Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
Hata hao wezi hawana Maisha bora.
tema mate chini .
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata hao wezi hawana Maisha bora.
Iko hivi.. Mlinzi tuliyempa dhamana ya kulinda mali zetu anashirikiana na wezi kutuibia.. CCM ndiyo impewa dhamana ya kulinda rasilimali zetu na kukusanya kodi na kutuletea maendeleo.. Sasa kwa kuwa iko dhahiri shahiri Mlinzi huyu anashikiriana na wezi kutuibia dawa ni moja tu.. Kumfukuza kazi na kumpeleka mahakamani..
TOA CCM MADARAKANI TANZANIA IPONE
Iko hivi.. Mlinzi tuliyempa dhamana ya kulinda mali zetu anashirikiana na wezi kutuibia.. CCM ndiyo impewa dhamana ya kulinda rasilimali zetu na kukusanya kodi na kutuletea maendeleo.. Sasa kwa kuwa iko dhahiri shahiri Mlinzi huyu anashikiriana na wezi kutuibia dawa ni moja tu.. Kumfukuza kazi na kumpeleka mahakamani..
TOA CCM MADARAKANI TANZANIA IPONE
Ndiyo mtaji mkubwa wa ccm
Ulishawahi kuona Mchagga anapewa kazi ya ulinzi?
Vipi kuhusu maazimio ya kamati kuu ya ccm.
Hatua zinahusu nini?
Fanya bidii yako binafsi kushindana na yote hayo yatakuondokea. Unangoja mtu akuchukulie hatua kwa ujinga wako?
Nyie ndiyo mnawaponza wasiojuwa Kiswahili vizuri, wanaanza kupiga hatua kutoa Geita sijui wapi huko wanajuwa wakifika Ikulu kila kitu safi, wakaishia rumande.
so sad!!!Mtaji wa ccm, nape aliwauliza watu tanga eti mnataka maji au katiba, wale watu wakajibu majiiiiii....! Mnataka barabara au katiba, wakajibu barabaraaa..! Umeme au katiba, umemeeee! Katiba itawasaidia nini nyie watu hakunaaaa.....! Kama si uenda wazimu ni nini?
so sad!!!
Nini kifanyike?
Nakubaliana na wewe FAIZA FOXY juu ya umuhimu ya juhudi binafsi. Lakini kama juhudi binafsi zinatosha viongozi wanachaguliwa kwa kazi gani? Siamini kuwa tunashabikia kuendelea kwa ujinga na umaskini na maradhi. Tatizo ni kubwa sana kama hata wanaowekeza kwenye ujinga na umaskini wetu tunawashabikia.
dawa ni kupiga chini ccm tu
tangu uanze ubaguzi umepata nini ?
​Nimesikitika sana kuona kuwa katika maadui wakuu wa tangu kale 1. Ujinga
2. Umaskini
3. Maradhi
Kwa WANASIASA wa leo hao ndio marafiki wao wakuu katika kutimiza agenda zao na uovu wao.
1. UJINGA.
Tunawekeza kwenye ujinga wa watu wetu. Kama sio ujinga wa watu wetu VIONGOZI wetu wasingethubutu kufanya na kusema tunayoyaona na kuyasikia. Hofu ya uelewa wa watu ingewaogopesha na kuwanyenyekesha. Huwezi kuona mahali duniani penye demokrasia ya kweli wananchi wakilazimishwa kufuata matakwa na vitisho vya watu wachache au kikundi cha watu wachache wanaoweza kubadilisha hata maamuzi ya wananchi. Huwezi kuona mahali ambapo Chombo cha wawakilishi wa wananchi kinafanyika mahali pa mipasho umbeya matusi bila hofu ya kuwajibishwa na waliokutuma.
Kila mahali ambapo elimu haikupewa kipaumbele tumeona ni mahali pazuri pa kupata UONGOZI hata kwa watu wasiokuwa waadilifu hawaogopi kwa kuwa wamewekeza kwenye ujinga wa watu.
Heshima kwa utawala wa sheria na uaminifu kwa KATIBA, KANUNI na taratibu zinapokiukwa bila heshima wala hofu ni ishara ya ujinga wetu.
2. UMASIKINI
Watu kwa umaskini wao wanarubuniwa kuuza utu wao na heshima yao. Wanalazimishwa na nguvu ya PESA kuwa wanafiki na kutokufuata dhamiri zao juu ya nani bora. Wakati wenzetu wengi wa nchi zilizoshinda masuala ya rushwa hutafuta pesa za kujitangaza na kueneza sera ili wakubalike sisi bado tunatafuta fedha za kuhonga watu wasiojua tunachoamini au kupanga kufanya. Badala ya kuunga mkono hoja wanaunga mkono aliyetoa pesa au kiasi cha pesa walichopokea bila kujali msimamo, UADILIFU na MISINGI anayosimamia mtoaji.
3. MARADHI
Haya yamegeuka kuwa mitaji ya wanasiasa wengi. Hatuboreshi lolote tunatumia maradhi ya watu wetu kuombea misaada bila kuwa na mpango wa DHATI toka moyoni wa kuyatokomeza.
UJINGA NA UMASKINI NA MARADHI NI MTAJI MKUU WA VIONGOZI WA KISIASA. Ni wakati wanasiasa waitendee HAKI dhamiri yao hata kama wataanguka kisiasa wakumbukwe kama Gorbashev na Fredrick De Clark waliofanya ya HAKI hata kama walikosa cheo.
HATUA GANI ZICHUKULIWE HAPA TANZANIA KUBADILISHA HALI HII.
Dunia hii haitaishiwa na matatizo hata uletewe mtume mwingine na si kiongozi tu wa kawaida, ikiwa wewe mwenyewe unashindwa kujiongoza usitegemee kuwa kiongozi atakuja kukushika mkono akuongeze.
Hivi, kiongozi kakuongoza vibaya na kwa lipi? maana tunaweza kubishana pengine kiongozi wako alikuja akakuongoza vibaya na sisi hatujuwi, tuanzie hapo.
Matatizo ya kutengeneza na ya kujitakia LAZIMA YAKOMESHWE!
Hatua zinahusu nini?
Fanya bidii yako binafsi kushindana na yote hayo yatakuondokea. Unangoja mtu akuchukulie hatua kwa ujinga wako?
Nyie ndiyo mnawaponza wasiojuwa Kiswahili vizuri, wanaanza kupiga hatua kutoa Geita sijui wapi huko wanajuwa wakifika Ikulu kila kitu safi, wakaishia rumande.