Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Serikali ya wanyonge inaponunua ndege za mabilioni ya pesa za Watanzania masikini kwa ajili ya kupanda matajiri wachache na kuacha kununua kivuko cha wananchi masikini cha kiasi cha bilioni 2 ni kituko cha karne
Umeandika upuuzi wa hali ya juu
 
We upo kwenye point
 
Sure mkuu
Bahati nzuri wanashughulikiwa ila yapaswa wafilisiwe.lazima wametajirika
Just imagine serikali inajua ni abiria 100 wewe unaweka 300 na zaidi afu hapo pia kuna siku unaeza danganya walikua 95
Na mshahara mwisho wa mwezi pia unaingia
Majizi sana yaani yanafaa yawekewe camera kila sehemu

Hawana haya wala ubinadamu, na mwisho wa siku wanakufaga maskini tu
 
BREAKING NEWS:

MBUNGE CHADEMA APINGANA NA UPOTOSHWAJI UNAOFANYWA NA VIONGOZI WA CHAMA CHAKE

Mh Michael Joseph Mkundi
MBUNGE WA UKEREWE ( CHADEMA)

_"Kuhusu hoja yangu niliyotoa kule Bungeni ilifanyiwa kazi na Serikali kwa uharaka sana na vizuri ambapo lilikuwa ni hitaji la INJINI MBILI ambazo Serikali ilitekeleza wito huo na zilipatikana kwa gharama ya (Tsh. Milioni 191) zikafungwa vizuri Mwezi Julai mwaka huu 2018 kwenye kivuko hicho cha MV NYERERE. Suala ambalo lilikuwa bado tunalifanyia kazi ni namna ya kuongeza idadi ya safari, mengne tumuachie Mungu nawashangaa wanasiasa kulichukulia suala hili kisiasa zaidi huu ni ujinga"_
 
mmh. mkuu tuwekee ushahidi hapa. isije ikawa upotoshaji juu ya upotoshaji..
 
Watasema kanunuliwa
 

..wanaweza kuishitaki serekali.

..serekali imekiri kwamba kivuko kilikuwa kinaendeshwa na "dei-waka."

..hiyo ni hoja ya msingi kuipeleka serekali mahakamani na kudai fidia.
 
Watu wakijiona wanapumua wanadhihaki wasiopumua

Hii mada imenisikitisha sana kama kweli akili zetu ziko hivi basi sisi ni mashetani

Utamchekaje mtu aliyekufa eti wamekufa kizembe!!!! Mita 50 tu

Pata picha upo katika pipa likielea majini ghafla limebinuka likakufunikia na kukukandamiza

Ujuzi na umahiri wako wa kuogelea utatokea wapi??

Acheni dhihaka jamani[emoji24] [emoji24] [emoji24]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…