Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

yaani serikali nzima ya jiwe na inapaswa kujiuzulu na siyo waziri peke yake, mbunge alikwisha ona kuna shida kwenye hicho kivuko na akatoa ushauri bungeni lakini serikali ya jiwe ikapuuza, leo hii roho za watanzania zimetekea! ila ma-CCM kiama chao kitafikaa tuu!
Mkuu soma vizuri taarifa.
Unaambiwa injini alizoomba mbunge zililetwa mbili mpya.

Hapo tatizo ni jingine tu. Inaonekana ni overloading and unbalanced loading.
 
Tatizo liko wapi hamuelewi maana ya maomboleza au vipi ..hizo siku nne kazi zisimame tuungane na ndugu wa marehemu kuwatia nguvu
 
Mleta mada ametumia bongo kufanya critical analysis,wewe unatumia mat.ko kumjibu,bado tuna safari ndefu sana...
Eti critical analysis!,Wabongo bhana ,chadema mmeshindwa Kuifanyia Critical analysis,pathetic
 
Barua fupi kwa watanzania wote:

Ndugu zangu watanzania, SIASA ni maisha, na tunapozungumzia maisha hakuna ushabiki. Siasa inamhusu kila mtanzania, mwana CCM, CHADEMA, CUF NA WAFUASI wa vyama vyote ikiwa pamoja na watanzania wengi ambao hawana vyama kwa vile sote tunahitaji kuishi..

Linapotokea janga kama hili walioathirika ni wana CCM , CHADEMA CUF, ACT + vyama vingine na wale wasiokuwa na vyama. Hivyo yanapokuja maswala makubwa yanayohusu MAISHA yetu tuache kabisa ushabiki kwa vile tu wewe ni CCM, tujadili hoja, tuunge mkono hoja, na hoja ile inayolenga kuboresha maisha yetu bila kuangalia nani kaitoa.

Napenda kuwafahamisha watanzania kuwa sasa hivi kuna nidhamu ya uoga, na hii itatugharimu sio pesa tu bali hata maisha yetu. Nasema hivi kwa sababu wapo walioyajua matatizo ya uendeshaji wa Meli hiyo, tena miongoni mwao ni wataalamu wakubwa tu na wapo katika uongozi. Ila ukikosoa utatumbuliwa, hivyo upepo uliopo sasa hivi ni kusifia tu, wewe ndio mzuri na hata ukuu wa wilaya utapewa. Sasa hii sio siasa, kwa vile hayo si maisha. Maisha ni kusifia pazuri na kukosoa pabaya ili parekebishwe.

Ni nani alikuwa hajui kuwa hii meli inachukuwa abiria mara 4 au zaidi kuliko uwezo wake? Ni nani alikuwa hajui madhara yaliyotarajia kutokea huko mbeleni? Unahitaji uchawi kujua hili. Mabasi yanaposimamisha tu , trafiki hamuachii dereva mpaka atoze faini. Hivi abiria wa kwenye mabasi wanathamani zaidi kuliko wa Melini? Kuna aliyelisema hilo.

Kama hatukuweza kuyasema hayo, tujue uoga ni thambi itayotutafuna. Kwa vile uoga umetawala makazini na kwa watendaji wakuu tutegemee vifo kama vilivyotokea huko mwanza vitajirudia katika sekta nyingi tu za serikali. Tumewabana waendeshaji binafsi kwa sheria zote na kuziacha huru sekta za serikali ili tu serikali ya CCM ionekane inaendeshwa vizuri. Hapa ndio kwenye uchawi, sumu na ushetani mkubwa. Mungu ibariki Tanzania.
 
Hebu rudia kusoma ulichojibu na ulicho ulizwa , halafu rejea qoute yako ya msingi niliyo kuuliza hayo maswali

Eti Mwinyi alikuwa waziri wa mambo ya ndani kwani huyu wa uchukuzi sio waziri ?

Umesema waziri hapaswi kuchukuliwa hatua nikakuuliza swali wakati Mzee Mwinyi anajiuzulu yeye alikuwa kule kwenye mahabusu ? Kwanini isiwe RPC ama OCD ?
Eti kuna tofauti kati ya hili la kivuko kuzama na mahabusu wa Mwinyi ,tofauti ni nini ? Hakuna vifo ambavyo vimesababishwa kwa uzembe ?
Unacho ulizwa sicho unachojibu halafu unajichanganya tu .
Kama Mwinyi ALILAZIMISHWA na Mwl JK. Nyerere ajiuzulum kwani ni kupu KIGUMI kwa huyu?
 
Kazi Zote Zitaendelea Kama Kawaida Huku Watu Wakiendelea Kuomboleza Ila Siyo Kwamba Watu Wanaofanya Kazi Watapumzika

Serikali Inapopata Tukio Kubwa La Msiba Huomboleza Kwa Kupepea Bendera Nusu Mringoti
 
Kwa kweli huyu jamaa jana kaniudhi sana kwa kukosa ubunifu. Boti iliyozama iko mita 50 toka nchi kavu. Huyu mkuu badala ya kuwasha genereta hata nne tano na kuziweka kwenye boti na kuwasha taa na kuendelea na uokoaji. Kirahisi tu huyu mkuu linasema kuna giza tukalale turudi kesho asubuhi. Kweli ? Really ? Leo baada ya kuhakikisha hakuna mtu aliye hai zoezi linaendelea usiku.
Huyu atumbuliwe kwa kukosa ubunifu akaongoze zizi
 
Wamechelewa sana kutoka na kusema neno,ilitakiwa watoke mapema kuonyesha kuguswa na hili janga.

Hata kama wangewahi. Neno Lao linafaida gani sasa? Hivi can you imagine the pain of losing a Family? All at once? How long such memories last? Can you imagine the trauma?

Nadhani tunachotaka kuona ni wahusika wote wa uzembee huu wanaadhibiwa. Lakini pia wananchi wa Tanzania wanayohaki ya kuwa na vivuko salama vya kutosha. Na sheria zinazohusu idadi ya Uzito na watu katika hivi vivuko imafuatwa.

Tulitakiwa tuwe tumeshajifunza zamani huko, baada ama hata kabla ya kuzama MV Bukoba.

Tunachukua muda mrefu sana kufanya mabadiliko. Na hii imekuwa transferred mpaka kwenye maisha yetu ya kila siku. We are tolerating a lot.

Hawa tunaowachagua ama kuwateua ni lazima wawe reaponsible yanapotokea majanga kama haya. Ni jukumu Lao kuhakikisha wanatumia resource the nchi kurahisisha maisha na shughuli za wananchi. Hata kama Hawa viongozi ni rafiki zetu, wakikosea ni lazima kuadhibiwa kama wengine wasio rafiki.

Hii inaonyesha ni kwa kiasi gani wananchi hatuko serious. We are not serious with our own lives.
 
Kwa kweli huyu jamaa jana kaniudhi sana kwa kukosa ubunifu. Boti iliyozama iko mita 50 toka nchi kavu. Huyu boya badala ya kuwasha genereta hata nne tano na kuziweka kwenye boti na kuwasha taa na kuendelea na uokoaji. Kirahisi tu hili boya linasema kuna giza tukalale turudi kesho asubuhi. Kweli ? Really ? Leo baada ya kuhakikisha hakuna mtu aliye hai zoezi linaendelea usiku.
Huyu atumbuliwe kwa kukosa ubunifu akaongoze zizi
Unataka double standard na yule aliyetuibia kodi zetu kwa kuleta fenicha?
 
Poleni wana Mwanza , Poleni ndugu na jamaa.

Raisi ametoa salamu za pole na kutangaza siku nne za maombolezo ikiwa ni pamoja na kupeperusha bendera nusu mlingoti.
Watu wengi wamekua wakiuliza kama siku hizo nne ni mapumziko ya kazi ?
Kama kuna mwnye ufafanuzi juu ya hilo basi awasaidie wadau.
Kazi zinaendelea kama kawaida kwa ofisi zote za serikali. Kiashiria kikuu kuwa tuna tukio kubwa na la majonzi la kitaifa ni Bendela ya Taifa katika ofisi zote za serikali kupepea nusu mlingoti.
 
lakini hapo kutakuwa na uwongo mwingine tunadanganywa sababu ukichukua 131+40=171 huku tunaambiwa kulikua na watu zaid ya 400 ina maana kuna watu wengne zaidi ya 270 wako chini ya maji au imekuaje..? tusipewe majibu marahisi kwamba chombo kimezama sababu ya overload tuambiwe ukweli labda ni ubovu wa chombo au ni nn?
 
Back
Top Bottom