatikana Uganda, sisi tusingenufaika. Yawezekana kuna waganda wanaomtukana pamoja na kazi hii nzuri anayofanya!
Rais Magufuli: Mradi huu ulichelewa! Coronavirus ilichelewesha huu mradi, ishindwe kabisa! Jana Mzee Museveni alinipigia simu, akasema Corona isiwe sababu ya mradi kuchelewesha mradi. Alisema atakuja na barakoa, nikamwambia hata uje na blanketi, njoo tu!
Rais Magufuli: Mradi huu wa Bomba la Mafuta ni ushindi wa Pili baada ya Vita vya Kagera. Tulichelewa kidogo katika hili juu ya kugawana faida. Tumekaa chemba dakika 5 chemba tu, nikamwambia Tanzania tupate 60% na 40% iende Uganda - Rais Museveni akakubali
Rais Magufuli: Tunaendelea na utafiti wa mafuta hapa Tanzania, endapo yatapatikana, tutayapitisha kwenye hili bomba. Endapo gesi itaanza kupatikana Tanzania, tutaipeleka Uganda sambamba na hili Bomba la Mafuta
Rais Museveni: Nilitumia wataalamu wetu tangu mwanzo hadi mwisho, watu wa nje walikuwa wanatuchezea. Baadhi ya waganda waliokuwa wamesomea masuala haya niliwapeleka kuongeza utaalam, waliporudi wakagundua mafuta haya mwaka 2006
Rais Museveni: Nataka watanzania na raia wa Afrika Mashariki tuamke! Huwa nafuatilia TBC1... Nitafanya mazungumzo na Rais Magufuli na CCM tuangalie jinsi ya kuimarisha masoko baina ya nchi zetu na kuimarisha undugu wetu
Rais Museveni: Hivi karibuni tutarudi Tanzania kuzungumzia masuala ya Gesi. Uganda ina uhitaji mkubwa wa gesi, namshukuru Rais Magufuli kwa utayari wa kupitisha bomba la gesi sambamba na bomba la mafuta! Huo ndo undugu
===
Rais John Magufuli wa Tanzania na Rais Yoweri Museveni wa Uganda wamesaini makubaliano ya kuanza ujenzi wa Bomba la Mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga, Tanzania
Rais Magufuli: Tumeshuhudia uwekaji wa saini wa ujenzi wa Bomba hili la Mafuta lenye km 1,445. Hii ni hatua muhimu sana kuelekea utekelezaji wa mradi huu. Ni mradi wa takribani USD 3.5 Billion
Rais Magufuli: Km 330 za bomba hili zipo Uganda. Kwa Tanzania, bomba litapita kwenye mikoa 8, wilaya 24 na kata 132. Tathmini kwa Tanzania, watu zaidi ya 90,000 watalipwa fidia; ni takribani bilioni 21
Rais Magufuli: Nampongeza Rais Museveni, amefanya mambo yasiyowezekana! Haya mafuta yasingepatikana Uganda, sisi tusingenufaika. Yawezekana kuna waganda wanaomtukana pamoja na kazi hii nzuri anayofanya!
Rais Magufuli: Mradi huu ulichelewa! Coronavirus ilichelewesha huu mradi, ishindwe kabisa! Jana Mzee Museveni alinipigia simu, akasema Corona isiwe sababu ya mradi kuchelewesha mradi. Alisema atakuja na barakoa, nikamwambia hata uje na blanketi, njoo tu!
Rais Magufuli: Mradi huu wa Bomba la Mafuta ni ushindi wa Pili baada ya Vita vya Kagera. Tulichelewa kidogo katika hili juu ya kugawana faida. Tumekaa chemba dakika 5 chemba tu, nikamwambia Tanzania tupate 60% na 40% iende Uganda - Rais Museveni akakubali
Rais Magufuli: Tunaendelea na utafiti wa mafuta hapa Tanzania, endapo yatapatikana, tutayapitisha kwenye hili bomba. Endapo gesi itaanza kupatikana Tanzania, tutaipeleka Uganda sambamba na hili Bomba la Mafuta
Rais Museveni: Nilitumia wataalamu wetu tangu mwanzo hadi mwisho, watu wa nje walikuwa wanatuchezea. Baadhi ya waganda waliokuwa wamesomea masuala haya niliwapeleka kuongeza utaalam, waliporudi wakagundua mafuta haya mwaka 2006
Rais Museveni: Nataka watanzania na raia wa Afrika Mashariki tuamke! Huwa nafuatilia TBC1... Nitafanya mazungumzo na Rais Magufuli na CCM tuangalie jinsi ya kuimarisha masoko baina ya nchi zetu na kuimarisha undugu wetu
Rais Museveni: Hivi karibuni tutarudi Tanzania kuzungumzia masuala ya Gesi. Uganda ina uhitaji mkubwa wa gesi, namshukuru Rais Magufuli kwa utayari wa kupitisha bomba la gesi sambamba na bomba la mafuta! Huo ndo undugu