Ujumbe kwa Waziri Ndugulile: Vibao vya anuani za makazi sasa liwe zoezi la lazima

Ujumbe kwa Waziri Ndugulile: Vibao vya anuani za makazi sasa liwe zoezi la lazima

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Waziri Ndugulile najua umechukua hii Wizara hivi karibuni. Baada ya kusimamia suala la vifurushi vizuri; nashauri sasa ugeukie Vibao vya Anuani za Makazi ili tuwe na mfumo rasmi wa utambuzi wa Makazi na zoezi hili liwe la lazima na liwe na vibao vya udongo inavyofanana kote nchini ili tuwe na utaratibu rasmi wa utambuzi wa makazi.

Katika hili nashauri majina ya mitaa utaratibu uwe ni makubaliano ya serikali ya mtaa kuhusu majina ya mitaa badala ya watu wachache kujimilikisha majina ya mitaa.

Aidha barabara za mitaani zilizowekwa mageti ya machuma kuzuia watu kupita huko yaondolewe kwa kuwa barabara sio mali ya watu binafsi wa mtaa huo ni mali ya umma.

Nawasilisha.

EvIa79uWYAESwcn.jpg
 
APP-B-2T.jpg

Cheki vitu vinavopendeza. Nasi tupendezeshe miji na vijiji vyetu yetu; tuwe wa kisasa. Mtu akikutumia mzigo kuufikisha issue. Vibaka wanapora watu sababu ya kuuliza uliza eti mtaa wa nani ni wapi!!
 
JPEG. NA. 1 (5).JPG
Zoezi hili walishawahi kulifanya TCRA kwa kushirikiana na serikali za mitaa lakini liliishia njiani...Liendelee kote nchini ili mambo yawe bul bul.
 
tiba.JPG

Ndugu waziri haya ndio Mawasiliano yenyewe. Hii kazi zamu hii ungewapa Posta washirikiane na TCRA kuhakikisha nchi nzima kunakuwa na anuani za makazi na mitaa. Ikiwezekana na jina la Mtaa liwepo kabisa.
 
Ila italeta shida kama vitaandikwa hivi Mtaa wa Gambia angalau waandike kama hiyo post yako ya 3 yaani "Kisarawe road" au Barabara ya Mchina" maana wakiweka jina la mtaa wa Gambia italeta mgongano na mgawanyo wa maeneo ya serikali za mtaa (jiji, manispaa na miji) kwa kuwa kila Kata inakuwa ina Mitaa kadhaa na kila mtaa unakuta una barabara kadhaa.

Nimeona kuna kuchanganyana hapa anauani ya makazi inakuonyesha unakaa Mtaa wa Gambia wakati eneo unaloishi kiutawala ni Mtaa wa Manzese ambapo kwenye mtaa huo huo wa Manzese unakuta kuna barabara imeandikwa mtaa Sudani.

Ili wasichanganye ilitakiwa kuna mtaa wa Manzese kwa mujibu wa mipaka ya Manispaa alafu hizo barabara zinazotambulisha anuani ya makazi zingeandikwa Barabara ya Gambia / Gambia way / Gambia road ili mtu anapojitambulisha anasema anakaa Kata Flani, Mtaa wa Manzese na Gambia road inakuwa rahisi
 
Ila italeta shida kama vitaandikwa hivi Mtaa wa Gambia angalau waandike kama hiyo post yako ya 3 yaani "Kisarawe road" au Barabara ya Mchina" maana wakiweka jina la mtaa wa Gambia italeta mgongano na mgawanyo wa maeneo ya serikali za mtaa (jiji, manispaa na miji) kwa kuwa kila Kata inakuwa ina Mitaa kadhaa na kila mtaa unakuta una barabara kadhaa...
Sahihi kabisa mwanabodi. Nashauri serikali za mitaa zihusishwe sana kwenye kupanga majina ya hiyo mitaa ili huu mkanganyiko usijitokeze.
 
Sahihi kabisa mwanabodi. Nashauri serikali za mitaa zihusishwe sana kwenye kupanga majina ya hiyo mitaa ili huu mkanganyiko usijitokeze.
Itakuwa poa aisee maana nimeshaona kwa baadhi ya maeneo kuna mitaa mingi inakinzana na ile ya halmashauri kumbe wakikaa pamoja itakuwa rahisi maana watendaji wa kata na mtaa ni kiungo muhimu kwa utendaji wa kazi za serikali
 
Itakuwa poa aisee maana nimeshaona kwa baadhi ya maeneo kuna mitaa mingi inakinzana na ile ya halmashauri kumbe wakikaa pamoja itakuwa rahisi maana watendaji wa kata na mtaa ni kiungo muhimu kwa utendaji wa kazi za serikali
Tatizo kuna mitaa watu binafsi ndio wanaibatiza majina kutokana na ushawishi wao kv umaarufu. Kazi ya kuipa mitaa majina waachie serikali
 
Bado tuko nyuma sana, yaani leo 17.3.2021 tunafikiria kuwa na majina ya mitaa na namba? Tumechelewa sana.
 
Back
Top Bottom