Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Mmh ...long time naona JF imekuwa kama "kijiweni".... admin tunaenda wapi na hii discussion style?
 
inaoekana mshauri mkuu wa mswahili ni mwanakjj. sasa mbona maandishi ya mwanakjj kwa mswahili hayapo? kuna sehemu tena inasema NASUBIRI JIBU LAKO NA NAOMBA USHAURI WAKO. sasa kama mswahili ana njama na wachagga basi mastermind ni mwanakjj unlesssa alete mawasiliano yao yote, vingenevyo inawezekama mwanakjj umezidiwa line kwenye deals zetu umeamua kum black mail mswahili.

Inawezekana ikawa wanajuana maana sielewi kwa nini PM zinamwagwa kwenye PUBLIC DOMAIN ili hali ilikumwa kwa Faragha
 
Mmh ...long time naona JF imekuwa kama "kijiweni".... admin tunaenda wapi na hii discussion style?

Hapana, jambo moja hili haliwezi kuharibu credibility ya forum. Forum ipo palepale, ila hii thread sasa ifungwe ili watu wapumzike kidogo, maana naona mapovu yanawatoka!

By the way, baadaye mwaka huu naenda TZ, pamoja na mambo mengine, nimejipa kibarua cha kuchunguza vya kutosha juu ya madai ya ukabila TRA na makampuni mengine halafu nitaimwaga report hapa neno kwa neno na takwimu kwa takwimu ila tumalize huu ubishi.
 
nnaunga hoja, kuwa kwa sasa hii thread ifungwe tupumue, kabla hatujafika pabaya sana.
mengi tayari tushayazungumza
 
Siifungi bali naisimamisha kwa muda. Inahamia kwenye kabrasha ambako kuchangia si rahisi. In case kuna cha kuongeza just send me a private message and I will return it.

Kumradhi kwa ambao hawatapendezwa na maamuzi haya!
 
Nimeshangazwa na utaratibu uliotumika kufuta mada ya ukabila ofisi mbalimbali.

jana mwanakijiji alisema kajitoa kwenye mjadala na sisi tukamwambie tunaendelea na kazi. ghafla leo mjadala umefutwa.

last week kulikuwa na mada ya Said Yakub na Mwanakijiji alileta hoja baada ya kumshinda kwa hoja thread ikafutwa.

na jana alisema amejitoa baada ya kuleta hoja zisizo na mashiko na nilimbana kila pembe, leo imefutwa.

Admin.

Tunajua baadhi ya watu humu ni Moderators sasa usitoe nafasi mtu akishindwa basi afute thread.

Naomba majibu nini kimepelekea thread ile ifutwe? kwanini tusiambiwe kabla?
au kuna wanabodi wenye nguvu kuliko wenzao humu? thread ile ilikuwa page 111 hadi jana na watu walikuwa wanafika elfu 19.

Admin.
sisi tunatumia resources kuweka vitu humu si busara mtu akishindwa hoja aifute.



Naam Mswahili, here you go!

Wakti naandika yaliyo juu huenda HUKUSOMA! Naomba ingia deep kwenye topic hii uchambue ofisi nyinginezo mkuu maana umeshatoa data za kutosha on TRA na wenye masikio na macho wamesikia na kusoma. Mbona hugusi Ikulu kuna nini? Kwingineko?

Itapendeza zaidi kuliko kuzodoana na kurushiana madongo badala ya kukata issues. Kweli; tunahitaji kujua ofisi nyinginezo zilizotajwa zinahusikaje na UKABILA ambao ni ugonjwa mbaya. Sioni sababu ya kufungua topics za kuandama Admin au Moderators.

Thanks

Invisible
 
Naam Mswahili, here you go!

Wakti naandika yaliyo juu huenda HUKUSOMA! Naomba ingia deep kwenye topic hii uchambue ofisi nyinginezo mkuu maana umeshatoa data za kutosha on TRA na wenye masikio na macho wamesikia na kusoma. Mbona hugusi Ikulu kuna nini? Kwingineko?

Itapendeza zaidi kuliko kuzodoana na kurushiana madongo badala ya kukata issues. Kweli; tunahitaji kujua ofisi nyinginezo zilizotajwa zinahusikaje na UKABILA ambao ni ugonjwa mbaya. Sioni sababu ya kufungua topics za kuandama Admin au Moderators.

Thanks

Invisible
Haya hamieni kwengineko wenye data.
 
kama tumeamua kuelekea sehemu nyengine ni vizuri yaliopita yeshapita, mzee mkjj na mswahili tuyaache tukate issue.

pia nnawashukuru mamoderators kwa kuweka wazi panapotatiza.

tukate issue tuna hamu ya kujua mengi kuhusu nchi yetu na kuchangia pale tutapokuwa na la kuchangia.

ila tujitahidini kutoweka chuki na hasira mbele tujitahidini tusiwe biased, na mamoderators jitahidini kuongeza subira kwani nnaamini kazi ni nzito na nyie ni binaadamu kwa hiyo tuzidi kuvumiliana.

ila msiogope mtu akifanya faulu kuonywa au kuadhibiwa, ila busara pana zifate mlomlongo wake( kama za spika(jokes))
 
Naam Mswahili, here you go!

Wakti naandika yaliyo juu huenda HUKUSOMA! Naomba ingia deep kwenye topic hii uchambue ofisi nyinginezo mkuu maana umeshatoa data za kutosha on TRA na wenye masikio na macho wamesikia na kusoma. Mbona hugusi Ikulu kuna nini? Kwingineko?

Itapendeza zaidi kuliko kuzodoana na kurushiana madongo badala ya kukata issues. Kweli; tunahitaji kujua ofisi nyinginezo zilizotajwa zinahusikaje na UKABILA ambao ni ugonjwa mbaya. Sioni sababu ya kufungua topics za kuandama Admin au Moderators.

Thanks

Invisible

usiyeonekana,

kwanza,pongezi kwa kuwa mtu mwenye hikma,busara na mvumilivu.....ningekuwa mimi...ningeshatoa onyo kitambo!na kama ukaidi ungendelea...ningetoa sababu,omba radhi...na kuifunga hii mada!.

pili,ningeifunga kwa sababu imeshaonekana kuwa kinachojadiliwa ni chuki,hisia,ushabiki,labda ukabila,labda udini...na mengineyo ambayo hayaleti mwanga wa kuichambua hoja,bali yanagombanisha watu humu....ni kama wamepewa virungu watiane ngeu.

tatu,kuna watu wamewasilisha baadhi ya data juu ya hii mada,lakini inaonekana aidha zimepuuzwa[kwa maana ya kuamsha uchunguzi wa nyingine au la]au hazikuwa na msaada kwa malengo yaliyokusudiwa juu ya hii mada[kwa maana yake halisi na si tuliyoaminishwa].

nne,yanaongewa maneno ambayo kama unatumia busara za kumwelewa mtu,utasema ameshikwa na hasira,anatania,ana utani na mtu,au agh!....lakini inatia shaka...kwani yanajirudia na yanazidi kuwa makali!.

tano,nikapata kujiuliza...kuna watu wako ulaya,sivyo?,...let say ujerumani...skin heads wanawajua?...hivi wanajisikiaje wakiwaona wako kundi mbele yao?. nikajiuliza...hivi...unapokaa kwenye kiti[bus au train]halafu ukainuka kushuka,mzungu akapapangusa kwanza kabla ya kukaa,unajisikiaje?. na maswali mengine mengi!.....

sita,kuna sehemu nshasema tu watu wa fitna siye waswahili!....na ndo maana hatutoendelea kamwe!....wageni watachukua vyetu mpaka kiyama,nasi tutaishi kwao au kufanya kazi kwao tena za hovyo...mpaka kiyama!.kisa ni fitna!

saba,nloyasema yanatosha!kila mtu anayo yake macho na wake uelewa! tumesoma humu vitu vingi,tutachambua wenyewe ndani ya akili zetu na kuikosoa mioyo yetu!.

usiyeonekana!...walaakhi hamna jipya litakaloibuka!...kwasababu halipo! muda utaonyesha hivyo...na majadiliano ndio yatathibitisha!
 
tano,nikapata kujiuliza...kuna watu wako ulaya,sivyo?,...let say ujerumani...skin heads wanawajua?...hivi wanajisikiaje wakiwaona wako kundi mbele yao?. nikajiuliza...hivi...unapokaa kwenye kiti[bus au train]halafu ukainuka kushuka,mzungu akapapangusa kwanza kabla ya kukaa,unajisikiaje?. na maswali mengine mengi!.....

sita,kuna sehemu nshasema tu watu wa fitna siye waswahili!....na ndo maana hatutoendelea kamwe!....wageni watachukua vyetu mpaka kiyama,nasi tutaishi kwao au kufanya kazi kwao tena za hovyo...mpaka kiyama!.kisa ni fitna!

usiyeonekana!...walaakhi hamna jipya litakaloibuka!...kwasababu halipo! muda utaonyesha hivyo...na majadiliano ndio yatathibitisha!



Nakuunga mkono katika haya niliyowakilisha. Ama kweli Dar si Lamu! Ukifuatilia hoja nyingi katika topiki hii ni indirect kicks [faulo] zinazohitaji mtu ajishike maeneo hatari kama uso na kwingineko asiumizwe.

Management ya watu mtandaoni ngumu sana na kujua dhamira ya aandikacho mtu ni kugumu sana. Zaidi unaambulia kushambuliwa kwa maamuzi hata kama kuna sheria. Kuna member anasema "Tunahitaji kiongozi gaidi mwenye visheni" nadhani hajakosea. Kwa namna watu wanavyochangia humu huwa maandishi mengine natamani niyachomoe na kumwita aloyaandika anieleweshe uso kwa uso anamaanisha nini. Sifai kuwa moderator mie!

Kingine kinachoshangaza ni kuona kabila moja tu ndilo limeshikiwa kidedea as if Tz ni ya kabila moja. Kwa uelewa wangu mwembamba saaana kila mtanzania/mwanadamu ana chembe kiduuuchu ya ukabila/kupendelea japo wengine hujikuta ni za kurithi. Kama naongopa jisute mwenyewe mara ngapi umependelea mtu flani kwakuwa wamjua (ndo ukabila mwenyewe na si lazima wote muwe wachagga/wakurya n.k).

Kinachotakiwa hapa ni kuainisha bayana maeneo yenye kukithiri ukabila na kutoa data ambazo zinaweza kuwasaidia wahusika na watanzania wote kutafuta namna ya kutatua tatizo. Kweli, TRA kulilalamikiwa siku nyingi kuwa na wachagga wengi, lakini asili yao ni hela hawa wanapenda sana kushika (hata kama si zao); na Chuo Kikuu wengi walikuwa wahaya (enzi hizo) nako ilikuwa sababu ya u-nshomile wao (maybe) ingawa kwa sasa Mkoa wa Mara umechukua nafasi kubwa kwa kuwa na uwingi wa wanafunzi vyuo vikuu vya Tanzania.

Napenda hoja zinazoruhusu watu kujirekebisha kuliko hoja za watu kujisikia wenye kudharauliwa hivyo kuwaongeza kibri! Na maamuzi ya wizara flani imejaa kabila flani hivyo tujaribu kuiweka sawa yaendane na elimu za wahusika na si kuwatendea visivyo walioingia kwa haki japo wa kabila lile ama hili.

Mfano mdogo ni huu:-

Kuna kanisa moja hapa Tanzania nadhani laitwa Morovian kama sijakosea; hawa ukifika kanisani ni kinyakyusa mtindo mmoja! Hawana cha kuwa Dar ama kuwa wapi! It's as if ni la wao tu. Kuna ofisi moja kubwa sana ya masuala yetu ya usalama; hapo ni kikurya asilimia kubwa sana. Haya ndiyo mambo ya kujaribu kuyachambua na kuangalia suluhisho lake.

Kumwandama flani kwakuwa wajua yeye kabila flani sidhani kama ni suluhu na inatoa mwanga kwa wasomaji wetu, ingependeza sana tukajaribu kutafuta suluhu ya kila tunakoona pamekithiri kwa kuajiri kabila flani kwa wingi na kuacha makabila mengine yenye qualifications zilezile.

Ukinyimwa kazi TRA isiwe sababu ya kuona kuwa kwakuwa wewe si mchagga. Hata mimi niliomba nikakosa, sidhani kama jina langu linaonesha uchagga au ujita!

Ni hayo tu kwa leo
 
mwanasiasa,
utakapomaliza kuchunguza TRA, hebu fanya kama umepotea kuchunguza na jeshini mambo yakoje. we have had as many CDFs from Mara, the same way we have had Commisioners of Customs/Tax from Kilimanjaro, or the "North."

kunahali ya watu kushika pua, na kuonea kinyaa, mahali[taasisi] iliyo na kiongozi mchaga, au inayohisiwa kuwa na wachaga wengi.

huu mjadala wa TRA unanitia wasiwasi, kwasababu kwa maoni yangu, yako maeneo[taasisi] yalipaswa kuchunguzwa[kutokana na wingi watu wa eneo moja] kabla ya TRA.

Ukabila siyo kuwa na idadi ya watu wa eneo fulani ktk maidara/taasisi. Ukabila ni hali ya kabila moja kuchukia, na kujitenga na makabila mengine. Ukabila ni hali ya kupania/kunuia/kuazimia kutokutoa ushirikiano kwa makabila mengine kwa namna na hali yoyote ile.

Kuna watu wanasema wana wachumba wakichaga. Wengine wanasema wana marafiki wa Kichaga. Sasa kama Wachaga wangekuwa na ukabila basi kuchumbia Uchagani ingekuwa kazi kubwa sana.

Jamani, Tanzania haina huo ukabila anaoupigia kelele mswahili. Lugha iliyokuwa ikitumiwa na baadhi ya wachangiaji humu ndani haikustahili kabisa kutoka kwenye vinywa vya Watanzania.


Dar Si Lamu,
Nashukuru kwamba umeliona suala la kupuuzia ushahidi ambao baadhi yetu tumejaribu kuuleta hapa.

Nimejaribu mara kadhaa kuleta ushahidi kwamba madai ya kuwa Waziri Mramba anahujumu barabara za kusini hayana uzito.

1.How long has Mramba served as the Minister of Infrastructure?

2.Barabara za kusini ujenzi wake umezorota tangu Rashidi Kawawa akiwa Waziri Mkuu. Edgar Maokola Majogo, naye alikuwa naibu waziri pale wakati wa Kiula. Anna Abdalah naye alikuwa Waziri for 5 solid years. Wakati wote huo hatukulalamikia Wachaga, mpaka alipotokea Mramba aliye-serve miezi kadhaa.

3.Mradi wa barabara ya jimboni kwa Mramba, ulianza wakati Waziri Magufuli akiwa wizara ya Ujenzi.

4.Taarifa za bajeti zinalingana na taarifa za Tanroads. Mradi wa barabara ya jimboni kwa Mramba uko katika hatua ya ujenzi, na ule aliokuwa akilalamikia mbunge uko katika hatua ya designs/fisibility study not sure which one.

TWO OFFICIAL SOURCES SEEM TO INDICATE NO WRONG DOING BY Min Mramba. Pamoja na hayo yote kwanini wanachama wana JF wanaendelea kumsakama? Na kwanini ashupaliwe kwa suala hili tu? Mbona zipo kashfa nyingine kubwa kubwa zinazomhusu Mramba? Au ni kwasabu kashfa hizo hazita-prove ukabila tunaojaribu kuulazimisha hapa?
 
You are right jokaKuu by this statement!

Ukabila siyo kuwa na idadi ya watu wa eneo fulani ktk maidara/taasisi. Ukabila ni hali ya kabila moja kuchukia, na kujitenga na makabila mengine. Ukabila ni hali ya kupania/kunuia/kuazimia kutokutoa ushirikiano kwa makabila mengine kwa namna na hali yoyote ile.


Na kuna wanaojadili hoja hii kikabila pia. You can easily trace em up!
 
WOrM,
No wonder you are holding a flashlight. I like your last sentence: you can easily trace em up!
 
Mtu yeyote mwenye busara anayetoa hoja kwa ustaarabu, hata kama hoja ni nzito na yenye uwezekano wa kuleta mfarakano katika jamii, anaweza akaeleweka vizuri; na watu wanaweza kuunga mkono kama maoni yake yanaushawishi na mantiki ndani yake.

Mtindo unaotumiwa humu (JF) na baadhi ya watu kujadili hoja hii ya ukabila inaonyesha wazi kuwepo na hisia za chuki; na pengine kama za uchochezi hivi.
Hatuwezi kutatua matatizo yetu kama waTanzania kwa njia hii.

Tatizo la ukabila sehemu zote hizo zilizotajwa linaweza likawepo au lisiwepo. Mimi binafsi siwezi kumhukumu Mh. Mramba au Bw. Kitilya kwa vile tu barabara imejengwa jimboni kwake, au kuwepo na waajiriwa wa kichagga wengi pale TRA. Itanisaidia kujua kuwa Kitilya ni mkabila kwa kuajiri wachaga pekee TRA endapo kama nitapata ushahidi unaoonyesha kuwa taratibu za uajiri zilizomo katika kila idara hazifuatwi. Kama kuna ushahidi unaoonyesha kuwa waomba kazi wa makabila mengine hawapewi nafasi licha ya kuwa na sifa zote zinazotakiwa. Mbona ushahidi mhimu kama huu hauletwi hapa, ili kila mtu aridhike?

Lililo baya zaidi katika mjadala huu ni dalili za kumhukumu kila mTanzania mwenye asili ya uchaga kuwa mkabila! Hata kama ikiwezekana kuthibitisha kuwa Mramba ni mkabila, hii sio sababu ya kuwahukumu wachaga wote kuwa wakabila. Hatuwezi kuwahukumu wa Saudi wote kuwa ma-terrorists, kwa vile tu bin fulani ni mtu wa huko. Na sio ma-Ibo wote ni majangiri kwa vile tu m-Ibo mmoja au wachache ni majangiri! Mtizamo wa namna hii ni wa kitaahira kabisa.

Mwisho, kutokubaliana katika majadiliano sio sababu ya kuanza kuwazulia mambo watu; na kuanza kuwaita wauza madawa, wavaa makaptura, n.k. Hii haiongezi uzito wowote katika hoja ya msingi.

Ni bora tusikubaliane katika msimamo wetu katika baadhi ya mambo; lakini tuendelee kuheshimiana kama watu wa taifa moja - waTanzania. Haitusaidii chochote kuumizana.

Hitimisho: Tutafute ushahidi unaokubalika kuhusu kuwepo kwa ukabila sehemu yoyote ile ya uajiri tukitumia njia za kisayansi kuthibitisha ukweli. Tutazame kama kuna taratibu za uajiri, na kama utaratibu huo unafuatwa vizuri. Kama haufuatwi, basi panaweza kuwepo na kila dalili za ukabila hapo, na ukabila huo ni wa hao wahusika hapo, na sio wa kila mtu katika kabila la huyo mtu.
 
Ndugu zangu hiii ni burudani katika bulogu, ni kwa nini watu wanachukulia mambo ya hapa serious kiasi hiki? Unless watu wengi humu mnafahamiana nje ya hii forum, mana mimi sijui mchagga ni nani na wala mnyakyusa, au mhaya mimi ninaona watu wakitoa mawazo yao, kulingana na wanavyofahamu, walivyowahi kuona, au wengine hata personal experience,

Lakini the bottom line ninaamini kuwa hatufahamiani na hakuna personal na sidhani kama Mramba yupo hapa, hii ishu imesemwa weee na bado inahitaji kuendelea kusemwa na mwisho itajiua yenyewe when the time is right, lakini I am lost na jinsi baadhi ya watu wanavyoyachukulia haya mambo so serious na hasira weee,

Kwani ni nini? wazee unless kuna kitu behind hiii ishu wengine hatukielewi tuambieni basi ili tuamke! Maana sielewi hiii hasira ni ya nini?
 
You better believe it Mzee Es; this is deadly serious business. Perception build into realty, and before you know it.........WHAM, you're clobbered.
 
Admin.
Naomba mamoderator wako uwatazame vizuri wengine wakishindwa mjadala wanatumia kofia ya Umoderator kutuumiza wanyonge.
wameomba interview na sisi tumekaa Gado jamaa wameingia mitini.

Mwanasiasa.

nitakutumia PM na nikupe watu wa TRA kule wakupe ukweli taasisi hiyo ilivyobalika na kuwa NGO ya Kilimanjaro.KAMA unahitaji msaada wa nauli tutakuchangia kwani tunakukubali kwani huongozwi na hisia za watu.

Kalamu na Jasusi.

Nyinyi mmeleta ushahidi gani wa sayansi? tunajua yenu yanakwenda kwa TRA kuwa mali ya kilimanjaro ndio maana hata DPP mnamtolea macho, sisi watu safi hatukosi usingizi hata kama DPP atakuwa masawe kwani hatuna vya haramu au vitendo haramu kama kina Allex Massawe ambao tumeshuhudia baada ya kukamatwa na polisi hatujaona tena ujambazi kuendelea.

Mramba.

Ni Mkabila sana na sasa ameingia hadi kwenye Ujimbo(Rombo) wachagga wa Rombo tu ndio anawasaidia sana kisa ashindane na Machame.
Huyu Mramba lilipobomoka daraja la Goba- bagamoyo hakuondoa hata mguu wake kwenda kutizama daraja huku akiwa waziri mwenye dhamana hiyo.
MRAMBA NDIYE ALILAZIMISHA NDEGE BOMU YA RAIS Inunuliwe hata kama NYASI WANANCHI TULE, kisa kuna kamisheni yake, mtu huyu hatufai.
 
Back
Top Bottom