Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ndugu wanabodi;
Ajali ya MV Nyerere imeleta msiba wa kitaifa ambapo zaidi ya Watanzania wenzetu 225 wamepoteza maisha.

Idadi hiyo ni kubwa sana kwa taifa letu. Hivyo ni matarajio yangu kuwa hill si suala LA kutuma uwakilishi Bali viongozi wote wa kitaifa wa vyama vya siasa,madhehebu ya dini na taasisi binafsi wakiongozwa na Rais wa JMT walipaswa kuhudhuria.

Sasa ukipeleka uwakilishi kwenye jambo kubwa la kitaifa kama hill yaani wewe unakuwa na jambo gani la kitaifa jingine?

Namshauri Rais afike Ukara yeye mwenyewe asisimuliwe na MTU ktk hili.Nawashauri viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa wafike wenyewe Ukara wasipige lamli wakiwa DSM.

Tukishindwa kuonesha umoja wetu kama Watanzania ktk hili tutaonesha maadili na umoja wa Utanzania wetu ktk lipi?

Nasisitiza tena Rais ufike Ukara,tena ktk kipindi hiki cha majonzi vinginevyo Mimi kama RAIA mwema nitaona umelichukulia janga hili sio kwa uzito unaostahili.Nakumbuka ulivyowatembelea wagonjwa na majeruhi mbalimbali huko muhimbili .Naamini hata ktk hili utafika huko Ukara kuwafariji wafiwa ktk kipindi hiki hiki cha majonzi na si muda mwingine.

Nasisitiza tena viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa,madhehebu ya dini na taasisi mbalimbali mnapaswa kufika Ukara kufariji wafiwa ktk kipindi hikihiki cha majonzi. Hii itasaidia kudumisha maadili yetu kama Watanzania na kuonesha mshikamano wetu kama taifa ktk shida na raha.
Rais hakwenda baada ya kutokakanisani ameenda kunywa chai na traffic. Viongozi wa upinzani wakienda wanaambiwa wanaingiza soasa kwemye msiba. Umesahau ya Lucky Vicent waliwekwa ndani hadi viongozi wa dini. Kagera walikwenda akina Mbowe na Lowassa wakaambiwa wanapeleka siasa kwenye maafa wakati wamwleenda kufariji na kutoa misaada. Rais mwenyewe alikuwa zake Dar. Tatizo nchi imejengewa ubaguzi mkubwa awamu hii
 
mbunge.jpg

Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa Chadema(@official_bavicha_taifa)
Mhe. Joseph Nkundi, ukiwa Mwakilishi wa wananchi wa Ukerewe tunakupa pole sana kwa kuondokewa na wananchi wako, ambao walikuchagua ili uwatetee lakini watawala wakaamua kuziba masikio yao kwa pambaa na kukupuuza kwa wito wako ulioutoa bungeni. Walitamani kusikia wanayopenda kwa masikio yao lakini sio kusikiliza mahitaji ya wananchi wako waliokutuma Bungeni. Usivunjike moyo endelea kupamabana naendelea kuwa sauti ya watu wa Ukerewe.
Hongera kwa kuwa mwakilishi sahihi
Pole sana kwa msiba mkubwa wa wapiga kura wako.
Pumzike kwa amani Walipoteza maisha wote.
Tunawaombea majeruhi kupona haraka.
Serikali hii inapaswa kuwajibika kwa kila uzembe ulipelekea hili kuanzia Waziri Mkuu.
Waziri hataki sisi kukosoa, tufungeni tu maana kama hamko tayari kuheshimu mawazo ya wawakilishi wa wananchi mnakuwa defensive bila aibu, tutasema mpaka muondoke siku moja, huu ni wajibu wetu, najua mawaziri wengi mnatamani kuwa katika nafasi tuliyopo sisi ili nanyi mkosoe maana hamko free.
Patrick Ole Sosopi
M/Kiti BAVICHA Taifa
 
Jiwe huwa hakanyagi sehemu ambazo serikali yake inalaumiwa. Hufika tu sehemu ambazo anaweza kujisifu na majigambo yake kurushwa live.
 
Funzo mtatoa kabisa sikupingi ila kwa kutumia kijani B 'aka' vyombo vya dola. Kama mnataka kutoa funzo na kujipambanua mnaweza kweli, tuweke tume huru na muache kutumia kijani b . Tutawanyoa ndevu bila dawa wala mashine mapema Sana. Boss zenu wanajuwa hilo ndio maana wamejipachika kijani b, full nguvu all the time.
Haya maneno ya kejeli yalitolewa sana na CCM kabla ya 2015 ila saivi CCM wanajitahidi kuwa wanyenyekevu. Kwa wazoefu humu watamkumbuka @MalariaSugu alikuwa na majibu na maneno ya kejeli na ya kujitoa akili kama haya. 2020 na nyie tutawapa funzo, muda wetu na sisi utafika ila mjue tu Ukerewe mmeshaipoteza.
 
Magamba wanajitoa akili, wametekenywa kwa mkutano wa pole tu, sasa hivi wanakata viuno kwa mtekenyo , waache wahangaike nalo hilo.
Akili zao wanazijua wenyewe ni waoga sana
 
View attachment 875561
Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa Chadema(@official_bavicha_taifa)
Mhe. Joseph Nkundi, ukiwa Mwakilishi wa wananchi wa Ukerewe tunakupa pole sana kwa kuondokewa na wananchi wako, ambao walikuchagua ili uwatetee lakini watawala wakaamua kuziba masikio yao kwa pambaa na kukupuuza kwa wito wako ulioutoa bungeni. Walitamani kusikia wanayopenda kwa masikio yao lakini sio kusikiliza mahitaji ya wananchi wako waliokutuma Bungeni. Usivunjike moyo endelea kupamabana naendelea kuwa sauti ya watu wa Ukerewe.
Hongera kwa kuwa mwakilishi sahihi
Pole sana kwa msiba mkubwa wa wapiga kura wako.
Pumzike kwa amani Walipoteza maisha wote.
Tunawaombea majeruhi kupona haraka.
Serikali hii inapaswa kuwajibika kwa kila uzembe ulipelekea hili kuanzia Waziri Mkuu.
Waziri hataki sisi kukosoa, tufungeni tu maana kama hamko tayari kuheshimu mawazo ya wawakilishi wa wananchi mnakuwa defensive bila aibu, tutasema mpaka muondoke siku moja, huu ni wajibu wetu, najua mawaziri wengi mnatamani kuwa katika nafasi tuliyopo sisi ili nanyi mkosoe maana hamko free.
Patrick Ole Sosopi
M/Kiti BAVICHA Taifa
 
Wananchi hswahitaji maziko ya kitaifa, wanahitaji ufumbuzi wa haraka wa vivuko, wanahitaji vivuko madhubuti. Kifupi usafiri ziwani Victoria ni ticking bombs. Kwa nini tusubiri hadi majanga yatokee ndio tu react? Why there is no proactive strategies?

Planning officers wawajibishwe.
 
Kwenye lii ajali ya kivuko siasa haikwepeki sababu imesababishwa na uzembe wa serikali iliyoko madarakani.
Ingekuwa janga la asili tungekubali ni makosa kuhusisha siasa.
RIP wahanga.
 
Mbona hazifanani na salaam za Pole? Salaam za pole zinaingiza kunangana?
 
Mkulu alisema mstafute kiki kwenye hili suara ila ccm wameona watumie fursa hii kwa viongoz kwenda huko
 
Mbona hazifanani na salaam za Pole? Salaam za pole zinaingiza kunangana?
 
Na hii ndio Siasa safi na ya ukomavu.....poleni sana wafiwa
 
Back
Top Bottom