Ujue Mtazamo wa maombi kwa mkristo ambao utakufanya uwe mchapakazi na mtu wa vitendo vingi

Ujue Mtazamo wa maombi kwa mkristo ambao utakufanya uwe mchapakazi na mtu wa vitendo vingi

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Isaya 65:24
Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu;

Sio kila kitu unatakiwa kuomba. Vingi unatakiwa kuamini unavyo, hivyo unaanza kutenda kwa msingi kuwa kabla hujaviomba Mungu ameshakujibu tayari.

Kwa hiyo, mfano ukitaka nyumba, badala ya kukesha na kufunga anza kuhulizia bei ya materials, fanya windowshopping, anza kuangalia gari linafikaje site bila kujali unahela au huna. Kimsingi anza mitachakato ya ujenzi sio kuomba. Anza vitendo vingi kwa kidogo ulichonacho ukiamini kabla hujaviomba umeshapewa. Mungu ataunga mkono jihudi zako kwa imani hii.

Hii itakufanya upunguze maombi ya kuombaomba vitu, huo muda uutumie kutenda, kufanya michakato, kukutana na watu sahihi, ili umpe nafasi Mungu kutekeleza kauli yake hii ya isaya.

Mtu mwenye uelewa huu maombi yake hata kama ni siku nzima ni kama kupiga story na Mungu, kufanya ushirika na Mwenyezi sio kulialia, kupiga misamba na kugaragara kama mwehu.

Mungu qkupe neema ya maisha ya mtu ambaye anaamini kabla hajaomba ameshajibiwa, hivyo utatenda kisha utashukuru. Maisha yako yajae na kuzungukwa na vitendo zaidi nq mqombi ya kushukuru pamojq na dua za ushirika na Mungu wako.

Hautakuwa mtu wa kawaida.
Barikiwa

Mtumishi Matunduizi
 
upo vizurii mtumishii mazee...neno liko sambamba na litasimamaa, makobaz yatabisha na kushuka humu na mitusi na uharo wao ila ndio basii...yapigwe tuu
 
Isaya 65:24
Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu;

Sio kila kitu unatakiwa kuomba. Vingi unatakiwa kuamini unavyo, hivyo unaanza kutenda kwa msingi kuwa kabla hujaviomba Mungu ameshakujibu tayari.

Kwa hiyo, mfano ukitaka nyumba, badala ya kukesha na kufunga anza kuhulizia bei ya materials, fanya windowshopping, anza kuangalia gari linafikaje site bila kujali unahela au huna. Kimsingi anza mitachakato ya ujenzi sio kuomba. Anza vitendo vingi kwa kidogo ulichonacho ukiamini kabla hujaviomba umeshapewa. Mungu ataunga mkono jihudi zako kwa imani hii.

Hii itakufanya upunguze maombi ya kuombaomba vitu, huo muda uutumie kutenda, kufanya michakato, kukutana na watu sahihi, ili umpe nafasi Mungu kutekeleza kauli yake hii ya isaya.

Mtu mwenye uelewa huu maombi yake hata kama ni siku nzima ni kama kupiga story na Mungu, kufanya ushirika na Mwenyezi sio kulialia, kupiga misamba na kugaragara kama mwehu.

Mungu qkupe neema ya maisha ya mtu ambaye anaamini kabla hajaomba ameshajibiwa, hivyo utatenda kisha utashukuru. Maisha yako yajae na kuzungukwa na vitendo zaidi nq mqombi ya kushukuru pamojq na dua za ushirika na Mungu wako.

Hautakuwa mtu wa kawaida.
Barikiwa

Mtumishi Matunduizi
Amen
 
mtazamo huu utakufanya uonekane muda mwingi sokoni ( market plqce) au kwenye industry yako badala ya kujifungia ndani au kujificha makanisani. Maana utaamini unapata kwa kutenda sio kuomba. Maana kabla hujakiomba kicho kitu tayari Mungu ameshakujibu. Tena wakati mwingine uombe ukiwa humohumo kwenye michakato.

Mtazamo wa kuomba ndio utende utakufanya uwe mvivu.
 
upo vizurii mtumishii mazee...neno liko sambamba na litasimamaa, makobaz yatabisha na kushuka humu na mitusi na uharo wao ila ndio basii...yapigwe tuu
Amina amina. Wale ni watu wema tu.
Wenye matusi huwa wanatumiwa na kale kamjamaa (adui) ili kuondoa utulivu na usikivu.
 
Back
Top Bottom