Ujenzi wa madarasa nchini na madhila wanayoyapata wakuu wa Shule

Ujenzi wa madarasa nchini na madhila wanayoyapata wakuu wa Shule

Hizi serikali za nchi za kiafrika ni bure kabisa. Kwa nini wasingetangaza tenda wampe mkandarasi mmoja au wawili au idadi inayofaa wajenge? Serikali ibaki kwenye usimamizi tu
...............tunapaswa kuwa makini sana tunapogusa masuala ya umma
 
Tumieni wakandarasi;

Tangaza tenda,
Mpe kazi mkandarasi,
Lipa kwa mujibu wa sheria.
Mfano;
25% malipo ya awali
25% nusu ya kazi
25/% akimaliza kazi
25% baada kuthibitisha
ubora wa kazi.
NB:
Kila h/mashauri ina mhandisi
na team ya ufuatiliaji.
Hamko peke yenu,chapeni
kazi.
Bei za wakandarasi wanapo bid kwenye tender zinakua kubwa kuliko allocated budget ya mradi.
Changamoto nyingine muda wa process za kufanya tender ni mrefu. Na hata muda wa execution ya miradi(delivery time) inatofautiana kati ya mkandarasi moja na mwingine .

On top of that mafundi wanaotumiwa na wakandarasi ni hao local ambao bei zao ni nusu ya bei za makandarasi(contractors)
 
Habarini wanajamvi!..
Tunafahamu kinachoendelea juu ya ujenzi wa madarasa kote nchini chini ya ufadhili wa IMF lakini kinachofanyika kimenisukuma kuandika haya.
Mosi, wakuu wa shule wamejikuta katika wakati mgumu sana kutokana na kuwepo kwa wimbi kubwa la wakaguzi na wafuatiliaji ambao kila mmoja amekuwa akitoa mapendekezo yake juu ya ujenzi licha ya kuwepo kwa muongozo katika Bill of Quantity (BOQ)
Pili, kumeibuka wimbi la watu wa kati wanaovuruga biashara ya vifaa vya ujenzi, jambo linalosababisha vifaa hivyo kuuzwa kwa bei kubwa kuliko kawaida yake.
Tatu, muda uliopangwa ili kukamilisha ujenzi wa madarasa hayo ni mfupi kiasi cha kutia mashaka juu ya ubora, mathalani hakuna muda wa kutosha ili kumwagilia maji majengo hayo licha ya kutumia saruji nyingi.
Nne, Bill of Quantity haijaonesha gharama zote mfano gharama za maji, umwagiliaji na usafiri.
Tano, licha ya ukweli kuwa kazi hii inahitaji usimamaizi wa karibu katika muda wote wa kazi, hakuna kiasi kilichotengwa kwa ajili ya chakula au maji ya wasimamizi.
Nina uzoefu sana juu haya. Wanaweza kukuletea mkandarasi nakuagiza uhakikishe anapitishwa. Watakueleza na muda na kiasi cha kumlipa isivo rasmi.
Penye pesa hakuna kunena kwa lugha, huwezi kemea mapepo.
Ukiwa na mradi mkubwa utatembelewa mara nyingi na inakubidi uandae chai au soda kwa wageni.
Kia mtu mtaani na hata walimu wenzako huamini kwamba huna njaa tena.
Ukuu wa shule ni mtego sana.

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
 
Walimu chapeni kazi nyie si ndio wamaccm na chama kinawaamini?

Mnasimamia uchaguzi sembuse ujenzi wa madarasa??

Tatizo kujipendekeza sana ili mpewe vyeo.
Walimu si ccm bali hupokea tu maelekezo wakiambiwa ole wenu ... Wanaogopa kupoteza ajira.
Walimu ni kama yaya hana ujanja mbele ya bosi wake.

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu, hawa walimu wakuu wanapata pressure kubwa sana kutoka kwa viongozi wa Halmashauri zao. Hii miradi inatekelezwa kisiasa zaidi. Na Mkuu wa Shule asipoangalia ang'oka!
Wakuu wa shule lazima mapigo ya moyo yaongezeke kukiwa na mradi wa ujenzi. Adui wa mwalimu pia ni mwalimu

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
 
Walimu si ccm bali hupokea tu maelekezo wakiambiwa ole wenu ... Wanaogopa kupoteza ajira.
Walimu ni kama yaya hana ujanja mbele ya bosi wake.

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
True ni wanyonge mno. Na wanaonewa kweli kweli. Kuna halmashauri ukionelana Mwl Ni mpinzani basi madili ya serikali hapati.
 
Back
Top Bottom