Ukabila TFF: Jamal Malinzi jibu/fafanua hili kabla sumu haijaenea


kweli wahaya mna matatizo, kujihami kote huko ni kwanini?
 
Jamani msije mkatoana macho na makabila yenu, sisi wafugaji tumeridhika na shughuli zetu za kuhama hama lakini tunaomba tu msije mkaweka kauzibe kwenye maeneo yenye marisho mazuri kule tutakakoona inafaa kuhamia la sivyo silaha zetu za jadi na magobore yatafanya kazi yake.
 

Boss wangu ni wa kiwangwa ni msomi aliyebobea ni muungwana asiyefananishwa. Tena anakiri kusoma shule za Nyerere. Kwa mkoa wa pwani mpo kwenye mikono mizuri sana. Ritz ni shahidi wangu pengine hamjafikiwa tu jaribuni kupaza sauti kidogo tu.
 
Last edited by a moderator:
kweli wahaya mna matatizo, kujihami kote huko ni kwanini?

Kauli ya Jaslaws hasa sentensi ya mwisho inakera sana. Nina demu wangu Mhaya huwa nampiga e teknologia ikika'katerero, kwa sababu hii namsamehe bure bila masharti.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mimi niko serious sizingui bange kama wewe unavyo taka ionekane hivyo. Unaweza niambia ni primarily gani (Rufiji) uliyo soma wewe yenye uwezo wa kutoa One uliyo toka nayo wewe? Rufiji hakuna primarily yenye uwezo wa kufaurisha wanafunzi 20 tu kwa mwaka. Labda uniambie KIBITI high school lakini siizaidi ya hapo.
 
Boss wangu ni wa kiwangwa ni msomi aliyebobea ni muungwana asiyefananishwa. Tena anakiri kusoma shule za Nyerere. Kwa mkoa wa pwani mpo kwenye mikono mizuri sana. Ritz ni shahidi wangu pengine hamjafikiwa tu jaribuni kupaza sauti kidogo tu.
Kiwangwa iko ktk wilaya gani mkoa pwani? Jamani sisi watu wa pwani ndio tulio dhulumika sana tena tangu utawala wa Nyerere. Kutoka mbagala (Dar-esalam) mpaka Bungu (pwani) nauli 4500, lakini huwezi amini lami tumeanza kutumia muhula wa mwisho wa utawala wa Mkapa, umeme ndio kwanza tunaanza kuutumia mwaka Jana. Jamani jamani nchi hii vita ya wenyewe kwa wenyewe haiepukiki. Tukiwepo tutaona, tukifa vishindo tutavisikia duniani.
 
Last edited by a moderator:
Malinzi c ubadili na wana michezo wote wawe wahaya ili muongozane na kucheza wahaya Tu????
 

Bagamoyo. Usilie sana mi nina maeneo kule viziwaziwa maendeleo yanaanza tayari wanaweka maji na umeme tumeahidiwa. Semeni mtasikiwa. Achana na hawa wanaojitoa akili wakilia na ukabila.
 
Nchi hii wanaoila ni Wachaga na Wahaya, kidoogo Wanyakyusa, sisi wengine tunaukimbiza mwenge tu. Roho inaniuma, harakati za kuikomboa nchi Kutoka kwa mabeberu zilianzia Pwani, lakini ndio mkoa ambo usio na wasomi wengi. Wilaya yangu ya Rufiji haijawahi kutoa hata Waziri, kilasiku wabunge tunaletewa tu sio chaguo letu.
 
Malinzi c ubadili na wana michezo wote wawe wahaya ili muongozane na kucheza wahaya Tu????

Kaone timu yake ya miaka yote kule kwetu. Anatengeneza vijana ili wawe wachezaji wakubwa. Msiomfahamu ndo mnapagawa hapa.
 

serikali yoyote duniani inaweka huduma za jamii pale penye uhitaji, pwani na rufiji unakozungumzia mmeweka ngoma mbele, ndoa za utotoni, na uvuvi, kuloga na kuwachukia waalimu, kutowekeza katika ujenzi wa shule pamoja na nyumba za waalimu! usitarajie mkazi wa dar au moshi, mwanza na arusha aliyezoea nyumba nzuri aje akalale rufiji kwenye mbavu za mbwa aache kwenda kwenye maeneo yenye huduma muhimu za msingi. Mimi kijiji nilichotoka kina shule nne za msingi mbili zilijengwa na kanisa na kutaifishwa na serikali mwanzoni mwa miaka ya sitini, mbili zimejengwa kwa nguvu za wananchi nikiwemo mimi nilibeba sana mawe na mchangaa mtoni, mwanzoni tulikuwa hatuna waalimu kutokana na tatizo la nyumba, uongozi wa kijiji ukaowaunganisha wanakijiji kuchangia nguvu na pesa na kufanikiwa kujenga nyuma kama nne za kisasa za waalimu mpaka sasa. Wanakiji wa kijiji changu wanapenda kujenga nyumba nzuri nyumbani lakini hata hawaishi huko, wengi ni wafanya biashara mikoani hivyo nyumba zao huwapangisha waalimu kwa gharama yaa kutunza shamba lake tu! Waalimu kutoka maeneo mbalimbali ya nchi hii wanatamani sana kufanya kazi kijijini kwangu kwani pamoja na mambo mengine niliyowaeleza mwalimu na padre wa kanisa katoliki wnaheshimika na kupendwa kama miungu watu, kwa mantiki hiyo waalimu pamoja na kukasirishwa na serikali bado wanafundisha kwa bidii. Shule za kata kijiji changu zipo mbili hazina waalimu wa kutosha ila mbunge wangu hupita vyuo vikuu na vya diploma mbalimbali kuwahimiza wakirudi likizo wakaokoe jahazi nyumbani zero zinaongezeka. KWENU MNATEGEMEA SERIKALI KILA KITU NA NYIE MNABAKIKUCHEZA NGOMA TU, POLE SANA NDUGU YANGU INGAWAJE NAJUA UKWELI UNAUMA!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…