Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Hivi kuanzia MV, MV spice islander, MV skagit na MV nyerere watanzania wangapi wamepoteza maisha ?

Mbona ajali hizi kama zinafanana sana hatujazitumia kama funzo ?
 
kimsingi ni siku 3 maana leo ijumaa ndio siku ya kwanza na imeishakwisha, ....., hii ni maombolezo bob, kama ni kazi binafsi kafanye ila za kiserikali kwa uzoefu nadhani ofisi zinafungwa kasoro zile tu ambazo huwa hakuna kusimama kufanya kazi mfano poliso, vituo vya afya na vingine kama hivyo.
Walau umetoa mwanga.
 
yaani serikali nzima ya jiwe na inapaswa kujiuzulu na siyo waziri peke yake, mbunge alikwisha ona kuna shida kwenye hicho kivuko na akatoa ushauri bungeni lakini serikali ya jiwe ikapuuza, leo hii roho za watanzania zimetekea! ila ma-CCM kiama chao kitafikaa tuu!
Hili janga si la ubovu wa meli kwani mbunge alilalamika na kivuko kikawekewa injini. Na hata isingewekewa injini bado kuzama kwa meli hakuwezi kutokana na ubovu wa injini. Meli inaweza kuzimika injini na bado ikaelea maisha mpaka itakapooza. Kinachoweza kuzamisha meli kirahisi ni upakiaji wa mzigo. Kuna taratibu za kupakia mzigo to kana na uzito, ujazo, mzigo wa kuhama hama n.k. Bila kuzingatia mpango sahihi wa kupakia mzigo lazima meli itazamani siku moja.
Hapa yaelekea zaidi ya abiria kuwa wengi mno na kuhamia upande mmoja yawezekana kivuko kilipakiwa mzigo mwepesi chini na mzigo mzito juu. Abiria walipohamia upande mmoja kutokana na hamasa ya kufika nchi kavu kivuko kikakosa balance - kikapinduka.
Wapo machief ofisa wazoefu wa meli wataligundua hili mapema tu kwenye uchunguzi.
Yote haya ni kwa sababu ya kukosana wakaguzi au ukaguzi wa vyombo vya mak
 
Hoja ya kup.umbavu kabisa.

Jambo la muhimu ilikuwa kuzuia maafa.

Mbunge wa Ukerewa amelalamika sana Bungeni. Alieleza jinsi alivyohangaika na alivyoonana na viongozi mbalimbali wa serikali kuelezea hali ya hatari iliyokuwa ikiwanyemelea watumiaji wa kivuko cha Nyerere lakini serikali haikuwahi kufanya chochote.

Leo wakati watu wamekwishakufa ndiyo wanajikusanya kwenda kisiwa cha Ukara. Unafiki mkubwa! Msaidie mtu kulinda uhai wake na siyo kubeba jeneza lake

Tena wakiwa hawana hata taa ya kumulika mita 100 as far ili kuokoa maisha ya watu waliokuwa wanagugumia na maumivu kuomba msaada.....

Badala yake RC, RPC na timu yake ya uokozi isiyo na zana za kuokolea maisha ya watu ktk janga kama hili giza lilipoingia wakaenda zao kupumzika kwenye Hotels wakijiburudisha na bia na nyama choma eti mpaka kesho yake asubuhi tena!!

Duuh, what a shame is this!!???

Ni kana kwamba "serikali ya awamu ya 5" ama sema "Serikali ya Magufuli" ama ukipenda iite " Serikali ya CCM" imewatoa "Kafara" wananchi hawa "wanyonge" na masikini kwa mtaji wao wa uchu wa kuendelea kushika madaraka ya uongozi wa dola!!
 
Kivuko kilibeba watu 400
Waziri kasema sa 12 watakuwa wameipata miili yote 228.
Ngoja tuone uongo wake
Nafikiri yiko under serious Stress.Na anaongea bila kuelewa ni nini hasa anchokizungumzia
Ila tumwelewe tu..
 
Huyu naye analinganisha ajali za barabarani na zile za ndani ya maji.

Analeta siasa zisizo na faida yoyote kwake yeye na kwa wasomaji. Thread ya udaku.
 
When fools yake advantage of a catastrophe to propagate a useless propaganda. Sasa Putin kutuma rambi rambi kwa waliofiwa itazuia vipi the same from occurring again? Mwenye kuleta Uzi huu angetuambia vile hawa responsible for this tragedy watachukuliwa hata na pia vile familia A waadhiriwa watasaidika na kwa njia ipi.
 
Sio hili tu, yapo mengi yanakuja na yataendelea kuja kwa sababu maisha yetu yanafanyiwa maamuzi na wanasiasa. Hivi ni leo wewe umesikia watu wakipigia kelele suala la vipaumbele vya nchi? Hakika wewe ni mwanasiasa ama mnufaika wa kisiasa, Huna hata chembe ya huruma.
vipaumbele vipi hivyo ambavyo serikali hii havijaguswa
 
Wakata tiketi wanatakiwa kufunga geti idadi ikitimia... Sasa kama wana wakatia tu kama pale magogoni una tegemea nini??? Kuwa naodha aje kuhesabu abiria??? Wakati wakatisha tiketi wana jua fika uwezo wa chombo na maelekezo mengine...

Umeona kinacho tokea ktk mwendokasi jioni na asubuhi... Gari lina pata shida... Dereva ndio aseme mshuke au abiria kuna muda wanatakiwa kujiongeza???
 
Nilitegemea kwa wakati huu KUB Mbowe angekuwa kisiwani Ukerewe kujumuika na mbunge wa jumbo hill ambaye ni wa Chadema pamoja na timu nzima ya viongozi wa serikali na vyombo vya dola. Kwanini Mbowe kamuacha mbunge wake akiwa mpweke katika wakati huu mgumu!
Usiulize hivyo :
Uliza hivi :Kwanini Nbowe hajanunua kivuko kipya wakati anakusanya kodi za Watanzania?
 
Back
Top Bottom