Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Wakuu vipi mahojiano na TRA? tulikuwa tunayasubiri kwa hamu? au mmenunuliwa?
 
Hii ni taarifa ya habari ya KLH NEWS!

Mchaga mmoja ambaye ni mwenyekiti wa taifa wa chama cha (Chagga development manifesto) au chadema kwa kifupi chake. amefeli mitihani miwili kati ya minne ya semister ya kwanza tu huku akiwa kafanyiwa course work zake.

tuliambiwa watu wa kilimanjaro kwa sababu za kihistoria ni watu waliokwenda shule na wana mapenzi ya shule.KULIKONI?

kwa habari zaidi tumsubiri Mwanakjj amuhoji ilikuwaje mwenyekiti kula za uso?
 
Bigotry = mtu anayeng'ang'ania imani yake kupita kiasi.

Nafikiri wamo humu watu wanaoonyesha waziwazi kwamba hoja zao ni za Chuki za KIKABILA. Leo itakuwa Wachaga, kesho Wapemba na Wakinga (wahangaikaji wazuri) .....

Hoja za aina hii zinapoteza nafasi ya kujadili masuala ya maana ya nchi yetu. Ambayo yako mengi. Ili kulinda hilo nafikiri ni wajibu wa Moderators ku-discourage hoja za aina hiyo na kidogokidogo kuelekeza fikra na muda wa wachangiaji kwenye mada za maana. Pamoja na kwamba watu wana uhuru wa kuchangia, hoja zinazolenga kujaribu kuwashawishi watu wachukie makabila fulani kwa sababu zisizo za kweli, just because you happen to hate the tribe, haziwezi kuwa nzuri.

Watanzania bado hawaoni mtu aliyeendelea kama mfano mzuri wa kuigwa. kufuatana na baadhi ya michango mingine ninayoiona humu. Its like a knee jack reaction, chuki badala ya admiration. Nafikiri tumelelewa vibaya na ni wajibu wetu kutoka huko haraka.

Kwa sababu CHUKI ni Barrier kubwa sana ya Maendeleo. Ukishamchukia mtu au watu basi unakuwa umejipunguzia nafasi moja ya kushirikiana naye/nao katika shughuli za maendeleo. Huwezi kufanya huwezi kufanya nao kazi tena hata kama kazi hiyo ni ya kukusaidia wewe.

I don't think we should get that low!

The haters should seek to reverse the roles, wafanye juhudi ya kuwapita hao wachaga ili baadaye haters watakajitokeza (hawakosekani) wawajadili wao wakiwa juu.
 
mtukwao,

maneno mazito hayo... ndugu zetu humu hawataki kukubali kuwa wanaongozwa na ukabila. Wakati wanadai kuna ukabila TRA , ukabila wao wenyewe unawekwa hadharani. Wanapopandikiza mbegu za kuwachukia wachagga, wakati huo huo wanarutubisha chuki ya kikabila ndani yao wenyewe. Leo hii tukisikia kiongozi mchagga amepewa nafasi basi tunajiuliza "kwanini Mchagga?"

Dhambi hii ya ukabila haikomi! Imeanzia kwa wachagga itaenda kwa Wahaya, Wanyakyusa, Wangoni (wa kunyumba) na ni kama mtu kula nyama ya binadamu! Ni mwiko mkubwa ambao ukishauvunja ni vigumu kujikomesha. Ndugu zetu hapa wanajifanya wanasukumwa na uzalendo! kumbe kinachowasukuma ni wivu usio na msingi na chuki isiyokaribishwa! Hawa ndugu tukiwapa nafasi wachague watu kwenye nafasi fulani, la kwanza watakalojiambia ni "wachagga, wahaya, wanyakyusa" hapana!! Wakiona jina la makabila hayo watayakwepa!

Bado tunaendelea kuwapinga, kuwakosoa, na kuwaonesha makosa yao! ili hatimaye wajirudi!
 
watetezi wa ukabila hawataki kunipa contacts zao! I'll be forced to cancel it.. maana nimewaomba wazee wa watu wakakubali kuja kuzungumzia hoja baada ya hoja..! lakini watetezi wa ukabila wanagwaya!
 
watetezi wa ukabila hawataki kunipa contacts zao! I'll be forced to cancel it.. maana nimewaomba wazee wa watu wakakubali kuja kuzungumzia hoja baada ya hoja..! lakini watetezi wa ukabila wanagwaya!
Nani na nani hawataki kutoa Contacts zao! Ni wangapi wamekubali kushiriki huo mjadala?tafadhali usiweke tamati au kuufuta nipe muda nitakuja na wazo jipya soon!
 
hadi hivi sasa. ni watu wa TRA tu ambao wako tayari kuzungumza...! wapiga kelele za "ukabila" wao wapo tu
 
hadi hivi sasa. ni watu wa TRA tu ambao wako tayari kuzungumza...! wapiga kelele za "ukabila" wao wapo tu
Ushauri wangu Usifute mahojiano kuna yale ambayo yaliletwa humu kama evidence ya kuwepo kwa ukabila kwanini tusiyachukue na kuyajengea maswali na ukawauliza hao wahusika na tukamaliza na hili?Na kama kuna wenye data zaidi za TRA waziweke hapa ili tuziunganishe na tuzijengee maswali na maswali yatajengeka katika msingi wa kuna wa dhana katika kuuliza.Kwani wenye uhakika wa data hizo hawataki kuzitetea. Je unaonaje kuhusu hili?
 
nimechukua maswali na hoja zote zilizotelewa na jamaa wako tayari kuzungumza kesi moja baada ya nyingine... lakini wanataka wale wanaodai ukabila kushirikishwa kuzungumza nao..
 
Mwanakijiji,
chukua tuhuma zilizojengwa hapa jamboforums na uzijengee maswali.
 
I can understand why inakuwa tabu kwa 'wapiga kelele wa ukabila' kutoa contacts zao. Unlike the TRA guys, these JF members need to maintain their anonymity kama wanavyotumia nick names hapa, kwa hiyo hawataki sauti zao zisikike humo redioni!

Labda Mkjiji awapatie namna nyingine ya wao kushiriki bila sauti zao kusikika. Ukisema watume maswali live via MSN or something .. utawapata tele!
 
duh.. Kulikoni hawajasema hilo.. tatizo ni kuwa mimi nikizungumza na watu wa TRA peke yake watetezi wa ukabila watasema niko biased kwa vile msimamo wangu unajulikana wazi. Ndio maana nataka wao ndio washindane kwa hoja na watu hao wa TRA. Nitahakikisha kuwa identity zao zinalindwa.
 
Nakubaliana na jamaa wa TRA ni vizuri pande zote ziwepo.

Ndio hilo tatizo la ujasiri! Watu wenye data hizi kule TRA wajitokeze. Mimi sioni tatizo kama madai yako sio uzushi! Kama mtu ana statistics credible za ukabila pale TRA anipe mimi nitajitolea kwenye kwenye hayo mahojiano tena kwa jina langu halisi. Kwa mfano, mwenye data zinazoonesha kuwa wengi wa wafanyakazi katika idara za kitaalamu na za kawaida katika TRA ni kutoka kabila moja anitumie mimi. Fanya an up-to-day breakdown vizuri, idara kwa idara na idadi ya wafanyakazi kwa kila idara. Tukishindwa hili, basi sisi ni wazushi, hatuna chochote na tunyamaze milele na hii mada ipelekwe kwenye kalabrasha la udaku!
 
Unajua tangia mwanzoni nilisema watu waache kutumia sababu binafsi kujengea "Nadharia za matatizo hata kama hayo matatizo hayapo"
Ni kawaida ya watanzania kutengeneza mazingira ya chuki, wivu, pale kwa watu au kundi la watu tusiowapenda au tulioshindwa kufikia kiwango chao.
Mifano ni mingi hapa JF na hata nje ya hapa.

Mfano tangia kule BCS na hata hapa JF watu wamekuwa wakisema Reginald Mengi anakwepa kodi na anadaiwa zaidi ya bilioni 5 kwa kodi ambayo hajalipa na kesi tayari imeshapelekwa Mahakama ya Biashara. Watu tulipouliza tuliambia kuna ushahid mwingi tu na tukaee mkao wa kula kwani kesi itaanza kunguruma, lakini cha kushangaza ni karibia miaka mitatu sasa hatujaona huo ushahidi siyo hapa tu hata mahakamani. Watu wanabakia kusema anatumia jina la Walemavu kuingiza mali zake binafsi, mara kaangiza benzi kwa kuzingizia ni la walemavu. Mtu mwenye akili timamu hawezi kusema kitu kama hicho, jamani tangia lini Mlemavu akaendesha Benzi sembuse baiskeli ya kusukuma.

Hata serikali hutumia nadharia pale inapoona mambo ya wapinzania ni bora kuliko yao. Chukulia mfano, serikali ya CCM inavyowaambia wananchi kuwa tuchagueni kwani wapinzani hawapendi au hawawezi kuleta maendeleo na hata hudhiriki kusema angalieni sehemu zinazoongozwa na madiwani na wabunge wa vyama vya upinzani yalivyo nyuma kimaendeleo, lakini wakibanwa hawana mfano.

Kuna wakati kuna mtu aliwahi pia kulalamika mbona madaktari na Manesi wengi waliosajiliwa ni kutoka Mikoa ya Kaskazini, nadhani aliyekuwa waziri wa Afya kipindi hicho aliwaambia katembelee huo mkoa utaona wana college ngapi za kusomea unesi kwani kila hospitali ina kituo cha kufundishia, na madaktari wengi tulio nao ni wale waliosomea kwenye vituo kama hivi na kuwa medical officer na baadaye kwenda kuongeza elimu hadi kupata hadhi ya Daktari kamili.

Binafsi siungi mkono upande wo wote ule kwa sasa ila ninataka watu wakilete kero basi wawe tayari kutetea kero zao mpaka mwisho na siyo maswala ya kuishia njiani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…