UKAWA kugomea kura ya maoni ya katiba ni kujivisha kitanzi uchaguzi mkuu 2015

UKAWA kugomea kura ya maoni ya katiba ni kujivisha kitanzi uchaguzi mkuu 2015

Hayo ni maoni yako ya kipumbavu. Watanzania tulitoa mapendekezo kuhusu maadili ya Viongozi pindi watakapofanya ufisadi, wizi au ubadhirifu wa mali ya umma. Hayo yote yameondolewa. Mafisadi kama akina Mkapa, Kikwete, Chenge, Tibaijuka na wengineo wengi wataachwa huru buka kufanywa lolote lile pindi wanapotuhujumu Watanzania. Wabunge wazembe ambao hawana manufaa yoyote kwa majimbo yao wataendelea kuwa Wabunge mpaka wamalize muda wao. Hii ni mifano miwili tu kati ya mingi ambayo ni motivation kubwa ya kuikataa hii katiba ya wahuni na mafisadi.

Hakika Ukawa Ni Wasaka Tonge Ndani Ya Ile Katiba Kuna Haki Za Wakulima,wafugaj,walemavu,wavuvi,vijana Na Wanawake Lakini Ukawa Haya Yote Hawayataki Wao Wanataka Mambo Ya Kuwapeleka Ikulu Tu,hakika Ukawa Hawana Uzalendo
 
.

Katika thead ya jana niliandika kuw ahoja ya mnyika haina maana kwa kuwa inawezekana sana haijashirikisha wenzao wa UKAWA pia madhara ya kusita kisha kuingia kichwa kichwa. Kama ni kususa jambo hili lingalifanyika mapema. Kitendo cha Mnyika kuanza kulialia ni ishara ya viongozi kukosa kujipanga sasa wanahofia defeat.


Nawaambieni hakuna mwaka wapinzani hasa CDM wamekoroga mambo kama mwaka 2015. Pia msije kuwa na mawazo ya kuitisha maandamano kwa kuwa wananchi hawaungi mkono hayo wananchi wanataka kupambana na CCM uwanjani
 
Tuko,

..uko sahihi by 50%.

..katiba kugomewa huku Tanganyika siyo jambo linaloweza kuitisha CCM.

..lakini Znz wakigoma ni jambo kubwa na la hatari sana ktk muungano wetu.

..kumbuka kwamba katiba inabidi ikubaliwe pande mbili za muungano, Tanganyika na Zanzibar.
Hili jambo niliwahi kuwatahadharisha UKAWA

Tuko yupo sahihi kuwa kutojiandikisha inaweza kuwa ni sehemu ya ‘voter suppression'' na kwamba uchaguzi mkuu ni CCM watakaokuwa wamejiandikisha
Hivyo hoja hapa ni kuwa lazima watu wajiandikishe kwa matayarisho ya chaguzi na si kura ya maoni

Kuhusu kura ya maoni, hilo lisusiwe kwasababu haikutokana na wananchi.
Na hadi sasa inaonekana imeshasusiwa.
UKAWA wasizungumzie kabisa kura ya maoni ili kutotoa uhalali wa mzoga

Kura ya maoni ya CCM hakuna namna ya kuizuia isishinde.
Kama Samwel Sitta amefanya madudu ya wizi bungeni kwenye watu 600 na kisha kupewa nishani kwa utendaji hovyo, hakuna namna tume ya uchaguzi (NEC) ya CCM inaweza kutoa matokeo tofauti na maelezo ya mgaogoni. Hatuna tume huru.

UKAWA waendelee kudai katiba, na kama itakuwa ni lazima basi ile rasimu ya Warioba irudi mezani si hii ya Chenge na genge la mafisadi wengine.

UKAWA wanaweza kutumia sheria za uchaguzi kukiukwa kama inavyofafanuliwa. Kwamba, JK anakiuka sheria alizosaini kwa kulazimisha kura ya maoni chini ya ratiba na muda uliopangwa


Mgogoro wa kikatiba hauepukiki, tayari JK ameshatengeneza fertile environment, nadhani si jambo jema lakini kuna busara ndani yake.

Hiyo ndiyo itakuwa lesson na turning point ya wananchi kusikilizwa. Itakuwa painful lakini tukubali kuwa haki haipatikani katika sahani ya dhahabu.
Haki haiombwi inatafutwa na huu ndio wakati wa kuwaambia watawala, tumechoka na tupo tayari kujitetea

Muhimu zaidi, wananchi waache kabisa kuzungumzia katiba ya Chenge.
Si maoni yao.Hata kama itachukua miaka 10 mingine, ni bora kuliko mafisadi walioandika katiba ili kuleta msisimko na kuficha wizi wao wa Escrow

Ukitaka kujua hilo angalia, wote waliokuwa vinara wa katiba ni sehemu ya ufisadi.
 
Last edited by a moderator:
.

Katika thead ya jana niliandika kuw ahoja ya mnyika haina maana kwa kuwa inawezekana sana haijashirikisha wenzao wa UKAWA pia madhara ya kusita kisha kuingia kichwa kichwa. Kama ni kususa jambo hili lingalifanyika mapema. Kitendo cha Mnyika kuanza kulialia ni ishara ya viongozi kukosa kujipanga sasa wanahofia defeat.


Nawaambieni hakuna mwaka wapinzani hasa CDM wamekoroga mambo kama mwaka 2015. Pia msije kuwa na mawazo ya kuitisha maandamano kwa kuwa wananchi hawaungi mkono hayo wananchi wanataka kupambana na CCM uwanjani

Kweli mkuu, wananchi wanashauku ya kuendelea kupambana na CCM kwa nguvu zao zote, mfano mzuri hamasa iliyokuwepo kwenye uchaguzi serikali za mitaa, sehemu nyingi wananchi wapigana sana kwa kulinda kura, UKAWA waache uoga, wananchi wakishuka morali huo utakuwa mwisho wa UKAWA
 
mi naona kuna mtu ama usalama wa taifa kajipenyeza anawashauri UKAWA hivi hawajui hili jambo limewaathiri sana baadhi ya raia
 
Hili jambo niliwahi kuwatahadharisha UKAWA

Tuko yupo sahihi kuwa kutojiandikisha inaweza kuwa ni sehemu ya ‘voter suppression'' na kwamba uchaguzi mkuu ni CCM watakaokuwa wamejiandikisha
Hivyo hoja hapa ni kuwa lazima watu wajiandikishe kwa matayarisho ya chaguzi na si kura ya maoni

Kuhusu kura ya maoni, hilo lisusiwe kwasababu haikutokana na wananchi.
Na hadi sasa inaonekana imeshasusiwa.
UKAWA wasizungumzie kabisa kura ya maoni ili kutotoa uhalali wa mzoga

Kura ya maoni ya CCM hakuna namna ya kuizuia isishinde.
Kama Samwel Sitta amefanya madudu ya wizi bungeni kwenye watu 600 na kisha kupewa nishani kwa utendaji hovyo, hakuna namna tume ya uchaguzi (NEC) ya CCM inaweza kutoa matokeo tofauti na maelezo ya mgaogoni. Hatuna tume huru.

UKAWA waendelee kudai katiba, na kama itakuwa ni lazima basi ile rasimu ya Warioba irudi mezani si hii ya Chenge na genge la mafisadi wengine.

UKAWA wanaweza kutumia sheria za uchaguzi kukiukwa kama inavyofafanuliwa. Kwamba, JK anakiuka sheria alizosaini kwa kulazimisha kura ya maoni chini ya ratiba na muda uliopangwa


Mgogoro wa kikatiba hauepukiki, tayari JK ameshatengeneza fertile environment, nadhani si jambo jema lakini kuna busara ndani yake.

Hiyo ndiyo itakuwa lesson na turning point ya wananchi kusikilizwa. Itakuwa painful lakini tukubali kuwa haki haipatikani katika sahani ya dhahabu.
Haki haiombwi inatafutwa na huu ndio wakati wa kuwaambia watawala, tumechoka na tupo tayari kujitetea

Muhimu zaidi, wananchi waache kabisa kuzungumzia katiba ya Chenge.
Si maoni yao.Hata kama itachukua miaka 10 mingine, ni bora kuliko mafisadi walioandika katiba ili kuleta msisimko na kuficha wizi wao wa Escrow

Ukitaka kujua hilo angalia, wote waliokuwa vinara wa katiba ni sehemu ya ufisadi.

..itabidi UKAWA wake creative/crafty kwa kuwashawishi wanachama wao kujiandikisha kwa wingi lakini wasishiriki ktk kura ya maoni.

..pia kwenye uchaguzi mkuu Ukawa wahakikishe kwamba wanashinda in the 1st round by knock out. wakizembea wakapata ushindi kiduchu, wajue imekula kwao. they need to win by such big numbers so that it impossible to rig the elections.

cc Molemo, Tuko, Candid Scope
 
Last edited by a moderator:
Binafsi naunga mkono wazo la ukawa kususia mchakato huu! Madudu yaliyofanyika kwenye mchakato huu hayavumiliki. Kuna watu wamefukuzwa kazi kwa kuonewa katika mchakato huu, mfano aliyekuwa mwanasheria mkuu wa zanzibar, kuna watu wametukanwa na kudhalilishwa mfano mh. Joseph warioba. Kwenye bunge maalumu kulikuwa na wajumbe wa upande mmoja ccm. Waachiwe wenye wao, walioukoroga na kuuvuruga mchakato huu. Heko ukawa.
 
Mkuu mimi siangalii matokeo ya kura ya maoni... bali impact yake kwenye uchaguzi mkuu ujao...

Wakishiriki ndio kabisaa watakuwa ''wameidhinisha'' uchaguzi wenyewe na hawatakuwa na cha kuwaambia wananchi. Infact mimi napendekeza hata wakiona uchaguzi mkuu hautakuwa fair wasikubali kushiriki. Unajua kule kujitoa kwenye bunge la katiba kumewanyayua sana sana UKAWA na wangeendelea kukomaa ndani kama watu wengine walivyoshauri matokeo yake yangekuwa mabaya. Mpaka sasa CCM hawajiamini na hawajui kilichopo mbele, hivyo wakisusiwa tena kura wataweza kufa kwa kihoro.
 
..itabidi UKAWA wake creative/crafty kwa kuwashawishi wanachama wao kujiandikisha kwa wingi lakini wasishiriki ktk kura ya maoni.

..pia kwenye uchaguzi mkuu Ukawa wahakikishe kwamba wanashinda in the 1st round by knock out. wakizembea wakapata ushindi kiduchu, wajue imekula kwao. they need to win by such big numbers so that it impossible to rig the elections.

cc Molemo, Tuko, Candid Scope
Ttatizo la UKAWA, mara zote hucheza mirindimo ya ngoma za CCM

Kwa mfano, niliwahi kumsikia Maalimu Seif na washirika wake wa CUF wakisema ''katiba haikubaliki, haipiti''

Kwamba wameridhika kwenda kwenye kura ya maoni ya mzoga.

Hapa si suala la kukubali au kukataa, si suala la kura ya Ndiyo au Hapana, ni suala la kutoongelea kabisa katiba ya Chenge.
Ni suala la kuwaambia wananchi madai ya katiba mpya kama walivyokuwa nayo badoo yapo pale pale

Wakipotea njia na kuanza kuzungumzia kura ya maoni, maana yake wameletewa mzoga na sasa wanachagua mzoga ni mbaya, mbaya sana au unalika.

Hii ni hatari kwasababu CCM wanatafuta legitimacy ya mjadala wakijua kura ya maoni watafanya ya ya aibu ya mzee John Samwel Sitta, kukaa na CCM na kuiba kura mbele ya bunge bila aibu haya au kujali umri wake.

Hoja hapa UKAWA waache kabisa kuzungumzia katiba, wao wahamasishe wananchi kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu.
Yaani hoja yao iwe, jiandikikisheni kwa ajili ya uchaguzi mkuu ili UKAWA washinde na kuandika katiba mpya.

Na mwisho UKAWA warudi katika tume huru ya uchaguzi.
Si suala la tume ndani ya katiba, bali marekebisho ya tume huru kuelekea 2015.

CCM hawataki kusikia tume huru kwasababu turufu waliyo nayo ni Tume ya uchaguzi.
Nadhani unaona jinsi mwenyekiti wa tume anavyopokea maagizo kutoka Ikulu.

Maagizo ya mwisho ilikuwa kuomba jeshi liandikishe wananchi.

Hivi mkuu wa tume ya uchaguzi ana uhusiano gani na jeshi?
Na ni lazima kuwa katiba lazima ipatakane leo? CCM wanajua kimbunga kinachokuja ni kikubwa, kofia na khanga hazifanyia kazi tena, vijijini wameasi, mijini hawataki kusikia CCM.

Njia iliyobaki ni moja tu, kutumia tume ya uchaguzi kupata matokeo wanayotaka kusikia na kwa maelezo ya Rais.

UKAWA wachange karata zao vizuri
 
watanzania watambue kuwa kunasheria na mipango pingamizi maalum iliyoandaliwa na chenge(vijisenti)hebu tafakari zoezi la uandikishaji teknolojia mpya(bvr)siwadau wala wahusika ni mazingaombwe,nakala za katiba pendekezwa nasheria ya kura ya maoni,nihadithi,nchi inayotawaliwa kwamujibu wa katiba kwamazingira haya utafanya nn kesho na keshokutwa ukiamini hujavunja katiba
 
Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba
ya Wananchi (Ukawa) vimetangaza
rasmi kutoshiriki katika mchakato wa
kura ya maoni ya katiba na kwamba
kuanzia sasa vitahamasisha wananchi
kuunga mkono.
Uamuzi huo umetolewa leo na
wenyeviti wa vyama wanaounda umoja
huo wa ukawa ambao ni Mwenyekiti wa
Chadema, Freeman Mbowe, Mwenyekiti
wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba,
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James
Mbatia na Mwenyekiti wa NLD, Makaidi.
Akizungumza wakati wa kutoa
msimamo huo Profesa Lipumba
amesema wamefikia uamuzi wa
kutoshiriki katika zoezi hilo kwa sababu
mchakato mzima haukuwa na
maridhiano ya kitaifa.
“Vyama vya siasa ikiwemo CCM
vilikubaliana mwaka jana kwamba zoezi
la kura za maoni lifanyike mwaka 2016
baada ya uchaguzi mkuu, tulisaini wote
na Rais Jakaya Kikwete alikubali, kwa
nini mabadiliko yafanyike ghafla”
amehoji Profesa Lipumba.
Amesema jambo la kushangaza, Rais
Kikwete aligeuka na kutangaza
kwamba Aprili 30, mwaka huu kuwa
siku ya kupiga kura ya maoni kuhusu
Katiba Mpya.
Amesema pamoja na kutangaza siku
ya kupiga kura, bado uandikishaji
katika daftari la wapiga kura haujaanza
kwa sababu wanasubiri vifaa.
“Hadi sasa vifaa vya Biometric Voter
Registration (BVR) vilivyopo ni seti 250
wakati vinavyohitajika ni seti 7500,
tume inasubiri hadi sasa, zoezi hili
litafanyika kweli?,” alihoji Lipumba.
“Mbinu hiyo inafanywa na Serikali kwa
sababu Wazanzibari ndiyo wanaona
kikwazo kwao,” alisema Makaidi.
Aprili 16 mwaka jana, Wabunge wa
Bunge Maalum la Katiba kutoka vyama
vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na
NLD walitoka nje wakidai bunge hilo
lilikuwa halijadili maoni ya wananchi
yaliyowasilishwa na Tume ya
Mabadiliko ya Katiba.
Usiache kusoma gazeti la Mwananchi
kesho kwa undani Zaidi..
 
Hili jambo niliwahi kuwatahadharisha UKAWA

Tuko yupo sahihi kuwa kutojiandikisha inaweza kuwa ni sehemu ya ‘voter suppression’’ na kwamba uchaguzi mkuu ni CCM watakaokuwa wamejiandikisha
Hivyo hoja hapa ni kuwa lazima watu wajiandikishe kwa matayarisho ya chaguzi na si kura ya maoni

Kuhusu kura ya maoni, hilo lisusiwe kwasababu haikutokana na wananchi.
Na hadi sasa inaonekana imeshasusiwa.
UKAWA wasizungumzie kabisa kura ya maoni ili kutotoa uhalali wa mzoga

Kura ya maoni ya CCM hakuna namna ya kuizuia isishinde.
Kama Samwel Sitta amefanya madudu ya wizi bungeni kwenye watu 600 na kisha kupewa nishani kwa utendaji hovyo, hakuna namna tume ya uchaguzi (NEC) ya CCM inaweza kutoa matokeo tofauti na maelezo ya mgaogoni. Hatuna tume huru.

UKAWA waendelee kudai katiba, na kama itakuwa ni lazima basi ile rasimu ya Warioba irudi mezani si hii ya Chenge na genge la mafisadi wengine.

UKAWA wanaweza kutumia sheria za uchaguzi kukiukwa kama inavyofafanuliwa. Kwamba, JK anakiuka sheria alizosaini kwa kulazimisha kura ya maoni chini ya ratiba na muda uliopangwa


Mgogoro wa kikatiba hauepukiki, tayari JK ameshatengeneza fertile environment, nadhani si jambo jema lakini kuna busara ndani yake.

Hiyo ndiyo itakuwa lesson na turning point ya wananchi kusikilizwa. Itakuwa painful lakini tukubali kuwa haki haipatikani katika sahani ya dhahabu.
Haki haiombwi inatafutwa na huu ndio wakati wa kuwaambia watawala, tumechoka na tupo tayari kujitetea

Muhimu zaidi, wananchi waache kabisa kuzungumzia katiba ya Chenge.
Si maoni yao.Hata kama itachukua miaka 10 mingine, ni bora kuliko mafisadi walioandika katiba ili kuleta msisimko na kuficha wizi wao wa Escrow

Ukitaka kujua hilo angalia, wote waliokuwa vinara wa katiba ni sehemu ya ufisadi.

Kwanza UKAWA wanatakiwa watambue kuwa wana karata ya turufu, kupita au kutopita kwa katiba mpya kunawapa nafasi ya kuhoji uhalali wa ccm.
Kwa mantiki hiyo wasipoteze muda mwingi sana kupigana vita ambavyo wameisha shinda tayari, ila waangalie ni kwa jinsi gani vita hii ya katiba inaweza kupoteza focus ya uchaguzi wa oktoba. Wapiga kura wetu walio wengi ni wazito katika kuyumba huku na huko, kwamba leo umwambie usipige halafu kesho useme piga kura, hii itawachanganya wengi.

Ni vizuri kwamba uandikishaji wa wapiga kura iwe priority no. 1. CCM wanajua kuwa wengi wa waliojiandikisha ni wafuasi wao (mawazo yangu), hivyo wanawaogopa zaidi hawa wapya. Wakifanikiwa ku-frustrate zoezi la kuandikisha new registered voters itakuwa ni ushindi mkubwa kwao

Kwamba wananchi wasusie kura ya maoni kwa sababu katiba haikutokana na wananchi, NO, haina mantiki kwa sababu hata kwenye uchaguzi mkuu sio wagombea wote watatoka kwa wananchi. Kuukataa uhalali wa mzoga you must say NO!

Kusimamia kura ya maoni ni kama mechi nyingine ya majaribio kuona udhaifu wa usimamizi ukoje. Hii itasaidia kuweka mikakati bora kwa tukio kuu la october.

Nachelea kusema ccm watapenda sana ukawa wasuse kama ilivyo kuwa kwenye bunge la katiba, iliwapa nafasi ya kufanya kila mbwembwe na hakuna aliyewauliza. Walipewa uhuru wa kupika mapishi wayapendayo.
 
Last edited by a moderator:
Kwamba wananchi wasusie kura ya maoni kwa sababu katiba haikutokana na wananchi, NO, haina mantiki kwa sababu hata kwenye uchaguzi mkuu sio wagombea wote watatoka kwa wananchi. Kuukataa uhalali wa mzoga you must say NO!

Kusimamia kura ya maoni ni kama mechi nyingine ya majaribio kuona udhaifu wa usimamizi ukoje. Hii itasaidia kuweka mikakati bora kwa tukio kuu la october.

Nachelea kusema ccm watapenda sana ukawa wasuse kama ilivyo kuwa kwenye bunge la katiba, iliwapa nafasi ya kufanya kila mbwembwe na hakuna aliyewauliza. Walipewa uhuru wa kupika mapishi wayapendayo.
Kuna mambo mawili pengine hujaweza kuyapambanua
UKAWA walipoondoka bunge lengo kubwa ni kutokuwa sehemu ya mchakato uliokuwa unachakachuliwa.
Hivyo walitaka kuji-dissociated na process nzima ambayo kwao ilikuwa null and void ab initio


Kwenda kuongelea kura ya ‘ndiyo au hapana' ni kutoa uhalali kwa mchakati ule ule walioukataa.
Endapo ni hivyo, kulikuwa hakuna sababu za wao kutoka kwasababu wangeweza kubaki na kupiga kura ya ‘hapana' bungeni ambayo sisingebailfilisha matokeo kutokana na process nzima kuwa ya hovyo kama Samwel Sitta alivyoiendesha


CCM walijua kuwa bunge ndicho kikwazo kwao. Ndio hasa maana ya kuchakachua kura hata pale walipobaki wenyewe.
Walitambua kuwa nje ya bunge uwezekano wa kutumia tume yao ya uchaguzi kufanya uhalaifu upo. Na hicho ndicho wanakifanya sasa.


Kuzungumzia katiba na kura ya maoni ndicho wanakitaka ili kutoa uhalali kuwa mchakato mzima ulikuwa umekubalika na kilichoamua ni kura ya maoni.Yaani wanatupa mzoga wakijua wana mbinu za wewe kuuchukua halafu unashiriki katika kuamua ima uchukue mzoga au la.

Mzoga ni mzoga hauna mjadala, hata wewe nyumbani kwako huwezi kuletewa mzogo wa paka, kisha mtu akwambie mjadiliane ndiyo au hapana. Kwa mtu mwenye akili, hatakubali hata kusikiliza hadithi za mzoga huo na hatafikiria kusema ndio au hapana.

Wananchi wasiingizwe mkenge kujadili katiba ya Chenge/Sitta. Waache CCM wapitishe ili wananchi nao wajenge uhalali wa kupata katiba yao.

Tatizo ulilonalo wanalo Watanzania wengi. Kwamba, basi hata hicho kibaya ni afadhali.

Hakuna haramu nzuri kidogo, haramu ni haramu na katiba hii iliyoandikwa na mafisadi ili kuficha escrow ni haramu

Unposema mechi ya majaribio, nakushangaa sana. Asali haijaribiwi kwa kisu. Katiba ikishaandikwa ndiyo basi tena, kuna majaribio gani unataka kufanya hapo?


Hata kama itachukua miaka 10 kupata nyingine, hoja si bora katiba ni katiba bora.
 
Hata mimi siungi mkono kususia kuara ya maoni. Kwa kuwa ni dhahiri kwamba katiba hii ingefia Zanzibar, bado credit na ushindi ungekuwa kwa UKAWA na hiyo ingewabeba hadi uchaguzi mkuu. Sasa najiuliza kama watasusia, je watahamasisha wanachama na wafuasi wao kujiandikisha? Itakuwa vigumu na hapo ndiyo itakuwa machinjio ya UKAWA.
 
kushiriki kupiga kura ni jambo zuri sana hata kama katiba itapita itakua imetoa kipimo cha nguvu ya UKAWA.
lakini kutoshiriki ni ujinga wa hali ya juu, uovu hauwezi kuonfolewa kwa kususa kama wanawake aibu kwa LIPUMBA, MBOWE na MBATIA laana itawandama
 
Kuna mambo mawili pengine hujaweza kuyapambanua
UKAWA walipoondoka bunge lengo kubwa ni kutokuwa sehemu ya mchakato uliokuwa unachakachuliwa.
Hivyo walitaka kuji-dissociated na process nzima ambayo kwao ilikuwa null and void ab initio


Kwenda kuongelea kura ya ‘ndiyo au hapana’ ni kutoa uhalali kwa mchakati ule ule walioukataa.
Endapo ni hivyo, kulikuwa hakuna sababu za wao kutoka kwasababu wangeweza kubaki na kupiga kura ya ‘hapana’ bungeni ambayo sisingebailfilisha matokeo kutokana na process nzima kuwa ya hovyo kama Samwel Sitta alivyoiendesha


CCM walijua kuwa bunge ndicho kikwazo kwao. Ndio hasa maana ya kuchakachua kura hata pale walipobaki wenyewe.
Walitambua kuwa nje ya bunge uwezekano wa kutumia tume yao ya uchaguzi kufanya uhalaifu upo. Na hicho ndicho wanakifanya sasa.


Kuzungumzia katiba na kura ya maoni ndicho wanakitaka ili kutoa uhalali kuwa mchakato mzima ulikuwa umekubalika na kilichoamua ni kura ya maoni.Yaani wanatupa mzoga wakijua wana mbinu za wewe kuuchukua halafu unashiriki katika kuamua ima uchukue mzoga au la.

Mzoga ni mzoga hauna mjadala, hata wewe nyumbani kwako huwezi kuletewa mzogo wa paka, kisha mtu akwambie mjadiliane ndiyo au hapana. Kwa mtu mwenye akili, hatakubali hata kusikiliza hadithi za mzoga huo na hatafikiria kusema ndio au hapana.

Wananchi wasiingizwe mkenge kujadili katiba ya Chenge/Sitta. Waache CCM wapitishe ili wananchi nao wajenge uhalali wa kupata katiba yao.

Tatizo ulilonalo wanalo Watanzania wengi. Kwamba, basi hata hicho kibaya ni afadhali.

Hakuna haramu nzuri kidogo, haramu ni haramu na katiba hii iliyoandikwa na mafisadi ili kuficha escrow ni haramu

Unposema mechi ya majaribio, nakushangaa sana. Asali haijaribiwi kwa kisu. Katiba ikishaandikwa ndiyo basi tena, kuna majaribio gani unataka kufanya hapo?


Hata kama itachukua miaka 10 kupata nyingine, hoja si bora katiba ni katiba bora.

Nimekuelewa, looks to be a more advanced strategy.
 
Tuko,

..uko sahihi by 50%.

..katiba kugomewa huku Tanganyika siyo jambo linaloweza kuitisha CCM.

..lakini Znz wakigoma ni jambo kubwa na la hatari sana ktk muungano wetu.

..kumbuka kwamba katiba inabidi ikubaliwe pande mbili za muungano, Tanganyika na Zanzibar.


cc Barubaru, takashi, Kibunango, Nguruvi3, GHIBUU

Usijidanganye, kura zitakazo pigwa ndo zitakazo hesabiwa, Kama wazanzibari watagoma, wazanzibara walobaki watapiga kura,hata kama Mia moja Kama katika Mia kuna theluthi mbili imepita.
 
Last edited by a moderator:
Huko nyuma CUF walisusia uchaguzi, matokeo yake ilikuwa ni ahueni kwa chama tawala, ni bora kama wana nia ya kweli kuingia kwenye upigaji kura na kufanya kampeni ya nguvu kuwahamasisha kura za hapana. Faida ni kwamba wanaweza kutaja vipengele vingi vyenye utata kwani kura ya hapana mtu anaweza kuipiga kwa kipengele kimoja tu kinachomgusa mpiga kura tofauti na kura ya ndio ambayo inahusu katiba nzima. Kwa matokeo yo yote upinzani utakuwa na nafasi kuingiza kipengele cha kubadilisha katiba katika manifesto (ilani ya uchaguzi)
 
Back
Top Bottom