Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

H
Nafikiri tusimlaumu mkuu wa mkoa pasi kujua vizuri sababu.kwanza tatizo limeanzia kwa wafanyakazi wa kivuko yamkini kupakia watu wengi kuzidi kiwango cha kivuko,shughuli ya uokozi inawatazama wataalamu wa majanga hayo na mkuu wa mkoa utakuta yeye hana taaluma hiyo,inawezekana giza lilipoingia wataalamu walimuomba kusitisha zoezi labda hata kwa kuepusha vifo vingine ambavyo ni vya waokozi wenyewe kwa uhaba wa vifaa yamkini vya kumulikia eneo husika na chini ya maji.zaweza kuwepo sababu nyingi hata wao na mkuu ni watu hawawezi kusitisha tu zoezi bila sababu na mle ndani kuna watu.sasa tukianza kumlazimisha Rais na kuweka uchochezi hapa wa kutamani kuona mkuu wa mkoa kafukuzwa kazi sioni kama ni sawa sana.
Hakuna anayemchukia RC wa Mwanza wala hakuna atakaye furahia au kufaidika na kuadhibiwa kwa mkuu Huyo. Unachopaswa kujua huwa kuna kitu kinaitwa HEKIMA au BUSARA, hata kama pasingekuwepo na njia yoyote ya kutoa msaada unapaswa kiongozi usome nyakati na hali ikoje.Taifa lote lilikuumbwa na Taharuki kila sikio LA Mtanzania mwenye wasaa wakati huo nahisi lilikuwa huko, ni bora kabisa angekaa kimya akawaondoa watu wake kimya kimya bila hata kuujulisha umma. Hapa kilichotakiwa ni busara tu na hekima ndugu yangu. Zaidi hata angeufumba umma kuwa hali ya HEWA ni mbaya kuliko kutumia kigezo cha GIZA.
 
Ni aibu kwa Watanzania.
1.Eti idadi ya watu waliongia ktk kivuko hawaijui.
2.Uzito halisi wahusika hawaujui.
3.Kivuko cha watu 150 wanaingia takriban watu 400 na mizigo zaidi.
4.Vivuko vingi vina screen tvs ila zote zinapiga miziki na bongo muvi tu badala ya kutoa elimu ya usalama na jinsi ya kujiokoa.
5.Ukosefu wa vifaa vya kujiokolea km life jackets nk.
6.Vifaa duni vya kuokolea....ajabu wamepeleka mitumbwi ya kasia hata kukigeuza kivuko wameshindwa.
7.Uokoaji ulisitishwa sababu ya giza....Hivi kweli hatuna teknolojia ya kupata hata mwanga tu, watu wakapiga kazi 24hrs.
HIVI WATANZANIA TUTAJIFUNZA KWA LIPI??
Points
 
Hakuna kitu kilihuzinisha kama Mhe. RC kusitisha zoezi la uokozi kwakweli. Ina maaana uwezo wake wa kufikiri ulikomea pale......
Temesa kutumia Jenereta na kununua SportLight za 240,000/= ambazo zingefanya eneo hilo kuwa mwanga wa kutosha alishindwa???
Alishindwa kuitisha karabai 50 za wavuvi wa dagaaa eneo zima lingegeuuka mchanaaaaa na Uokozi ungeeendelea vizuri.
Ktk hili ningekuwa mwenye mamlaka RC wa aina hiii HAPANA.
 
Ukiiwazia sn hii ajali kwa ujumla huwezi kujijibu vzr na hata huenda usipate mtu wa kukusaidia kupata majibu yenye msaada hadi uelewe. Taarifa za awali zinasema ni kuzidisha uwezo wake wa mizigo,huenda ika-play kwa kusogea tu karibu na ukweli lkn upande wangu nakuwa sijaridhika kabisa. Kwa tuliowahi kusafiri na ile ferry na kwa muundo wake,napata shida kuamini kwamba ikiwa kweli ilikuwa overloaded na ndiyo sabb yake kuzama,basi ingeweza kuzamia katikati ya safari yake ambako kuna mawimbi makubwa sn. Nikikadiria distance iliyopo Bugorola-Ukara ni almost 50-60km na imeenda kuzama ikiwa ishayapita mawimbi makubwa ambayo yangeweza kuidhuru mapema. Ukubwa wa mashaka yangu pia ni namna gani tukio la kuzama liliweza kutokea kwa ghafla sn ferry nzima ikawa imetumbukia na kupinduka!! Mimi niendelee kuvuta subira tu nikiwa na majonzi makubwa lkn nikitazamia taarifa ya uchunguzi itakuja na majibu yaliyo sahihi zaidi na si kuimbiana huu wimbo wa ilizidisha abiria na mizigo. Imani yangu,pamoja na hiyo bado tutapata sababu nyingine itakayosapoti hii tuliyonayo.
 
Wakati wa tetemo la ardhi Bukoba na watoto waliofariki kwa ajali Arusha,serikali ililalamikiwa kubadirisha matumizi ya rambimbirambi. Badala ya kupatiwa wahanga moja kwa moja ikaelezwa kuwa kiasi kitajenga miundombinu. Wananchi walilalamika kamba ile ni kazi ya serikali.

Leo watanzania tumepatwa na janga kubwa limetuumiza na halitapoa milele. Ni budi tukakumbushana mambo muhimu wakati wa msiba.

Tukahamasisha pia wale waliojiapiza kutotoa rambirambi kwa misiba ya kitaifa kama hii. Serikali ijitafakari iepuke kusema rambirambi zitajenga miundombinu ya kifuko.

Nyongeza

Rais Magufuli ameguswa sana na msiba huu,naamini yupo njiani kuja kuwapa pole wananzego.

Nyongeza 2

Siasa zitaepukwa msibani,kila mtu ana haki ya kutoa pole,awe Lowasa,Mbowe au Sumaye

Kwa niaba ya wanaJF wote, tunasema tumeumia sana.
 
Msiba wa Taifa uliotokea katika visiwa Vya Ukerewe sI pigo TU KWA N YETU NA FAMILIA ZILIZOPOTEZA WAPENDWA WAO bali pia ni AIBU kwa TAIFA letu.

HATUJIFUNZI ama hatutaki KUJIFUNZA maksudi kutokana na majanga yaliyowahi kutokea huko nyuma
ikiwemo utayari wa UOKOAJI.
Janga hili lingeweza KUZUILIKA ila basi tu....!!!

i
Kwa kifupi. hii NEGLIGENCE/UZEMBE wa hali ya juu sana ambao mtu ama watu wanahitaji KUWAJIBISHWA!!

Uzembe huu si tu kwa nahodha wa chombo hicho au waliokuwa wakikata tikikti bali ni UZEMBE
wa WIZARA na Tassis zake HUSIKA.

Katika nchi zilizoendelea janga kubwa kama hili likitokea ambalo LINGEWEZA KUZUILIKA lakini likaachwa lijishughulikie lenyewe basi
WAZIRI huwa anachukuwa jukumu la KUJIUZULU.
Si kwa sababu YEYE ALIHUSIKA DIRECTLY bali kama kuchukuwa POLITICAL RESPONSIBILITY la uzembe WOWOTE uliotokea wizarani mwake.

Je hili linaweza kutokea Tanzania?
Jibu ni ndiyo ikiwa mioyo yetu itajielewa.
Picha hii ya kujiuzulu huonyesha nchi kuwa hata mkuu wa nchi huwa AMEMKERWA.

Nawaachia WAHUSIKA wajihoji NAFSI zao!!
Wakiamua kuwa "HAMNA" na ni business as usual basi bado ni sawa tuhata hivyo I have given out my mind!/Nimetoa maoni yangu.
Pia alie kuwa kiongozi wa bunge siku mbunge wa Ukerewe alipo uliza swali akajibiwa utumbo kwa sababu za ijinga na ushabiki wa kipimbavu wa wabunge wa Ccm nae aachie ngazi.
Ki uhalisia Ccm na serikali yake wanatakiwa kulaaniwa kwa hili tatizo
 
Habari ya mchana wana Jamvi

Natanguliza pole kwa ndugu wote waliofikwa na msiba wa kufa maji jamaa zao wa karibu.
Mungu awape faraja ya kipekee.

Kwa namna moja nimeshangazwa na maamuzi yaliyo fanywa na baadhi ya viongozi wetu Mwanza baada ya ajari kutokea.

Maamuzi ya kusitisha safari ya meli (boti) za Mv Clarias (serikali) na mv Nyeunge (mwarabu) zilizo kua zikifany safari yake kutoka Nansio kwenda Mwanza muda wa mchana ili kwenda kusaidia swala la uokoazi. Ambapo meli ya Mv clarias ilikua tayari imeanza safari ya Kueleke Mwanza ikabid irudi ishushe Abiria na kuelekea eneo la tukio vile vile Nyeunge ilifanya vivyo ivo pamoja na kushusha Magari yalio kua yakivushwa.

Sawa ni Jambo jema
Ila habari ya kusikitisha ni kuwa mpaka muda huu hizo meli hazijarudi kuendelea na Huduma yake ya kuvusha watu kati ya Nansio (Ukerewe) -Mwanza watu wamekwama watu wameshindwa kufika ma offisin watu wameshindwa kuvusha biashara zao watu washindwa kwenda kuona wagojwa wao, walio kua wakienda mbali wameachwa na ndege na hasara nyingine nyingi.

Je serikali haina mbadala wowote wa uwokozi kiasi kwamba Huduma za kijamii zimesimama?
Kwa nin serikali asinge agiza meli za mizigo zisaidei uokoaji izo za abiria zikaendelez Huduma?
Kwa nini wa si ruhusu meli moja itoe huduma na iyo moja iendelee na uokozi wa miili?

Au ni maamuzi ya bila kufikiria ya Viongozi wetu?

SAWA AJARI IMETOKEA ILA LAZIMA MAISHA YAENDELEE

PUMZIKENI KWA AMANI NDUGU ZETU . TUTAWAKUMBUKA DAIMA [emoji120]
 
Mkuu
Picture Ile Jana Imezagaa Baadhi Yetu Tukasema JW Wapo Kazini Kumbe Hakuna Siyo Ya Tukio


Mungu Awape Pumziko La Milele
Sio picha ya tukio mkuu.
Wanahabari wetu ni wavivu sana,sijui ndivyo wanavyofunzwa huko vyuoni?
Au ndio tabia ya kupenda kuwa wakwanza kutoa taarifa.
 
Katibu wa UVCCM Mwl Raymond Stephen Mwangwala (MNEC) kupitia taarifa iliyotolewa na Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi Ndugu Hassan Bomboko amewaelekeza makatibu wa mikoa ya kanda ya ziwa iliyopo jirani na mkoa wa Mwanza haraka sana kujiunga na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Kheri Denice James (MCC) katika kusaidia zoezi la uokoaji.
IMG-20180921-WA0132.jpeg
 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema mazishi ya watu waliopoteza maisha katika ajali ya Mv.Nyerere iliyotokea Septamba 20 huko kisiwani Ukara, Ukerewe mkoani Mwanza yatakuwa ya kitaifa ambapo viongozi wakuu wa kitaifa wanatarajia kushiriki mazishi hayo.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe.
Akiongea na ITV Mhandisi Kamwelwe amesema shughuli za mazishi hayo zitagharamiwa na Serikali na kwamba utaratibu kamili wa eneo yatakapofanyika mazishi hayo utatolewa baadaye.

Hata hivyo Mpaka sasa zoezi la uokoaji na uopoaji wa miili ya watu waliokuwa kwenye kivuko cha MV.Nyerere linaendelea ambapo miili 94 ya watu imeopolewa na waliookolewa wakiwa hai wanazidi 40.

Vikosi vya uokoaji mkoa wa Mwanza vimeongezewa nguvu na vikosi vya mkoa wa Mara katika eneo la tukio ili kuongeza kasi ya kuopoa miili ya watu waliopinduka na kivuko hicho.

Aidha uongozi wa wakala wa meli mkoa wa Mwanza umetambua wafanyakazi wa kivuko watano ambao wamepoteza maisha akiwemo nahodha, fundi, Karani, mlinzi na mkuu wa kivuko, Kivuko hicho kilikuwa na wafanyakazi wanane.

Mamia ya wakazi wa Ukerewe wamekusanyika nje ya kituo cha afya cha Bwisya kutambua miili iliyoopolewa kwenye ajali ya kivuko cha MV.Nyerere iliyotokea wakati wakisafiri kutoka kisiwa cha Bugorora kwenda Ukara kwenye gulio.

Mwandishi wetu aliyepiga kambi katika eneo hilo ametueleza kuwa wengi wa walioopolewa hadi sasa ni wanawake.
Hivi huyu waziri bado yuko kwenye wadhifa wake na hana mpango wa kujiuzulu?? Shameee
 
Katibu wa UVCCM Mwl Raymond Stephen Mwangwala (MNEC) kupitia taarifa iliyotolewa na Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi Ndugu Hassan Bomboko amewaelekeza makatibu wa mikoa ya kanda ya ziwa iliyopo jirani na mkoa wa Mwanza haraka sana kujiunga na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Kheri Denice James (MCC) katika kusaidia zoezi la uokoaji. View attachment 873389
Uamuzi wa busara,nampongeza
 
Back
Top Bottom