Ujinga, Umaskini na Maradhi ni mtaji mkuu wa wanasiasa wa Tanzania

Ujinga, Umaskini na Maradhi ni mtaji mkuu wa wanasiasa wa Tanzania

ni ukweli mchungu na unaumiza. penye ujinga,na hata umasikini ccm imetamalaki. mifano iko mingi.
 
ni ukweli mchungu na unaumiza. penye ujinga,na hata umasikini ccm imetamalaki. mifano iko mingi.

Kwahiyo una maana CCM wote ni wapumbuva na wajinga ndio maana wanakimbia midahalo ya wazi including mwenye kigoda wao?!
 
Kwahiyo una maana CCM wote ni wapumbuva na wajinga ndio maana wanakimbia midahalo ya wazi including mwenye kigoda wao?!
ushahidi wa wazi huu hapa .
10413289_443379535821384_8736472890136950428_n.jpeg
attachment-4.jpeg
attachment-1.jpeg
attachment.jpeg
attachment-13-2.jpg
 
Kwahiyo una maana CCM wote ni wapumbuva na wajinga ndio maana wanakimbia midahalo ya wazi including mwenye kigoda wao?!

mkuu viongozi wa ccm ni werevu sana hasa kwa maslai yao binafsi. kukataa midahalo ni janja ya nyani ili wasikosolewe.
 
Kwa sisi vijana tuliozaliwa miaka ya 1980+ nadhani kwenye siasa za nchi hii tutakuwa tumezifahidi sana kwa kujioneea na kuziishi pamoja na kuzisikiliza kwa makini na ukaribu zaidi ni siasa za wakati wa Rais Kikwete anawania nafasi ya kuingia IKULU.

Hapo tulipewa matumaini mengi sana hasa kwa sisi tunaoishi kwenye huu umasikini, kwani kwa mara ya kwanza swala la kila mtanzania kuwa na maisha bora tena kwa kasi na hali mpya liliongelewa sana na kuelezea mikakati na mipango ya jinsi tutakavyo jivua JOHO la umasikini.

Kufufua na kuanzisha ya viwanda, kuacha kuudha mazao ghafi, mikataba mibovu, rushwa, maji, afya (wazazi kujifungulia chini), ajira (hasa vijana) , michezo (hadi kushiriki kombe la dunia kwenye soka) yote haya tuliambiwa na kuaminishwa yanawezekana tuwape nafasi, na watanzania wakawapa.

Baada ya miaka kumi kupita nilitegemea leo watangaza nia wote kupitia CCM wangekuja na habari mpya ambazo nilitegemea nyingi zitakuwa zinaelezea watanzania tukiwa tayari kwenye maisha bora na sasa tunaelekea kwenye maisha ya juu zaidi.

Matokea yake kila kila mtu anakuja na lake, mara huyu anauchukia umasikini mwingine umasiki sijausoma nimeuishi na mwingine yeye ni mtoto wa masikini na wote wakiahadi kuotokomeza umasiki ambao wote hawataki kueleza kuwa kama chama kwanini wameshindwa swala hilo kwa miaka zaidi ya 35 ya CCM.

Zaidi, wote ukiwasikiliza kwa makini wanakiri kuwa nchi ipo kwenye hali tete kiuchumi ila wenyewe watakuja kutupeleka nchi ya ahadi huku wakisema kwa sasa Rushwa imezidii na watapambana nayo kwa vitendo, mikataba mibovu nitatizo, elimu mbovu, umasikini umezidiii, Ajira ni BOMUU, afya ni tatizo, hakuna uwajibikaji kwa watendaji na mengine mengi.

Sasa nadhani huu ndio wakati wa vijana wa leo tujiulize na CCM watueleze ni kipi kimewafanya 35 hadi sasa hawaongelei swala la watanzania kuwa kwenye hali bora na matokeo yake UMASIKI wetu umeendelea kuwa ndio ‘mtoko” kwa mara nyingine tena.

Au tuamni kuwa UMASIKINI wetu ndio mtaji wenu?
 
wakuu nimekuwa nikitafakar mara kwa mara badae nikagundua kuwa watz weng ni wapore na waoga wa kuhoji ndio maana hata leo tunashuhudia mafisad waki chukua form wagombee tena ingelkuwa sio upore wetu mpaka sasa tungelkuwa barabaran tukipinga kwa nguvu zote zarau hizi ambazo zinafanywa kupitia mgongo wa democracy
my take: nchi hii akipewa fisad watoto wetu watatuona mamburura maana hawatakuta hata chembe ya raslimali ambazo zipo.
ni hayo tu yakwangu
 
Uchaguzi wa Rais na wabunge ule unakuja umesha piga kona. Wanasiasa watia nia katika kugombea nafasi za ubunge sasa hivi hawalali.

Ni wakati wa vikao usiku na mchana kwa ajili ya kampeni za kupata ushindi.

Asilimia kubwa ya wapiga kura katika kila jimbo wana ufahamu mdogo sana juu ya nafasi ya ubunge na mchango wa maendeleo katika jimbo lao wanaloishi.

Vitu vidogo vidogo wa hongo kama vile unga, sukari, chumvi, viberiti, tshirt na kofia, pesa na pombe ukivitoa unaweza kujipatia kura kiurahisi sababu watu wanaweza kukukubali kama mwenzao, na pia usisahau uhadi za uongo.

Rushwa inabadili mfumo mzima wa upigaji kura toka kwenye vikao vya vyama hadi kwa wananchi.

Wengi wa watia nia sasa hivi wameshajitangazia kamati zao kwa ajili ya kupora ushindi aidha kwa njia ya haki au nyingine yeyote ile.

Mungu ibariki Tanzania
 
Back
Top Bottom