Elections 2015 UKAWA kusimamisha mgombea Urais 2015

Elections 2015 UKAWA kusimamisha mgombea Urais 2015

Warioba atawafaa maana wanafanana naye kwa kugeukageuka kama kinyonga:
-Kwanza alisema Serikali 3 ni maoni ya walio wengi,
-lakini baada ya kubwanwa na kwa hoja za kitakwimu akageuka,
-akasema pale kwenye mkutano ubungo kwamba walizingatia hoja na siyo takwimu.
Huyu ndiye Warioba mtatanishi.
 
Mkuu hata akisimama Warioba bado watamwaga fedha..... dawa ni kula hela za wajinga halafu kura unapiga kwa unayemtaka

Mkuu Mungi 2010 Karatu iliwashangaza watu, walivaa Kofia, Skafu, vitenge vya CCM kwenye kampeni na kura wakapigia CDM, matokeo yalipotangazwa na kofia zao, skafu zao, vitenge vyao wanashangilia ushindi wa CDM.
 
Nimetafakari kwamba UKAWA ina wagombea wawili Prof Lipumba na Dr Slaa. Wote ni wagombea na viongozi bora. Ila tactically angepewa Prof Lipumba kama compromise candidate. Sababu ni kwamba ni rahisi Lipimba kukibalika pwani na bara au maeneo ya waislam na wakristo. Dr slaa atapigwa vita ya udini hasa kwamba alikuwa padri itamuumiza maeneo ya waislam. Chadema wakubali kikubwa ccm itoke kwanza
 
Mbona unakurupuka bro? Ukawa inaendeshwa kisayansi zaidi. Mambo ya udini ni ya ccm na vibaraka wake. Na muda wa kujadili mgombea urais huku kwetu bado ni kwenu maccm ndio mnataka kutoana roho kwa uroho wa madaraka. Tena nadhani Le Mutuz atawafaa sana maana huko kila mtu anadhani atakuwa raia. Hata Mwigulu!
 
Yeyote aliye ndani ya ukawa anatufaa kuwa mkuu wetu wa nchi. Ni swala la muda tu tulieni mtapenda wenyewe muda ukifika.kwa sasa tunajadili katiba mpya iliyobakwa na magamba
 
kwani Lipumba hazungumzi msikitini? kwa hiyo maneno ya waislam ndio yamzuie mkristo kugombea nafasi za uongozi? kama maneno yana nafasi kubwa kiasi hicho itabidi na wakristo waanze kuiga maneno hayo yakibaguzi maana yana nafasi kubwa kumbe kiuongozi.
 
Maoni yangu kwa watu wasio na uwezo mkubwa wa kufikiri hawawezi kuyaona ya maana. Lipumba atakubalika kuanzia Pemba hadi Biharamulo. Ukweli Dr SLaa ana watu wengi zaidi ila CCM watapunguza sana kura za maeneo niliyotaja kwa karata ya udini ambayo kwa kiasi fulani ita work. Lipumba ni ngumu kutumia hoja yeyote kumpinga na ndio maana nikasema atakuwa tactical candidate🙂 sioni kitakachomzuia Lipumba asishinde
 
hizi habari za uzushi hazina ukweli wowote
 
Asalaam waungwana,
Neno langu ni moja kuhusu mkutano mkuu wa chadema.
Leo UKAWA wametoa salamu nzito kwa ccm,umoja na mshikamano ndani ya UKAWA.
Slaa amewaita Lipumba na Mbatia ndugu wa damu,Mbowe awewasalimia Lipumba na Mbatia kwa kuwakumbatia(hagging) ilhali amemsalimu Mangula kwa kumpa mkono kwa mbali.
Kwa mwendo huu ccm wajiandae kisaikolojia
 
Mimi ni CCM damu, ila linapokuja suala la maslahi kwa Taifa huwa CCM huwa inakuwa nambari MBILI. Manake tulio wengi huwa tunachezeshwa ngoma tusiyoijua na wapenda madaraka ili waendelee kututawala. Mzee Sinde Warioba pamoja na makada wenzetu wa CCM ambao waliteuliwa kukusanya maoni kwenye tume ya mabadiliko ya katiba walitanguliza Utanzania kwanza na kuacha UCCM kando na ndio maana wakaja na mapendekezo yaliyotokana na watanzania pamoja na kuangalia mahitaji ya sasa kwa Watanzania, cha ajabu wapenda Uraisi wakaona mapendekezo haya ya watanzania yanaweza yakawa kikwazo cha wao kusaka uraisi.

Ushauri wangu ni kwamba ili kazi iliyofanywa na tume ya Warioba ya kutuletea katiba mpya ambayo ndio mkataba kati ya watawala na watawaliwa na hivyo kuwa msingi mkuu wa maendeleo yetu, hivyo ningewashauri UKAWA waachane na kusaka uraisi na kumshawishi Mzee Warioba Akubali kusimama kama mgombea kupitia mgombea atakayeteuliwa na ukawa na hapo ndipo ukombozi wa Mtanzania utapatikana kwa kila mmoja wetu kuwaunga mkono.

Mkisimama peke yenu hamuwezi kuishinda CCM kwani wana fedha za kumwaga.

Mtazamoo wako
 
Kwa hali ya kisiasa nchini, Chadema imeimarika zaidi ya miaka ilio pita kama 2010, naweza kusema kwamba Chadema jinsi ilivyo imarika ni Mara Mbili au tatu an zaidi ya 2010, hivi tujiulize ccm 2015 itakuwa hai? Kwa vigezo vipi? Hebu tuangalie uchaguzi wa 2010.
MATOKEO RASMI YALIYOTANGAZWA LEO

1. KUGA PETER MZIRAY APPT - MAENDELEO: 96, 933 (1.12%)

2. KIKWETE JAKAYA MRISHO/CCM: 5,276,827 (61.17%)

3. SLAA WILLIBROD PETER/CHADEMA: 2,271,941 (26.34%)

4. LIPUMBA IBRAHIM HARUNA/CUF: 695,667 (8.067%)

5. RUNGWE HASHIM SPUNDA/NCCR-MAGEUZI: 26,388 (0.31%)

6. MGAYWA MUTTAMWEGA BHATT/TLP:17,482 (0.20%)-

7. DOVUTWA YAHMI NASSORO DOVUTWA/UPDP: 13,176 (0.15%)

----------------------------------------------

WALIOJIANDIKISHA KUPIGA KURA: 20, 137, 303

WALIOJITOKEZA KUPIGA KURA: 8, 626 (42.64%)

KULA HALALI ZILIZOPIGWA: 8,398,394

KURA ZILIZOHARIBIKA 227,889 (2.64)

Ukiangalia hapo ccm imeanguka asilimia 20 ukilinganisha uchaguzi wa 2000 -2005, hivyo 2015 tunaizika, tuanze kushona sanda, ah haina haja mana hawa wamekula mali za umma sana.

Ukawa oyeee,
Tanganyika kwanza
Zanzibar kwanza,
Shirikisho daima
 
Kwa hali ya kisiasa nchini, Chadema imeimarika zaidi ya miaka ilio pita kama 2010, naweza kusema kwamba Chadema jinsi ilivyo imarika ni Mara Mbili au tatu an zaidi ya 2010, hivi tujiulize ccm 2015 itakuwa hai? Kwa vigezo vipi? Hebu tuangalie uchaguzi wa 2010.
MATOKEO RASMI YALIYOTANGAZWA LEO

1. KUGA PETER MZIRAY APPT - MAENDELEO: 96, 933 (1.12%)

2. KIKWETE JAKAYA MRISHO/CCM: 5,276,827 (61.17%)

3. SLAA WILLIBROD PETER/CHADEMA: 2,271,941 (26.34%)

4. LIPUMBA IBRAHIM HARUNA/CUF: 695,667 (8.067%)

5. RUNGWE HASHIM SPUNDA/NCCR-MAGEUZI: 26,388 (0.31%)

6. MGAYWA MUTTAMWEGA BHATT/TLP:17,482 (0.20%)-

7. DOVUTWA YAHMI NASSORO DOVUTWA/UPDP: 13,176 (0.15%)

----------------------------------------------

WALIOJIANDIKISHA KUPIGA KURA: 20, 137, 303

WALIOJITOKEZA KUPIGA KURA: 8, 626 (42.64%)

KULA HALALI ZILIZOPIGWA: 8,398,394

KURA ZILIZOHARIBIKA 227,889 (2.64)

Ukiangalia hapo ccm imeanguka asilimia 20 ukilinganisha uchaguzi wa 2000 -2005, hivyo 2015 tunaizika, tuanze kushona sanda, ah haina haja mana hawa wamekula mali za umma sana.

Ukawa oyeee,
Tanganyika kwanza
Zanzibar kwanza,
Shirikisho daima

ndoto za mchana safiii?
 
Hakuna mgombea ukawa wote hawajitambui wafanye yao urais siyo kazi yao.
 
Back
Top Bottom