Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Inasikitisha zaidi kwa mkuu wa nchi kuwashukia wapinzani kama mwewe angali ajali imesababishwa na watendaji wake

Badala aende kwenye uokoaji anafanya press na kuwananga wapinzani

No mbaya zaidi kwa mtoa mada kama wewe kuona kichaa aliyofanya ni sawa
 
Inatia uchungu sana unapogundua mtu uliyekuwa unamheshimu kuwa ni mtu makini na mwenye busara ndani ya JF ni "bwege na mlamba viatu" Mimi nimefiwa na ndugu zangu kwa uzembe wa serikali siwezi kupokea maoni ya kipumbavu kama haya ya kwako mleta mada na vimada wenzio. Naijua MV Nyerere, naijua MV Ukara. Najua matatizo yake siku nyingi na jinsi tatizo la usafiri lilivyo kubwa Ukara na Ukerewe kwa ujumla. Najua upuuzi wa wapuuzi wanaoshughulikia usafiri wa majini ndani ya ziwa Victoria. Kama ajali ingetokea siku 2 nyuma Mimi nisingekuwa naandika hapa na picha ya maiti yangi ingekuwa mitandaoni ingawaje wengine wasingejua huyu ndiye Bila bila. Kazi yangu imenipeleka katika visiwa hivi vya Ukerewe, Ukara, Kweru, Ilugwa, Kamasi nk. Naongea ninachokijua, hivyo watu wanapolaumu serikali wanajua wanachokiongea kwa jinsi kifo kilivyokuwa usoni mwetu kila siku tunayopanda kivuko hiki. Nanyamaza ila Mungu anawaona nyie wenye HERI.
 
God give us strength hili Janga linachoma Moyo na linaumiza kichwa. Wanaokamata watu kwa makosa ya mtandao wasikamate yeyote tunapoongea kwa uchungu kuhusu hali hii yenye ukakasi.
 
Mkuu, uwe mpole, limeshatokea. Hii sababu ni technical reason kuwa ni kwa nini hakikuzama mwanzoni mwa safari au hata katikati na badala yake kikazama just 100 mts kabla ya kutua.
Bado naungana na wewe kuwa ni uzembe kuzidisha watu au mizigo.
NI kawaida, Sijui kapteni aliondokaje lakini anaweza kuwa alianza safari kwa tahadhari kwa kujua abiria aliokuwa nao. akishafika karibu, anaona ana uhakika wa kufika na huenda uangalifu ukapungua.
 
Wewe hebu funga bakuli lako walahi!
Allah!
 
Kwanza nianze kabisa kutoa pole zangu tena kwa Watanzania wote kwa Msiba mkubwa uliotokana na Ajali ya Kuzama kwa Kivuko cha MV Nyerere katika Ziwa Victoria. Naomba Mwenyezi Mungu azipokee Roho za Wapendwa wetu wote waliopoteza maisha na pia awape Faraja,Rehema na Uvumilivu wale Wafiwa wote hasa katika Kipindi hiki Kigumu sana Kwao.

Baada ya Utangulizi huo naomba sasa nirudi katika Hoja yangu ya msingi ambayo pia imenisukuma Kuanzisha huu Uzi. Niseme tu ukweli tangia Ajali hii itokee nilichokishuhudia kutoka kwa Wahusika ‘ Kimamlaka ‘ ni 98% ‘ Kulaani ‘ kama si ‘ Kukemea ‘ na hizo 2% zilizobaki ndizo ya ‘ Masikitiko ‘ ya tukio zima.

Kuna Shuhuda mmoja Mwanamama nimemsikia asubuhi hii katika taaria ya Habari ya Channel Ten iliyosemwa na ‘ Mr. Google ‘ Kibwana Dachi kiukweli nimepatwa na ‘ Mshangao ‘ mkubwa na kuanza kuhisi kama siyo kudhani kwamba Watanzania siku hizi tumewekeza mno katika ‘ Uzushi ‘ pamoja na ‘ Uchochezi ‘ bila kusahau na ‘ Umbea ‘ kidogo.

Ifuatayo ni sehemu ndogo ya nukuu yake huyu Mwanamama ‘ Mhanga ‘ wa Ajali ya MV Nyerere kama nilivyomsikia na bahati nzuri alikuwa akisema huku ‘ akitabasamu ‘ kwa mbali japo alikuwa Kitandani Hospitalini akiendelea kupatiwa matibabu yake…” Kiukweli Mimi chanzo cha Ajali siwezi kusema ni nini ila kwa nilichokisia ni kwamba ( Dereva ) akimaanisha Nahodha alikuwa akichati na Simu na ghafla akafika sehemu ya Kona akashtuka ndiyo akakata kwanguvu na kupelekea Kivuko Kupinduka na Kuzama

Katika hali isiyokuwa ya kawaida kabisa nimejaribu kuwafuatilia ‘ Watawala ‘ wawili watatu wenye ‘ Mamlaka ‘ kabisa na nchi hii wakihamisha sasa ‘ goli ‘ kwa kuanza Kulaumu Manahodha huku ‘ wakiamrisha ‘ Viongozi wa ‘ Marine ‘ huko Mwanza wakamatwe upesi na haraka sana ‘ Uchunguzi ‘ ufanyike.

Kama kawaida yangu GENTAMYCINE huwa siyo na haitotokea naitakuja kuwa ‘ Muumini ‘ wa aina hii ya ‘ Unafiki ‘ na nitakuwa wa mwisho kuamini kwamba Ajali hii imetokana na ‘ Uzembe ‘ wa Nahodha / Manahodha bali naamini kama ni Watu wa Kwanza ‘ Kushtakiwa ‘ kama hilo lingehitajika bali walitakiwa wawe ni hao hao ‘ Watawala ‘ tena wa Kuanzia ngazi ya Serikali na wala siyo hao Watu wa ‘ Marine ‘ kama ilivyoelekezwa sasa.

Hivi ni nani ambaye hajui kwamba ‘ tahadhari ‘ ya Kivuko hiki ilishatolewa muda mrefu tu tena na Mbunge husika lakini kama kawaida yetu ‘ Watawala ‘ wa Tanzania tumewekeza sana ‘ dharau ‘ na ‘ kupuuza ‘ mambo lakini likitokea ‘ tatizo ‘ ndipo tunajifanya ‘ tumeguswa ‘ sana, kuumia mno na kutoka ‘ maelekezo ‘ ya Kukomoana ili Kumuumiza au Kuwaumiza fulani / akina fulani ili tu Kuficha ‘ madhaifu ‘ yetu.

Leo hii mnakasirika na kuchukia kwamba kwanini hicho Kivuko cha MV Nyerere kilikuwa kinabeba ‘ Ujazo ‘ usio wake. Hivi hapa inahitaji kweli ‘ akili ‘ kubwa kujua kwamba ‘ Kisaikolojia ‘ ni kwamba pakiwa na chombo kimoja tu cha Usafiri eneo husika Watu wengi huamua ‘ Kujazana ‘ humo ili kuwahi ratiba na shughuli zao? Kwahiyo mlitaka MV Nyerere ikienda ng’ambo nyingine iende na abiria 50 wakati hadi ifike huko inachukua Saa hata 4 hadi Saa 5 hadi kurudi ng’ambo ya pili. Hivi kama leo hii ‘ Watawala / Mamlaka ‘ nchini mngebanabana tu matumizi yenu mengine ya ‘ Kibajeti ‘ msingeweza Kununua Kivuko kingine ili kiweze kurahisha hali ya Usafiri huko Ukerewe / Ukara?

Na nina uhakika kwamba sasa baada ya kutokea kwa hii Ajali ndiyo ‘ mtajitutumua ‘ kujifanya mnatafuta Kivuko kingine imara na kikubwa kwa Watu wa Ukerewe. Kwahiyo kumbe mlikuwa mnasubiri hadi Kwanza Watanzania ‘ Wafe ‘ ndiyo muwapelekee Kivuko kipya? Hivi hapa ‘ Vichaa ‘ kama sisi akina GENTAMYCINE tukihisi kuwa pengine Ajali hii ni sehemu ya ‘ Kafara ‘ la Watu fulani pengine kutokana na ‘ Upepo ‘ wa Kiutawala na Kimvuto kuwa mbaya Kwao tutakuwa tunakosea au kumkosea Mungu?

Mwisho nimalizie tu kwa kusema kwamba Watawala wa / Mamlaka za Kitanzania tuacheni tabia ya kupenda kuangalia pale tulipoangukia na kusahau kutizima kwa umakini kabisa ni wapi tulijikwaa na ikiwezekana kama kuna Kozi inatolewa Chuo Kikuu chochote ya kuweza kuondokana na ‘ Unafiki ‘ basi jitahidini mwende mkahudhurie upesi kwani siyo Siri ‘ mmetukuka ‘ kwa ‘ Unafiki ‘ ambao hauvumiliki tena.

GENTAMYCINE nitakuwa wa mwisho kuamini kwamba Chanzo cha Ajali ya MV Nyerere sijui ni Nahodha ‘ Deiwaka ‘ na ‘ visingizio ‘ vyenu vingine vyote ambavyo katika Watu wenye IQ kubwa na zilizotukuka hazikubaliki ila nikiambiwa kwamba Chanzo Kikuu cha Ajali hiyo ni ‘ Uzembe ‘ kutoka kwa Watawala / Mamlaka tena za juu kabisa nitaamini kwa 100%

Nimeshatema tayari ‘ Nyongo ‘ yangu na kwa wale mtakaoninunia au kunichukia poa tu ila najua ‘ message sent and delivered ‘ kule ambako hakika nimetaka ifike. Msidhani Watanzania ni Mapopoma / Wapumbavu kivile. Na hili jambo / huu Msiba ‘ chonde chonde ‘ msianze sasa Kuuhusisha za Siasa zenu za kutafuta ‘ Kiki / Sifa ‘ bali tambueni Msiba huu ni wa Watanzania wote. Na hata mnapokuwa mnaongea na ‘ Media ‘ jaribu kuwa na Sura za ‘ Huzuni ‘ na siyo za ‘ Kununa ‘ kwani mnatufanya tuzidi Kuwashangaa tu pamoja na Elimu zenu Kubwa mlizonazo.

Nawasilisha.
 
Sijaona rais akiwa mwewe na kumshukia Mbowe. Ni kutafuta u DC jf.
 
Huyo abiria anajuaje kuwa max limit ni abiria 400???????Hapa mamlaka hazikwepi lawama!
 
Avatar yako tu inaonesha kuwa wee ni zwazwa "you need some evolutions to be a real human being" Zinjanthropus mkubwa wewe!!!!
 
Kwa hiyo mbowe ndiye aliyezamisha meli au hakupaswa kuongelea hiyo ajali

Naona mmemgeukia mbowe kama chanzo cha ajali hamtaki kuelewa na kujifunza juu ya uzembe wenu Ili ajali isitokee tena

Kazi yenu kuhangaika na mbowe ili mtutoe kwenye reli
Na mtapiga hela mpaka tukio liishe ..sio kazi rahisi kutengeneza propaganda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…