steveson manumbu
JF-Expert Member
- Apr 1, 2014
- 887
- 178
kabisaa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
kabisaa
Hebu tushauri nini kifanyike?Ndiyo mtaji mkubwa wa ccm
kabisaa
Bidii ya mtu mmoja mmoja humaliza matatizo yake binafsi, tunamaanisha kuwapa lishe bora, kuwapa elimu na maradhi bora watu wa familia husika... Elimu bora ni shule na vyuo bora...... shule na vyuo bora sio mali ya muhusika ila ni mali ya Serikali na taasisi fulani..... na ukumbuke huyu mtu hulipa kodi nyingi sana ili apatiwe zile huduma ambazo ni public kwa gharama nafuu na kwa misingi ya taifa husika ili lijengwe na watu husika. Kama huyu mtu anatakiwa ajibidiishe na afanye kila kitu mwenyewe basi hakuna haja ya kuwa na serikali wala watu kukatwa kodi kwani hapa kila mtu atajibidiisha mwenyewe na kuwa na serikali yake ili ajilinde, aiishi kwenye nyumba bora akiwa na solar yake au generator yake full time, huyu mtu atachimba kisima chake mwenyewe na kutreate maji yake kwa sulphur/mawe/shabu, huyu mtu atanunua gari la 4*4 ili apite kwenye barabara mbovu ( wazungu watatuletea tu magari na meli zao za michangani kwani tutakuwa hatuna bandari)... kama wanachukua kodi zetu na wanaweka kodi kwenye bidhaa na tunalipa, wanakusanya kodi kwenye viwanda na wanataka tujibidiishe ili tumudu zile public service ambazo ni makukumu yao basi wasichukuwe kodi zetu, kila kitu kisiwe na kodi na tusiwe na serikali ili kila mtu ajiongoze mwenyewe...
Mwananchi anamajukumu yake na Serikali ina majukumu yake,,, kazi ya mwananchi ni kufanya kazi, kulipa kodi na kuangalia familia yake na yeye mwenyewe.. kazi ya Serikali ni kutawala watu wote, kukusanya kodi na kuzifanyia kazi stahiki kwa maendeleo ya nchi,,, sasa kama unataka mwananchi kufanya kazi ya serikali mfano kujenga maabara basi haina haja ya kuwa na serikali....
Mwananchi anaweza kujibidiisha akawa na hela/utajiri na akalipa kodi lakini akiugua hospitali hazina madawa, shule hazitoi elimu bora na maeneo mengine hazipo, umeme hauwaki, barabara hazipitiki na maji hakuna sasa hapo nani atakuwa ameshindwa kazi SERIKALI /MWANANCHI...
DADA FAIZAFOX HAMNA NAMNA YAKUITOA CCM KATIKA UMASIKINI WA TANZANIA NA WATANZANIA KWA UJUMLA MAANA WANAKUSANYA KODI NYINGI KILA MAHALI,, MISAADA KWA WAHISANI, KODI KWENYE MADINI HALAFU WANASEMA WATU WAJIBIDIISHE WAKATI 85% YA KODI INATOKA KWA WANANCHI.....SASA SIJUI WANGEKUWA HAWAJIBIDIISHI HIYO KODI INGETOKA WAPI???
HIVI DADA UPO TANZANIA KWELI HAPA NA UNAONA YANAYOTOKEA PHYSICALLY AU UNAONGEA TU NA HUIJUI HALI HALISI YA HUKO NAMANYELE, ENDASAKI, ENDAGAW, UJIJI, MASUMBWE, KATORO, NK??
Dunia hii haitaishiwa na matatizo hata uletewe mtume mwingine na si kiongozi tu wa kawaida, ikiwa wewe mwenyewe unashindwa kujiongoza usitegemee kuwa kiongozi atakuja kukushika mkono akuongoze.
Hivi, kiongozi yupi kakuongoza vibaya na kwa lipi? maana tunaweza kubishana pengine kiongozi wako alikuja akakuongoza vibaya na sisi hatujuwi, tuanzie hapo.
Ugonjwa wa kupenda tiba yake lazima utendwe vibaya sana ndio waweza kushituka, wakati mwingine mapenzi hayo hutia ganzi kiasi kwamba usione wala usisikie. Naipenda TZ lakini siupendi utawala uliopo kwa upendo ulionao FaizaFoxy. Wewe umeamua kuweka pamba masikioni mwako na kuvaa miwani ya mbao. Kwamba huuoni uongonzi mbaya wa serikali yetu mpaka sasa. Just to name a few
1. Wizi wa fedha za uma (EPA, ESCROW, RADA n.k.) unazorotesha maendeleo.
2. Maamuzi hafifu yanapoteza rasilimali za nchi. Leo nimemsikia mh. Kafulila akielezea uamuzi wa serikali kujenga bandari ya kisasa Bagamoyo bila kufanya economic analysis yenye kuleta tija
3. Kushindwa kushughulikia uhalifu, waTZ wanauawawa kama kunguni
4. Mikataba yenye kunufaisha watu wachache (au wewe umo katika kundi hili) bila kujali maslahi ya wananchi
Hao mitume sio sehemu yao katika mjadala huu. Kubali kiungwana tubadilishe uongozi safari hii (hata kama atakaye ondoka ni mjomba wako), achana na mambo ya zimwi likujualo.
Hatua zinahusu nini?
Fanya bidii yako binafsi kushindana na yote hayo yatakuondokea. Unangoja mtu akuchukulie hatua kwa ujinga wako?
Nyie ndiyo mnawaponza wasiojuwa Kiswahili vizuri, wanaanza kupiga hatua kutoa Geita sijui wapi huko wanajuwa wakifika Ikulu kila kitu safi, wakaishia rumande.
Hizo zote ni porojo tulizoziwea kila siku, bado hujasema huo uongozi ulikuongoza vipi vibaya?
Tunajuwa mnalalama sana kwa kuwa huu uomgozi uliopo umewabana mbavu na hamna pakuhemea.
Huo mnaousema wizi mngeujuwa bila uongozi wa sasa kuushughulikia apaswavyo?, si mlikuwa mnajiibia mnavyopeda, sasa mmeminywa mbavu barabara na hamna mbinu isipokuwa kufanya "character assassination", lakini mbinu zenu zote hazijafuwa dafu na wala hazitafuwa dafu na mbavu mtaendelea kuminywa.
Na msifikiri huyo ataekuja baada ya Kikwete atawawachia au kuwapa mwanya tena, huyo ndiyo mtalalama zaidi ya leo.
Hizo zote ni porojo tulizoziwea kila siku, bado hujasema huo uongozi ulikuongoza vipi vibaya?
Tunajuwa mnalalama sana kwa kuwa huu uomgozi uliopo umewabana mbavu na hamna pakuhemea.
Huo mnaousema wizi mngeujuwa bila uongozi wa sasa kuushughulikia apaswavyo?, si mlikuwa mnajiibia mnavyopeda, sasa mmeminywa mbavu barabara na hamna mbinu isipokuwa kufanya "character assassination", lakini mbinu zenu zote hazijafuwa dafu na wala hazitafuwa dafu na mbavu mtaendelea kuminywa.
Na msifikiri huyo ataekuja baada ya Kikwete atawawachia au kuwapa mwanya tena, huyo ndiyo mtalalama zaidi ya leo.
Hatua zinahusu nini?
Fanya bidii yako binafsi kushindana na yote hayo yatakuondokea. Unangoja mtu akuchukulie hatua kwa ujinga wako?
Nyie ndiyo mnawaponza wasiojuwa Kiswahili vizuri, wanaanza kupiga hatua kutoa Geita sijui wapi huko wanajuwa wakifika Ikulu kila kitu safi, wakaishia rumande.
Bidii binafsi bila sera safi ni ngumu sana, mfano ni shule za kata bila walimu, vitabu, maabara, juhudi gani binafsi italeta first class?!
ESCROW ndio juhudi binafsi?!
Sometimes you must be impartial when you discuss issues which really matter!!!
Waalimu mpaka sasa tumeanza kuchukuwa wahitimu wa vyuo vikuu, uko wapi wewe? Kuna wakati Tanzania hii umewashika kuajiri walimu wengi kuliko sasa? Kina wakati kuna sekondari nyingi kuliko sasa? Kuna wakati shule imekuwa na maabara kuliko sasa? Vitabu? Wakati Kikwete anachukuwa nchi ilikuwa kitabu kimoja kwa wanafunzi 20 leo ni wawili na mwakani kila mtu na chake. Cheza na Kikwete wewe?
Reposted:
MWISHO WA KUCHAKACHUA NI SASA!
Zamani ilikuwa
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI!
IDUMU SIASA YA UJAMAA NA KUJITEGEMEA!
Sasa UKWELI ni
KIGUMU CHAMA CHA MAPINDUZI - KUACHANA na UFISADI
NI NGUMU FIKRA ZA MWENYEKITI - ZA kuwalinda mafisadi na bado CHAMA kipone.
Ni NGUMU SIASA ya unyama na kujitegea - Inayoendelea ( unyama - wapigwe tu!)
NI NGUMU SIASA YA UNYAMA NA KUJIMEGEA - Inayoendelea. ( bila kujali hali duni ZA wananchi)
KAMA TUNA AKILI TIMAMU NI VIGUMU CHAMA CHA MAPINDUZI KUVUKA MWAKA HUU.
Source ya unayoyasema ni hipi? Kaangalie BEST na UNESCO reports na jinsi trend ilivyo ndipo utakaposema vizuri. Haya tazama kwenye hii report Tanzania ilivyo http://www.uis.unesco.org/Education/Documents/africa-regional-education-data-presentation-en.pdf
Source yanini na kila kitu kiko wazi? huna macho, huna masikio? au ndiyo macho unayo lakini hayaoni, masikio unayo lakini hayasikii?
Wewe hata oresentation uliyoiweka huielewi maana yake, ikiwa ni mtihani na jinsi nilivyoiona hiyo presentation basi Tanzania imefaulu kwa sana tu. Kaitazame upya uielewe.
Dalili ya mvua mawingu. Juzi 80%.