Afisa Mteule Drj 2
JF-Expert Member
- Mar 21, 2017
- 3,865
- 4,506
Dikteta wa kibanyankole na dikteta wa kisukuma kukutana
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pinga pinga katika ubora wako.Sina tatizo na kuahirishwa na ninakubaliana na hilo kabisa. Je kuna haja gani ya kukusanya kundi lile lile la viongozi, kuweka mkataba ambao ulikuwa umeahirishwa? Shaka yangu ni hii, wakati ule Tanga wazungu wa Total walikuwepo, na mradi haukwenda kama tulivyoaminishwa, ila leo igizo ni lile lile bila hao wazungu. Ninachoona hapo ni wanaccm ambao hawana hata kumi ya kutoa kwenye huo mradi, huku wazungu wenye pesa hawako kwenye hizo hii episode II. Naona ni kampeni zaidi.
Ninasema hivyo maana nina uzoefu na huyo Museveni. Aliwahi kupewa sehemu ya bandari ya Tanga aendeleze lakini hakufanya hivyo, hilo bomba alishakubali kulipitisha Kenya lakini kabidili porojo kalileta Tanzania! Kuna mengi ila leo sio mada, lakini huyo Museveni ni tapeli kama matapeli wengine, na ndio maana naona kwa sasa ni kampeni zaidi kuliko kinachoongelewa.
Hakuna majibu, na huyo Museveni kaishia kumuombea Magufuli kura, maana ndio kilichomleta. Hilo la uzinduzi wa mradi ni utapeli tu.
Watanzania ni wajinga kuanzia viongozi wetu hadi maCCM yanafurahia miradi ya watu wengine ya kwetu ikidolora kama Haina wenyewe. Hilo Bomba la mafuta ni mradi wa Uganda kwa asilimia 100% hapa kwetu Bomba na mafuta ghafi yatakuwa yanapita tu kwenda kwa wateja wa Uganda na watumishi muhimu wote watakuwa Waganda, Watanzania labda watakuwa wafagiaji. Kuna TAZAMA Pipeline kwenda Zambia sasa lina miaka zaidi ya 50 lakini Watanzania wengi hawajui kuwepo kwa Bomba hilo wala faida yake kwa nchi yetu. Kama TAZARA, Miradi hii inaanzishwa kisiasa inaishia kutokuwa na faida kwa nchi kiuchumi na hata kuwa mizigo. Miradi ya kisiasa ni balaa, tutaona mingi tu!Ni ujinga kufurahia mradi wa mwenzako wa mafuta, kwako umeua mradi wa gas ambao ulikuwa mkubwa zaidi ya mara 10 ya unaoufurahia.
Leo Mozambique ni nchi ya pili Duniani katika uwekezaji mkubwa wa gas kwa mwaka 2019/2020.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkataba wa kuanza ujenzi ndo umeingiwa sasa.Nakumbuka huu mradi ulizinduliwa 2016 Kwa mbwembwe saaana na mikataba ikasainiwa hadharani na tukajulishwa kuwa mradi utakamilika mwezi wa nne Mwaka 2019 nashangaaa tena Leo eti unazinduliwa na katika uzinduzi huo nimesikia maneno kuwa tunataka mazungumzo yafanyike mapema ili michakato ianze haraka, sijaelewa...
Mwambie ameshafeli kabla hajaanzaNimemsikia Rais Mseveni akimuombea Kura Rais Magufuli na ccm kuwa itapatapa ushindi.
Hili linaweza kuchukuliwa vibaya na wafuasi wa vyama pinzani japo ziara yake ilikuwa ya kikazi na yenye faida kubwa kwa Tanzania lakini hili la uchama litaondoa mazuri yote aliyo kuja nayo.
Lakini pia ni dhahiri Rais Museveni kuwa mwana ccm halisi baada ya kuomba nyimbo za zamani za Tanu enzi hizo akiwa Tanzania.
Rais Museveni ametembelea tanzania Kikazi
===
Rais John Magufuli wa Tanzania na Rais Yoweri Museveni wa Uganda wamesaini makubaliano ya kuanza ujenzi wa Bomba la Mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga, Tanzania
Rais Magufuli: Tumeshuhudia uwekaji wa saini wa ujenzi wa Bomba hili la Mafuta lenye km 1,445. Hii ni hatua muhimu sana kuelekea utekelezaji wa mradi huu. Ni mradi wa takribani USD 3.5 Billion
Rais Magufuli: Km 330 za bomba hili zipo Uganda. Kwa Tanzania, bomba litapita kwenye mikoa 8, wilaya 24 na kata 132. Tathmini kwa Tanzania, watu zaidi ya 90,000 watalipwa fidia; ni takribani bilioni 21
Rais Magufuli: Nampongeza Rais Museveni, amefanya mambo yasiyowezekana! Haya mafuta yasingepatikana Uganda, sisi tusingenufaika. Yawezekana kuna waganda wanaomtukana pamoja na kazi hii nzuri anayofanya!
Rais Magufuli: Mradi huu ulichelewa! Coronavirus ilichelewesha huu mradi, ishindwe kabisa! Jana Mzee Museveni alinipigia simu, akasema Corona isiwe sababu ya mradi kuchelewesha mradi. Alisema atakuja na barakoa, nikamwambia hata uje na blanketi, njoo tu!
Rais Magufuli: Mradi huu wa Bomba la Mafuta ni ushindi wa Pili baada ya Vita vya Kagera. Tulichelewa kidogo katika hili juu ya kugawana faida. Tumekaa chemba dakika 5 chemba tu, nikamwambia Tanzania tupate 60% na 40% iende Uganda - Rais Museveni akakubali
Rais Magufuli: Tunaendelea na utafiti wa mafuta hapa Tanzania, endapo yatapatikana, tutayapitisha kwenye hili bomba. Endapo gesi itaanza kupatikana Tanzania, tutaipeleka Uganda sambamba na hili Bomba la Mafuta
Rais Museveni: Nilitumia wataalamu wetu tangu mwanzo hadi mwisho, watu wa nje walikuwa wanatuchezea. Baadhi ya waganda waliokuwa wamesomea masuala haya niliwapeleka kuongeza utaalam, waliporudi wakagundua mafuta haya mwaka 2006
Rais Museveni: Nataka watanzania na raia wa Afrika Mashariki tuamke! Huwa nafuatilia TBC1... Nitafanya mazungumzo na Rais Magufuli na CCM tuangalie jinsi ya kuimarisha masoko baina ya nchi zetu na kuimarisha undugu wetu
Rais Museveni: Hivi karibuni tutarudi Tanzania kuzungumzia masuala ya Gesi. Uganda ina uhitaji mkubwa wa gesi, namshukuru Rais Magufuli kwa utayari wa kupitisha bomba la gesi sambamba na bomba la mafuta! Huo ndo undugu
umeongea kwa uchungu sana dah,lakin ndio hivyo project inaanzaWakati ule pale chongoleani Tanga mkawaweka wale wazungu wa Total kwenye jua, mlikuwa mnafanya utapeli wa nini? Huyo Museveni ni bonge la tapeli, aliwahi kuomba enzi za Mkapa RIP, apewe sehemu ya bandari ya Tanga ili apitishe mizigo ya Uganda. Mpaka Mkapa anaingia juzi kaburini hajawahi hata kuona tofali moja! Nilidhani kwakuwa hizi mbwembwe zilifanyika na mradi haukuanza, hakukuwa na haja tena ya kukusanya kundi lile lile la viongozi kula pesa za wananchi, wakati huu wa kampeni kurudia jambo lile, sana sana mnaonekana mnafanya kampeni za kitapeli, ndio maana kumejaa nguo za ccm kwenye huo utapeli. Ukitaka kujua hizo ni kampeni za kitapeli, wale wazungu wa Total mbona leo hawapo maana hela ni zao?
Kilichotangazwa hapo ni CIA (Chato International Airport) na siyo mbuga ya Burigi - Chato.Hater