Ujinga, Umaskini na Maradhi ni mtaji mkuu wa wanasiasa wa Tanzania

Ujinga, Umaskini na Maradhi ni mtaji mkuu wa wanasiasa wa Tanzania

Mtaka Haki

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2010
Posts
492
Reaction score
149
Nimesikitika sana kuona kuwa katika maadui wakuu wa tangu kale
1. Ujinga
2. Umaskini
3. Maradhi

Kwa WANASIASA wa leo hao ndio marafiki wao wakuu katika kutimiza agenda zao na uovu wao.


1. UJINGA

Tunawekeza kwenye ujinga wa watu wetu. Kama sio ujinga wa watu wetu VIONGOZI wetu wasingethubutu kufanya na kusema tunayoyaona na kuyasikia. Hofu ya uelewa wa watu ingewaogopesha na kuwanyenyekesha. Huwezi kuona mahali duniani penye demokrasia ya kweli wananchi wakilazimishwa kufuata matakwa na vitisho vya watu wachache au kikundi cha watu wachache wanaoweza kubadilisha hata maamuzi ya wananchi. Huwezi kuona mahali ambapo Chombo cha wawakilishi wa wananchi kinafanyika mahali pa mipasho umbeya matusi bila hofu ya kuwajibishwa na waliokutuma.
Kila mahali ambapo elimu haikupewa kipaumbele tumeona ni mahali pazuri pa kupata UONGOZI hata kwa watu wasiokuwa waadilifu hawaogopi kwa kuwa wamewekeza kwenye ujinga wa watu.

Heshima kwa utawala wa sheria na uaminifu kwa KATIBA, KANUNI na taratibu zinapokiukwa bila heshima wala hofu ni ishara ya ujinga wetu.


2. UMASIKINI

Watu kwa umaskini wao wanarubuniwa kuuza utu wao na heshima yao. Wanalazimishwa na nguvu ya PESA kuwa wanafiki na kutokufuata dhamiri zao juu ya nani bora. Wakati wenzetu wengi wa nchi zilizoshinda masuala ya rushwa hutafuta pesa za kujitangaza na kueneza sera ili wakubalike sisi bado tunatafuta fedha za kuhonga watu wasiojua tunachoamini au kupanga kufanya. Badala ya kuunga mkono hoja wanaunga mkono aliyetoa pesa au kiasi cha pesa walichopokea bila kujali msimamo, UADILIFU na MISINGI anayosimamia mtoaji.


3. MARADHI

Haya yamegeuka kuwa mitaji ya wanasiasa wengi. Hatuboreshi lolote tunatumia maradhi ya watu wetu kuombea misaada bila kuwa na mpango wa DHATI toka moyoni wa kuyatokomeza.

UJINGA NA UMASKINI NA MARADHI NI MTAJI MKUU WA VIONGOZI WA KISIASA. Ni wakati wanasiasa waitendee HAKI dhamiri yao hata kama wataanguka kisiasa wakumbukwe kama Gorbashev na Fredrick De Clark waliofanya ya HAKI hata kama walikosa cheo.


HATUA GANI ZICHUKULIWE HAPA TANZANIA KUBADILISHA HALI HII.
 
Pia, na sisi wana nchi tuache uvivu wa kufikiria katika kufanya maamuzi sahihi na uvivu wa kufanya kazi pia.
 
Wana jamvi kwa ufupi kabisa nimegundua kuwa ccm wanashinda ovyo katika chaguzi kwa sababu kubwa 3;

1;ujinga wa tanzania wengi kutotambua madhila wanayopata yanatokana na utawala uliopo;
2;umaskini mkubwa unawafanya wawe watumwa hata sahani ya ubwabwa,kofia,fulana na mabango tu yanatosha kusahau maumivu kwa muda mfupi,kama vile ukosefu wa huduma muhimu;
3;kulewa propaganda kirahisi toka kwa ccm kwa kueneza vitisho kuwa vyama pinzani vitaleta vita,udini,ukabika ikiwa ni pamoja na kuchafua sifa za wagombea wa upinzani; naomba ongezeni nyengine sababu
 
Chama tawala kinapaswa kuonyesha mfano wa kuheshimu elimu ya watu kwa kuweka mipango madhubuti. Wanapojiandaa kuhutubia wajiandae kama wanaoenda kuhutubia UN. Ila wawasilishe kwa njia nyepesi na kwa heshima ya watu wake.
 
Huo ndiyo mtaji mkubwa kwa CCM... Ukiangalia sehemu ambazo UJINGA, MARADHI NA UMASIKINI vimeota mzizi ndoko CCM wananishinda kwa kishindo..

Huhitaji kuwa na degree ku-prove hili


UMASIKI + UJINGA + MARADHI = USHINDI WA KISHINDO WA CCM

nini KIFANYIKE ?
 
Huo ndiyo mtaji mkubwa kwa CCM... Ukiangalia sehemu ambazo UJINGA, MARADHI NA UMASIKINI vimeota mzizi ndoko CCM wananishinda kwa kishindo..

Huhitaji kuwa na degree ku-prove hili


UMASIKI + UJINGA + MARADHI = UCHINDI WA KISHINDO WA CCM
Uko sahihi sana .
 

Attachments

  • attachment-1.jpeg
    attachment-1.jpeg
    10.8 KB · Views: 921
  • 10426173_1537633659847262_5991407606801374031_n.jpeg
    10426173_1537633659847262_5991407606801374031_n.jpeg
    15.5 KB · Views: 184
  • attachment-13.jpeg
    attachment-13.jpeg
    14.3 KB · Views: 986
  • attachment-4.jpeg
    attachment-4.jpeg
    10.7 KB · Views: 902
nini KIFANYIKE ?

Iko hivi.. Mlinzi tuliyempa dhamana ya kulinda mali zetu anashirikiana na wezi kutuibia.. CCM ndiyo impewa dhamana ya kulinda rasilimali zetu na kukusanya kodi na kutuletea maendeleo.. Sasa kwa kuwa iko dhahiri shahiri Mlinzi huyu anashikiriana na wezi kutuibia dawa ni moja tu.. Kumfukuza kazi na kumpeleka mahakamani..

TOA CCM MADARAKANI TANZANIA IPONE
 
Nini kifanyike!? Tuambie tuambie, tufuate njia gani!?

Hii ni topic nzuri ambayo natazamia wanaJF watatupia hekima zao bila kuangalia itikadi zao au ushabiki. Swali la "nini kifanyike" ni kwa waTZ wote. Mimi nianze kwa kupendekeza yafuatayo
1. Katika kujinadi kwenye uchaguzi ujao, vyama husika vitoe kauli kuhusu sera zao kuhusiana na mambo hayo matatu. Isiwe ahadi zile zisizotekelezeka
2. WaTZ tuweke kwenye katiba mpya kuwa mambo ya msingi kama elimu mpaka degree ya kwanza, matibabu yote ya kawaida yatolewe bure kwa waTZ wote
 
Hatua zinahusu nini?

Fanya bidii yako binafsi kushindana na yote hayo yatakuondokea. Unangoja mtu akuchukulie hatua kwa ujinga wako?

Nyie ndiyo mnawaponza wasiojuwa Kiswahili vizuri, wanaanza kupiga hatua kutoa Geita sijui wapi huko wanajuwa wakifika Ikulu kila kitu safi, wakaishia rumande.
 
Hatua zinahusu nini?

Fanya bidii yako binafsi kushindana na yote hayo yatakuondokea. Unangoja mtu akuchukulie hatua kwa ujinga wako?

Nyie ndiyo mnawaponza wasiojuwa Kiswahili vizuri, wanaanza kupiga hatua kutoa Geita sijui wapi huko wanajuwa wakifika Ikulu kila kitu safi, wakaishia rumande.

Vipi kuhusu maazimio ya kamati kuu ya ccm.
 
Back
Top Bottom