Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Mwenye macho haambiwi tazama. Japo ukweli daima unauma na kwa kuwa sasa hivi tuna aina fulani ya siasa na mwelekeo mpya wa maigizo katika maisha. Twendelee tu kusema siasa isichukue nafasi ilihali matamko ya kisiasa yakichukua na mwelekeo wa kisiasa yakichukua nafasi ya kipekee na kutamalaki kwa sana
 
Mkuu,Nabii Nuhu alizingatia hesabu za idadi ya wanyama aliopaswa kubeba kwa mujibu wa kanuni alizopewa.Tatizo letu ni kupuuzia mambo ya msingi.
 
Ujinga tu. Kwa hyo angekuwemo mule jemedali wetu john pombe wange ahirisha zoezi kwa sababu ya giza?tuache siasa yashapita.
 
Kuna upotoshaji mkubwa unafanywa kwa kutengeneza kauli/maneno yanayosemekana kutoka kwangu. Naomba kauli hizo zipuuzwe. Tokea kutokea kwa ajali ya kivuko cha MV Nyerere nimekuwa na mawasiliano ya karibu na viongozi wangu wa chama na nina support ya hali ya juu ya viongozi wangu kipindi chote na hakuna kipindi chochote nilichotofautiana na yeyote. Aidha, baadhi ya viongozi wangu wangu wa chama wapo eneo hili la tukio mda wote tokea siku ya tukio hili. Naomba wote walio nyuma ya upuuzi huu wawaheshimu wakerewe, wawaheshimu marehemu wetu tuliowapoteza. Nina majonzi, nina masikitiko na ninaomba mtambue hill.
Mhe. Joseph Mkundi (mb)
Ukerewe
 

Kwa wakerere, wakara, wajita, wakwaya na waruri kilichotokea ni kupinduka (KWIFUMA) na siyo kuzama (KUSIKA). Kama ingesika (kuzama) ni hakika wangetumia uzoefu wao wa kuogelea na wangeokoka wengi. Kwa vile imepinduka ikawafunika ndiyo maana wamekufa kibudu na wengi kiasi hicho. MUNGU AWAPE PUMZIKO LA AMANI
 
Wapuuzi ni walioshindwa kupeleka kivuko kinachokidhi mahitaji sababu mbunge wa eneo husika ni wa chadema.
 
Wewe mleta mada umeenda Mazishi au fashion show kuangalia watu wamevaa nini?
 
Kapicha kangenoga zaidi
 
Mwenyezi Mungu hamfichi mnafiki. Hawa ndo waliosema wanasiasa wasitafute kiki kupitia huu msiba lakini wamekuwa wa kwanza kwenda na vijora vya kijani msibani.

CCM huwa nawaona kama mchawi aliyechelewa kurudi toka makaburini alikokuwa anawanga!
 
Kweli tuna matatizo ya kuchambua mambo kwani wanaposema tusiweke mambo ya siasa na mambo ya vyama wana maana ya watu wasivae nguo za vyama vyao? Nadhani hapo kuna shida ya kutafakari mambo
Kwani wakienda na nguo za kawaida inawapunguzia nini? Matukio yakitokea wanakimbilia nyumbani kubsdili nguo na kuvaa ya kijani ili tuone hicho chama kinawapenda watu, mbona hamkwenda na uniform kufunga injini mpya za kivuko kuokoa maisha ya mamia ya Watanzania wenzetu waliozama majini?
 
Costa Concordi ilijikwaa kwenye jiwe na hii imepinduka tofautisha hapo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…