UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

Mkuu Mchambuzi, inaonekana pamoja na usomi wake wote, Mkandara hajui hata mfumo tulio nao hivi sasa unafanyaje kazi. Ngoja nimpe A,B,C ya tunaouita mfumo wa serikali mbili ndani ya nchi mbili...tunazo mamlaka tatu;

  1. Kuna mamlaka inayosimamia mambo ya Muungano.
  2. Kuna mamlaka inayosimamia mambo yasiyo ya Muungano kwa Zanzibar
  3. Kuna mamlaka inayosimamia mambo yasiyo ya Muungano kwa (Tanganyika) Tanzania bara.
Mtizamo wa watu kama Mkandara naufananisha na msimamo wa Wamarekani wasiompenda Obama. Utawakuta wakipinga kinachoitwa Obama care huku wakiisifia ACA, Affordable Care Act bila kujua ni kitu hicho hicho. Saha hapa mtu anakiri kwamba mamlaka ziko tatu lakini hapo hapo anapinga serikali tatu bila kujua kwamba ni kitu kile kile. Inaonekana wasichotaka kukisikia ni maneno serikali ya Tanganyika na wakati huo huo hawaoni tatizo kuitaja na kuitetea serikali ya Zanzibar; eti serikali ya Zanzibar ikae na serikali ya Muungano ili waongee nini? Mambo ya Zanzibar, ya Muungano ama ya Tanganyika? CCM ilijiunga na CUF kuunda serikali lakini leo Chadema ikijiunga na CUF hiyo hiyo kudai katiba ya wananchi, huo umoja unatiliwa shaka na kuhusishwa na ugaidi/usultani! Akili gani hizi?

Mkandara, ukweli ni kwamba hapa hatuna Muungano, tuna shirikisho, period. Hatuwezi kuwa na Muungano tukawa na serikali mbili, tatu, nne, tano na kuendelea! Matapeli wa kisiasa ndio wanataka watuaminishe kuwa tuna Muungano wa serikali mbili wapate pa kuficha uovu wanaoutendea Tanganyika, wapate kichaka cha kufujia rasilimali za Watanganyika na wapate kambi ya kuendeshea ufisadi kwa kung'ang'ania madaraka. Sasa ilichofanya Tume ni kuuambia utawala kuwa mbinu zao chafu wananchi wamezishtukia, Watanganyika kama walivyo Wazanzibar wamechoka kudhulumiwa kwa kivuli cha Muungano. The good news kwao ni kwamba wapo watu kama wewe, tena wasomi, mko tayari kutumiwa/kutumika kutetea hiyo hali; the bad news kwenu ni kwamba wananchi walio wengi wameamka na kwa sauti kubwa wamesema imetosha.
Mkuu wangu nashindwa kukujibu maana jibu umeliweka wewe mwenyewe. sasa ikiwa ktk muungano huu wa serikali 2 kuna serikali 3 unaitaka serikali ya 3 ili iweje? hapo ndipo mnaponishinda maana sioni kuwepo kwa jina la Tanganyika kutabadilisha mfumo wa uliopo ama kuondoa MAPUNGUFU ila yawezekana ikapoza kero zilizopo. Nimesema sana na nitarudia kusema ya kwamba nyote mnaopendekeza serikali hizi iwe 1, 2 au 3 mnafanya hivyo kwa kutazama njia ya kuondoa kero zilizopo wakati kero ni matokeo ya mahitaji kupitiliza. Kama vile kukosekana kwa barabara nzuri za Usafiri Dar, serikali na Manispaa imeamua kuwafungia Daladala na Boda boda kutofika mjini wakati ukweli ni kwamba foleni za magari bado zitaendela kuwepo na njia pekee ni kuongeza na kupanua mabarabara ya mjini sii kuongeza usafiri wa mabaus wala kuwafutia watu liseni za biashara wasifike mjini.

Sipingi kuwa na serikali 1 maana huko ndiko tulikotakiwa kwenda lakini sidhani kama ni suluhisho ikiwa bado KATIBA yetu imebeba kwa sehemu kuwa ITIKADI ya siasa ya Chama cha MAPINDUZI. Hofu ya CCM sio ujio wa serikali 3 kwa maana hii isipokuwa wanahofia kupoteza nguvu yao Zanzibar kwa chama cha CUF ambacho wao wanajua fika kina wafuasi wengi wa HIzbu, hivyo CDM mnapoungana na CUF pasipo kujua wenzenu wanapigania nini ktk mfumo huu ni kujiweka ktk nafasi mbaya sana kisiasa. Na kibaya zaid nasikia UKAWA watakuwa Zanzibar kuwashtakia wananchi badala ya kundi hili kuendelea na mjadala bungeni kutushawishi sisi wananchi ili kesho katiba itakapo letwa mbele yetu tuikatae!

Kinachoendelea Bungeni ni sawa na Bunge la Taifa yaani watu wanabishana pasipo kujua dhumuni la Ubishi wao. Pale wanatakiwa kutushawishi sisi wananchi ambao ndio sauti ya mwisho. Kupiga kwao kura haina maana ndio mwisho wa utunzi wa Katiba kwa sababu ni lazima sisi wananchi tuikubali katiba hiyo. Hivyo kama wananchi wanaitaka serikali 3 mbele ya utunzi wa Katiba wataikataa katiba ilopitishwa na Wajumbe wengi wa CCM.
 
Nguruvi3,
Mkuu hata sijui nikujibu nini. Hakuna ndoa isikuwa na matatizo kila ndoa toka babu zetu, baba zetu hadi sisi wenyewe lakini haina maana ndoa ni kero. Quebec wanachodai hakina tofauti na Zanzibar na kwa muda mrefu wamekuwa wakisumbua sana. Ila ukitazama mamlaka waloyataka yote wamepewa na kila wanapojaribu kuwashawishi wananchi vyama vingine vimekuwa mstari wa mbele kuwatahadharisha wananchi vile vile. Kwa kila mapungufu ya swala la Quebec yana picha mbili, na mara zote wananchi wamechagua kubakia Canada wala sii swala la serikali ngapi ndani ya ngapi. Quebec wanapigania haki zao kikatiba tofauti na sisi tunaopigania jina wala sii mila au utawaduni wa Mbara.

Hivyo utaona matatizo ya Quebec ni ya kisiasa zaidi. Kuna makucha ya Mfaransa na Muingereza na sijui kama unaelewa ya kwamba Canada bado ni Dola ya Malkia, hivyo Quebec wanataka kujikata kwa sababu hawataki kujifananisha na Malkia zaidi ya kuwa karibu na Ufaransa. Hali hii sisi hatuna ila kama mtaendelea kuwasikiliza kina Jussa mnaweza tufikisha huko.
 
Mkandara

Karibu sana ndugu, kama upo mjini posta nakukaribisha,

Msimamo wako juu ya suala la katiba unanyesha wazi huyajui ama kuna mambo yanayoendelea kutukia wewe unayaona kwa jicho la kiimani zaidi,
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,
Mkuu hata sijui nikujibu nini. Hakuna ndoa isikuwa na matatizo kila ndoa toka babu zetu, baba zetu hadi sisi wenyewe lakini haina maana ndoa ni kero. Quebec wanachodai hakina tofauti na Zanzibar na kwa muda mrefu wamekuwa wakisumbua sana. Ila ukitazama mamlaka waloyataka yote wamepewa na kila wanapojaribu kuwashawishi wananchi vyama vingine vimekuwa mstari wa mbele kuwatahadharisha wananchi vile vile. Kwa kila mapungufu ya swala la Quebec yana picha mbili, na mara zote wananchi wamechagua kubakia Canada wala sii swala la serikali ngapi ndani ya ngapi. Quebec wanapigania haki zao kikatiba tofauti na sisi tunaopigania jina wala sii mila au utawaduni wa Mbara.

Hivyo utaona matatizo ya Quebec ni ya kisiasa zaidi. Kuna makucha ya Mfaransa na Muingereza na sijui kama unaelewa ya kwamba Canada bado ni Dola ya Malkia, hivyo Quebec wanataka kujikata kwa sababu hawataki kujifananisha na Malkia zaidi ya kuwa karibu na Ufaransa. Hali hii sisi hatuna ila kama mtaendelea kuwasikiliza kina Jussa mnaweza tufikisha huko.
At least you know that si kila mmoja anaweza kumeza namba bila fikra.
Labda ueleze Puerto Rico na USA nao vi
Hivyo hoja yako ya kuwa miaka 200 hawana matatizo ya muungano sasa ipunzike, haina mashiko.

Sisi tunapigania utamaduni wa Mtanganyika. Huwezi kupigania utamaduni ukiwa huna Identity.
Wewe ni Mkerewe ambayo ni ID yako, halafu tunaangalia utamaduni wa Wakerewe.

Ni kwasababu hizo, znz wana ID na ndio maana wana uwezo wa kusema 'sisi'.
Sisi hatuna, utamaduni wetu ni wa wzn pia sasa kuna utamaduni hapo?
 
Nguruvi3,
Mkuu hata sijui nikujibu nini. Hakuna ndoa isikuwa na matatizo kila ndoa toka babu zetu, baba zetu hadi sisi wenyewe lakini haina maana ndoa ni kero. Quebec wanachodai hakina tofauti na Zanzibar na kwa muda mrefu wamekuwa wakisumbua sana. Ila ukitazama mamlaka waloyataka yote wamepewa na kila wanapojaribu kuwashawishi wananchi vyama vingine vimekuwa mstari wa mbele kuwatahadharisha wananchi vile vile. Kwa kila mapungufu ya swala la Quebec yana picha mbili, na mara zote wananchi wamechagua kubakia Canada wala sii swala la serikali ngapi ndani ya ngapi. Quebec wanapigania haki zao kikatiba tofauti na sisi tunaopigania jina wala sii mila au utawaduni wa Mbara.

Hivyo utaona matatizo ya Quebec ni ya kisiasa zaidi. Kuna makucha ya Mfaransa na Muingereza na sijui kama unaelewa ya kwamba Canada bado ni Dola ya Malkia, hivyo Quebec wanataka kujikata kwa sababu hawataki kujifananisha na Malkia zaidi ya kuwa karibu na Ufaransa. Hali hii sisi hatuna ila kama mtaendelea kuwasikiliza kina Jussa mnaweza tufikisha huko.

Mkandara,

Zanzibar wanapigania haki zao kikatiba na tayari walishabadilisha katiba yao 2010 na kuwa "nchi".
Leo hii waziri wa fedha wa Jamhuri ya Muungano amerudi toka Marekani alikoenda kikazi akifuatana na waziri wa fedha toka "nchi" ya Zanzibar! Huu ndio uhuni CCM wanataka kuuendeleza.

Kuhusu hoja kuwa 'hata kwenye ndoa kuna kero'. Nikukumbushe kuna kitu kinaitwa "talaka". So, tell us something new.
 
Mkandara,
Leo hii waziri wa fedha wa Jamhuri ya Muungano amerudi toka Marekani alikoenda kikazi akifuatana na waziri wa fedha toka "nchi" ya Zanzibar! Huu ndio uhuni CCM wanataka kuuendeleza.
Mawaziri wote ni kutoka "nchi" nyingine. Hayo ndio JK alimaanisha kwenye hotuba yake kuhusu kutatua kero za Zanzibar.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
At least you know that si kila mmoja anaweza kumeza namba bila fikra.
Labda ueleze Puerto Rico na USA nao vi
Hivyo hoja yako ya kuwa miaka 200 hawana matatizo ya muungano sasa ipunzike, haina mashiko.

Sisi tunapigania utamaduni wa Mtanganyika. Huwezi kupigania utamaduni ukiwa huna Identity.
Wewe ni Mkerewe ambayo ni ID yako, halafu tunaangalia utamaduni wa Wakerewe.

Ni kwasababu hizo, znz wana ID na ndio maana wana uwezo wa kusema 'sisi'.
Sisi hatuna, utamaduni wetu ni wa wzn pia sasa kuna utamaduni hapo?
Mkuu wangu bado hunielewi? Maswali yenye majibu google sipendi kuyajibu kwa sababu hata wewe unaweza kuyasoma hivyo ya Purto Rico nakuachia wewe. Nachochangia hapa ni fikra zangu mimi juu ya maswala yanayonihusu na mchango wangu kama raia wa nchi hii. Haya niyasemayo ni mawazo yangu mimi kinyume cha chama changu, viongozi wangu na hata baadhi ya marafiki na majirani zangu.

Katiba sii swala la Uanachama, dini kabila wala Ubara ila ni mwongozo wetu sote kwa matabaka yetu ili tuweze kuishi pamoja. Haya maswala ya Talaka unayaleta wewe ambaye ktk swala hili unataka kuudanganya Umma kwamba talaka haivunji muungano.

Sasa kama kweli wewe unaamini mimi ni Mkerewe kwa nini mnapinga Uraia wa nchi mbili? kwa nni mnasema mimi ni mkimbizi japo sikuwa mkimbizi maana tafsiri ya mkimbizi inajulikana. Hofu na woga huu ndio sababu ya watu kuitaka serikali ya 3 kwa sababu tu CCM wote wanatetea serikali 2. Sababu zao CCM ni tofauti kabisa na mnavyofikiria lakini maadam chale zimewacheza kuona CCM waitaka serikalik 2 basi lazima Upinzani watofautiane, bora kuwaunga mkono kina Jussa na Sultan kuliko kuunga mkono CCM..Ndio hivyo hivyo kuogopa Wazawa wanaoishi nje kuwa watakuja sijui kuiba sijui kipi na kupeleka nje, lakini wepesi wa kuwapokea Wachina, Wahindi na Waarabu na kuwapa Uraia lakini sii Mkerewe miye..

Hizi fikra za vilaza ndizo zinazoturudisha nyuma japo mifano kibao juu ya Diaspora wanavyoweza kulisaidia Taifa. Kwenu ni talaka, talaka talaka hadi zifike 3 kisha mnamlaumu Mungu mnapokuwa na shida ya kuishi na wanawake wengine. Ajizi nyumba ya umaskini.
 
Mawaziri wote ni kutoka "nchi" nyingine. Hayo ndio JK alimaanisha kwenye hotuba yake kuhusu kutatua kero za Zanzibar.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Na ukirudi kwenye kusimamia Muungano wenyewe kazi hiyo inaratibiwa na Makamu wa rais, kwa sasa Gharib Bilal pamoja na Waziri Samia Suluhu. Wote wanatoka Zanzibar! "kero" zitatuliwa vipi kama wote wanatoka upande mmoja?
 
Na ukirudi kwenye kusimamia Muungano wenyewe kazi hiyo inaratibiwa na Makamu wa rais, kwa sasa Gharib Bilal pamoja na Waziri Samia Suluhu. Wote wanatoka Zanzibar! "kero" zitatuliwa vipi kama wote wanatoka upande mmoja?
Hvi kweli wewe unaamini rais akitoka zanzibar ataitetea Zanzibar kuliko Bara! Ebu nikumbusheni Mwinyi alifanya nini kikubwa kwa Zanzibar au Mkapa, JK wamefanya nini kikubwa kwa Tanganyika kiasi kwamba tujisifie kuwa na rais Mtanganyika. Kusema kweli siwaelewi kabisa zidi ya kuona fikra hizi hazina tofauti kabisa na Jussa ila kwa upande wa pili wa shilingi!
 
Hvi kweli wewe unaamini rais akitoka zanzibar ataitetea Zanzibar kuliko Bara! Ebu nikumbusheni Mwinyi alifanya nini kikubwa kwa Zanzibar au Mkapa, JK wamefanya nini kikubwa kwa Tanganyika kiasi kwamba tujisifie kuwa na rais Mtanganyika. Kusema kweli siwaelewi kabisa zidi ya kuona fikra hizi hazina tofauti kabisa na Jussa ila kwa upande wa pili wa shilingi!
Maana kubwa ya FJM na Mchambuzi ni kuwa kutokuwepo kwa Tanganyika kuna jenga hisia hizo. Kwa mfano, JK alizungumzia malalamiko ya znz peke yake katika hotuba. Tunaelewa yapo ya Tanganyika lakini kwa kutaka kuwafurahisha wznz akaamua kuzungumzia reli.

Mfano, kuna ubaya gani znz ikichangia reli? Nusu ya wznz wanaishi na kufanya kazi bara, je si vema kuwa na miundo mbinu itakayotusaidia pamoja?

Lakini pia JK hakueleza ubaguzi wa wazi na tatizo kama waziri mkuu kuomba kibali cha kufanya kazi znz.

Katika kutatua kero Gharibu Bilal na Samia hawawezi kusimamia haki ya Mtanganyika. Ni hawa walikuwa bungeni hawakukemea uhuni wa znz kuiweka katiba ya JMT chini yao, leo wana uchungu gani na Tanganyika.

Hao wapo kwa ajili ya kuongeza nafasi na fursa kwa wznz kutokana na choyo na ubinafsi wao.

Lini umemsikia Gharibu Bilal akikemea uhuni wa watu kubaguliwa znz?
Lini umemsikia Samia akizungumzia ubaguzi wa wznz kwa Mtanganyika.
Hawawezi kwasababu lengo lao ni moja kumtumia na kuitumia Tanganyika to maximum.

Mkandara, unapokuwa na JMT ambayo znz ipo na inawakilishwa na Gharibu bilal na Samia Suluhu, upande wa pili ukawa na Makamu Seif Idd kutoka SMZ halafu ukasema unazungumzia kero ni kujidanganya. Huwezi kuwa na kocha mchezaji na refa mchezaji mchezo ukawa katika level field. Hakuna.

Kutokana na hayo, masilahi ya Mtanganyika hayana mlinzi.
Ndiyo maana znz wanasema suala la uvuvi si la muungano kwasababu wanajua hiyo inawanufaisha. Lakini wznz hao hao hawasemi kuwa elimu ya juu si muungano kwasababu inawanufaisha kuwa sehemu ya JMT.

Kwa maneno mengine waziri wa uvuvi wa znz yupo kwa znz, halafu wakitaka kunufaika na fursa za bara wanasema wao ni Watanzania wa JMT.
Hayo yakitokea wapo mbele kuweka vikwazo kwa raia wa JMT akiwa kule kwao kwa kumwita Mtanganyika.

Hivyo masilahi ya Tanganyika ni shamba la bibi.
Tunasema hapana, tunataka Tanganyika ili tufanye mambo yetu bila kuomba kibali baraza la wawakilishi.

Hii habari ya kutaka kujenga nyumba za walimu wetu eti tusubiri watu 50 wasema 'ndiyo' ni uhuni usiovumilika na hatutavumilia, hatutapumzika hadi Tanganyika waliotuachia mababu zetu izinduke.

Leo kero zote ambazo wanasema zimebaki 3 zimetatuliwa si kwa maridhiano bali kuwapa wznz wanachotaka.Wanataka kutoka mifukoni mwetu, hapana! sasa basi.

Kuna mambo 7 yamekubaliwa, kama hawataki tuvunje jahazi.
Sisi na umasikini wetu tutaendelea hivyo hivyo.

Tuna uzoefu wa EAC ambayo Kenya ilidhani tutafutika katika uso wa dunia, leo tupo toe on toe nao, seuse watu laki tano!



 
Last edited by a moderator:
Hvi kweli wewe unaamini rais akitoka zanzibar ataitetea Zanzibar kuliko Bara! Ebu nikumbusheni Mwinyi alifanya nini kikubwa kwa Zanzibar au Mkapa, JK wamefanya nini kikubwa kwa Tanganyika kiasi kwamba tujisifie kuwa na rais Mtanganyika. Kusema kweli siwaelewi kabisa zidi ya kuona fikra hizi hazina tofauti kabisa na Jussa ila kwa upande wa pili wa shilingi!
Unaongelea zama tofauti mkuu wangu. Wakati wa Mwinyi katiba ya 2010 haikuwepo. Wakati huo hakukuwa na vibali vya kufanya kazi wala hakukuwa na ubaguzi wa ukaazi.

Kwasasa political landscape imebadilika. Kuna katiba ya znz ya 2010 inayoitambulisha znz kwa kila kitu.
Katiba imsema wana Amir jeshi mkuu wao, wana mipaka inayolindwa na rais wa znz ingawa gharama anabeba Mtanganyika. Wana kila jambo lililowekwa makusudi kumhujumu na kumkomoa Mtanganyika.

Hilo ndilo limeibua curiosity ya muungano na Tanganyika ikaona jinsi gani inavypinda mgongo kwa kubeba mzigo ambao ujira wake ni matusi, kashfa, dharau na kiburi. Hivi kweli watu 50 wa BLW la nchi jirani ya znz wanaweza kuwaamuliwa Watanganyika lini wajenge Hospitali zao!!! Real, hawa akina Pnadu na Jusa wakae na kupanga lini wanakubali tuongeze shule zetu! lini tujenge maternity ward za akina mama! Hilo Mkandara unaliona sawa kabisa.
Tukuulize kwa faida gani unadhani tunaihitaji znz kwa gharama kubwa namna hiyo.

Unapopeleka mswada wa bunge la JMT lenye wabunge 320 waliwemo wznz 81 ili ukajadiliwe na watu 50 ni kuidhalilisha Tanganyika sana. Hilo halikutokea kwa Nyerere, Mwinyi au Mkapa.
Limetokea kwa JK ambaye kutokana na udhaifu wake amekubali kuiuza Tanganyika.

CCM na wengine watalazimisha wanachotaka, tuna uhakika wa jambo moja, tutaipigania Tanganyika hadi irudi.
Mwingereza alipewa akaikalia hatimaye akairudisha. Hatuwezi kushindwa, hatutapumzika hadi tuwaachie watoto na wajuu wetu taifa lao lenye historia yao. Hadi tuwaachie kile tulicho nacho.
 
Mkuu wangu bado hunielewi? Maswali yenye majibu google sipendi kuyajibu kwa sababu hata wewe unaweza kuyasoma hivyo ya Purto Rico nakuachia wewe. Nachochangia hapa ni fikra zangu mimi juu ya maswala yanayonihusu na mchango wangu kama raia wa nchi hii. Haya niyasemayo ni mawazo yangu mimi kinyume cha chama changu, viongozi wangu na hata baadhi ya marafiki na majirani zangu.

Katiba sii swala la Uanachama, dini kabila wala Ubara ila ni mwongozo wetu sote kwa matabaka yetu ili tuweze kuishi pamoja. Haya maswala ya Talaka unayaleta wewe ambaye ktk swala hili unataka kuudanganya Umma kwamba talaka haivunji muungano.

Sasa kama kweli wewe unaamini mimi ni Mkerewe kwa nini mnapinga Uraia wa nchi mbili? kwa nni mnasema mimi ni mkimbizi japo sikuwa mkimbizi maana tafsiri ya mkimbizi inajulikana. Hofu na woga huu ndio sababu ya watu kuitaka serikali ya 3 kwa sababu tu CCM wote wanatetea serikali 2. Sababu zao CCM ni tofauti kabisa na mnavyofikiria lakini maadam chale zimewacheza kuona CCM waitaka serikalik 2 basi lazima Upinzani watofautiane, bora kuwaunga mkono kina Jussa na Sultan kuliko kuunga mkono CCM..Ndio hivyo hivyo kuogopa Wazawa wanaoishi nje kuwa watakuja sijui kuiba sijui kipi na kupeleka nje, lakini wepesi wa kuwapokea Wachina, Wahindi na Waarabu na kuwapa Uraia lakini sii Mkerewe miye..

Hizi fikra za vilaza ndizo zinazoturudisha nyuma japo mifano kibao juu ya Diaspora wanavyoweza kulisaidia Taifa. Kwenu ni talaka, talaka talaka hadi zifike 3 kisha mnamlaumu Mungu mnapokuwa na shida ya kuishi na wanawake wengine. Ajizi nyumba ya umaskini.
Muungano ni maridhiano, hatuhitaji kuwa na muungano tukilaumiwa kuwanyonya ndama wasio na viwele. Ni kutudhalilisha. Tume imesema kuna mambo 7 yanayoweza kutuunganisha tena tukiweka nguvu pamoja.

Hatuna sababu za kusikiliza wznz wanataka muundo gani, tunasababu za kueleza kwanini Tanganyika irudi.

Kurudi kwa Tanganyika kutafufua muungano huo uliokufa ambao Mkandara anadhani upo.
Kilichopo ni mazingaombwe. Unakuwaje na muungano ambao Makamu wa Rais wa JMT amebaki kufanya kazi Tanganyika tu. Unakuwaje na muungano, Waziri mkuu wa JMT anahitaji kibali cha kufanya kazi znz

Unakuwaje na muunagano ambao Katiba ya muungano ni chini ya katiba ya SMZ.

Unakuwaje na muungano wenye ma-Amri Jeshi wawili, wa JMT na SMZ

Unakuwaje na muungano ambao Rais wa JMT anamsubiri rais wa SMZ kwenye mkutano

Unakuwaje na muungano ambao Rais wa JMT anabaki ukumbini, wakati rais wa znz akifunga mkutano

Unakuwaje na muungano ambao znz inaweza kwa kujiamulia kuongeza au kutoa jambo katika JMT bila kuuliza wenye serikali na nchi yao, wanaolipia muungano huo?

Muungano gani wakati mmoja anachota mwingine anabeba gharama

Unakuwaje na muungano ambao Rais wa JMT anamwangalia rais wa SMZ akipigiwa mizinga 21

S3 zitapunguza matatizo, na kama yupo anayedhani zitaua muungano kama Mkandara, mtu huyo ajiulize kwani sasa hivi kuna muungano?
 
Mawaziri wote ni kutoka "nchi" nyingine. Hayo ndio JK alimaanisha kwenye hotuba yake kuhusu kutatua kero za Zanzibar.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Hata waziri wa afya tumeajiri raia wa nchi jirani.
Sioni kwanini tusiajiri kutoka malawi, zambaia na Uganda. Kumbuka afya wanayosema imeingizwa kinyemela inaongozwa kinyemela pia na waziri wa nchi jirani.
 
SHEREHA ZA MUUNGANO 26.4.2014
MTAZAMO KUHUSU HOTUBA YA RAIS


RAIS KUWAFINYANGA UKAWA KWA KUPOTOSHA HOJA ZAO
ATASUKUMA AGENDA YA CCM KUELEKEA SERIKALI 2

MAANDAMANO YA KUMUUNGA MKONO YATAFUTA

Sehemu ya I

Wanajamvi
Kwanza tuwaombe radhi kutoka nje ya mada tarajiwa kuhusu UKAWA. Hii ni kutokana na ukubwa na unyeti wa suala zima la katiba linaloendelea.

Kesho ni siku ya muungano ukitimiza miaka 50. Siku za nyuma sherehe hizo ziliadhimishwa bila hotuba ya viongozi. Leo inatarajiwa rais atalihutubia taifa katikati ya mtafaruku wa bunge maalam la katiba (BMLK)

Wajumbe wa UKAWA walitoka nje ya bunge na kuliacha likiwa na CCM.
Ombwe la kuondoka kwao linaonekana kwa mijadala kukosa ladha, heshima au hekima.
Mjadala wa katiba umegeuka kuwa kijiwe cha mipasho.Thamani ya mjadala wa kitaifa imekufa.

Samwel Sitta aliyepewa jukumu la kuhakikisha maoni ya tume ya Warioba yanavurugwa na kuchomekwa rasimu ya CCM naye amekwazika. Ingawa aliingia kwa tambo, kazi ya uenyekiti imempwaya.
Bunge lilikuwa livunjwe , kwa kuogopa aibu hiyo, bunge limeendelea kibubusa busa. Ni kama hakuna.

Sitta alikwenda znz kumpa taarifa Rais wa nchi ya znz kuhusu kinachoendelea bungeni.
Wajumbe wa znz upande wa upinzani ni wengi kiasi kwamba CCM imekosa 2/3.
Mbinu za kupitia kura ya bunge kupata idadi nazo zimekwama.

Ziara ya Sitta ililenga kumshauri Rais Shein afanye utenguzi na uteuzi mpya wa wajumbe wasiotokana na baraza la wawakilishi. Hilo litawezesha kupatikana kwa 2/3 kutoka znz ambayo italeta sura ya muungano.

Kwa muda wa wiki moja UKAWA wamenyimwa nafasi za kufanya mikutano.
Katika mabandiko I-V tumeeleza ni kwanini inafanyika hivyo. Tulionya kuwa kukaa kimya hadi tarehe 26 ni kutoa nafasi ya wao kukaangwa kwa kupotosha hoja zao. Ndicho atakachokifanya JK leo.

Tunakumbuka jinsi JK alivyomshambulia Warioba kwa kuchukua changamoto alizozisema bila kugusia jambo moja jema la S3. Lengo lilikuwa kumfinyanga kwa kupotosha hoja za tume.

Leo JK atarudia mbinu zile zile alizotumia kwa warioba kuwakaanga UKAWA.

Tuangalie mtazamo wa hotuba yake siku ya Leo.

Inaendelea....
 
Sehemu ya II

MTAZAMO NA MWELEKEO WA HOTUBA YA JK

Katika hotuba yake ya leo JK atajaribu sana kutozungumzia mambo ya tume ya Warioba. Anafahamu kuendelea kuwananga wazee hao ni kujishushia hadhi baada ya kukosa kuungwa mkono katika hotuba ya kuzindua bunge.

JK atawasifia sana wazee na tume hiyo ili kuondoa hasira na chuki za wananchi zilizoelekezwa kwake kwa kuwadhalilisha watu aliowatuma.
JK hataongelea maoni ya tume kwani kufanya hivyo ni kufumua vidonda vinavyovuja damu.


JK ataelezea faida za muungano kwa miaka 50 akiwalenga wazanzibar kwa kuonyesha faida wanazozipata na hasara watakayopata. Hatawasema kwa hoja mahususi, ataongelea kwa ujumla wa mambo ya kuoleana, biashara na uchumi. Lengo ni kuwavuta wazanzibar ili 2/3 ipatikane

Pili, ataongelea muungano wa Tanzania kama mfano akiwapamba sana Nyerere na Karume.
Atatumia muda mwingi kueleza yanayowahusu waasisi hao kama kuunganisha TANU na ASP.

Tatu, JK atalifanya suala la muungano kuwa si agenda ya wananchi wanaohitaji mambo mengine. Atazungumzia umuhimu wa katiba na mambo yanayotokana.
Hii ni kujaribu kuonyesha muungano si tatizo, tatizo lipo kwa viongozi na tamaa za madaraka.


Nne, ataonyesha matatizo ya muungano 'kero' na jinsi yalivyoshughulikiwa na kubaki 3.
Hataeleza kiini cha malalamiko, bali kero tu kwa maana ya neno la kuwachanganya wananchi


Tano, ataelezea namna alivyoanzisha mchakato wa kuandika katiba.
Matatizo yaliyojitokeza na jinsi alivyokaa na wapinzani na kukubali hoja zao.
Hata kama hakuzikubali atajenga hoja ya uungwana ili aonekane yeye si tatizo.


Sita, ataeleza nini tume ya Warioba ilichotumwa kwa kuzingatia kulinda muungano.
Atamaanisha muungano uliopo ndio msingi wa mjadiliano na wala si kubadilisha muundo wake. Hii ni kutaka kuwaanisha wananchi wananchi tume imeweka maoni yake na si ya wananchi.


Saba, ataeleza ugumu wa BMLK kuanzia uandikaji wa kanuni na taratibu zilizoamuliwa kwa pamoja kufikia muafaka. Hii ni kuonyesha kuwa UKAWA walikubaliana na taratibu hata kama zimekuwa zinakiukwa.

Nane, atamshambulia sana Tundu Lissu kwa kumuonyesha hana nidhamu ya kutukana waasisi wa muungano. Katika kufanya hivyo suala la hati ya muungano litachukua nafasi kubwa sana.

Tisa, atatumia hati ya muungano kama kielelezo kuwa UKAWA walikuwa na vipingamizi visivyo na msingi na CCM imewakubalia kila jambo.
Ataeleza kuwa UKAWA hawana sababu za maana za kususia bunge la katiba.


Kumi, ataonyesha jinsi ambavyo uongozi wa bunge la Samwel Sitta ulivyo tayari kukaa nao lakini wao hawapo tayari kwa majadiliano.

Kumi na moja, kama kawaida yake atawaomba wajumbe wakae kitako kumaliza tofauti zao.
Hii ni katika ile hulka ya kupendeza pande zote hata kama anauma upande mmoja.

Kumi na mbili, ataonyesha umuhimu wa umoja wa taifa na jinsi ambavyo amani na utulivu vinavyoweza kuondoka akiwanyooshea kidole UKAWA. JK atazungumzia hali mbaya ya matusi na kashfa na kuzionyesha kuwa zinavunja umoja na kuwagawa Watanzania. Hapa atakuwa amelenga kujitenga na kauli ya Lukuvi kwa kuonyesha anachotaka ni umoja na si kuligawana taifa.

Baada ya kuongelea mambo hayo, JK atakuwa amejenga hoja ya namna ya kutengua uteuzi wa wajumbe wasio wabunge wa bunge la JMT kama ilivyopendekezwa na Mwigulu Nchemba.

Lakini pia atachomeka uwezekana wa kanuni kubadilishwa ili isiwe 2/3 kwa msingi kuwa bila hivyo hakuna maridhiano.

Katika kujenga hoja zake vichwani mwa wananchi, safari hii hatatumia mfano wa jeshi. Atatumia wingi wa wabunge wa CCM kama kiashirio cha wananchi walio wengi kutaka katiba mpya iendelee kuandikwa.Na kwa mandate hiyo atahakikisha bunge linaendelea akimaanisha apewe uwezo wa kuteua wajumbe wengine.

UKAWA wana hali gani?

Itaendelea.....
 
Sehemu ya III


UKAWA SASA KUJITETEA


Tahadhari ilitolewa kwa UKAWA kueleza nini wanachosema na kipi kimewatoa bungeni. Mabandiko ya nyuma tumewaeleza kuwa UKAWA hawana rasilimali za kutosha na wala wasitegemee magazeti na radio ambazo zinazounga mkono serikali.

Dunia ya sasa imebadilika, vita haipiganwi tena kwa mishale au mikuki. Hata makombora sasa yanapoteza nguvu. Vita ya sasa ni ya zama za elektroniki na digitali.
UKAWA wameamua kukaa kimya hata kutumia media isiyo rasmi inaonekana wameshindwa.

Hoja inayojengwa ni kuwa kulikuwa na njama za kuleta vurugu ili waonekane wanavunja amani na wala katiba si lengo lao.

Ipo hoja kuwa hawakutaka kuingia katika majibizano kwa kutumia UKAWA isiyojulikana kisheria.

Kwa hali yoyote UKAWA walikuwa na nafasi mbili au zaidi
1. Kutumia mitandao na vyombo vya habari binafasi kuelezea ujumbe wao
2. Kutumia vyama vyao katika haki ya kukusanyika

Kitendo cha wao kukaa kimya kwa muda wote kitatoa nafasi ya hoja zao kupotoshwa.
Baada ya hotuba ya JK mikutano yao itaruhusiwa.
Hapo hawatakuwa na agenda isipokuwa kujitetea. Watakuwa wamevutika na mpira unachezwa katika eneo la goli lao. Badala ya kushambulia watakuwa wanashambuliwa.

Itabidi watumie nguvu nyingi sana katika kuvunja hoja, kujibu hoja na kueleza hoja zao kwa wananchi.Kisaikiolojia UKAWA wajitayarishe has hapo kesho

Na pia, UKAWA waelewe sehemu kubwa ya jamii haiwaelewi na hivyo nafasi waliyokuwa nayo kueleza ni kama wameipoteza.

Kwa mkakati wowote ule waliojiwekea, kitendo cha kuwa mbali na media rasmi na zisizo rasmi haukuwa mkakati mzuri. Time will tell.

CCM KUTUMIA MIKAKATI YA MAANDAMANO

Baada ya hotuba ya JK bungeni iliyopokelewa kwa ubaridi na sehemu kubwa ya jamii, JK na CCM walianza makakati wa kualika wazee waende Ikulu kunywa chai.
Kwanza, walianza wa Muheza, halafu Tanga na kisha Zanzibar.

Mkakati huo hauonekani kuchukua sura iliyokusudiwa hasa baada ya mijadala bungeni.
Misafara ya wazee ilikuwa kuunga mkono S2 bila kuwa na sababu za kuunga au kukataa S3. Ilikuwa misafara ya kufundishwa tu.

Mpango uliopo kwasasa ni kuwatumia vijana kuandaa maandamano ya kuunga mkono S2.
Tayari makundi ya vijana kutoka taasisi mbali mbali yameshanunuliwa na kuanza harakati za makongamano na kutumia vyombo vya habari.

Hotuba ya JK leo itafuatiwa na maandamo katika kumuunga mkono.
Jambo hili linaweza kuwa na athari kubwa kwa UKAW tukizingatie elimu na uwezo wa watu wetu kupambunua mambo.

Sijui ni kwa njia zipi, duru tunasema hivi, UKAWA wana mkakati madhubuti au ni mkusanyiko unaofaa tu na ambao hutengeneza mazingira bila kujali vigezo na nyenzo nyingine?

Tusemezane
 
Nguruvi3,
Mkuu wangu sema wewe huelewi jinsi mfumo wa serikali 2 ulivyoasisiwa na ufahamishwe vizuri laa sivyo unazidi kupotoka. Kama usemavyo ndivyo kwa nini leo Znz wanadai mamlaka kamili? nini maana ya mamlaka kamili wanayodai ikiwa nguvu yote hiyo wanayo tayari?

Sikia bro, Hadi hapa walipo Zanzibar hawana makosa kabisa kuunda serikali ya nchi ya Muungano (Republic) kama inavyotakiwa kuwa leo hii. Tatizo lao kubwa ni kufanya hivyo kinyume cha Katiba ya CCM (unitary system.) ambayo haiitambui Zanzibar kama ni nchi kutokana na mabadiliko yalokwisha fanywa kuelekea serikali 1. Na pia nyie mmeshtuka kwa sababu fikra zenu bado ni za kijamaa kutokana na katiba ilotulea sote na ndio somo pekee mbele ya macho yetu. Tatizo letu ni Katiba hii sio Muungano uliopo..

Soma mara 100 katiba iliyopo bado utakuta mambo mengi sana ktk msahafu huu ni ya Kikomunist ikiwa ni pamoja na hao Ma RC, DC, Halamashauri na kadhalika bado ni kama China, Russia. Usipokuwa mwanachama wa chama tawala ama mlezi, lobbiest, basi hata ujumbe wa nyumba 10 huwezi kuupata. CCM wame control where the money is na kuwaachia vyama vingine Ubunge huku waki control serikali kuu, msajili wa vyama, TISS, sheria maana hata mahakimu wa mahakama kuu wanapitishwa na rais na lazima wawe wanachama wa CCM (japo wewe na mimi hatujui).

Kwa upande mwingine wa sheria na haki za republic ndani ya Muungano ni mamlaka ya nchi kuendesha shughuli za serikali na huwezi kuwa na serikali kama huna nchi. Kama nilivyokwisha kuambia toka zamani, KIla nchi ndani ya Muungano wowote uwe wa kisiasa au federation nchi husika zote wana vitu vitatu acha mbali serikali kuu ya Muungano. Kila nchi ina serikali yake, ina mahakama yake na ina bunge lake. hii nenda USA, Canada, Australia, na kila nchi yenye muungano utakuta haya tena kila nchi ina Bendera yake acha hiyo ya Taifa maana kila nchi iklikuwa HUru kabla ya Muungano. Hivyo Kwa Zanzibar kuwa na vitu hivyo ni kawaida kabisa hasa pale sisi wenyewe (Pinda na Watanganyika) tulipodai kuwa Zanzibar sio nchi.

Napingana na mawazo ya CCM wanaposema Zanzibar sio nchi kwa sababu ya Mapinduzi na kwamba Zanzibar wanayoijua wao ni ile ya siku 22 tu. Basi hiyo hiyo kama wanaikubali ndio Zanzibar huru wakubali pia kuwa Zanzibar ni nchi na rais wake wa kwanza ni Marehemu Abeid Aman Karume akiwa na baraza lake la mawaziri 10.

Hakuna sababu yoyote iloondoa Uhuru wa Zanzibar kama nchi huru ktk Muungano wetu maana unasema wazi tuliungana nchi 2 na Ile ya Tanganyika sio kwamba haipo -Ipo isipokuwa mamlaka ya shughuli za Tanganyika zitasimamiwa na Bunge la Taifa kuepuka mzigo wa matumizi. Hapa huwezi kudai tanganyika haipo ila tumeua tu jina la Tanganyika maana shughuli za Tanganyika zinasimamiwa na serikali kuu, bunge la taifa na Mahakama ya Taifa tupewe nini zaidi?..

Hadi hapa hapakuwa na tatizo isipokuwa kosa kubwa la kwanza ni kuzigawa wizara zetu ktk makundi ya Muungano na yasokuwa ya Muungano badala ya shughuili zote za wizara hizi zisimamiwe na nchi husika. Kwa kufanya hivyo Na maadam serikali kuu inasimamia mambo ya Tanganyika, sisi tukatumia nafasi hiyo na mwanya huo kujinufaisha zaidi. Haya maswala yasokuwa ya Muungano ndio yenye pato kubwa na kama ukusanyaji wa fedha hizo unakwenda serikali kuu, na benki kuu ipo ktk serikali kuu Zanzibar walikuwa kama wako nje ya Muungano.

Hivyo hatua yao ya kuandika katiba mpya ya Zanzibar ni kutokana na serikali kuu kushindwa kuondoa mapungufu ya Katiba yalokuwepo na hasa huu mpango wa mambo ya Muungano na yasokuwa ya Muungano hasa baada ya mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi. Kufikia mwaka 1984 mabadiliko ya Kiuchumi na pia mwaka 1993 mabadiliko ya vyama vingi Zainzibar ilizidi kupoteza nguvu yake Kitaifa. Serikali kuu, bunge la Taifa na mahakama kuu zote zikageuka kuwa chombo cha Tanzania bara (Tanganyika). Katika hali hiyo ndio ubishi ukaanza na Mh. Pinda akafunga bazara kwa kusema Zanzibar sio nchi!

Wewe ulitegemea Zanzibar wafanye nini? kuwa na rais ni jina tu kinachopinwmwa ni mamlaka yake. Rais wa Zanzibar hana mamlaka ktk serikali ya Bara wala ya Muungano ni sawa na Premier wa Ontario au Quebec na kote hukoserikali, mahakama na mabunge yao. Jeshi la Polisi la Ontario halina mamlaka Quebec, Lakini kuna jeshi la Polisi ya Taifa RCMP ambao wana mamlaka Canada nzima. Hii ya kwua na kiongozi fulani kwa jina la Rais isikutishe ni title tu unaweza kumwita waziri mkuu au Premier wa Zanzibar maana unatazama kwanza mamlaka alokuwa nayo.

Ukinambia unaipinga katiba ya Zanzibar kwa sababu ilitokana na muafaka baibna ya CCM na CUF pasipo ridhaa ya wananchi hapoo nitakubaliana nawe. Ukinambia katiba ya Zanzibar inapingana na katiba ya JMT hapo nitashtuka kwa sababu ni Katiba hiyo hiyo hata sisi tunataka kuibadilisha pasipo ridhaa ya wananchi maana sijui kama tulifanya referendum kuhusiana na madai ya Katiba mpya.

Hivyo tusiwalalumu wao kwani CCM wanayajua fika yolotokea na kwa nini Zanzibar wameandika katiba Mpya na nina hakika JK na viongozi wa CCM waliipitisha kwanza. Hii ni kutokana na kwamba bado CCM imeshika hatamu na serikali yetu kuu ipo ktk mfumo wa UJIMA. Haijalishi hata kidogo kama tutakuwa na serikali 1, 2 au 3 kama tutaendelea kuwa na akili hii ya kuwaachia CCM waandike Katiba mpya basi UJIMA utaendelea kuwepo na mabadiliko hayatakuja leo wala kesho.

Nyie sumbukeni na huo Muungano lakini CCM wanajua wanachokifanya. Hofu yao kubwa ni CUF ktk debate nzima ya bunge la Katiba kwa sababu CUF wakichukua Zanzibar basi ndio utakuwa mwanzo wa CCM kuanguka na CUF wamejipanga yaani waloalikwa walikuwa na wazo moja kama CCM. Chadema na wajumbe wengine wa Taasisi wameitwa na kujikuta ni wao tu wapo pale kama wao. Hivyo Chadema hawajui wanacheza na moto ambao kina Jussa wanaukoleza. Ebu tujiulize ni viongozi wangapi wa CUF wanaamini kuwa Mapinduzi ya mwaka 1964 yalikuwa halali na wapo tayari kujmuenzi Mh. Karume! Ukiwapata 10, nitakubali serikali 3.
 
Mkandara: Kwa upande mwingine wa sheria na haki za republic ndani ya Muungano ni mamlaka ya nchi kuendesha shughuli za serikali na huwezi kuwa na serikali kama huna nchi. Kama nilivyokwisha kuambia toka zamani, KIla nchi ndani ya Muungano wowote uwe wa kisiasa au federation nchi husika zote wana vitu vitatu acha mbali serikali kuu ya Muungano. Kila nchi ina serikali yake, ina mahakama yake na ina bunge lake. hii nenda USA, Canada, Australia, na kila nchi yenye muungano utakuta haya tena kila nchi ina Bendera yake acha hiyo ya Taifa maana kila nchi iklikuwa HUru kabla ya Muungano
Alaa kuuumbe! sasa bendera, na serikali ya Tanganyika ipo wapi?

Kumbuka Ontario wanavyo halafu wana mambo ya federation. Sasa tuambie sisi, kwavile unakubali kila nchi ilikuwa huru na ina haki ya mambo hayo, vipi, serikali ya Tanganyika ipo wapi?
Hebu nionyeshe mfano mmoja wa huko majuu unaolingana na muundo wetu.
 
Mkandara: Na kinachonifanya nipingane na Warioba zaidi ni kwamba yeye kapewa kazi ya kuratibu Katiba MPYA hivyo malengo ni kukusanya mawazo ya wananchi kuhusiana na katiba ya nchi ilokuwa na mapungufu ktk mahitaji ya wananchi.

Sasa yeye na kamati yake badala ya kutafuta utunzi wa Katiba wametuingia choo cha kike kuanza kujadili Muungano wetu.
Then
Mkandara: Ukinambia unaipinga katiba ya Zanzibar kwa sababu ilitokana na muafaka baibna ya CCM na CUF pasipo ridhaa ya wananchi hapoo nitakubaliana nawe. Ukinambia katiba ya Zanzibar inapingana na katiba ya JMT hapo nitashtuka kwa sababu ni Katiba hiyo hiyo hata sisi tunataka kuibadilisha pasipo ridhaa ya wananchi maana sijui kama tulifanya referendum kuhusiana na madai ya Katiba mpya
Mkandara, muombe radhi Yericko Nyerere kwa alichokisema hapo nyuma.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3,

Kuna mtu huku "saiti" tukiwa kijiwe cha kahawa na kashata amejenga hoja kwamba pengine ukimya wa UKAWA ulilenga kuacha kwanza Rais Kikwete azungumze anachotaka kuzungumza kabla na wao hawajaanza kujibu mapigo. Nini mtazamo wako juu ya hili.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom