Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Majibu hovyo kabisa. Mimi ni auditor wa usalama na mifumo ya usalama mahali pa kazi kwa ngazi ya kimataifa.

Ajali hii imetuumiza sote lakini kama Taifa, kuna uzembe wa hali ya juu.

Kwenye usalama huwa tunasema, 'All accidents are avoidable except natural disasters and terrorism.

Baada ya maombolezo, nitafafanua uzembe uliofanyika na uwezekano wa ajali zinazosubiriwa.
Mkuu jibu hoja ya Mongela!
 
Bahati mbaya ndugu yangu innocent abiria huwa ni innocent and ilitrates kwenye masuala ya usafiri. Na kwa mujibu wa sheria wasimamizi wa vyombo vya usafiri ndio watu technical ambao wanawajibika na chombo cha usafiri kama kiko fit kubeba abiria na kwa kiwango gani. Abiria wa kawaida hawezi kuyajua hayo kwamba hii meli au feri au basi inatakiwa ibebe watu wa ngapi. On the other hand abiria hajui hataka akiona meli au feri limejaa consequences za kujaa huko. Usiwatetee hao wasimamizi wa hiyo feri lazima wajibu mahakamani vifo vya abiria innocent waliopoteza maisha yao kikatili kwa sababu ya tamaa za pesa kwa wachache wajinga na wapumbavu
Mimi sioni kama waliyopakia watu wanatatizo lolote kwasababu akuna abiria ata mmoja aliyelazimishwa kupanda hiyo feri ikiwa imejaa mimi mwenyewe nikiona kitu hiki ni hatari siwezi kufanya kwasababu natambua kuishi ni mara moja tu siwezi kubet maisha yangu ila waliyopanda feri ikiwa imejaa walikuwa na akili timamu kabisa wala awakulazimishwa kupanda iweje walaumiwe wao
 
Mkuu wetu wa Mkoa
hana hayo mawazo kiza uliyonayo wewe Etwege ya uchonganishi.
Waliolalamika wengi walikuwa ni Ndugu za waliosafiri na kivuko siku hiyo.
Hata ingekuwa wewe, ingekuwa mkeo( mfano) , kazama, mke wa jirani yako kaokolewa hai,giza likaingia, usingesema? Kuwa jamani tuwashe hata tochi au generator tuendelee hadi usiku kuokoa mkeo?
Hii ni human nature na siyo siasa.
Mkuu wa Mkoa nimemsikia hajataja mtu,amejibu kwa busara.
Nashauri mods, futeni huu uzi chonganishi.
Una utaalam wa masuala ya Diving mkuu!?
Au unajaza server za JF na wewe uonekane! Kuna masuala ni ya kitaalam na hayahitaji Siasa na mihemko.
Mkuu wa mkoa alishauriwa na wataalam (Divers) kusitisha zoezi hilo kutokana na hali iliyojitokeza ndani ya maji.
Hayo masuala ya mke wako sijui mke wa jirani yaache huko huko kwenye vijiwe vya kahawa.
 
Je, pesa zinazotumika kununua ndege zinazopandwa na wenye pesa, zingetumika kununua kivuko kikubwa hali ingekuwaje huko Ukara?
 
Amani ya bwana.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh John Mongella akihojiwa na vyombo vya habari ametolea ufafanuzi ule upotoshaji mkubwa uliofanywa na wanasiasa watafuta kiki mara baada ya kutokea ajali ya kuzama kwa kivuko cha Mv Nyerere kwenye ziwa victoria.

RC Mongella amesema yeye ni mkuu wa mkoa tu na wala si mtalaamu wa maswala ya uokoaji, hivyo alichokifanya na anachokifanya sasa hivi ni kupokea na kufanyia kazi maoni ya watalaamu wa uokoaji majini (divers).
Kabla ya kusitisha zoezi la uokoaji siku ya kwanza aliambiwa hali ya maji ziwani imeanza kuwa mbaya na kutokana na usiku ,hivyo angetumia kofia yake ya ukuu wa mkoa kulazimisha divers waendelee na kazi angeweza kusababisha madhara zaidi na angeweza hata kuwapoteza hao wataalamu wa uokoaji.

Maelezo ya mkuu wa mkoa ni majibu safi kabisa kwa wanasiasa wakurupukaji wanaopenda kudandia mambo bila kuwa na ushahidi wa maelezo ya kutosha.
Mara baada ya kutokea ajali hiyo wanasiasa kama Zito, Mbowe na Mbatia walikuwa na uwezo wa kufika eneo la tukio na kushirikiana na wafiwa kwa haraka mno hata kwa kutumia ndege lakini hawakufanya hivyo badala yake wakaanza kuitisha waandishi wa habari wakiwa Dar kutoa matamko na kupotosha watu ,huku wakijifanya wanaijua sana hali ya ajali kuliko watu waliopo eneo la tukio!!

Hali hiyo ya kutafuta kiki za kisiasa kupitia ajali na matatizo ya watanzania ilikemewa vikali na Rais wetu mpendwa Dr Magufuli. View attachment 875133
Maagizo ya serikali hayawaruhusu viongozi wa upinzani kufanya shughuri zozote kwenye majimbo ambayo si yao, tukumbuke mhe. Zitto licha ya kuwa mwenyekiti wa taifa wa ACT lakini alikamatwa Morogoro kwa kufanya siasa eneo ambalo si mbunge!
 
Mongela wasamehe bure.Hizo ni hasira na frustrations zao za kushindwa chaguzi wameaamua KU STEAM OUT FRUSTRATION zao kwenye hiyo ajali.

Wamegeuka ghafla wasomi na wataalamu wa vivuko.Nyoooo!!!! wangekuwa wasomi na wataalamu si wangetumia usomi na utaalamu wao kushinda chaguzi?. Wakshindwa chaguzi hata za udiwani tu hugeuka na kujifanya wasomi na wataalamu waliobobea wa ku analyize mambo ya kitaifa na kimataifa!!!! ha ha ha ha

Kwani sasa hivi kushinda uchaguzi hapa Tz kuna hitaji usomi? au ni kuwa na madaraka ya kuagiza tume ya uchaguzi imtangaze umtakaye kwani unamlipa mshahara na kumpa gari, kisha jeshi la polisi lisimamie hiyo dhuluma? Bahati nzuri wananchi wako digital hawapigi kura tena, huku viongozi wamebaki analogue wakitumia nguvu na kupika matokeo ya uchaguzi.
 
bila kumsahau mhonga nyumba..
aliyezoea kuchezea maisha ya watanzania..
ni desturi yake kupiga dili kodi zetu na kutununulia vitu vibovu..
MV Nyerere ishaua..
MV Dar es salaam huko mafya chukueni tahadhari
..
hostel mpya za udsm zinakarabatiwa kila siku..
 
Hicho ndo cha kushukuru wangeitoboa kama MV bukoba, ingezama Jumla ikawa kaburi la milele
Nami ndo nilichoshukuru..... ila kwenye rescue mission bado tunatatizo hasa kwa nchi zote za africa..
 
Mongela wasamehe bure.Hizo ni hasira na frustrations zao za kushindwa chaguzi wameaamua KU STEAM OUT FRUSTRATION zao kwenye hiyo ajali.

Wamegeuka ghafla wasomi na wataalamu wa vivuko.Nyoooo!!!! wangekuwa wasomi na wataalamu si wangetumia usomi na utaalamu wao kushinda chaguzi?. Wakshindwa chaguzi hata za udiwani tu hugeuka na kujifanya wasomi na wataalamu waliobobea wa ku analyize mambo ya kitaifa na kimataifa!!!! ha ha ha ha
Kama nchi ilitakiwa ijifunze kutoka ajali ya Mv bukoba. Amaizing ni kwamba toka 1996 bado tu.. hatuna team ambayo iko standby kwa maafa kama haya. Simlaumu RC mongela maana amefanya upande wake kama yeye..
Ila serikali ilitakiwa iwe na vifaa, technologia ya kutosha , na kikos maalumu toka 1996 .
 
Amani ya bwana.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh John Mongella akihojiwa na vyombo vya habari ametolea ufafanuzi ule upotoshaji mkubwa uliofanywa na wanasiasa watafuta kiki mara baada ya kutokea ajali ya kuzama kwa kivuko cha Mv Nyerere kwenye ziwa victoria.

RC Mongella amesema yeye ni mkuu wa mkoa tu na wala si mtalaamu wa maswala ya uokoaji, hivyo alichokifanya na anachokifanya sasa hivi ni kupokea na kufanyia kazi maoni ya watalaamu wa uokoaji majini (divers).
Kabla ya kusitisha zoezi la uokoaji siku ya kwanza aliambiwa hali ya maji ziwani imeanza kuwa mbaya na kutokana na usiku ,hivyo angetumia kofia yake ya ukuu wa mkoa kulazimisha divers waendelee na kazi angeweza kusababisha madhara zaidi na angeweza hata kuwapoteza hao wataalamu wa uokoaji.

Maelezo ya mkuu wa mkoa ni majibu safi kabisa kwa wanasiasa wakurupukaji wanaopenda kudandia mambo bila kuwa na ushahidi wa maelezo ya kutosha.
Mara baada ya kutokea ajali hiyo wanasiasa kama Zito, Mbowe na Mbatia walikuwa na uwezo wa kufika eneo la tukio na kushirikiana na wafiwa kwa haraka mno hata kwa kutumia ndege lakini hawakufanya hivyo badala yake wakaanza kuitisha waandishi wa habari wakiwa Dar kutoa matamko na kupotosha watu ,huku wakijifanya wanaijua sana hali ya ajali kuliko watu waliopo eneo la tukio!!

Hali hiyo ya kutafuta kiki za kisiasa kupitia ajali na matatizo ya watanzania ilikemewa vikali na Rais wetu mpendwa Dr Magufuli. View attachment 875133
UPUUZI MTUPU ,MARA GIZA MARA HALI MBAYA CHINI YA MAJI , TANGU LINI CHINI YA MAJI KUKAWA NA HALI NZURI?
 
Kwa mara nyingine CCM imenunua msiba ambalo ulitarajiwa ufanyike kiserikali bila jezi za kijani. Kwenye eneo la maziko nguo za kijani zimeanza kutawala na ni za haohao wanaoshauri tuache tofauti za kiitikadi za kisiasa! Hali hii ndiyo inayotufarakanisha watanzania na lawama wanapewa wanaotengwa!
 
Maagizo ya serikali hayawaruhusu viongozi wa upinzani kufanya shughuri zozote kwenye majimbo ambayo si yao, tukumbuke mhe. Zitto licha ya kuwa mwenyekiti wa taifa wa ACT lakini alikamatwa Morogoro kwa kufanya siasa eneo ambalo si mbunge!
Kumbe alikuwa anafanya siasa!!
 
Back
Top Bottom