UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

Nguruvi3

Platinum Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
15,773
Reaction score
32,431
CCM MAJI YA SHINGO,AIBU YATAWALA, BUNGE LAVUNJIKA KIAINA
WAGAWE UWATAWALE, MBINU INAYOPIKWA DHIDI YA UKAWA
UKAWA KUREJEA MAKOSA YA SIKU ZA NYUMA (JUISI NA CHAI IKULU)


Sehemu ya I

Ndugu wana wanajmvi na wanaduru
Si mara moja au mbili tumeonyesha mwisho wa BMLK(Bunge maalumu la katiba) kutokana na hila zinazoendelea.Wiki iliyopita tulisema ndani ya wiki mbili bunge litavurugika.
Ukweli ni siku 10 tangu tuyaseme.

Kuondoka kwa wajumbe wa UKAWA ndani ya BMLK ni mwiba kwa CCM.
Chama tawala kilikuwa mbioni kuingiza rasimu yao ya mafichoni, soma hapa.... ili ipate ridhaa ya wajumbe kutoka uwakilishi wote hivyo kujenga uhalali.

Rasimu ya CCM iliyoandikwa na kikundi cha watu wachache inaongozwa na Samwel Sitta,soma hapa...... .

Mbinu zilianza ndani ya bunge la JMT kupitisha miswada kibabe kukiwa na mkono mkubwa wa Rais wa JMT. Mbinu zikahamia bungeni, Sitta akapewa jukumu la kusimamia rasimu ya CCM kwa malengo maalumu na dhamira maalumu na wala si wanachama wa CCM.

Ili kuhakikisha rasimu ya CCM inafanikiwa wabunge wa CCM wakakalishwa kitako na kufundishwa nini cha kusema. Hawakupewa nafasi ya kutumia akili zao, wanachotakiwa ni kuimba tu, ndivyo ilivyo sasa bungeni.

Mbinu ya kuhalalisha rasimu ilichomekwa katika kamati za CCM bungeni.
Huko 2/3 ikakosekana. Mh Samwel Sitta akairudisha mbinu hiyo kwa kujadili rasimu kifungu 1 na 6 ndani ya bunge. Mh Sitta alikuwa na sababu, na alifanya hivyo ili kupata 2/3 kwa nguvu.

Katika kamati 2/3 ni ngumu kupatikana, kwa wingi ndani ya bunge na ile 'kamba' ya kura ya wazi 2/3 ingepatikana. Hilo ndilo Sitta, mwakilishi wa kundi la rasimu ya CCM alilolenga.

Sitta akiwa ametumwa na CCM alipanga waongeaji, wengine wakiwakilisha maoni yao na si ya kamati kama alivyofanya Ummy Mwalim.

Kwa kuelewa mpango Mzima Makamu mwenyekiti akaruhusu watu waeleze maoni yao na si ya kamati wakitumia neno 'walio wengi' bunge likachafuka

'Walio wengi' ilikusudia kuubabaisha umma kuwa suala zima linaungwa mkono na wengi.
Hili ni suala la katiba, kinachoangaliwa si wingi bali hoja na mantiki.

Tunakumbuka mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa 'walio wengi' walikataa.
Busara zikaelekeza kuwa hoja na nyakati ni muhimu kuliko walio wengi.

Haiwezekani kuwepo 'walio wengi' tukijua CCM iliwafungia na kuwalazimisha wawe 'wengi'
Mbunge Lembeli alipotoa maoni yake, CCM mkoa ikamshukia kwasababu alikwenda kinyume na 'mafunzo' yaliyoamuliwa na chama. Wapi hoja ya walio wengi inapopatikana?

sehemu ya II bunge linakokotwa kuepeuka aibu

Tutaendelea.........

https://www.jamiiforums.com/great-t...shaji-na-kiwewe-cha-kuzinduka-tanganyika.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...a-katiba-je-katiba-itatokana-na-wananchi.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...-gharama-za-muungano-siri-isiyozungumzwa.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...ba-ya-jk-kuzindua-bunge-maalum-la-katiba.html
https://www.jamiiforums.com/great-t...asa-vijana-katiba-mpya-na-kiu-ya-uongozi.html
 
Sehemu ya II

MBINU ZINAZOPANGWA NA CCM DHIDI YA UKAWA

Baada ya kubainika 2/3 haipatikani, Samwel Sitta akashauri bunge liahirishwe kupisha la bajeti.
Ilijulikana bunge la JMT lazima likae kwa bajeti, ni sababu tu za kukwepa, mbinu zimegonga mwamba.

Sababu hizo zina nguvu zaidi kwa wakati huu. Ingawa Sitta anasema idadi ya wabunge imetimia kuendelea na mjadala, lakini katiba na inahitaji maridhiano.
Kukosekana kwa UKAWA si kwamba kunazidi kuondoa uhalali uliokwishaondoka, bali unatoa picha kuwa CCM ndio inaandika katiba.

Well, CCM wanaweza kufanya hivyo kwavile ubabe ni sehemu ya utamaduni wao, watakachokumbana nacho kwa wapiga kura wao hawana majibu. Ni dalili njema kuwa taifa linahitjai kubadili mwelekeo. Kudharau maoni ya wananchi si njia bora ya kutawala nchi.

CCM na Samwel Sitta wanataka kuitumia nafasi ya kuahirishwa bunge kufanya mambo mengi

1. Kumtumia Rais kutafuta mwafaka na UKAWA kama alivyowahi kufanya.

Rais atatumia hotuba ya April 26 2014 kubadilisha na kuwazulia UKAWA mambo mazito

2. CCM kuwatumia viongozi wake kuzunguka nchini kutisha watu kuhusu rasimu ya Warioba, kupendekeza wanachotaka na kuahidi makubwa kwa wazanzibar. Katika matisho ni yale ya jeshi kuchukua nchi chini ya serikali 3, wazanzibar kufukuzwa na kuua muungano

3. Kuwatisha wabunge wao zaidi katika vikao

Kutakuwa na vikao vya kuwashughulikia walioonyesha kutoridhishwa na maamuzi yaliyopanga msimamo wa serikali 2. Hili halitahusu kuwafukuza, ni kuwatisha ili wawe mfano kwa wengine

4. Kuwanunua wajumbe wa UKAWA kwa hila na mbinu

Wajumbe waliobaki watapewa nafasi sana ya kuongea ili kuondoa hisia za uCCM.
Wale wenye msimamo wa kati na wasiojitambua, aghalabu watafungiwa kitita ili wanyamaze

5.Kuwachonganisha viongozi wa UKAWA ili wafarakane

Kutakuwa na mpango wa kuwachonganisha viongozi wa ukawa kwa kutumia wanachama wa vyama vyao ambao ni mapindikizi.

Kurekebisha sheria zitakazo wapa 2/3 .

Idadi ipatikane kwa waliopiga kura na si wajumbe wote ili kuwezesha kupatikana 2/3 kwa kutumia CCM pekee

6. Kutumia bunge la bajeti kuonyesha kero za znz zimeshughulikiwa

Zanzibar itatengewa fungu kubwa la bajeti kutoka bunge la JMT. ili kuwanyamazisha.
Gharama zakuwafurahisha wazanzibar atazibeba, mkulima, mvuvi na mfanyakazi wa Tanganyika kwa vile kodi zao ni za Tanzania ambayo znz inastahili

7. Kuwashawishi wajumbe wa BLW chini ya Kificho uwezekano wa kurekebisha katiba 2010 inayoleta matatizo na ugumu kwa CCM.

Ni ngoma nzito lakini jaribio lipo mbioni
Wazanzibar CCM watashawishiwa ili kuepuka serikali 3, hakuna budi kubadili katiba ya 2010 inayoleta taabu kwa upande wa CCM sasa hivi.

9 Kuzuia mikutano ya vyama na Ukawa
Hili limeshaanza na lina malengo makubwa mawili

a) Kutoa nafasi ya rais kuwaeleza wananchi kuhusu kususia kwa UKAWA, akiwananga kwa kutumia hoja zao. Tukio litafanyika April 26 siku ya muungano.Kwa kawaida Rais hahutubii, safari hii atafanya hivyo iwe mbeleya mkutano au kuelekea wiki ya maazimisho ya muungano

b) Kuzuia UKAWA kuchukua ‘attention' ya wananchi wakati CCM wanaendelea na bunge lao Dodoma. Kuruhusu mikutano ya UKAWA kutamaanisha kupuuzwa kwa hoja za upotoshaji Dodoma kusikika na kutitia katika masikio ya Watanzania.


Inaendelea ....

 
Sehemu ya III

UKAWA KURUDIA MAKOSA YA NYUMA

Ili kuweka sawa mtiririko wa makosa ya Upinzani ulioungana na ukawa inabidi tupitie baadhi ya matukio muhimu yaliyotokea. Ni katika kuonyesha makosa ya nyuma ambayo leo wapinzani na ukawa wanalipia gharama kubwa.

1. Suala la katiba mpya:
Ilikuwa ni sera ya vyama vya upinzani. Kwa bahati mbaya hakukuwa na umoja. CUF wakipeleka rasimu yao bila mpango, Chadema wakiliongelea bila msisitizo.
Hoja ikatekwa na kugeuzwa kuwa ya CCM mbele ya safari.
Wapinzani wakwa wasikilizaji na si wapangaji wa utaratibu wa kupata katiba mpya.

2. Wapinzani wapongeza hotuba ya kuanza mchakato
Kiongozi wa upinzania bungeni mh Mbowe alisikika akisema amefurahishwa na Rais kutanganza kuanza kwa mchakato. Hili maana yake akakabidhi hoja ya wapinzani kwa CCM.

3.Mswada wa Rasimu wa kwanza
Wapinzani wakaendelea kujadili ili kuuboresha bila upinzani mkubwa. Upinzani mkubwa ukatokea znz uliolazimisha suala la muungano kujadiliwa.
Upinzani ukawa nyuma ya wananchi na si wananchi nyuma ya upinzani

4. Marekebisho ya mswada wa sheria ya kuunda tume
Wapinzani wakaitwa Ikulu na kufikia makubaliano wanayoyajua bila kuwashirikisha wananchi.
Mswada ukapitishwa kinyemela wakiwa na juisi mkiononi

5. Mswada wa uteuzi wa wabunge
Wapinzania wakagomea mswada . Wakaitisha maandamano nchi nzima.
JK akahutubia taifa na kuwataka warudi Ikulu kujadiliana.

Wapinzania wakasitisha maandamano kwa kuamini ni heshima kwa Rais.
Wakati wanaondoka wakaahidiwa mswada hautajadiliwa.
Walipoweka glass za juisi, Rais akazunguka ofisi nyingine na kusaini mswada ule ule waliogomea tena ukiwa na umepitishwa na wajumbe 100.

6. Wapinzania wataka kujitoa tume
Hii ilikuwa kupinga taratibu za serikali kuiingilia mambo ya tume.
Prof Mwesiga Baregu akasimama na kusema ‘taifa kwanza' na kama ni kuchagua , atachagua taifa na si chama.

7. Kuundwa kwa kanuni
Wapinzani wakiwa UKAWA wakagomea kanuni 37 na 38 kuhusu upigaji wa kura.
Kamati ya maridhiano ikiwahusisha akina John Mnyika ikaridhia kuwepo kwa kituko cha kura ya wazi na siri. Hilo ndilo CCM walilitaka kwasababu nia yao ilikuwa ni kuwabana wabunge wao.

8. Kuitwa Warioba
UKAWA wakagomea suala hilo kwasababu Sitta alikukiuka taratibu.
Mwisho wa siku wakakaa kitako kumsikiliza Kikwete wakijua lengo lilikuwa kumvuruga Warioba, kuingilia na kuvuruga mchakato. UKAWA walikuwa na fursa hizi
a) Kukaa bungeni na kuzomea hadi JK ashindwe kuhutubia kama walivyofanya kwa Warioba
b) Kutohudhuria kabisa bungeni ili kuonyesha kutoridhika
c) Kuhudhuria na kasha kutoka nje ya bunge
Hawakufanya lolote kati ya hayo

9. Kuweka utaifa mbele
Licha ya Vitimbwi vyote waheshimwa James Mbatia na Prof Lipumba walisikika wakisema kuwepo kwao bungeni ni kwasababu ya ‘kuweka taifa kwanza'

Kwa maana wanaridhika kupambana wakiwa ndani hata kama wanajua mwisho na matokeo ya mapambano yao

10. UKAWA yaweka kikao
Kuamua hali ya baadaye. Tundu Lissu akisema wananchi hawatawelewa kwa kupinga unyanyasaji. Ni vema waendelee na mapambano ndani ya bunge

11. Kuteuliwa
UKAWA ikagomea utaratibu uliotumika kupata viongozi wa kamati.
Lipumba akajitoa. Mbowe akateuliwa, hakuna uhakika kama yumo au alijitoa.

12. UKAWA yajitoa
Baada ya kunyanyaswa sana na Mh Sitta kwa kupindisha sheria, taratibu na kanuni UKAWA wakaamua kuondoka bungeni.

Inaendelea...
 
Sehemu ya IV
UKAWA YAITISHA MKUTANO ZNZ

Mkutano wa ukawa ukazuiliwa kwa kisingizio cha ugaidi.
Hii ni hoja dhaifu sana. Huwezi kuacha kukamata magaidi ukazuia mkutano.
Kinyume chake mkutano ungetumika kubaini magaidi kwasababu Polisi walikuwa na ‘taarifa'

Jambo hili ni kutimiza yale tuliyosema hapo mwanzoni. Zuia mikutano hadi Kikwete atakapohutubia. Zuia mikutano ili wananchi wasikilize Dodoma.

Kwa mtiririko hapo juu bandiko III ni wazi kuwa UKAWA haijajipanga vema.
Kuna hali ya kusita sita nap pengine kutojua wakati muafaka wa kuchukua hatua.
Kuna kukosa ‘timing' katika maamuzi jambo linalowaweka katika nafasi tata sana.

Kama UKAWA wataridhia kwenda kuonana na Rais ambaye ana orchestrate mpango mzima hiyo itakuwa sawa na kwenda kuongea na Tumbili kuhusu suala la mahindi yaliyoliwa na Ngedere. Makosa ya huko nyuma yawafundishe ili wajue kuwa JK hucheza karata zake apendavyo kutokana na udhaifu wao.

UKAWA hawapaswi kuitisha mikutano kama UKAWA, bado wana nafasi kubwa ya kuitisha mikutano kama vyama vya siasa na kualika viongozi wa ukawa.

Ni lazima wawe makini na muda uliobaki. Nafasi ya wao ku set tone ya agenda yao ni kati ya leo na April 26. Baada ya hapo watakuwa wamevurugwa kama mzee Warioba.
Wakumbuke hawana vyombo vya propaganda

UKAWA wanaweza kutumia semina na makongamano ambayo ni tofauti na mikutano ya kisiasa. Ni lazima hilo litokee ndani ya wiki moja kuanzia sasa.

Jaribio la kuitwa na kina Sitta na wao kulikubali ni kukabidhi hoja yao kwa wale wale wasiowatakia mema. UKAWA haipo katika level ya Samwel Sitta.
Samwel Sitta najulikana kwa ubabe wake wa kuitetea CCM.

Sitta yupo tayari taifa liingie katika mtafaruku kwa matumaini yake binafasi. Kuendelea kuongea naye ni kuendelea kupanga mikakati ya tatizo kubwa linaloonekana huenda likaikumba nchi.

UKAWA lazima wawe na agenda ya kutosha mbele ya wananchi. Hoja zao zijikite katika elimu ya umma na si kejeli wala matusi. Zijikite katika kubainisha udhalimu unaoendelea, kupuuzwa kwa maoni ya umma na nini watarajie kama wataruhusu katiba mpya ya CCM kuendelea kutumika.

UKAWA wamefanya makosa mengi huko nyuma, itakuwa ni ajabu kama hawatakuwa wamejifunza kutokana na makosa hayo. Ni lazima wafike mahali wachukue dhima ya wananchi kwa udhati .

Inaendelea sehemu ya mwisho
 
Mkuu Nguruvi3,
Mbona umejazana kuutetea UKAWA huku ukijua ni muungano BATILI kisheria?
Si ndio hao hao waliodiriki kumtukana Baba wa Taifa juu ya Muungano wa Tanzania ambao kwa maoni yao ni BATILI? Mbona na wao pia wanafanya yale yale?
Wametoka Bungeni wakilalamika kutukanwa lakini Prof Lipumba alisikika akiwaita walio na mawazo tofauti na ya kwake "Interahamwe!"
Sasa ya nini kulalamika wakati wewe nawe unafanya yale yale?
 
Last edited by a moderator:
Sehemu ya V

UKAWA WAFANYE NINI KWA SASA

1. Mikutano ni lazima na ni haki yao.
Watumie wiki hii kabla ya muungano ili kuzuia mambo yafutayo
a)Athari za upotoshaji unaotarajiwa April 26
b) Kupeleka ujumbe wananchi wakiwa na hamu ya kufahamu kabla ya kuptoshwa
c) Kuondoa attention kutoka Dodoma ili wananchi wasiendelee kupotoshwa na CCM

UKAWA watambue kuwa ni lazima njia za kuwaeleza wananchi zianze sasa wakiwa na nguvu (Momentum) na hili litokee kati ya sasa na April 26.

Wasikubali kunyimwa haki ya kukusanyika bila sababu. Kukubali hayo ni sawa na kuiuza agenda yao kwa bei rahisi sana.Mikusanyiko ni haki yao, hawapaswi kuelezwa uhalifu wanapaswa kupewa ulinzi.

Katika mikutano ya UKAWA, ni lazima wawe na agenda muhimu zinazoeleweka kwa wananchi.
Waepuke matusi, kujeli na dharau.

Kama ni kuwashauri ningesema kwa sasa Tundu Lissu ima afafanue kwa usahihi hoja yake.
Aeleze alilenga nini kuhusiana na yale aliyosema, au awe mbali na wananchi kwasababu hoja yake inaweza kuwa msumeno, unakata mbele na nyuma. Tahadhari

Ukawa wadai haki ya kukusanyika kwasababu waziri mkuu Pinda kasema hata wao watazunguka nchi nzima. Tofauti na CCM inayodhamiria kuwatisha wananchi, UKAWA wajikite katika mambo haya;

1. Kueleza madai ya wananchi kuhusu matatizo ya muungano

2. Kueleza kiini cha manung'uniko ya matatizo hayo kwa pande zote bila kuona haya au aibu lakini kwa adabu na heshima. Masuala ya muungano yaongelewe kwa kujali sensitivity yake, hii haina maana hayawezi kuongelewa, la hasha! bali kuwepo na communication isiyoweza kutumiwa
kuwadhuru.

3. Kueleza namna CCM isivyokuwa na majibu kwa miaka 50 na tume zaidi ya 10 kuhusu malalamiko ya muungano kwa pande zote.

4. Kueleza jinsi gani CCM hawana mbadala wa hoja za Warioba isipokuwa kutaka serikali 2 kwa kufundishwa.

5. Kueleza hatari ya kushindwa kwa hoja za CCM na jinsi akina Lukuvi wanavyoingiza mambo ya kisiasa katika dini ili kuungwa mkono. Ukawa ieleze hatari za jambo hilo kwa mustakabali wa taifa

6. Ukawa waonyeshe jinsi ambavyo Tanganyika ipo hadi sasa na inafanya kazi na kwamba kinachoogopwa ni jina na wala si maudhui au haki za Tanganyika.

7. Wananchi waelezwe kwa uwazi athari za kutokuwepo kwa Tanganyika katika shughuli, mambo na mahusiano yao na wenzao wa znz leo na siku za baadaye. Waeleze ni kwanini Tanganyika inatakiwa izinduke rasmi hapo ilipo, itasimamia nini na kwa faida zipi kwa ustawi wa muungano.

8. Waeleze jinsi ambavyo malalamiko ya wznz kuhusu muungano yalivyotafutiwa ufumbuzi na tume ya Warioba na jinsi CCM isivyo na majibu sahihi ya yale ya Warioba.

9. Waonyeshe upotoshaji ambao CCM inaufanya kama ule wa majeshi matatu na jinsi gani tume ilivyopendekeza jeshi moja. Waweke wazi kuhusu majeshi mawili yaliyopo sasa hivi, JMT na la vikosi maalumu

10. Wafafanue upotoshaji wa gharama, wakionyesha vyanzo na jinsi gani pesa zinapotea ambazo zinaweza kuhudumia serikali nyingi tu.

11. Waonyeshe vyanzo vya mapato ya sasa , nani nagharamia na shirikisho litapunguza vipi hizo gharama na washirika wawajibika vipi kama wabia sawa.

12. Muhimu zaidi, waziangalie hoja za CCM, watafute mapendekezo ya tume za CCM, waonyeshe jinsi CCM ilivyoshindwa kwa kutumia tume zake.
Ni vema wakazitumia tume za CCM kujenga na kuobomoa hoja za CCM.

13. Wachukue thadhari katika mikutano, kwa kuzingatia kuwa CCM inaweza kupandikiza vurugu ili kujenga hoja za kuwatisha wananchi.

14. Kwa vile CCM inaonekana kutokuwa na hoja bali mbinu na ulaghai, UKAWA isiishie katika hoja za katiba. Ni muda muafaka kwa wao kuendeleza agenda za kitaifa kwa kuwa na rainbow coalition kuelekea 2015. Katika kutumiza hilo lazima wawe na dhamira ya kweli na dhati.

Hoja ya katiba mpya ni silaha bora waliyo nayo kwasasa kuelekea 2015.
Ni wajibu wao kuitumia silaha hiyo vema ili kuonyesha mbadala madhubuti wa taifa hili siku za usoni. Hilo litafanikiwa kuanzia sasa na kuendelea.

Tumalizie kwa kusema, kama taifa ni kwanza, hiyo iwe kauli mbiu ya wote na wala si UKAWA tu pale wanapodai haki zao. Kauli hiyo inamhusu JK na wenzake pia

UKAWA Wakiridhia tena kurudi Ikulu kwa juisi ya maembe kama walivyofanya huko nyuma, umma na taifa halitawaelewa tena.

Mumebabaika sana siku za nyuma, this is the second chance. It is do or die , UKAWA!
Umma upo nyuma yenu

Tusemezane
 
Mkuu Nguruvi3,
Mbona umejazana kuutetea UKAWA huku ukijua ni muungano BATILI kisheria?
Si ndio hao hao waliodiriki kumtukana Baba wa Taifa juu ya Muungano wa Tanzania ambao kwa maoni yao ni BATILI? Mbona na wao pia wanafanya yale yale?
Wametoka Bungeni wakilalamika kutukanwa lakini Prof Lipumba alisikika akiwaita walio na mawazo tofauti na ya kwake "Interahamwe!"
Sasa ya nini kulalamika wakati wewe nawe unafanya yale yale?
Sidhani kama UKAWA ni batili zaidi ya Rasimu ya CCM iliyoandikwa mafichoni na watu 27 wengine wakiwa hawana hata moral authority ya kutamka neno katiba.
Sidhani kama ni batili zaidi ya wahuni na wahalifu wanaogeuza maoni yao kuwa ya wananchi na kudharau maoni ya wanachi.

Sidhani kama ni BATILI zaidi ya watu 400 kutoa takwimu za kuwakilisha watu milioni 40, zikipingina na takwimu za watu 17,000 kwa kiwango hicho. Sidhani kama sample size ya watu 400 inakubalika katika population yetu tena wakiwa chini ya 'gereza' la kisiasa.
 
Mkuu Nguruvi3

Baada ya taarifa ya Polisi kule Unguja kuzuia mkutano wa Ukawa nilianda hivi,


Kosa kubwa na litakalotugharimu kwamiaka zaidi ya 50 mingine ni UKAWA kukubaliana na jeshi la polisi kusitisha mkutano huu wa kesho 19/04/2015 pale Zanzibar, jambo muhimu ni kulazimisha mkutano ili viongozi wakamatwe na maandamano rasmi ya ukombozi yatokee tena yasiyokoma.

Naamini kosa kubwa ambalo ccm hawatalifanya ni kuwakamata viongozi, wanajua kufanya hivyo kutaibua machafuko makubwa yenye kuiondoa ccm madaraka.

UKAWA wakifanikiwa kufanya mkutano pale Unguja basi na maeneo mengine mikutano itafanyika bila kikinza, lakini wakikubali tu kuufyata basi kamwe hawatapa uwanja wakuendesha mkutano wa UKAWA katika ardhi Tanganyika au Zanzibar, itawalazimu kuchagua moja, ama kurudi bungeni au kurudi nyumbani na kuacha Interahamwe waendelee kutunga katika yao,

Ieleweke kuwa Zanzibar ukitofautiana na seif, Jusa, Duni, Moyo na Abubakar umetofautiana na Wazanzibar.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Buchanan,

Katika bandiko #5 hapo juu unarudia makosa yale yale. Wiki kadhaa zilizopita ulikuja na bandiko ukijenga hoja kwamba "LISSU KAJIKAANGA KWA MAFUTA YAKE MWENYEWE" - uki qestion uhalali wa elimu ya lissu, cv yake etc kwamba iwapo anasema katiba iliyopo sio halali, basi elimu yake, n.k nayo sio halali kwa vile imepatikana chini ya katiba asiyoitambua kama halali. Nilikujibu lakini haukunirudia. Leo umerudi na hoja ile ile.

Nilisema hivi -
Kinachotazamwa hapa is our desire:
1. For a constitutional government and a fair administration ambayo inatawala kwa mujibu wa, na kufuatana na sheria.

2. For the laws themselves kuwa JUST, FAIR and EQUITABLE.

Hoja yetu (mkipenda tuite wachache) ni kwamba TANU na baadae CCM has breached both conditions above. Katika hili, Shivji nae analizungumzia in "let the people speak: Tanzania Down the road to neo-liberalism(1995, page 95) kwamba:

If one is to judge by the standards of constitutionality, which are proclaimed today, our union has hardly had a constitutional government for the last thirty years. there were so many major breaches - including surreptitious manipulations of the constitution - that in reality we did not live by our constitution. We even forgot to swear by it. We, at the Hill, stopped teaching Constitutional Law in 1971 o 1972!

Kuna haja pia ukaelewa kwamba katiba isn't simply a legal document, bali its also a political document. Kimsingi, its a political document than a legal document. Lazima kwanza iwe na political legitimacy kabla ya kuwa enacted into law. Lakini kabla haijapata political legitimacy na kustahili obedience and loyalty ya watawala na watawaliwa, lazima ipatikane kwa consensus ndani ya jamii. That's what a constitution is all about, umuhimu wake wa kuwa na "political legitimacy", sio legalities and technicalities as the primary motive.

Pamoja na Katiba ya sasa kukosa sifa zote hizi,lakini haina maana kwamba serikali ya TANU na CCM ilikosa uhalali wa kutawala. Uhalali ulikuwepo lakini chanzo chake hakikuwa Katiba ya nchi bali:

1. Charisma and integrity ya Mwalimu.

2. Azimio la Arusha lililolenga kumwinua mwananchi.

3. Na mafanikio ya TANU katika kupigania wanyonge ndani na nje ya nchi.

Hizi ndio factors au sources zilizoipa CCM uhalali wa kutawala, kuunda serikali, kukamata dola, na kuendesha shughuli zote za kijamii, kisiasa na kiuchumi. Lakini kwa bahati mbaya, all these sources of legitimacy zimeporomoka, CCM imeziua yenyewe, ndio maana sasa katika mazingira ya leo, the only source of legitimacy kwa ccm au chama chochote kutawala ni Katiba ya nchi itayo tokana na maoni ya wengi. Period.

Pia nilikueleza kwamba - tuchukulie mfano wa Afrika ya Kusini. Kwa miaka mingi (wakati wote wa ubaguzi wa rangi), serikali ya makaburu ilidai kwamba inatawala kwa mujibu wa katiba. In the process, kina mandela, tambo, sisulu na wengine bado walisoma, walifanya kazi za uwakili kutetea wenzao weusi chini ya katiba na sheria zile zile za makaburu, walikamatwa na kufungwa kwa sheria zile zile, na hatimaye wakaachiwa huru, katiba mpya ikaandikwa, na uhuru kupatikana. Je hali ya Lissu na wanaharakati wote hawafanani na hali hii ya Mandela? Je kina Mandela walijikaanga na mafuta yao wenyewe?

Mwalimu Nyerere alisoma chini ya sheria za mkoloni, akatumia mfumo wao kufanikisha harakati nyingi za uhuru, na akaja kupinga mfumo huo huo kwa hoja kwamba haukuwa mfumo halali, na matokeo yake, elimu, uzoefu na mafanikio ya Mwalimu chini ya mfumo na utawala wa mkoloni hayakubadilika kwa sababu tu alikuja pingana na mfumo huo, na alipoingia tu madarakani, akaibadili Katiba na pia mfumo uliomlea, mwelimisha, na kumfikisha siku ile ya uhuru wa Tanganyika. Je Mwalimu Nyerere alijikaanga na mafuta yake mwenyewe?

Turejee kwenye mfano wa Afrika ya Kusini. During apartheid, kwa makaburu, wao, a constitutional government simply meant that the government was following the letter of the constitution and the law. Na hii pia ilikuwa ni hoja ya muda mrefu ya CCM katika kupinga haja ya Katiba mpya. Lakini kwa makaburu (na pia ccm sasa), it became obvious kwamba the pre-requisite of a constitutional governmment ni kwamba the constitution and the laws themselves have to be just, fair, and equitable. Sio tu kwamba serikali ikifuata katiba na sheria bila ya kujali kama sheria ni just, fair and equitable basi serikali hiyo ijulikane kwamba ni halali kikatiba. Legitimacy inakuja iwapo katiba ni just, fair and equitable kwa maoni ya walio wengi (wananchi), ambao ndio msingi wa katiba.

Iwapo hili halikuwa a prerequisite, basi serikali ya Makaburu ingeendelea kuwa moja ya constitutional governments in the world - kwani katiba ya kikaburu followed the letter of the constitution and the law. Lakini ingekuwa ni upuuzi kuwaambia wapiganaji wa ANC kwamba they should strictly follow and respect the law. Kama ANC wangefanya hivyo, basi wasingeweza kuanzisha harakati for their right to self determination ambayo ilikuwa denied by the constitutional and legal order ya wakati ule.

Katika muktadha wa Tundu Lissu, same applies - harakati za Tanganyika zinalenga our right to self determination ambayo ipo denined by the current constitutional and legal order.

Nirudie kusema tena:
Mzee Mandela alisoma katika mfumo alioupinga, akafanya kazi za sheria katika mfumo huo huo, akakamatwa na kufungwa kwa kupinga mfumo ule, miaka 27 baadae akatolewa jela na taifa likaandika katiba mpya na kuupata uhuru. Mandela akawa rais wa kwanza mzalendo. Leo mandela ni shujaa na mfano wa kuigwa kwa kila mwanadamu duniani. Je, unataka kutuambia kwamba Mandela alijikaanga kwa mafuta yake mwenyewe? Kumbuka hata yeye alikuwa mwanasheria aliyepinga katiba na mfumo wa kikaburu, na alipata upeo huo baada ya kusoma katika mfumo ule ule na kufanya kazi katika mfumo ule ule.

Kama nakumbuka vizuri, Nguruvi3 alikujibu kwa mifano ya Martin Luther na rosa parks - kwamba hawa walipigania mabadiliko ndani ya mfumo ule ule dhalimu na kufanikiwa.

Buchanan, ebu tuache masihara. Tuungane na UKAWA kuizindua Tanganyika yetu kwa manufaa ya Tanganyika, Zanzibar na Muungano.


Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3

Baada ya taarifa ya Polisi kule Unguja kuzuia mkutano wa Ukawa nilianda hivi,
Yericko, haki ya kukusanyika ni ya msingi kwa kila raia. Ni wajibu wa Polisi kutoa ulinzi na si kueleza mambo wanayodhani yapo.

Tangu Polisi watoe katazo hakuna aliyekamatwa kwa ugaidi. Intelligence gani hiyo?
Hizi ni mbinu za kuzuia mikutano ya UKAWA kama ilivyo kwa habari kupitia TBC

UKAWA lazima wawe na mbinu za kukabiliana na changamoto za uonevu na udhalilishaji.
Ni lazima wawe ahead of time wakitambua kuwa muda ni kitu muhimu sana kwao.

UKAWA wakusbiri April 26, wao watakuwa katika kujibu tuhuma na si kueleza tuhuma.
Ndivyo JK alivyofanya kwa Warioba. JK alivunja tume haraka ili kusiwe na nafasi ya Tume kujitetea.

Alichokifanya Dodoma mbele ya mzee Warioba ni kuchukua changamoto zilizotajwa akazifanya kama agenda.
Hakuzungumzia mambo mazuri ya tume hata kidogo.

Kabla au ikifika April 26, JK atatumia mwanya huo kutunga tungo za kuwadhalilisha akina UKAWA.
Kwasasa ilitakiwa wawe mbele wakieleza umma, inavyoonekana wiki moja sasa hawajaeleza kinaga ubaga wananchi wakaelewe. Si lazima mikutano, tumieni media na kila aina ya mawasiliano na wananchi.

UKAWA ninyi mna resource chache, ni wajibu wenu muzitumie kikamilifu na utimilifu kwa sasa.
Muda, narudia muda ni jambo muhimu sana katika mikakati yenu. Short of that mtaishia kulaumiana.
 
Ombi langu kwa Mh. James Francis Mbatia, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba na Mh. Freeman Aikaeli Mbowe na wote wale wanaowaunga mkono ndani ya Bunge Maalum La Katiba; jahazi la taifa linaenda mrama na kwa sasa makasia yako mikononi mwenu, ni jukumu lenu kutuvusha salama sisi wananchi. Hao manyang'au ya CCM hayana nia wala sababu za kuheshimu maoni ya wananchi na mkilegeza tu juhudi zenu katika kuliokoa taifa, tumezama. Tafadhalini msituangushe...mkifanya kosa, historia itawahukumu.
 
Ombi langu kwa Mh. James Francis Mbatia, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba na Mh. Freeman Aikaeli Mbowe na wote wale wanaowaunga mkono ndani ya Bunge Maalum La Katiba; jahazi la taifa linaenda mrama na kwa sasa makasia yako mikononi mwenu, ni jukumu lenu kutuvusha salama sisi wananchi. Hao manyang'au ya CCM hayana nia wala sababu za kuheshimu maoni ya wananchi na mkilegeza tu juhudi zenu katika kuliokoa taifa, tumezama. Tafadhalini msituangushe...mkifanya kosa, historia itawahukumu.
Mkuu, katika bandiko III hapo juu tumewakumbusha UKAWA jinsi walivyopotezwa huko nyuma na makosa waliyofanya, mengine ya juzi tu katika bunge la katiba

Wananchi wamewapa benefit of doubt za kutosha sana. Wananchi walianza kwa kusema ni wageni katika game, wakasema ni wachanga, wanajifunza, wanapeleka mambo kwa utaratibu n.k
Sasa ni miaka takribani 20 tangu CCM ianze kupata upinzani.
Hakuna cha uchanga, kujifunza au ugeni.
Ni wakati wa kuonyesha vision, maturity and leadership.

Kuitwa katika majagi ya juisi halafu Salva aitishe mkutano na kusema mswada ulisainiwa siku ile ile mliokuwa na mjadala na Rais ilikuwa kuwadhalilisha sana.
Kwamba waite, hawana lolote, wape juisi wakimaliza waondoke! come on!

Tunakumbuka Rais aliposema Wapinzani waende kuzungumza na lukuvi jinsi ya kurekebisha mswada.Kwamba Lukuvi aliyeshindwa siku za nyuma ndiye Rais anaona anafaa kuzungumza nao.

Mkikubali kwenda kunywa juisi taifa halitawaelewa. Rais Kikwete na CCM hawana dhamira njema.

 
UKAWA MSISUBIRI KUZUIA NA KUYEYUSHA MASHAMBULIZI, TUPENI 'MAKOMBORA'

UKAWA, wazungu wanasema 'time is of essence' kwamba, jambo lifanyike katika muda muafaka.

Ushawishi wa kutaka mrejee katika meza ya mazungumzo ni njia za kupoteza muda ili muda ukifika mfanyiwe ambush.
Jitihada za kuzuia mikutano yenu zimelenga katika kuahirisha muda kwa lengo lile lile la ambush.

Kati ya leo na jumapili mnaweza kujikuta mkicheza nafasi ya ulinzi kuliko ushambuliaji.
Mtakapokuwa katika kulinda mtajikuta mnacheza na maneno ya CCM na mwenyekiti wao.
Mtakuwa mnajibu tuhuma zinazotengenezwa dhidi yenu badala ya kueleza tuhuma za CCM

Mikutano ni haki yenu iwe kupitia UKAWA au vyama vya siasa. Resource zenu ni ndogo hivyo mzitumie kwa umakini. Mna hoja mIkononi, nini kinawashinda kuueleza ulimwengu?

Mathalan, kuna hoja za mchakato ulivyopelekwa kwa mizengwe kuanzia hatua za bunge la JMT, uteuzi wa wajumbe. Kuna hoja za kanuni na jinsi zilivyokiukwa.

Zipo hoja za rasimu ya CCM kuchomekwa, upendeleo wa kuendesha bunge, njama za kutupa rasimu ya tume n.k. ambazo zikiorodheshwa si chini ya 25 tena zikiwa nzito.

Juzi hoja imeongezeka tena nzito sana machoni mwa wananchi.
Waziri Lukuvi alitumwa na Waziri mkuu kupeleka ujumbe wa Serikali ya JK kanisani kuhusu serikali 3 na majeshi kuchukua nchi. Hii ni hoja muhimu sana mbele ya umma.

Umuhimu wake ni kuonyesha jinsi ambavyo Rais alivyofikia mahali kuwatuma watendaji wake waende kwenye vyombo vya dini kuanza kuchonganisha wananchi kwa misingi ya dini.

Hata pale Lukuvi alipoitwa kujieleza, akiwa mbele ya waziri mkuu alisema huo ni msimamo wake.

Lukuvi hakwenda kama mtu binafsi, alikwenda kama serikali. Kila alichosema na kufanya kilikuwa katika heshima ya serikali. Hakuna excuse ya maneno kuwa yake kama alivyosema.

Ili kulinda heshima ya serikali na umoja wa taifa, Kikwete alipaswa kumwajibisha Lukuvi mara moja. Katika nchi za wenzetu mtu wa wadhifa wa Lukuvi, tuhuma tu za kumnyanyasa mkewe zinatosha serikali kumweka pembeni.

Kumweka pembeni si adhabu, ni kulinda heshima ya serikali.
Leo Kikwete na serikali yake wanaonekana kama watu wenye dhamira ovu ya kuleta machafuko ya dini kupitia Lukuvi.

Inawezekanaje Kikwete au Pinda wakasimama sehemu moja na Lukuvi kama wajumbe wa baraza la mawaziri na umma ukawaamini?

Inawezekanaje Kikwete akamtuma Lukuvi kama msaidizi wake kwa jambo lolote la kitaifa.
Jibu ni kuwa kujifungamanisha na Lukuvi ni kuidhalilisha serikali na kujipaka matope zaidi.

Kwanini UKAWA wasusie vikao
1. Tukio la Lukuvi limelenga kuvuruga na kuleta machafuko nchini.
Kwavile serikali na JK hawataki kumwajibisha mhusika, ni dhahiri Lukuvi ametumwa na serikali.
Kuendelea kujadili katiba inayolenga kuwagawa wananchi, kuleta vurugu na machafuko ni kuidhinisha uhalifu.

2. Serikali ya CCM kwa kuwatumia wanachama wake imekiuka misingi ya haki za binadamu na taifa kwa kuchochea Urangi. Leo wapo wanaoitwa kwa majina ya rangi zao na wanaofanya hivyo ni CCM, viongozi wakiendelea kukaa kimya.
Matusi ya CCM znz mbele ya Pinda ni kielelezo cha idhini ya kuchochea vurugu za rangi.

3. Njama za kuandika katiba ya CCM na kudharau maoni ya wananchi ni kinyume cha demokrasia, ni kupalilia vurugu na machafuko. Kuendelea kuwemo bungeni ni kubariki uchafu.

UKAWA wanahoja za msingi kabisa, tatizo linaloonekana ni wao kutojiamini au kutojua waanze na wamalizie wapi. Inakuwaje mkutano uzuiliwe na watu waseme hewala. Nchi hii katiba inaruhusu Mikusanyiko bila kuvunja sheria. Kama zipo dalili za ugaidi, mkutano ufanyike eneo jingine.

UKAWA wakishindwa kuitumia nafasi waliyo nayo na momentum iliyopo, basi wasubiri kunyanyaswa vilivyo.

Ukawa wanadhani wanao muda, wasichotambua ni kuwa CCM ndio waliokamata saa.

Tusemezane
 
Naunga mkono hoja. Lakini kwa vile UKAWA waliondoka bungeni baada ya Lipumba kuhitimisha juu ya athari za hotuba ya Lukuvi ndani ya kanisa, ni muhimu pia Ukawa ukalifafanua hilo zaidi, huku ikishinikiza Lukuvi aachie ngazi ili "asiwe mfano wa kuigwa", vinginevyo nchi itaingia katika machafuko. Ukawa ueleze wazi kwamba Lukuvi ameenda kinyume kabisa na alichotuasa Mwalimu mwaka 1993/4 juu ya athari za kutumia udini kujadili muungano. Mwalimu alisema haya (Shivji,2005:Let The People Speak:Tanzania Down the Road to Neo Liberalism):

Na katika hali ya mazungumzo tuliyonayo, hapa tunayoyazungumza haya, wakubwa wanatuita tuje tuanze maelewano ya kupunguza chuki. Wanajua wakubwa kwaba hali tuliyonayo ni ya chuki. Tumechoka na wazanzibari, tumechoka na wazanzibari. Hayo ndio mazungumzo. Mkiunda serikali ya Tanganyika kutokana na msukumo huu unaowasukumeni wa chuki wa zanzibari na uislamu, nasema mbele yenu na nasema mbele ya mungu, kuna msukumo 'tumechoka na wazanzibari' lakini ndani yake humo humo umo udini. Tumechoka na wazanzibari na ndani ya humo humo umo udini. Nimewatest watu mimi, umo udini mkubwa ndani. Kwasababu wewe ndugu rais, wewe muislam, wewe mzanzibari, umefanya madhambi. Basi rais, mzanzibari, muislam amefanya makosa,, mzanzibari, muislamu amefanya makosa. Kwahiyo kuna msukumo, msukumo huu wa uzanzibari na uislamu unaosukuma jambo hili. Kwahiyo nasema nini mimi? Nasema mkijenga, mkiunda serikali ya Tanganyika kutokana na misingi hiyo ya kuchoka na wazanzibari - na chini chini mmechoka na uislamu. Sababu hizo mbili, hizo hizo zitakazoua muungano. Mkiunda serikali ya Tanganyika kwa msukumo huu, muungano utakufa, na muungano ukifa kwa ukabila (maana uzanzibari ni ukabila tu) na udini, sababu hizi mbili za ukabila na udini zitakazoua muungano, zitaua Tanganyika.

Lukuvi ana lenga kulifanya suala la utanganyika kuwa ni suala la udini.

Mbali ya hili la udini, Lukuvi pia amevunja Sheria ya Usalama wa Taifa Na. 3 ya 1970 iliyorekebishwa mara nne kati ya mwaka 1989-98 na marekebisho:

1. Namba 17 ya mwaka 1989.
2. Na.82/1994.
3. Na.9/1996.
4. Na 12/1998

Sheria hii inapiga marufuku kwa mtu yoyote kulichokonoa JESHI.

Kuna haja ya Ukawa kuhakikisha kwamba wanacheza vizuri na haya mawili kushinikiza Lukuvi ajiuzulu au awajibishwe. Hatua hiyo itawapa a political mileage katika harakati za kuhakikisha kwamba maoni ya wananchi yanalindwa.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu Buchanan,

Katika bandiko #5 hapo juu unarudia makosa yale yale. Wiki kadhaa zilizopita ulikuja na bandiko ukijenga hoja kwamba "LISSU KAJIKAANGA KWA MAFUTA YAKE MWENYEWE" - uki qestion uhalali wa elimu ya lissu, cv yake etc kwamba iwapo anasema katiba iliyopo sio halali, basi elimu yake, n.k nayo sio halali kwa vile imepatikana chini ya katiba asiyoitambua kama halali. Nilikujibu lakini haukunirudia. Leo umerudi na hoja ile ile.

Nilisema hivi -
Kinachotazamwa hapa is our desire:
1. For a constitutional government and a fair administration ambayo inatawala kwa mujibu wa, na kufuatana na sheria.

2. For the laws themselves kuwa JUST, FAIR and EQUITABLE.

Hoja yetu (mkipenda tuite wachache) ni kwamba TANU na baadae CCM has breached both conditions above. Katika hili, Shivji nae analizungumzia in "let the people speak: Tanzania Down the road to neo-liberalism(1995, page 95) kwamba:



Kuna haja pia ukaelewa kwamba katiba isn't simply a legal document, bali its also a political document. Kimsingi, its a political document than a legal document. Lazima kwanza iwe na political legitimacy kabla ya kuwa enacted into law. Lakini kabla haijapata political legitimacy na kustahili obedience and loyalty ya watawala na watawaliwa, lazima ipatikane kwa consensus ndani ya jamii. That's what a constitution is all about, umuhimu wake wa kuwa na "political legitimacy", sio legalities and technicalities as the primary motive.

Pamoja na Katiba ya sasa kukosa sifa zote hizi,lakini haina maana kwamba serikali ya TANU na CCM ilikosa uhalali wa kutawala. Uhalali ulikuwepo lakini chanzo chake hakikuwa Katiba ya nchi bali:

1. Charisma and integrity ya Mwalimu.

2. Azimio la Arusha lililolenga kumwinua mwananchi.

3. Na mafanikio ya TANU katika kupigania wanyonge ndani na nje ya nchi.

Hizi ndio factors au sources zilizoipa CCM uhalali wa kutawala, kuunda serikali, kukamata dola, na kuendesha shughuli zote za kijamii, kisiasa na kiuchumi. Lakini kwa bahati mbaya, all these sources of legitimacy zimeporomoka, CCM imeziua yenyewe, ndio maana sasa katika mazingira ya leo, the only source of legitimacy kwa ccm au chama chochote kutawala ni Katiba ya nchi itayo tokana na maoni ya wengi. Period.

Pia nilikueleza kwamba - tuchukulie mfano wa Afrika ya Kusini. Kwa miaka mingi (wakati wote wa ubaguzi wa rangi), serikali ya makaburu ilidai kwamba inatawala kwa mujibu wa katiba. In the process, kina mandela, tambo, sisulu na wengine bado walisoma, walifanya kazi za uwakili kutetea wenzao weusi chini ya katiba na sheria zile zile za makaburu, walikamatwa na kufungwa kwa sheria zile zile, na hatimaye wakaachiwa huru, katiba mpya ikaandikwa, na uhuru kupatikana. Je hali ya Lissu na wanaharakati wote hawafanani na hali hii ya Mandela? Je kina Mandela walijikaanga na mafuta yao wenyewe?

Mwalimu Nyerere alisoma chini ya sheria za mkoloni, akatumia mfumo wao kufanikisha harakati nyingi za uhuru, na akaja kupinga mfumo huo huo kwa hoja kwamba haukuwa mfumo halali, na matokeo yake, elimu, uzoefu na mafanikio ya Mwalimu chini ya mfumo na utawala wa mkoloni hayakubadilika kwa sababu tu alikuja pingana na mfumo huo, na alipoingia tu madarakani, akaibadili Katiba na pia mfumo uliomlea, mwelimisha, na kumfikisha siku ile ya uhuru wa Tanganyika. Je Mwalimu Nyerere alijikaanga na mafuta yake mwenyewe?

Turejee kwenye mfano wa Afrika ya Kusini. During apartheid, kwa makaburu, wao, a constitutional government simply meant that the government was following the letter of the constitution and the law. Na hii pia ilikuwa ni hoja ya muda mrefu ya CCM katika kupinga haja ya Katiba mpya. Lakini kwa makaburu (na pia ccm sasa), it became obvious kwamba the pre-requisite of a constitutional governmment ni kwamba the constitution and the laws themselves have to be just, fair, and equitable. Sio tu kwamba serikali ikifuata katiba na sheria bila ya kujali kama sheria ni just, fair and equitable basi serikali hiyo ijulikane kwamba ni halali kikatiba. Legitimacy inakuja iwapo katiba ni just, fair and equitable kwa maoni ya walio wengi (wananchi), ambao ndio msingi wa katiba.

Iwapo hili halikuwa a prerequisite, basi serikali ya Makaburu ingeendelea kuwa moja ya constitutional governments in the world - kwani katiba ya kikaburu followed the letter of the constitution and the law. Lakini ingekuwa ni upuuzi kuwaambia wapiganaji wa ANC kwamba they should strictly follow and respect the law. Kama ANC wangefanya hivyo, basi wasingeweza kuanzisha harakati for their right to self determination ambayo ilikuwa denied by the constitutional and legal order ya wakati ule.

Katika muktadha wa Tundu Lissu, same applies - harakati za Tanganyika zinalenga our right to self determination ambayo ipo denined by the current constitutional and legal order.

Nirudie kusema tena:
Mzee Mandela alisoma katika mfumo alioupinga, akafanya kazi za sheria katika mfumo huo huo, akakamatwa na kufungwa kwa kupinga mfumo ule, miaka 27 baadae akatolewa jela na taifa likaandika katiba mpya na kuupata uhuru. Mandela akawa rais wa kwanza mzalendo. Leo mandela ni shujaa na mfano wa kuigwa kwa kila mwanadamu duniani. Je, unataka kutuambia kwamba Mandela alijikaanga kwa mafuta yake mwenyewe? Kumbuka hata yeye alikuwa mwanasheria aliyepinga katiba na mfumo wa kikaburu, na alipata upeo huo baada ya kusoma katika mfumo ule ule na kufanya kazi katika mfumo ule ule.

Kama nakumbuka vizuri, Nguruvi3 alikujibu kwa mifano ya Martin Luther na rosa parks - kwamba hawa walipigania mabadiliko ndani ya mfumo ule ule dhalimu na kufanikiwa.

Buchanan, ebu tuache masihara. Tuungane na UKAWA kuizindua Tanganyika yetu kwa manufaa ya Tanganyika, Zanzibar na Muungano.


Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
chambuzi hapa unachapia maana Profesa Shivji alichomaanisha ni ukiukaji wa Katiba na sii katiba yenyewe. Kwa manaa ya kwamba ktk miaka 30 iliyopita tumekuwa na Mafisadi ambao waliapa kuilinda katiba lakini wameivunja mbele ya macho yetu na wakaachwa huru. Kuna vifungu vingi sana ndani ya katiba vilivyobadilishwa ili kukidhi haja za viongozi, kuna rushwa zimefanyika kinyume cha viapo na kadhalika lakini haina maana Katiba yenyewe haikuwa halali.

Huu mtindo wa kuwakashifu waasisi wa Muungano ambao ndio umewawezesha wao kukaa pale walipo na wengine hata kufika ktk jengo la Bunge la Muungano kuzungumzia KATIBA YA MUUNGANO ilihali wao wanaamin Jamhuri yenyewe sii halali ni UPUMBAVU mkubwa sana wala hauna kip[imo cha elimu maana kama kweli alijua kwamba Muungano wetu sii halali angekataa kujiunga na bunge hilo na kutoa maelezo yake kwa nini hakujiunga na kundi la wajumbe hao.

Iwapo Muungano wa Marekani kuna States zililazimishwa kujiunga baada ya kutekwa vita mbona wao hawasemi mnayoyadai nyie maana nijuavyo hakuna Muungano ulokuwa halali kisheria. Upuuzi huu wa kuturudisha nyuma maana sisi wengine tunategemea Katiba mpya kabla ya uchaguzi ili twende mbele na sii kuturudisha nyuma miaka 50 iliyopita. Basi kama ndivyo mbona hamzungumzii kwamba hata Uhuru wetu tulipewa sii Kihalali maana tulikuwa bado hatujawa tayari. Na hata ukitazama kura zilizopigwa wakati ule hazijai mkononi ukilinganisha na population maaa hapakuwa na utadfiri wala daftari la kura. Tanganyika tuloijua sisi ilikuwa ni pamoja na Rwanda na Burundi hao wazungu wakatugawa na kuunda nchi pasipo ridhaa yetu m,bona nalo halizungumziwi.

Waswahili wanasema Ukimchambua sana kuku hutamla na ndicho mnachokifanya hapa. CCM sio adui yetu ila sis wenyewe tumepumbazwa na hii rasimu ambayo inatugawa zaidi ya kutujenga kwa sababu tatizo letu sote ni kuendelea kuwa na mfumo wa Kijamaa ambao serikali kuu bado inafanya biashara na kushikilia mamlaka yote kikatiba. Viongozi wanajipa Urithi wa miradi yote pasipo kuijali nchi kwa sababu they are above the law! Nani anajua mali za JK, Lowassa, Kingunge na hata wabunge wa CCM na vyama vya upinzani, MaMeya na kadhalika. Katiba ni pambo la Ukutani tu kila kiongozi anatazama maslahi yake na ndio maana wanapinga sana ujio wa miiko ya Uongozi.

Tuna mfumo wa Uongozi ambao tuna RC na DC kama wawakilishi wa Rais hata ktk majimbo ambayo CCM imepoteza. Huu mpango wa kuwa ma wizara zisizokuwa za muungano ndio umepelekea Zanzibar kudai mamlaka hayo kwa sababu ktk muungano wowote shughuli zote za serikali sii za muungano, bali wizara zote ni za Muungano na hivyo kuifanya serikali kuu kuwa na mamlaka juu ya zile za nchi (republic).

Nyie mnatajka kuifanya serikali kuu dhaifu kisha JK akisema Jeshi litachukua nchi mnaanza kulalama pasipo kujua kwamba serikali kuu yenye wizara mnazopendekeza itakuwa haina vyanzo na hawawezi kupewa kitu ikiwa wizara zote za mapato ya taifa sii za Muungano. Hao wabunge wote wa bunge maalum la Katiba leo kila mmoja wao kisha kula zaidi ya millioni4 na bado wanazidi kujiongezea siku zaidi wakitoka hapo wote ni mamillionea. Halafu mnasema ati wana uchungu sana na Taifa hili! acheni zenu!

Sasa ikiwa madini, kilimo na Utalii ndio yanachangia zaidi ya asilimia 99 ya pato la taifa mkiyafanya kuwa sii ya Muungano hiyo serikali kuu itajiendesha vipi? ama Mnataka kuifaanya serikali kuu ya Kisultan au Kifalme. Nigewaelewa tu kama hoja hii inatoka Zanzibar lakini kwetu sisi Bara sidhani kama tunauhitaji muungano wa aina hiyo hata chembe. Na kama mnabisha wekeni mapendekezo haya bayana rasimu hii kwa wananchi kama ilivyo na sii maswali ya kuvizia kisha mtaona matokeo yake. Kifupi muundo wa serikali 3 hauna mashiko kabisa maana sioni faida ya kuwa na serikali kuu ikiwa kila nchi inaweza kujiendesha.
 
Mkuu Mkandara

Kwanza kabisa, wewe na wapenda amani lazima walaani kitendo cha JK na serikali yake kutumbukiza siasa katika maeneo ya dini. Hili halina kukwepa kama unaitakia nchi hii mambo mema.

Pili, unapotosha.
1. Znz hakuandika katiba kwasababu kuna mambo ya muungano yaliyoondolewa. Hakuna kwasababu haikuwepo sehemu ya kuyaweka. Hakuna jambo hata moja la muungano lililoondolewa, kama lipo litaje.
ZNZ ilikwenda solo kwasababu ina identity yake.

2. ZNZ inalalamika kuhusu Tanganyika kuvaa koti la muungano.
Unawezaje kuondoa malalamiko hayo kwa kuwa na JMT na ZNZ.

3. Unasema serikali ya shirikisho itakuwa haina vyanzo vya uhakika vya mapato.
Hebu tuambie vyanzo vya serikali ya sasa vya uhakika vinapatikanaje na vinatoka wapi.

4. Mfumo wa serikali 2 unaopendekeza utaondoaje malalamiko ya pande mbili bila kuwa na washirikia wa pande hizo.

Halafu tutaendelea.
 
Iwapo Muungano wa Marekani kuna States zililazimishwa kujiunga baada ya kutekwa vita mbona wao hawasemi mnayoyadai nyie maana nijuavyo hakuna Muungano ulokuwa halali kisheria. Upuuzi huu wa kuturudisha nyuma maana sisi wengine tunategemea Katiba mpya kabla ya uchaguzi ili twende mbele na sii kuturudisha nyuma miaka 50 iliyopita. .



Tuna mfumo wa Uongozi ambao tuna RC na DC kama wawakilishi wa Rais hata ktk majimbo ambayo CCM imepoteza.
Huu mpango wa kuwa ma wizara zisizokuwa za muungano ndio umepelekea Zanzibar kudai mamlaka hayo kwa sababu ktk muungano wowote shughuli zote za serikali sii za muungano,

Sasa ikiwa madini, kilimo na Utalii ndio yanachangia zaidi ya asilimia 99 ya pato la taifa mkiyafanya kuwa sii ya Muungano hiyo serikali kuu itajiendesha vipi? ama Mnataka kuifaanya serikali kuu ya Kisultan au Kifalme. Nigewaelewa tu kama hoja hii inatoka Zanzibar lakini kwetu sisi Bara sidhani kama tunauhitaji muungano wa aina hiyo hata chembe. Na kama mnabisha wekeni mapendekezo haya bayana rasimu hii kwa wananchi kama ilivyo na sii maswali ya kuvizia kisha mtaona matokeo yake. Kifupi muundo wa serikali 3 hauna mashiko kabisa maana sioni faida ya kuwa na serikali kuu ikiwa kila nchi inaweza kujiendesha.
Ukishamsoma Mkandara aliyeandika leo utajiuliza kama ndiye yule aliyeandika maneno haya wiki mbili zilizopita
Nguruvi3,
Kwa miaka 50 tumeomba mikopo na misaada kwa Jina la JMT kwa manufaa ya bara, tena kibaya zaidi misaada hiyo viongozi wameifisadi hivyo leo tuna deni la Taifa kubwa kutokana na sisi. ......

Unajua kuna hadithi moja (ya kweli) ambayo nitakusimulia, Kuna mama mmoja (jina lake kapuni) alirithi nyumba ya vyumba sita Kinondoni. katika maisha akafunga ndoa na mume ambaye baadaye kwa kutumia NDOA na mama huyo, alienda benki na kukopesha fedha nyingi tu na akaweka ile nyumba kama rehani. Baada ya muda mzee wa watu akashindwa kurudisha deni ikabidi benki waje kuikamata nyumba.

Siku walofika wakamkuta yule mama ambaye ndiye haswa mrithi wa nyumba. Wakamwambia kilichotokea na kinachafuata. Yule mama akasema hana taarifa yoyote kuhusu nyumba ile kuwekwa rehani na wala mume sii yake, yeye ndiye haswa mwenye nyumba. . Yamekwenda wee ikaonekana hata yule mama hakuwahi kubadilisha jina la mirathi ya nyumba, yule mzee pia sijui hati ya nyumba aliipata vipi hadi benki ikamkubali.

..Hivyo basi kwanza sisi bara tunatakiwa kukubali makosa.
Tukubali ni kweli sisi tumelitumia jina la Muungano kuchukua mikopo na misaada inayoiendesha mambo yasokuwa ya muungano. Mfano wa reli ya kati. Kisha baada ya kuyakubali makosa sasa ndio itafutwe njia nyepesi ya kuondoa tatizo hilo.

Hii kutokubali makosa na kuanza kunyoosheana vidole haitatufikisha popote na nina hakika hata hilo bunge la katiba watafika mahala watakwama kutokana na kwamba huko Bungeni kwenyewe Tayari kuna Utanganyika na Uzanzibar hakuna muungano hapo. Hatua hizi zinachukuliwa kutokana na jazba, hasira na karaha mlozidumisha kwa miaka 5
Kwa ufupi, Mkandara wa wiki mbili zilizopita alituambia Tanganyika imevaa koti la muungano na kuwanyonya wazaznibar. Leo Mkandara anasema znz waliondoa baadhi ya mambo kwavile Tanganyika iliyaondoa kwanza katika muungano! Angali contradiction hiyo, halafu anasema ' Hatuwezi kuwa na serikali 3 kwasababu zitakuwa ni dhaifu' hasa ile kuu. Wakati huo huo wiki iliyopita alisema serikali kuu ya sasa inainyonya znz. Hivi unawezaje kuwa na serikali kuu inayonyanya leo kesho ukadai muundo huo huo ni mzuri?

Mkandara, my dear friend !
 
Tuna nchi mbili ndani ya muungano, na kuna nchi moja nje ya Muungano hivyo tuna serikali 2, moja ni ile ya Znz na nyingine ni ya Jamhuri. kama nimesema tuna nchi 2 na kuiita ile ya muungano ni kutokana na matumizi ya hili neno ndio maana nika switch to Taifa. taifa ni moja na kuna nchi ya Zanzibar hivyo Mzanzibar anafungwa na katiba ya Znz na pia katiba ya JMT. Sisi kwa upande wetu hatuna nchi tena ila Tanzania na ndio maana hatutumii Utanganyika wala Ubara isipokuwa ktk mazungumzo.
Serikali ya Tanganyika haiwezi kuwepo ikiwa tumekubali kubadilisha jina na mipaka yetu kuwa Tanzania.

Swala hapa ni kutazama je Tanganyika inapoteza nini tunapotumia jina la Tanzania ilihali Tanganyika ipo ndio maana nikasema

labda nikukumbushe vizuri kama wewe ni Old school au middle school ya kwamba Tanganyika ni nchi kubwa sana na kulionekana hatari ya kuimeza Zanzibar kama tungekuwa na serikali 3.

................Hivyo basi ndio kuwepo kwa serikali 2 ambazo mtoto Zanzibar ana bakuli lake na anaweza kuchota toka sahani kubwa.
Sisi hatuna haja wala sababu ya kuchota sahani la mtoto ila kuna mchango wake ktk menu hiyo.

kama nilivyokwisha sema Wazanzibar hawajui ama wanafanya makusudi kabisa kuomba serikali 3 kwa sababu nina hakika BLM halitapendelea mfumo huo.

Na mfumo huo utakuwa Mzito sana kwa Wazanzibar kuliko wanavyofikiria na hakika muungano utavunjika kwa sababu bara itazuia vitu vyake kwa roho ya kimaskini maana tunachogawana ni umaskini.

Leo hii Wazanzibar wanafanya choyo kwa kitu wasichhokuwa nacho (roho ya maskini) na bara hatudhuriki maana tuna ardhi kubwa, maliasili na rasilimali za kutosha lakini itakapo geukia kwao hapo ndipo watakiona cha moto na sio wao tu ita affect Muungano mzima.
Hivi Mtoto, mwanao kweli akililia wembe kweli unatakiwa umpe?

Taabu itakuwa kwao Wazanzibar maana nchi yenyewe ndogo
, hesabu kubwa ya Wazanibar iko bara na nje, hao wakirudi pale patakuwa kama Rwanda, sasa je ndivyo mnavyotaka?..


Jibu jingine ni serikali 1, lakini hili haliwapendezi
Wazanzibar wote iwe wa BLM ama BLW hivyo ni kinyume cha makubaliano yalounda nchi yetu. Hatuwezi kuuvunja muungano ama kuufanyia majaribio Muungano hili nalikataa kwa sababu Tanzania haitakuwa Tanzania tena, tutafika walikofika Sudan au Ethiopia. Tusitake kuibadilisha Historia hapa katikati wakati Zanzibar ina historia yake na Tanganyika tunayo ambayo sisi tumekubali kuondokana na Tanganyika na kuchukua kipya kinyemi Tanzania - Chai ya Maziwa!.
nachotaka kusema hapa ni sisi kutazama interest za TAIFA letu hata kama hatukubaliani. Swala ni kuzitanmbua kero zenyewe na kisha kuzitafutia suluhu sio kuunda serikali 3 au 1 kutokana tu na kero za wanasiasa wala sii wananchi maana wananchi wamejazwa ujinga huu na hivyo hawatumii tena akili zao.
Msomeni vizuru Mkandara.
1. Mkandara anasema sisi Tanganyika hatuna nchi, nchi yetu ni Tanzania ambayo znz wamo.
Kwa upande mwingine znz wana nchi yao. Mkuu anasema serikali 3 zitaimeza Zanzibar. Hivi kutenganisha ni kumeza au ni kuweka wazi.

Mkuu wangu anasema znz ni sawa na mtoto anayeruhusiwa kuchota kutoka sahani kubwa. Kwamba ni sawa znz ikihudumiwa na kodi za Mtanganyika, hilo halina tatizo. Mkandara ana maana hata wakishinda wanacheza bao sisi Tanganyika tunawajibu wa kulipa kodi kubwa na kupinda migongo kuwahudumia.

Halafu anasema katika sahani kubwa mtoto ana mchango pia. Miaka 20 huyo mtoto hajachangia, anasubiri kuibuka na mapande ya nyama tena si kwa kuomba ni kwa kiburi na jeuri. Leo amepanga chumba 2010 katiba, Mkandara anasema ni sawa tumlipie kodi ya huko alikopanga kwa jeuri, akija tumpe za kununua sigara. Mkandara huyo si mtoto ni fedhuli na mznz respionsible atamwadabisha

Anasema znz ni nchi ndogo, wakirudi kwao itakuwa Vita. Mkandara hajakemea uhuni wa katiba ya 2010. Kuna udogo gani wakati mtoto amefikia mahali anamtaka baba yake aombe ruhusu kwakwe kabla ya kumsogelea mama. Huyo si mtoto ni baradhuli, mzazi responsible hakubali uhuni huo.

Mkandara anasema znz ina historia na ihifadhiwe, sisi yetu ipo ila kupotea kwa jina la Tanzania sio big deal.

Halafu anasemea tulinde muungano, wakati huo huo anasema serikali 1 wznz hawakubali.
Hivi Mkandara hawa wznz ni watu wa aina gani na sifa gani kiasi cha sisi kukaa na kuwasikiliza wanataka nini?

Kama hawatki serikali 1 sisi tunasema 3, kama hawataki 3 njia nyeupe waondoke.
Watu 1.2M hawawezi kutusumbua kila siku. Tena nusu yao wakiishi kwetu.

Tanganyika irudi kuondoa utegemezi, kuondoa ukupe.
Hatuwezi kuishi na watu wasiotaka kuishi na sisi. Tumechoka kubeba furushi lilislo na maana kwetu eti kwasababu muungano ni mfano Afrika.

Ubaguzi wa mznz kwa Mtanganyika, Mkandara anasema ni historia! Please
 
Sehemu ya II

MBINU ZINAZOPANGWA NA CCM DHIDI YA UKAWA

Baada ya kubainika 2/3 haipatikani, Samwel Sitta akashauri bunge liahirishwe kupisha la bajeti.
Ilijulikana bunge la JMT lazima likae kwa bajeti, ni sababu tu za kukwepa, mbinu zimegonga mwamba.

Sababu hizo zina nguvu zaidi kwa wakati huu. Ingawa Sitta anasema idadi ya wabunge imetimia kuendelea na mjadala, lakini katiba na inahitaji maridhiano.
Kukosekana kwa UKAWA si kwamba kunazidi kuondoa uhalali uliokwishaondoka, bali unatoa picha kuwa CCM ndio inaandika katiba.

Well, CCM wanaweza kufanya hivyo kwavile ubabe ni sehemu ya utamaduni wao, watakachokumbana nacho kwa wapiga kura wao hawana majibu. Ni dalili njema kuwa taifa linahitjai kubadili mwelekeo. Kudharau maoni ya wananchi si njia bora ya kutawala nchi.

CCM na Samwel Sitta wanataka kuitumia nafasi ya kuahirishwa bunge kufanya mambo mengi

1. Kumtumia Rais kutafuta mwafaka na UKAWA kama alivyowahi kufanya.

Rais atatumia hotuba ya April 26 2014 kubadilisha na kuwazulia UKAWA mambo mazito

2. CCM kuwatumia viongozi wake kuzunguka nchini kutisha watu kuhusu rasimu ya Warioba, kupendekeza wanachotaka na kuahidi makubwa kwa wazanzibar. Katika matisho ni yale ya jeshi kuchukua nchi chini ya serikali 3, wazanzibar kufukuzwa na kuua muungano

3. Kuwatisha wabunge wao zaidi katika vikao

Kutakuwa na vikao vya kuwashughulikia walioonyesha kutoridhishwa na maamuzi yaliyopanga msimamo wa serikali 2. Hili halitahusu kuwafukuza, ni kuwatisha ili wawe mfano kwa wengine

4. Kuwanunua wajumbe wa UKAWA kwa hila na mbinu

Wajumbe waliobaki watapewa nafasi sana ya kuongea ili kuondoa hisia za uCCM.
Wale wenye msimamo wa kati na wasiojitambua, aghalabu watafungiwa kitita ili wanyamaze

5.Kuwachonganisha viongozi wa UKAWA ili wafarakane

Kutakuwa na mpango wa kuwachonganisha viongozi wa ukawa kwa kutumia wanachama wa vyama vyao ambao ni mapindikizi.
Kurekebisha sheria zitakazo wapa 2/3 .
Idadi ipatikane kwa waliopiga kura na si wajumbe wote ili kuwezesha kupatikana 2/3 kwa kutumia CCM pekee

6. Kutumia bunge la bajeti kuonyesha kero za znz zimeshughulikiwa

Zanzibar itatengewa fungu kubwa la bajeti kutoka bunge la JMT. ili kuwanyamazisha.
Gharama zakuwafurahisha wazanzibar atazibeba, mkulima, mvuvi na mfanyakazi wa Tanganyika kwa vile kodi zao ni za Tanzania ambayo znz inastahili

7. Kuwashawishi wajumbe wa BLW chini ya Kificho uwezekano wa kurekebisha katiba 2010 inayoleta matatizo na ugumu kwa CCM.

Ni ngoma nzito lakini jaribio lipo mbioni
Wazanzibar CCM watashawishiwa ili kuepuka serikali 3, hakuna budi kubadili katiba ya 2010 inayoleta taabu kwa upande wa CCM sasa hivi.

9 Kuzuia mikutano ya vyama na Ukawa
Hili limeshaanza na lina malengo makubwa mawili

a) Kutoa nafasi ya rais kuwaeleza wananchi kuhusu kususia kwa UKAWA, akiwananga kwa kutumia hoja zao. Tukio litafanyika April 26 siku ya muungano.Kwa kawaida Rais hahutubii, safari hii atafanya hivyo iwe mbeleya mkutano au kuelekea wiki ya maazimisho ya muungano

b) Kuzuia UKAWA kuchukua ‘attention' ya wananchi wakati CCM wanaendelea na bunge lao Dodoma. Kuruhusu mikutano ya UKAWA kutamaanisha kupuuzwa kwa hoja za upotoshaji Dodoma kusikika na kutitia katika masikio ya Watanzania.


Inaendelea ....
Tulionya mapema sana kuhusu hayo yaliyoandikwa. Hoja namba 4,5 na 9 zimeanza kufanyiwa kazi.
Hii ni kuwakumbusha UKAWA.

Mwanzo wa bandiko tumeweka haya
CCM MAJI YA SHINGO,AIBU YATAWALA
WAGAWE UWATAWALE, MBINU INAYOPIKWA DHIDI YA UKAWA
UKAWA KUREJEA MAKOSA YA SIKU ZA NYUMA
 
Mkuu Mkandara

Kwanza kabisa, wewe na wapenda amani lazima walaani kitendo cha JK na serikali yake kutumbukiza siasa katika maeneo ya dini. Hili halina kukwepa kama unaitakia nchi hii mambo mema.

Pili, unapotosha.
1. Znz hakuandika katiba kwasababu kuna mambo ya muungano yaliyoondolewa. Hakuna kwasababu haikuwepo sehemu ya kuyaweka. Hakuna jambo hata moja la muungano lililoondolewa, kama lipo litaje.
ZNZ ilikwenda solo kwasababu ina identity yake.

2. ZNZ inalalamika kuhusu Tanganyika kuvaa koti la muungano.
Unawezaje kuondoa malalamiko hayo kwa kuwa na JMT na ZNZ.

3. Unasema serikali ya shirikisho itakuwa haina vyanzo vya uhakika vya mapato.
Hebu tuambie vyanzo vya serikali ya sasa vya uhakika vinapatikanaje na vinatoka wapi.

4. Mfumo wa serikali 2 unaopendekeza utaondoaje malalamiko ya pande mbili bila kuwa na washirikia wa pande hizo.

Halafu tutaendelea.
Swala la kulaani tahadhali ilotolewa ni kutokubali ukweli kama mnavyoendelea kuamini. Hatari ya Udini ipo na lazima izungumziwe kila inapowezekana tatizo la JK ni pale anaposhindwa yeye mwenyewe kutumia mamlaka alopewa kuhakikisa vitendo hivi haviendelei badala yake anatumia jukwaa kulalamika kama vile yeye sii mhusika.

1. Swala la Zanzibar na kuandika katiba.

Kama unapinga jambo ni muhimu wewe mwenyewe uwe na ukweli kwa majibu unayoyatoa. Unaposema Zanzibar ilikwenda solo kwa sababu ya Identity yake una maana gani maana Zanzibar ilikuwa na Identity yake ilikuwepo na ndicho wanachodai muda wote kuwepo kwa Zanzibar isipokuwa nyie ndio hamkubali kuwa Zanzibar ni nchi. Na wala sii kosa kwa nchi kuandika katiba yake ikiwa Utawala wa pande mbili walikaa na kufikia muafaka ambao kero nyingi ziliondolewa.

Kishria kama hili ni kosa basi kuna makosa mengine mengi yalofanyika ktk kuondoa maswala yasokuwa ya muungano na kuyafanya ya muungano pasipo ridhaa ya wananchi ama Bunge bali pia viongozi wa CCM walikaa na wale wa baraza la Mapinduzi wakakubaliana kuongeza mambo hayo toka 11 hadi 22.

Hivyo makosa yote haya yametokea kwa sababu serikali kuu imekuwa ikiendelea kutuongoza ktk mfumo wa Kijamaa ambao chama tawala kinatumia itikadi yake kuwa mwongozo wa Kitaifa na wenye mamlaka pekee ya kufanya mabadioliko ya Katiba pasipo ridhaa ya wananchi. Na kwa sababu hiyo hadi leo tunatumia katiba ya Tanganyika ama niseme CCM kuongoza Muungano.

Hivyo maadam hatukufanya mabadiliko makubwa ya Katiba mwaka 1984 na 1993 kuondoa mamlaka hayo kwa chama tawala ni sisi wenyewe wa kujilaumu maana miaka yote 30 tumekuwa tukiendeshwa na mwongozo ule ule ulofanyika ammendmenrs na chama tawala. Mwaka 2010 Zanzibar walikaa na chama tawala tena na kufanya makubaliano ambayo yalipelekea kuandikwa kwa katiba mpya ya Zanzibar. Usinambie uongozi wa Tanganyika ama CCM hawakujua kinachofuatia. Na ndio maana JK na serikali yake wako kimyal na wameendelea ,kusema KERO nyingi za Muungano zimeondolewa kiasi kwamba leo hii tumebakia na 6 tu.

Nitakubaliana na mtu yeyote atakaye sema Katiba yetu sio halali kwa sababu bado tunaendelea kutumia katiba ya Tanganyika na CCM kama mwongozo wa Jamhuri ya Muungano japo leo hii yupo ktk mfumo wa vyama vingi na kiucjhumi ktk soko huria na utandawazi. Hii haihusiani kabisa na Muungano isipokuwa zile taratibu na sheria zinayotumika kufanya ammendments ya Katiba na sheria.

Hii ndio sababu ya kwanza kabisa sisi tumeitajka Katiba Mpya, tumetaka mabadiliko makubwa ktk mwongozo huu ili kuondokana na itikadi za chama kimoja iliyopelekea muafaka bana ya CCM na CUF na hatimaye kuwepo kwa katiba ya Zanzibar. Hili sii swala la Zanzibar kuwa nchi ama kuandika katiba kwa sababu yalikuwepo maridhiano ya kisheria chini ya Katiba ya CCM wenye mamlaka yote ya dola wakivaa mgozi ya demokrasia.

2 Tanganyika kuvaa koti la Muungano

Ni muhimu kwanza ufahamu maana ya neno hili na kwa nini Zanzibar wamedai hivyo. Kama hufahamu huwezi kuelewa hata kidogo na ndio maana mnashindwa kutambvua kwamba sii swala la serikali 2 au 3 bali pale serikali ya Tanganyika inapochukua mikopo kwa kutumia jina la Tanzania (muungano) kuendesha miradi yake. Sasa wewe nambie ikiwa bajeti ya serikali ya Muungano inategemea wahisani kwa asilimia 40 lakini fedha hizo zinatumika Bara unafikiri hii sio kuvaa koti la Muungano?

Ndio kueema hivi kweli mkeo akikopa fedha benki akitumia nyumba yenu kama rehani kisha akafanya yale yanayompendeza yeye huoni kama mkeo katumia jina la ndoa yenu kupata mkopo huo? na itakuwa vibaya ikiliweka wazi?

2. Vyanzo vya Mapato

Mkuu kuhusu hili unataka kunambia hujui ya kwamba serikali ile ya 2 ya Muungano ndio inamiliki wizara zote za Uzalishaji, dhamana ya mikopo na grants? Unapoondoa mamlaka haya na kuyaweka mikononi mwa nchi kama Tanganyika/Zanzibar tena kwa mfumo wa Chako chako, changu changu kwa sababu tu Zanzibar wanadai Chetu changu, changu changu. Mnashindwa kuiona logic hapo japo nyie wenyewe wake zenu nyumbani chao ni chao na chako ni chenu nyote kwa kwa sababu maalum ya kwamba mkeo ni dhaifu ktk mfumo dume hivyo ili kumlinda asimezwe na ndoa hiyo unamuwezesha yeye kuweka pato lake kwa shida zake.

Ni utamaduni wetu wa Kiafrika ulotuongioa kuunda huu Muungano ambao Zanzibar ilikuwa na watu laki 3 wakati sisi ni mil.11 ni zaidi ya mara 30 na leo hii sii kwamba asilimia hiyo imepungua bali bado ni kubwa kutokana na Wazanzibar wengi kuhamia Bara.
Kifupi ukiifanya serikali kuu kuwa ndogo isiokuwa na mamlaka juu ya wizara zake ati wizara sii za muungano badala ya shghuli kutokuwa za Muungano utaidhoofisha serikali hiyo na kuwa kama ya Kisultan ama Kifalme ambayo inategemea zaidi nguvu ya Jeshi lake na sii nchi ya demokrasia. Hii habari ya Chako chako changu changu ya serikali 3 inaondoa kabisa uwezo wa serikali kuu kujiendesha maana kila nchi haita ihitaji serikali kuu bali serikali kuu itazitegemea nchi washiriki.

4. Mfumo wa serikali 2 Utaondoaje malalamiko ya pande mbili!

Labda hujanisoma vizuri mkuu wangu maana narudia maneno yale yale kila siku. Labda nianze upya, Kwa nini napendekeza serikali 2.
a) Kwa sababu naamini malaalamiko ya pande mbili hayahusiani na muundo wa serikali bali mfumo wa Utawala ulotawaliwa na katiba ya CCM ambayo wao waliifanya ammendements kukidhi mahitaji ya chama tawala na sio wananchi wa pande mbili husika.

b) Tunaweza kulivua koti la Muungano ndani ya serikali 2 au 3 ikiwa tutafikia muafaka wa kwamba Kila nchi itachangia mfuko wa Taifa kwa asilimia kadhaa tuseme asilimia 60 kwenda mfuko wa Taifa, na 40 kubakia ktk nchi husika tokana na makusanyo ya kodi. Hivyo chochote kinachokusanywa bara kitahesabika kama ni pato la bara na chochote kitakacho kusanywa Visiwani kiyahesabika kama pato la visiwani.

Kila transaction ya mauzo lazima iwe na kodi mbili - 1 ya Nchi kwa asilmia 40 ile na 2 ya Taifa kwa asilimia 60. Wizara zote zitakuwa za muungano isipokuwa tunakuwa MAMLAKA ya usimamizi wa shughuili za serikali ndio sio ya Muungano. Kwa maana ya kwamba wizara ya Kilimo ni ya Kitaifa na waziri wake anahusika pande zote za muungano kwa sababu serikali kuu inategemea panga lake la asilimia 60. Ila shughuli za uendeshaji wa kilimo ktk nchi hizo unaendeshwa na serikali za nchi hizo.

Hivyo waziri wa serikali kuu ni waziri wa Tanganyika na JMT awe katoka Bara au visiwani kwa sababu tusifikirie kwamba waziri akitoka Bara basi huyu atakuwa mzuri kwa Tanganyika kuliko waziri wa Kilimo kutoka Zanzibar hataijali Bara! Fikra hizi ni potovu maana mawaziri woote walokwisha shika nyadhifa za juu za seruikali ya Muungano wamehamia Bara wao na familia zao kuliko walobakia Znz. Mkuu wangu kugawana umaskini tutaficha zaidi makucha ya kina EL/Rostam ambao wanatumia nafasi hizi kutoipata Katiba mpya itakayo wavua mamlaka kwa kusimika - MAADILI na MIIKO ya UONGOZI. Tunaihitaji katiba mpya kuliko kujadili Muungano ulokwisha zaliwa iwe kiharamu ama kwa msahafu. Kitanda hakizai haramu!

5, Kwa nini sipendekezi serikali 3.

a) kwa sababu inaturudisha nyuma sana kuanza kuifufua Tanganyika na itachukua miaka 2 ijayo.

b) Serikali 3 ilopendekezwa ni ya kipekee ambayo ukiisoma kwa makini ni kugawana umaskini CHAKO CHAKO, CHANGU CHANGU, Ndoa ya aina hii haiwezi kudumu na hakika mnaitaka serikali 3 kwa sababu ya hasira, ghadhabu na kiana ni utenganisho yaani wasitubabaishe hao! Hapa hatujengi ila tunabomoa. Ni kusema dalili ya kukata tamaa na kusema - Aaaah na Liwako liwe!

c) Ningeipokea tu serikali 3 kama ingekuja kabla ya mchakato wa katiba mpya ama baada ya katiba mpya. Ujio wake ni ktk wakati mbaya sana ambao mabadiliko ya Katiba kutoka mfumo wa Ujima (CCM) ulojificha kwa ngozi ya Demokrasia (kondoo) lazima uondolewe haraka sana ili demokrasia ya kweli isimame.

Kesho Chadema au CUF wakishinda uchaguzi wa Majimbo wao ndio wanakuwa na dhamana na mamlaka ya kuongoza shughuli zote za Maendeleo ya mikoa hiyo. Kuendelea kuwa na mfumo wa TANU/CCM kiutawala ni kushindwa kuelewa chimbuko la malalamiko yote haya.
 
Back
Top Bottom