UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

Mkuu Nguruvi3,

Kuna mtu huku "saiti" tukiwa kijiwe cha kahawa na kashata amejenga hoja kwamba pengine ukimya wa UKAWA ulilenga kuacha kwanza Rais Kikwete azungumze anachotaka kuzungumza kabla na wao hawajaanza kujibu mapigo. Nini mtazamo wako juu ya hili.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3,

Kuna mtu huku "saiti" tukiwa kijiwe cha kahawa na kashata amejenga hoja kwamba pengine ukimya wa UKAWA ulilenga kuacha kwanza Rais Kikwete azungumze anachotaka kuzungumza kabla na wao hawajaanza kujibu mapigo. Nini mtazamo wako juu ya hili.
Mkuu nadhani kuwa mkakati huo wa UKAWA kama upo utakuwa na mapungufu zaidi.
Walipotoka bungeni walikuwa na momentum ya kuendelea mbele wananchi wakiwasubiri kusikia kilichotokea na kwanini wamechukua hatu hiyo.

Tunafahamu wazi kuwa vyombo vya serikali kama Polisi na media kama habari leo, daily news n.k. haviwezi kuandika habari za watu wa ukawa na hupokea maelekezo ya serikali. Unaona jinsi ambavyo TBC inayoendeshwa kwa kodi inavyotumiwa na CCM na serikali kuwafinyanga wapinzani. Hivi kweli mvua zinaweza kukata matangazo tena wakati mtu fulani anahutubia halafu akimaliza mawasiliano yarudi!

Nilichotegemea ni UKAWA kupitia vyama vyao kuanza kupambana na mazingira hayo kwa kutumia njia za kisasa. Kuna social media, mitandao n.k. Walipaswa kwanza kuanza kupenyeza habari zao ili zivume masikioni kabla ya kukutana na wananchi.

Leo CCM wametangaza timu ya upotoshaji. Unaweza kuona akina Makonda walivyoandika mambo ya jabu na ya kupotosha sana. Hawa ndio wameanza kazi ya upotoshaji.

Hii maana yake UKAWA watakuwa katika mazingira ya kujitetea kwanza halafu kujenga hoja. Hapo watakuwa wameshajiwekea kikwazo.

Kwa kutambua kuwa UKAWA wamezembea CCM wamechukua agenda ya Lukuvi ili waishughulikie kichama.
Ukweli ni kuwa hakuna uchama wa aina yoyote bali ni kujionyesha kuwa CCM inajali na ipo tayari kuchukua hatua.

Hii ya Lukuvi ilikuwa ni agenda nzuri ya kuonyesha aina ya mchakato tulio nao. Nadhani wana hoja za msingi, lakini hoja hizo ni vema zikasimama na vithibitisho. Kwa mfano, hoja ya JK na serikali yake kutisha watu ilikuwa ni suala la kuonyesha jinsi mbinu chafu zilivyoanza kutumika.

UKAWA walikuwa na nafasi nzuri ya kueleza mchakato hadi tume ya Warioba na jinsi ilivyodhalilishwa.
Haya ni mambo yaliyokuwa moto sana ambayo hayakuhitaji nafasi.

Kwasasa bunge la CCM limeahirishwa na makada wao watakuwa mitaani wakipambana na UKAWA. Wana resource za kutosha na vyombo vya umma. Hilo nalo litakuwa na ugumu kwa UKAWA ambao ukiutazama vizuri bado haujajipanga vilivyo.
 
Ni dhahiri kwamba mchakato wa katiba umekwama. Tutafika uchaguzi mkuu ujao bila ya katiba mpya. Huu ni msiba mkubwa sana kwa CCM, lakini kutokana na UKAWA kukosa umakini, msiba huu unaweza kuwa mkubwa kwa upinzani badala ya ccm. Nguruvi3 alijadili hili vyema sana. Tunabaki jiuliza - nini kinaendelea ndani ya UKAWA????

Upinzani una karata kubwa sana ya kutumia kisiasa iwapo uchaguzi ujao utakuja bila ya katiba au na katiba ya ki-ccm. Hoja za upinzani ni rahisi na za wazi:

*Wangepita mijini na vijijini kuwaambia wananchi kwamba mmetaka katiba mpya lakini CCM wamewakatalia kwa kutumia wingi wao bungeni.
*CCM na makada wake hawapo tayari kuheshimu maoni ya raia.

Upinzani ulitakiwa watumie ripoti ya tume na kusema yale ndio maoni ya wananchi.

Baada ya hapo, upinzani ungewaomba wananchi kura kwa ahadi kwamba wakipata madaraka, watatekeleza maoni yao bila ya hila wala ghiriba.

Upinzani ukifanya kazi nzuri, sioni jinsi gani ubabe wa ccm utaendelea kwa muda. Wananchi wengi sasa hawapo tayari kuendelea kuwa chini ya katiba isiyowatendea haki na ambayo ina halalisha ukandamizaji wa wananchi kwa wazi kabisa.

Upinzani ulitakiwa uwe busy kuwahakikishia wafanyakazi serikalini kupata mafao ya kwa wakati muafaka;

Ahidi wananchi usimamizi mzuri wa rasilimali zao na kodi zao;

Kuboresha huduma zote za kijamii, hasa kulenga watoto, kina mama, na vijana.

Kutoa ujira wa haki na kwa mujibu wa sheria, sio kwa fadhila, au huruma ya watawala.

Upinzani ungekuwa busy kuelezea ufisadi ulivyo kithiri serikalini na jinsi gani serikali mbili zinavyofanikisha hili - EPA, Radar, mabilioni ya uswisi. Hapa wangetaja jina moja hadi jingine la mamilionea wa uswisi kwa mgongo wa walala hoi. Wangetaja wenye akaunti, wadhamini wanavyoonekana kwenye nyaraka za benki, nafasi yake kwenye uongozi, hata kama ni mstaafu etc etc.

Upinzani ungemwaga hadharani nyaraka za fedha zilizoibiwa na kupelekwa nje ya nchi. Mali za viongozi dubai, london, capetown etc. Wangeonyesha mali na fedha hizi zimetokana na miradi gani ya fedha za umma. Wangeonyesha taifa limepata hasara kiasi gani kwa kurudhia mikataba ya kinyonyaji.

Yote haya yange set tone ya haja ya katiba mpya, lakini pia madudu ambayo upinzani utaenda kuyafanyia kazi "kimfumo", huku upinzani ukiahidi kuandaa tume itakayopita nchi nzima kutafuta maoni ya wananchi juu ya Dira mpya ya taifa iweke vipaumbele gani. Dira ikipatikana, iwe implemented in 3 years. Na kazi za serikali zipimwe kwa utekelezaji wa dira hiyo. Hapo tutakuwa tumepata taifa jipya lenye kufufua matumaini ya wali wengi.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Alaa kuuumbe! sasa bendera, na serikali ya Tanganyika ipo wapi?

Kumbuka Ontario wanavyo halafu wana mambo ya federation. Sasa tuambie sisi, kwavile unakubali kila nchi ilikuwa huru na ina haki ya mambo hayo, vipi, serikali ya Tanganyika ipo wapi?
Hebu nionyeshe mfano mmoja wa huko majuu unaolingana na muundo wetu.
Nguruvi3, serikaili ya tanganyika ndio serikali kuu na ndio maana wanasema tumevaa koti la Muungano. Kama hujui undani wa maneno hayo inabidi urudi nyuma kwanza kabla ya kuendeleza malumbano.

Ikiwa mambo yote ya Tanganyika yanashughulikiwa na serikali kuu wewe unaitafuta Tanganyika yenye bendera yake ya nini, ili iweje? Hivi unaweza nambia ni serikali gani ilopinga OIC kwa Znz kama sio serikali ya Tanganyika? Walokataa mahakama ya kadhi ni kina nani kama sio serikali ya tanganyika?..Hiyo bendera itabadilisha kipi ktk kero ama mapungufu ya Katiba iliyopo.

Nimeshasema wazi kuwa ikiwa kila waziri ktk serikali kuu una mamlaka ya shughuli za Tanganyika huoni kama hapa tumevaa koti la muungano. Abrahaman Babu katuletea reli ya Tazara leo hii sii mali ya Muungano ila Tanganyika kwa sababu ya hayo mambo yasokuwa ya muungano - huoni kama hapa tunatumia jina la Muungano kutufaidhisha bara lakini Znz wanapotaka mambo yao inabidi kwanza yapitishwe na serikali kuu.

Uliona wapi mfumo wa kidemokrasi ambao shughuli za serikali bado mamlaka yake yanatoka serikali kuu. RC hana nguvu isipokuwa kwa rais, Meya wa jiji hana mamlaka isipokuwa kupitia RC wa rais, waziri pia ni mbunge mwanasiasa sii lazima awe na uwezo wa kuongoza. Haya ndio maswala ya kuzungumzia sio muungano hata kidogo.

Pwenye demokrasia, mamlaka ya kuendesha shughuli zote za serikali hupewa vyombo vilivyoundwa kwa ushiri9kiano na serikali kuu sio hii habari ya serikali 2 au 3. Kama Mfumo utaendelea kuwa kama ulivyo haijalishi kama tutakuwa na serikali 3 au Muungano maana bado CCM watajkuwa na mamlaka yote yanayotakiwa wao kuendeleza mfumo wa ujima. Tutakuwa kama China japo wanaendelea lakini ni asilimi 1 tu ndio wanatajirika wakiwaacha mabillioni ya wananchi ktk umaskini wa kutupwa.

Leo hii China inaongoza kwa umalaya na kusafirisha nje Malaya, bwimbwi linauzwa kama njugu tena kwa bei kubwa kuliko Ulaya, Cocaine na Opium inatajirisha cartekl za kichina kiasi kwamba watu hawaendi tena Thailand kutafuta dogo. Lakini hutamkuta mtoto wa kiongozi wa China akiteseka wote wanaspoma Ulaya na Marekani ni matajiri wa kutupwa na kwetu dalili zinaanza kujitokeza kutokana na nguvu ya chama tawala.

Hapa ndipo tunapotakiwa kujikita, hakuna sababu ya kubishana na kupishana na CCM kwaa kila jambo kwa sababu tu hatuwaamini ama sisi ni wapinzani. Tutachekesha kesho kama kweli tutaendelea na Ubishi huu.
 
Nguruvi3, serikaili ya tanganyika ndio serikali kuu na ndio maana wanasema tumevaa koti la Muungano. Kama hujui undani wa maneno hayo inabidi urudi nyuma kwanza kabla ya kuendeleza malumbano.

Ikiwa mambo yote ya Tanganyika yanashughulikiwa na serikali kuu wewe unaitafuta Tanganyika yenye bendera yake ya nini, ili iweje? Hivi unaweza nambia ni serikali gani ilopinga OIC kwa Znz kama sio serikali ya Tanganyika? Walokataa mahakama ya kadhi ni kina nani kama sio serikali ya tanganyika?..Hiyo bendera itabadilisha kipi ktk kero ama mapungufu ya Katiba iliyopo.

Nimeshasema wazi kuwa ikiwa kila waziri ktk serikali kuu una mamlaka ya shughuli za Tanganyika huoni kama hapa tumevaa koti la muungano. Abrahaman Babu katuletea reli ya Tazara leo hii sii mali ya Muungano ila Tanganyika kwa sababu ya hayo mambo yasokuwa ya muungano - huoni kama hapa tunatumia jina la Muungano kutufaidhisha bara lakini Znz wanapotaka mambo yao inabidi kwanza yapitishwe na serikali kuu.

Uliona wapi mfumo wa kidemokrasi ambao shughuli za serikali bado mamlaka yake yanatoka serikali kuu. RC hana nguvu isipokuwa kwa rais, Meya wa jiji hana mamlaka isipokuwa kupitia RC wa rais, waziri pia ni mbunge mwanasiasa sii lazima awe na uwezo wa kuongoza. Haya ndio maswala ya kuzungumzia sio muungano hata kidogo.

Pwenye demokrasia, mamlaka ya kuendesha shughuli zote za serikali hupewa vyombo vilivyoundwa kwa ushiri9kiano na serikali kuu sio hii habari ya serikali 2 au 3. Kama Mfumo utaendelea kuwa kama ulivyo haijalishi kama tutakuwa na serikali 3 au Muungano maana bado CCM watajkuwa na mamlaka yote yanayotakiwa wao kuendeleza mfumo wa ujima. Tutakuwa kama China japo wanaendelea lakini ni asilimi 1 tu ndio wanatajirika wakiwaacha mabillioni ya wananchi ktk umaskini wa kutupwa.

Leo hii China inaongoza kwa umalaya na kusafirisha nje Malaya, bwimbwi linauzwa kama njugu tena kwa bei kubwa kuliko Ulaya, Cocaine na Opium inatajirisha cartekl za kichina kiasi kwamba watu hawaendi tena Thailand kutafuta dogo. Lakini hutamkuta mtoto wa kiongozi wa China akiteseka wote wanaspoma Ulaya na Marekani ni matajiri wa kutupwa na kwetu dalili zinaanza kujitokeza kutokana na nguvu ya chama tawala.

Hapa ndipo tunapotakiwa kujikita, hakuna sababu ya kubishana na kupishana na CCM kwaa kila jambo kwa sababu tu hatuwaamini ama sisi ni wapinzani. Tutachekesha kesho kama kweli tutaendelea na Ubishi huu.
Ok, sasa niambie kwa kutumia S2 tunawezaje kufanya mambo na kuondoa dhana ya kuvaa koti la muungano?
Hapa ndipo hutaki kutueleza. Tufafanulie wewe na CCM mnataka S2, tuna solve vipi problem hamtuelezi.
Nafasi hii ni ya swali moja, JMT na SMZ zitafanyaje kazi ili kutenganisha mambo ya muungano na yasiyo ya muungano kuondoa dhana ya kuvaa koti la muungano?
 
Ok, sasa niambie kwa kutumia S2 tunawezaje kufanya mambo na kuondoa dhana ya kuvaa koti la muungano?
Hapa ndipo hutaki kutueleza. Tufafanulie wewe na CCM mnataka S2, tuna solve vipi problem hamtuelezi.
Nafasi hii ni ya swali moja, JMT na SMZ zitafanyaje kazi ili kutenganisha mambo ya muungano na yasiyo ya muungano kuondoa dhana ya kuvaa koti la muungano?
Swadakta! hujawahi kuniuliza swali hili na japo majibu yangu yamo ktk maandishi yangu mengi tu.

Mkuu wa sasa hivi sisi wananchi tunaitaka KATIBA MPYA tu, katiba ambayo itaondoa nguvu ya chama kimoja kuwa tawala wa kila kitu, nguvu ya kundoa mamlaka ya shughuli za serikali kuwa chini ya serikali kuu kiasi kwamba vyama vya kisiasa vinaposhinda uchaguzi viwe na mamlaka ya kuongoza shughuli hizo ktk sehemu zao badala ya kukinga bakuli kuiomba serikali ya CCM. Yanayotokea Dodoma leo ni ushahidi tosha wa jinsi gani CCM ina nguvu kubwa juu ya maamuzi yoyote na nguvu hiyo huwezi kuiondoa kwa kuwa na serikai 3.

Tunataka mabadiliko makubwa ktk uendeshaj wa shughuli za serikali, kiasi kwamba Halmashauri za miji ziwe na jukumu kubwa la ujenzi wa wilaya, miji, majimbo na kadhalika. Mkuu wa mkoa (gavana) achaguliwe na wananchi, Mawaziri wasiwe wabunge hii ni ktk kuondoa ushindani wa fedha na takrima ambazo zimetumiwa sana na nchi za Kikomunist. Accountability kwa mawaziri waloteuliwa na chama kilichoshinda kupewa dhamana hiyo na hivyo kuanziosha ushindani wa vyama ktk ujenzi wa Taifa

Kuhusiana na swala la S2, nimesema wazi kwamba sioni sababu ya kuwa na serikali 3 kwa sababu lengu la muungano wetu ulikuwa ufikia S1. Hivyo kama kero kubwa ya Wazanzibar ni Tanganyika kulivaa koti la Muungano basi tulivue na sii lazima tuvue nguo zote. Tulivue koti kuelewa koti hilo sii mzigo ila mzigo kwetu ni lawama zenye logic kuvaa koti wakati wa jua kali kuombea wafadhili watutowe!

1. Kwanza tutambue na kukubali kwamba Zanzibar ni NCHI kwa sababu Znz ina sii tu serikali yake, bali ina mahakama yake na bunge lake. Mihimili hii mitatu ndio nguzo thabiti za utawala wowote wa NCHI. Hivyo ni makosa makubwa kusema Zanzibar sio nchi ati tuna serikali 2 ktk nchi 1, huu ni Uongo na unafiki maana hatusemi Znz sio tu wana serikali yao, wanazo pia Mahakama na bunge lao. Sisi tuna nchi 2 zilizoungana kuunda TAIFA MOJA. Hutawasikia kina Warioba wakitamka hili neno TAIFA japo watasema tunao wimbo wa TAIFA na Bendera ya TAIFA. Huwezi kusema bendera yetu kuwa ni bendera ya NCHI ama tuna wimbo wa NCHI (Tanzania). Tanganyika ipo na ndio serikali kuu kwa sababu tunatumia bado katiba ile ya CCM iloboreshwa kuondoa matumizi makubwa ya serikali.

2. Kutokana na mageuuzi ya Kiuchumi (soko Huria) na kisiasa (vyama vingi, Katiba iliyopo imepitwa na wakati hasa ktk kuuboresha muungano. Hii habari ya Mambo yasokuwa ya Muungano kuwa ndio shughuli za serikali ni makosa kuendelea kutumiwa leo hii kutokana na hali halisi ya leo. Kwa maana ya kwamba hakuna Mambo yasokuwa ya Muungano ktk Taifa lolote unless tunabaguana.

Mambo yote ni ya Muungano isipokuwa shughuli zake ndizo huwa za serikali, hivyo ndio kusema wizara ya ELIMU inatakiwa kuwa ni uya Muunngano isipokuwa uendeshaji wa shughuli za elimu ndipo tunapotofautisha kati ya Zanzibar na Bara. Mamlaka hayo watapewa serikali za Zanzibar na serikali ya Bara kama ilivyo. Mwafunzi anaweza kwenda popote kusoma pasipo kubaguliwa yoka darasa la kwanza hadi chuo kikuu. Kilimo na wizara zote ziwe chini ya serikali kuu ambayo itafaidika kwa asilimia 60 ya pato toka pande hizi mbili.

Kama tumeweza kujua mchango wa tanganyika ktk mfuko wa Taifa leo hii ndani ya serikali 2 binafsi sioni saabu ya kuunda serikali ya 3 ili tujue lile lile linalojulikana leo maana gharama za uendeshaji serikali hutokana na kodi za wananchi. Kodi akilipa Bakhresa akiwa Dar inahesabika ni makusanyo ya Bara haihitajiki kuweka jina tanganyika kutambua kodi ya Bakhresa imetoka wapi. Hii ni hawa kwa uwekezaji wa nje maada makao makuu ya Azam yapo bara basi kodi yake inakusanywa na itaendelea kukusanywa Bara ndani ya serikali zozote.

3. Kulivua koti hili la Muungano ni pale sisi bara tutakapo weza kutambua kwamba Zanzibar ni sehemu ya Tanzania. Wana mchango mkubwa sana ktk Taifa hili kulingana na location ya visiwa hivyo. Tusiutazame mchango wa Zanzibar kwa kupima fedha ama bendera ama katiba yao bali tunawezaje kuitumia Zanzibar kuboresha GDP ya Taifa zima. Kwa mfano tukijenga bandari kubwa Zanzibar na kuifanya freeport (sii sales Tax), Kujenga soko kuu la kilimo, spices, matunda na nyama kwa ajili ya export kuvuta nchi za asia na Ulaya kutoka na freepot hivyo imports na exports zitalenga kupitia Znz.

4. Tutalivua koti kwa kuhakikisha kila mikopo, misaada na grants zinayochukuliwa nje kwa ajili ya ujenzi wa Tanzania iwe Bara au visiwani inafaidisha Taifa zima kwa ile asilimia 60 wanayochukua serikali kuu. Kwa maana hiyo kama Dhahabu ya Geita au reli ya kati, Tazara inachagia mfuko wa Taifa basi mfuko huo ni wetu sote.Na kama Karafuu ya Zanzibar inauzwa nje, basi wajue asilimia 60 ya kodi ama ushuru wake inakwenda moja kwa moja ktk mfuko wa Taifa wao watabakia na asilimia 40 ya makusanyo ya kodi. Ugonvi mkubwa baina yetu na Znz umetokana na hili, haya nimesoma kuwa JK kapata mkopo mkubwa toka IMF kuboresha reli ya kati kwa jina la Tanzania, sasa tujiulize iweje pato la reli hiyo halitakuwa la muungano hata kwa asilimia 1 kwa sababu tu ati sii mambo ya muungano?. Kwa nini isiwe shughuli za uendeshaji wa reli hiyo ndio uwe ni mamlaka ya bara, lakini kitakacho ingizwa 40% ya bara na 60% ya Muungano huko tuna kisu kingine.

Kwa haya machache kati ya mengi Kero hazitakuwepo..


.
 
Mkuu Mkandara nimekusoma hapo juu na nakuhakikishia hujajibu swali na sijui kama kuna msomaji amekuelewa.

Nitarudi kufafanua, isipokuwa ukweli unabaki kuwa hujajibu swali la jinsi tunavyojivua koti.
Nikupe dondoo, 2/3 ya bajeti ya znz inatoka Tanganyika, wewe unaamini kujenga bandari ndilo suluhissho.
Hiyo sales tax kwasasa haitoki znz wewe unaamini itatoka tukiendelea na muundo huu.
Hujagusia kuwa ile ni nchi (katiba 2010) wewe unaamini ni Watanzania. Nani kakwambia wznz wanahitaji Utanzania? Wangekuwa wanahitaji utanzania wasingekuona wewe kama kicheche. Hivi unawajua au unawasikia.

Nitarudi, ninachokuhakikisha umeandika lakini hakuna jibu, hukujibu kabisa just beating around the bush.
Mkandara walk the talk
 
Mkuu Mkandara nimekusoma hapo juu na nakuhakikishia hujajibu swali na sijui kama kuna msomaji amekuelewa.

Nitarudi kufafanua, isipokuwa ukweli unabaki kuwa hujajibu swali la jinsi tunavyojivua koti.
Nikupe dondoo, 2/3 ya bajeti ya znz inatoka Tanganyika, wewe unaamini kujenga bandari ndilo suluhissho.
Hiyo sales tax kwasasa haitoki znz wewe unaamini itatoka tukiendelea na muundo huu.
Hujagusia kuwa ile ni nchi (katiba 2010) wewe unaamini ni Watanzania. Nani kakwambia wznz wanahitaji Utanzania? Wangekuwa wanahitaji utanzania wasingekuona wewe kama kicheche. Hivi unawajua au unawasikia.

Nitarudi, ninachokuhakikisha umeandika lakini hakuna jibu, hukujibu kabisa just beating around the bush.
Mkandara walk the talk
Mkuu wewe unataka majibu gani kama sii yale unayotaka kuyasikia. Unauliza swali wakti majibu unayo ama unataka kufahamishwa?..
Sasa ikiwa leo sales tax haitoki Znz kuchangia mfuko wa Taifa, unataka kusema maadam hakuna mchango huo ktk serikali 2, basi hawawezi kulipa tena hata kama Katiba mpya inasema wanatakiwa ila kwa mserikali 3.

Pili, Unaposema Znz asilimia 2/3 ya bajeti yake inatoka Bara hiyo bara wewe umeipata wapi ikiwa wewe unaidai Tanganyika ambayo haipo?

Wewe umetaka kujua bara tutaweza vipi kulivua koti la Muungano na nimekueleza kwa kirefu na yote yana maana kwa undani wake. Unapojenga Bandari Znz kwa fedha ya Jamhuri inaondoa koti kwa sababu itakuwa kwa mara ya kwanza serikali ya Jamhuri imejenga miundombinu Znz. Na kama umefuatilia ilani ya JK ktk kuadhimisha sikukuu ya Muungano kawaahid Znz kuwajengea miradi mikubwa ambayo hadi sasa kelele nyingi zimeondoka. Wazanzibar wengi wamerudi ktk kuikubali serikali 2 na sii kama ilivyokuwa awali.

Kuhusu Bajeti, nachoweza sema mimi pato lolote lililopo ktk mfuko wa Taifa ni pato letu sote bara na visiwani hivyo mipango yoyote ya maendeleo ktk mfuko huo lazima uzihusishe nchi mbili na sii kugawana madaraka ya Urais na Umakamu. Wananchi wanataka kuona maendeleo na sii Hamad kapewa cheo gani ama Znz imekuwa na bendera gani..

Hivyo hata kama 2/3 ya bajeti ya Znz Inatoka bara (Serikali ya Muungano), ndivyo hata serikali za Marekani, Canada na Uingereza hutegemea fedha toka mfuko wa Muungano (serikali kuu) kuendesha shughuli za nchi zao. Mfano:- State ya New York (Nchi) hutegemea fedha za Federal Government kukamilisha bajeti yao ya kila mwaka. . Tazama Ontario yetu Federal budget 2014: Ottawa turning its back on Ontario, Wynne says | National Post Hakuna dhambi.

Wazanzibar nimeishi nao na naishi nao hawana tofauti na Watanzania wengine tena naweza sema sisi Watanganyika tuna roho mbaya zaidi yao. Wao wanashirikiana sana lakini sisi kama mifisi kazi yetu ni kuviziana. Leo Chadema na CCM ni maadui wakubwa na sidhani kama wanaweza kaa meza moja.

Leo hii wewe Nguruvi3 mambo yakikuchanganyikia tu utawaona wakipanga msitari na mabakuli yao lakini ziondoke hutamuona hata ndugu yako. Shida shida yako.. Hii habari ya matusi na kadhalika sisi wenyewe tunatukanana kama jambo la kawaida kabisa. Dharau ya makabila ipo hadi keshio. Wahindi na Waarabu wote wanatudharau lakini kina nani wanaoheshimmiwa bara kama sii Wahindi na Waarabu tena wa Bara.

Katiba yao ya mwaka 2010 ni maridjhiano baina ya CCM na CUF kabla ya uchaguzi wa mwaka huo na maridhiano hayo yalivunja uhusiano baina ya CUF na Chadema. Ni mchezo wa kisiasa ambao CUF waliingizwa Mkenmge na CCM. Nguvu hii ya CCM kuweza kutoa mamlaka makubwa kwa Znz pasipo kupitia bunge la Taifa, pasipo ridhaa ya wananchi ndi nguvu tunayiotakiwa kuiondoa. Ni katiba mpya tu inayoweza kuidhoofisha CCM kt mamlaka yake sii serikali 2 ama 3.
 
Last edited by a moderator:
Mkandara;9388985]Kuhusiana na swala la S2, nimesema wazi kwamba sioni sababu ya kuwa na serikali 3 kwa sababu lengu la muungano wetu ulikuwa ufikia S1. Hivyo kama kero kubwa ya Wazanzibar ni Tanganyika kulivaa koti la Muungano basi tulivue na sii lazima tuvue nguo zote. Tulivue koti kuelewa koti hilo sii mzigo ila mzigo kwetu ni lawama zenye logic kuvaa koti wakati wa jua kali kuombea wafadhili watutowe!
Mkandara amegeuka, hapo nyuma amesema anakubali serikali 3, wiki moja baadaye anasema hataki S3.(Rekodi ipo jf ikihitajika)

Kero unazozungumzia ni wznz, vipi Watanganyika hawana?
Kubaguliwa si kero. Waziri mkuu kuomba kibali cha kazi znz na kibali cha kuishi si kero?

Mtanganyika kuchomwa moto ili aondoe biashara zake znz si kero?
Mwanafunzi wa Tanganyika kunyimwa mkopo znz si kero?

Mtanganyika kunyimwa ardhi, na znz kutoa ardhi kwa watu wa mombasa, Oman na wataliano si kero? Watanganyika kunyimwa ardhi znz si kero?
Katiba ya muungano ambayo ni ya Tanganyika kwa mujibu wako au serikali ya bara kama unavyosema ni chini ya katiba ya nchi jirani ya znz, hiyo si kero

Tumekuuliza tunavua vipi koti umezunguka hukusema kitu kikaeleweka. Huwezi kuvua koti kwa kuacha kujenga bandari Mtwara ili ijengwe nchi ya jirani. Kwanini tusiache Kenya wakajenga tudhani znz ni muhimu sana. Biashara kati ya Kenya na Tanganyika ni kubwa mara 1000 ya biashara kati ya Tanganyika na znz.
 
Mkandara Kwanza tutambue na kukubali kwamba Zanzibar ni NCHI kwa sababu Znz ina sii tu serikali yake, bali ina mahakama yake na bunge lake. Mihimili hii mitatu ndio nguzo thabiti za utawala wowote wa NCHI. Hivyo ni makosa makubwa kusema Zanzibar sio nchi ati tuna serikali 2 ktk nchi 1, huu ni Uongo na unafiki maana hatusemi Znz sio tu wana serikali yao, wanazo pia Mahakama na bunge lao. Sisi tuna nchi 2 zilizoungana kuunda TAIFA MOJA. Hutawasikia kina Warioba wakitamka hili neno TAIFA japo watasema tunao wimbo wa TAIFA na Bendera ya TAIFA. Huwezi kusema bendera yetu kuwa ni bendera ya NCHI ama tuna wimbo wa NCHI (Tanzania)[/QUOTE Mkandara kasome tena taarifa ya Warioba. Tume imezungumzia vizuri sana kuhusu utaifa na hatari iliyopo.
Kasome taarifa msimwekee maneno na CCM wenzenu mzee wa watu. Taarifa hujaisoma
 
Last edited by a moderator:
Mkandara: Kwanza tutambue na kukubali kwamba Zanzibar ni NCHI kwa sababu Znz ina sii tu serikali yake, bali ina mahakama yake na bunge lake. Mihimili hii mitatu ndio nguzo thabiti za utawala wowote wa NCHI. Hivyo ni makosa makubwa kusema Zanzibar sio nchi ati tuna serikali 2 ktk nchi 1, huu ni Uongo na unafiki maana hatusemi Znz sio tu wana serikali yao, wanazo pia Mahakama na bunge lao. Sisi tuna nchi 2 zilizoungana kuunda TAIFA MOJA. Hutawasikia kina Warioba wakitamka hili neno TAIFA japo watasema tunao wimbo wa TAIFA na Bendera ya TAIFA. Huwezi kusema bendera yetu kuwa ni bendera ya NCHI ama tuna wimbo wa NCHI (Tanzania)
Mkandara kasome tena taarifa ya Warioba. Tume imezungumzia vizuri sana kuhusu utaifa na hatari iliyopo. Kasome taarifa m
simwekee maneno na CCM wenzenu mzee wa watu. Taarifa hujaisoma
 
Mkandara: Tanganyika ipo na ndio serikali kuu kwa sababu tunatumia bado katiba ile ya CCM iloboreshwa kuondoa matumizi makubwa ya serikali.

2. Kutokana na mageuuzi ya Kiuchumi (soko Huria) na kisiasa (vyama vingi, Katiba iliyopo imepitwa na wakati hasa ktk kuuboresha muungano. Hii habari ya Mambo yasokuwa ya Muungano kuwa ndio shughuli za serikali ni makosa kuendelea kutumiwa leo hii kutokana na hali halisi ya leo. Kwa maana ya kwamba hakuna Mambo yasokuwa ya Muungano ktk Taifa lolote unless tunabaguana
.Mkuu tena anasahau alituambia kuwa Tanganyika ilikufa na kuwa Tanzania (Rekodi ipo JF ikihitajika tutaitoa)

Leo anasema Tanganyika ipo ndiyo serikali kuu. Sasa JMT ni kitu gani mkuu? au ndiyo Tanganyika yenyewe.Kama Tanganyika ipo na ndiyo serikali kuu ya JMT, ZNZ imeungana na zimwi gani? Muungano upi uliopo
 
Mkandara: Mambo yote ni ya Muungano isipokuwa shughuli zake ndizo huwa za serikali, hivyo ndio kusema wizara ya ELIMU inatakiwa kuwa ni uya Muunngano isipokuwa uendeshaji wa shughuli za elimu ndipo tunapotofautisha kati ya Zanzibar na Bara. Mamlaka hayo watapewa serikali za Zanzibar na serikali ya Bara kama ilivyo. Mwafunzi anaweza kwenda popote kusoma pasipo kubaguliwa yoka darasa la kwanza hadi chuo kikuu. Kilimo na wizara zote ziwe chini ya serikali kuu ambayo itafaidika kwa asilimia 60 ya pato toka pande hizi mbili
Mkuu anasema mambo yote ni ya muungano.
Wznz wanasema hivi kuna mambo ya muungano na mambo yasiyo ya muungano.

Kuna wizara kama uvuvi si ya muungano. Elimu ya juu si muungano, afya si muungano. Ukifanya kila jambo ni muungano, SMZ itashughulikia nini?

Hapo juu umesema znz ni nchi nasi tukakakubali, sasa nchi gani isiyo na serikali kwasababu mambo yote si ya nchi hiyo.

Kama yapo ya znz, utawezaje kusema hili ni la muungano na hili ni la znz. Waziri wa kilimo wa znz atakuwa mdogo kwa yule wa muungano!

Hivi huoni unatafuta ugomvi na wznz ambao muungano kwao ni kero.
Hata wznz wenyewe hawakuelewi kwa hoja hii na sioni mantiki yake kabisa.

Unasema kila upande ufaidike na 60 asilimia ya pato la taifa. Ipi hiyo?
Znz haina mchango katika pato la taifa unataka inufaike na nini zaidi maana sasa hivi inanufaika tu bila mchango.

Huna sababu za kusema pande zote wakati tunajua ni upande mmoja. ZNZ haina uwezo wa kutoa chochote kwa ulingano na Tanganyika, si leo au kesho daima milele. Huo ni ukweli.

Tanganyika yenyewe tu ni asset bila kuhesabu watu.
Znz inawezaje kugawana mapato sawa na Tanganyika.

Hakuna usawa mkuu, znz ni kupe, period! usigeuze kupe kuwa ng'ombe wa maziwa, kupe ni kupe na atabaki mgongoni kunyonya damu ya ng'ombe aliyembeba na kuwa kero. Ndiyo tabia ya kupe.
 
Mkandara: Kama tumeweza kujua mchango wa tanganyika ktk mfuko wa Taifa leo hii ndani ya serikali 2 binafsi sioni saabu ya kuunda serikali ya 3 ili tujue lile lile linalojulikana leo maana gharama za uendeshaji serikali hutokana na kodi za wananchi. Kodi akilipa Bakhresa akiwa Dar inahesabika ni makusanyo ya Bara haihitajiki kuweka jina tanganyika kutambua kodi ya Bakhresa imetoka wapi. Hii ni hawa kwa uwekezaji wa nje maada makao makuu ya Azam yapo bara basi kodi yake inakusanywa na itaendelea kukusanywa Bara ndani ya serikali zozote
Mchango wa znz ni upi kama tunajua wa Tanganyika. Tunachotaka ni kuwa mchango wa Tanganyika umnufaishe mlipa kodi wa Tanganyika si wa nchi jirani uliyosema ya znz.

Kodi za Bakhresa zikusanywe anakofanya biashara hata kama ni Uganda hakuna shida. Akikusanya Tanganyika ibaki Tanganyika kwasababu ndiyo yenye soko. Kwanini asiweke viwanda znz. Zantel walikimbia kwa kufanya biashara na watu laki 5 nusu yao wakiwa watoto wa shule.

Kuhusu bandari huru hakuna sababu za Tanganyika kuacha mambo yake ya maendeleo ili kumpendeza nchi jirani ya znz.

Ni sawa na kutuambia tuache kujenga bandari zetu kwasababu Kenya wanajenga.Hata hivyo kwa ubinafasi na roho ya wznz hakuna kitakachovuka bahari.

Nikupe kidogo, unajua hilo liliwahi kufanyika.
Kilichofuatia ni wahuni kuteremsha bidhaa zao znz na kuingiza bara buree. Pesa zinaliwa na wajanja wa znz na SMZ.

Huo ni ujinga ndio maana serikali ikaweka kodi mbili.
Maalim Seifa amekiri kuhusu uhuni uliofanyika.
Hatuwezi kuacha bandari ya Mtwara ife eti tuwafurahishe watu wa nchi jirani ya znz.

Wao wanakitu gani Mkandara? Yaani upo radhi Tanga ifunge shughuli ili znz ambayo ni nchi jirani inufaike, kuna kitu gani cha maana unachokijua kuhusu znz ambacho hatukijui.

Znz ni nchi kama Comoro tu kwetu sisi muungano ni msaada kwao, hatuwahitaji to be honest.

Hata muungano ukifa leo we lose nothing. Kama unaona ni wa maana let them go, we don't need them iota mkuu.

Tutajenga bandari zetu kwa watu wetu, kuacha eti wajenge wznz ni ujinga. Ni nani wao, hebu tuambie znz wanakitu gani unachokijua ni cha maana tusichokijua sisi.

Halafu mkuu hebu tueleze serikali ya bara ni ipi na ya muungano ni ipi!!!! ?
 
3. Kulivua koti hili la Muungano ni pale sisi bara tutakapo wezakutambua kwamba Zanzibar ni sehemu ya Tanzania.Wana mchango mkubwa sana ktk Taifa hili kulingana na location ya visiwa hivyo.Tusiutazame mchango wa Zanzibar kwa kupima fedha ama bendera ama katiba yaobali tunawezaje kuitumia Zanzibar kuboresha GDP ya Taifa zima. Kwa mfano tukijengabandari kubwa Zanzibar na kuifanya freeport (siisales Tax), Kujenga soko kuu la kilimo, spices, matunda na nyama kwa ajili yaexport kuvuta nchi za asia na Ulaya kutoka na freepot hivyo imports na exportszitalenga kupitia Znz.
Mkuu, wazanzibar hawataki Tanzania, mbonahuwaelewi. Sisi tumejiita Watanzania miaka 50, wao hawataki kabisa. Mkuu somakatiba yao uone kama kuna sehemu wanautambua utanzania
 
4. Tutalivua koti kwa kuhakikisha kila mikopo, misaada nagrants zinayochukuliwa nje kwa ajili ya ujenzi wa Tanzaniaiwe Bara au visiwaniinafaidisha Taifa zima kwa ile asilimia 60 wanayochukua serikali kuu. Kwa maanahiyo kama Dhahabu ya Geita au reli ya kati, Tazara inachagia mfuko wa Taifabasi mfuko huo ni wetu sote.Na kama Karafuu ya Zanzibar inauzwa nje, basi wajueasilimia 60 ya kodi ama ushuru wake inakwenda moja kwa moja ktk mfuko wa Taifawao watabakia na asilimia 40 ya makusanyo ya kodi. Ugonvi mkubwa baina yetu naZnz umetokana na hili, haya nimesoma kuwa JK kapata mkopo mkubwa toka IMFkuboresha reli ya kati kwa jina la Tanzania, sasa tujiulize iweje pato la relihiyo halitakuwa la muungano hata kwa asilimia 1 kwa sababu tu ati sii mambo yamuungano?. Kwa nini isiwe shughuli za uendeshaji wa reli hiyo ndio uwe nimamlaka ya bara, lakini kitakacho ingizwa 40% ya bara na 60% ya Muungano hukotuna kisu kingine. Kwa haya machache kati ya mengi Kero hazitakuwepo..
Mkuu mikopo na granta si lolote sichochote ukilinganisha na msaada wanaopata sasa hivi. Hatuna sababu za kuwapazaidi ya wanachopata maana wanapata hata wasichostahili.


Bajetiyao ni bilioni 700, makusanyo ya znz ni bilioni 320, zilizobaki takribanibilioni 400 zinatoka hazina Dar.

Muunganoambao wafanyakazi wao unalipiwa na Tanganyika.
ZNZ inachangia nil, sifuri,zero

Mweziwa January wamepewa bilioni 80 kuvusha umeme kwenda Pemba.
Kabla ya hapo SMZilikuwa inatumia bilioni 800 kwa mwezi kulipia umeme.
Gharama za sasa kutokapemba imechukua Tanesco ambayo italipwa na JMT ambayo ni kodi ya Mtanganyika huku mznz akipunga upepo, huo ndio muungano Mkandara anaotaka.

Zanzibarhaijui ulinzi na usalama.
Jeshi na Polisi ikiwa ni pamoja na mambo ya njeinalipwa na Tanzania.
Hizogharama huzioni unaonaona mikopo na misaada.

Tanganyikainatoa ajira kwa wznz ambao wangebaki kwao wangepigana mapanga.
Huwezi kuonahiyo kama sehemu ya misaada.

Elimuya juu si muungano.
Mwaka jana Tanganyika imesomesha wanafunzi 1000 zaidi yaSMZ. Mwaka huu imechukua wanafunzi 1700 ambao ni uzanzibar tu wala si creditkwa gharama za Tanganyika.
Mlipa kodi wa Tanganyika anamenyeka wakati kuna mtu anachukuasi mkopo bali msaada. Huioni hilo mkuu

Balozizinalipiwa na Tanganyika.
znz haiwezi kumudu gharama za balozi 30 labdawabinfasishe kwa akina Bakhresa.

Bajetiya bilioni 700 ambayo nusu inatoka hazina haiwezi kulipia.
Wakatihuo huo hawawezi kulipa umeme leo unasema tugawane mikopo.

Denila taifa ni trilioni 22, tukianza kugawana mikopo na deni tutagawana.
ZNZwakiambiwa walipe asilimia 2 ya trilioni 22 hawawezi.
Kama hawawezikulipa Tanesco watawawezaje kulipa IMF.

Hiihaina maana hawawezi, la hasha, ni kiburi tu kwasababu wanaamini kwa dhati kuwawao wanahaki ya kulipiwa kila kitu, kwasababu zile zile ulizo nazo za 'niwazanzibar' ambao wewe unadhani ni muhimu sana, sisi tunasema, no! not at all

Gharamani lazima uangalie deni la ndani na nje.
Mikopo na misaada ni kidogo sanaulilinganisha na zigo analobeba Mtanganyika
1.Kulipia muungano
2.Kuendesha SMZ
3.Kuhudumiawznz waishio bara

MkuuMkandara huwezi kusema znz ina nia njema tuelekee S1.
Kuna njia moja tuiliyobaki, serikali 3 za mambo 7 au vunja muungano.
Tanganyika tunapoteza kitugani. Hebu waeleze Watanganyika watapoteza nini hasa.

 
Mkandara amegeuka, hapo nyuma amesema anakubali serikali 3, wiki moja baadaye anasema hataki S3.(Rekodi ipo jf ikihitajika)

Kero unazozungumzia ni wznz, vipi Watanganyika hawana?
Kubaguliwa si kero. Waziri mkuu kuomba kibali cha kazi znz na kibali cha kuishi si kero?

Mtanganyika kuchomwa moto ili aondoe biashara zake znz si kero?
Mwanafunzi wa Tanganyika kunyimwa mkopo znz si kero?

Mtanganyika kunyimwa ardhi, na znz kutoa ardhi kwa watu wa mombasa, Oman na wataliano si kero? Watanganyika kunyimwa ardhi znz si kero?
Katiba ya muungano ambayo ni ya Tanganyika kwa mujibu wako au serikali ya bara kama unavyosema ni chini ya katiba ya nchi jirani ya znz, hiyo si kero

Tumekuuliza tunavua vipi koti umezunguka hukusema kitu kikaeleweka. Huwezi kuvua koti kwa kuacha kujenga bandari Mtwara ili ijengwe nchi ya jirani. Kwanini tusiache Kenya wakajenga tudhani znz ni muhimu sana. Biashara kati ya Kenya na Tanganyika ni kubwa mara 1000 ya biashara kati ya Tanganyika na znz.
Mkuu wangu hivi kweli wewe mgumu kiasi hiki kuelewa?

1.Nimesema sikubaliani na serikali 3 kwa sababu nyingi tu kwanza sii muda wake aidha tumechelewa ama iwe baada ya Katiba mpya kupatikana ndio majadiliano yanaweza kuanza na iwe kupitia referendum. Hata kujitenga kwa Znz niliwahi sema kupitia referendum. Kuna record kubwa huko nyuma nikiunga mkono serikali 3 kwa wakati ule na muundo ambao hadi sasa hivi nauzungumzia na sii huu wa Warioba ama wa Katiba iliyopo.

2.sababu kubwa ya kupinga seikali 3 za sasa ni mawazo ya kuwa na Mambo yasokuwa ya Muungano kama ilivyo ktk serikali 2 kwa sababu huu ndio mzizi wa matatizo yote. Chako chako, changu changu sii Muungano bali Muungano watu hugawana shughuli kaa unavyogawana mamlaka ya shughuli ndani ya ndoa yako. Nampingana na Mambo yasokuwa ya Muungano kuwa sehemu ya muundo wa Muungano iwe ktk serikali 2 au 3.

3. Muungano tulokuwa nao umeweza kudumu kwa miaka 50, hii ni record kwa nchi za Kiafrika japo unazua kero zilizizopo. Kero zitaendelea kuwepo iwe ktk mfumo wowote ule wa Muungano maana lazima kila nchi itavutia upande wake. Kinachohitajika ni Katiba inayotufunga kamba za shingo na strong leadership ili sote tuwe wamoja

4. Unaweza cheza na Katiba ya nchi kufanya amendments ama ukaibadilisha kila changes zinapohitajika lakini huwezi kucheza na Muungano wa nchi.

Ikiwa Znz ni sehemu ya Jamhuri ya Tanzania, wewe Utaifananishaje na Kenya? Hivi kweli unajua maana ya Muungano wa Nchi kuunda Jamhuri moja, na Muungano wa Mataifa kiuchumi kuunda nguvu ya soko moja! Hata kama EAC tutakuwa na sarafu moja bado pato la Kenya litabakia Kenya na pato Tz litabakia TZ hakuna ndoa wala undugu hapo ni utafiki wa kula yamini tu, hivyo sisi kuendelea kuwa na mambo yasokuwa ya Muungano ni sawa na kuifanya Znz shirikisho kama Kenya, Hili ndilo nalopinga mimi . Hakuna Mambo yasokuwa ya Muungano baina yetu na Zanzibar ila yapo mengi yasokuwa ya Muungano baina yetu na Kenya.

Mara 10 Kidogo nimesema tatiz kubwa la kuipata suluhu yetu ni kule kuendelea ku deal na KERO. Kero ni kero tu zipo na zitaendelea kuwepo mahala popote penye watu wawili, mimi sikosi usingizi na Kero kwa sababu najua Kero ni matokeo ya kulimbikiza makosa ama mapungufu ambayo yalihitaji ufumbuzi. Hivyo njia za kukidhi mapungufu hayo haziwezi kubadilika kwa sababu ya Kero bali zinabakia bvile vile hata kabkla ya kuwa Kero. Nikatoa mfano wa Usafi kwa jiji la Dar, Mfano mwingine wa Usafiri kwa jiji la Dar. Maamuzi yalofikiwa kuusafisha mji kwa kufukuza wauza chips na hata wachoma nyama nje ya Restaurant ni makosa na Ujinga kwa sababu uchafu sio bidhaa wanazouza ila mabaki ya taka ambayo hatuna utamaduni wa usafi, miundombinu na vifaa.

Kufungiwa kwa bidhaa hizi mjini ni maamuzi yanayotokana na watu kufikiria jinsi ya kuondokana na Kero, badala ya kuha,kikisha wachoma nyama wanaweka mazingitara yao safi wakiacha uchafui wapigwe fine kubwa. Halamashauri ya jiji iwe na vifaa vya kutosha kukusanya uchafu unaolundikwa pembezoni mwa barabara. Mifereji ya majitaka ijengwe, barabara bora za lami na pana zijengwe, Highways na belt (fly over) hivi ndio unaweza ku control Usafi na traffic jam zinazotokea mjini Dar.

Mawazo yako wewe ni yanatokana na Kero na hapa ndipo tunapotofautiana kwa sababu mimi natazama mapungufu ya MNuungano wetu sio muundo wa serikali bali mfumo wa shughuli za serikali bado upo chini ya serikali kuu ambayo ni CCM. Na ndio maana ktk bunge la Katiba CCM wote wa Bara na Zanzibar wamekuwa kitu kimoja kuendelea ku control mamlaka ya Ujima wakitumia jina la demokrasia.
 
Mwenzenu, hili la UKAWA bado sijalielewa vizuri sana japo najaribu sana kulielewa. Sijaelewa kama ni Muungano unaotaka kuja kuongoza taifa letu au ni muungano ambao unataka kuiondoa CCM; sijafahamu vizuri kama ni Muungano wenye lengo la kuhakikisha tu Tanganyika inarudi na Zanzibar inakuwa na mamlaka yake au ni Muungano unaotaka kuboresha Muungano kwa kuleta Serikali Tatu. Maana nina hofu - na sitashangaa kuwa zitakuwa kweli - kuwa tusije kushuhudia kama ule Muungano wa kwanza wa kina Mwai Kibaki na wengine walipojaribu kuiondoa KANU ambapo walionekana wameungana mwaka 2002; na kwa kweli waliweza kuiondoa KANU madarakani. Lakini sote tunajua matokeo yake yalikuwa nini ilipofika 2007.

Binafsi sijaona kama muungano huu ulifikiriwa sana kabla ya kufanyika (hatukuona wamejiorganize kabla ya Bunge la Katiba wakati wa kura za maoni n.k) ni kama more reactionary than anything. Na kinachowaunganisha ni suala la Tanganyika na Zanzibar hatujui itakuwaje watakapofika kwenye mambo mengine yaliyomo kwenye rasimu kama wataweza kuwa pamoja hasa kama mitazamo ya kivyama itapishana.
 
Mwenzenu, hili la UKAWA bado sijalielewa vizuri sana japo najaribu sana kulielewa. Sijaelewa kama ni Muungano unaotaka kuja kuongoza taifa letu au ni muungano ambao unataka kuiondoa CCM; sijafahamu vizuri kama ni Muungano wenye lengo la kuhakikisha tu Tanganyika inarudi na Zanzibar inakuwa na mamlaka yake au ni Muungano unaotaka kuboresha Muungano kwa kuleta Serikali Tatu. Maana nina hofu - na sitashangaa kuwa zitakuwa kweli - kuwa tusije kushuhudia kama ule Muungano wa kwanza wa kina Mwai Kibaki na wengine walipojaribu kuiondoa KANU ambapo walionekana wameungana mwaka 2002; na kwa kweli waliweza kuiondoa KANU madarakani. Lakini sote tunajua matokeo yake yalikuwa nini ilipofika 2007.

Binafsi sijaona kama muungano huu ulifikiriwa sana kabla ya kufanyika (hatukuona wamejiorganize kabla ya Bunge la Katiba wakati wa kura za maoni n.k) ni kama more reactionary than anything. Na kinachowaunganisha ni suala la Tanganyika na Zanzibar hatujui itakuwaje watakapofika kwenye mambo mengine yaliyomo kwenye rasimu kama wataweza kuwa pamoja hasa kama mitazamo ya kivyama itapishana.

Wapinzani wa Tanzania ni Pasua Kichwa. Mara nyingi husema, aina hii ya wababaishaji ni "reflection" ya sisi kama taifa. playbook ya wapinzani, wanaichukua CC Dodoma, wakizidiwa mbinu wanalalama. Hivi kuna anayeshangaa kwa nini kibao kimewageukia wapinzani mara baada ya Mangula na Kinana kupewa Marungu?tunafikiri hii ni coincidence? sidhani, hii ni gameplan, kinachoendelea CCM wanakijua Vizuri, wapinzani wanakisia. Inakera na kuudhi sana, kwa kuwa wengi wa wapinzani wetu hawapendi kupokea ushauri. kwao kuikosoa CCM ni ajenda kuu, kwao kupinga kila kitokacho CCM ni ajenda kuu, wakati walitakiwa wajenge taswira yao mbele ya wananchi. Inafikia mahala sasa CCM wanatoa proposal Nzuri, lakini kwa kuwa wapinzani wamekariri tafsiri yao ni kuwa kinyume cha CCM basi wanapinga. Bila kupima upepo. Mfano mzuri ni issue ya Lissu na Nyerere. CCM walikuwa Sahihi kumtetea yule babu, hata kama alikuwa na makosa yake ya kibinadamu. Upinzani wenye akili ulitakiwa kuji-distance na maneno yao na kuweka "redaction". Kerry juzi amefanya hivyo. lakini wanasiasa wetu wanaona sifa wakiitwa wana Msimamo, hata kama msimamo wao unawa-cost Kura.

Kitu kingine, wapinzani wanatakiwa kujua kuwa kabla hawajaongoza nchi, wanatakiwa washinde uchaguzi. So, far hakuna mkakati wa kushinda uchaguzi. wanategemea watumie ruzuku zao wazurule nchi nzima kueleza makosa ya CCM bila kushawishi wananchi wawapigie kura. Watanzania wenyewe ndio hawa hawa wa zimwi likujualo.

Katiba bahati mbaya imegeuka kuwa ajenda ya Kisiasa, wakati lilitakiw aliwe jambo ambalo kofia za kichama zingevuliwa na zingevikwa kofia za nchi. Binafsi nilitegemea hata hadithi za Ukawa etc zisingekuwapo.nilitegemea kusiwe na maoni ya CCM,maoni ya Kanisa, wala ya Msikitini, nilitegemea kuwe na sauti moja ya watanzania. walioamua kwa dhati kukaa chini kujenga nguzo za taifa imara kwa kizazi kijacho.

Kinachoendelea sasa Dodoma ni aibu kuu. Kinachoendelea Dodoma kianoesha kuwa 2015 wanachi watafanya waliyoyazoea. kuchagua zimwi walijualo. na inawezekana wakatumia katiba waijuayo vile vile, kwani hat amuundo wa serikali, wanasiasa wanataka ubaki ule ule waujuao. "funny creatures we are".
 
Mwenzenu, hili la UKAWA bado sijalielewa vizuri sana japo najaribu sana kulielewa. Sijaelewa kama ni Muungano unaotaka kuja kuongoza taifa letu au ni muungano ambao unataka kuiondoa CCM; sijafahamu vizuri kama ni Muungano wenye lengo la kuhakikisha tu Tanganyika inarudi na Zanzibar inakuwa na mamlaka yake au ni Muungano unaotaka kuboresha Muungano kwa kuleta Serikali Tatu. Maana nina hofu - na sitashangaa kuwa zitakuwa kweli - kuwa tusije kushuhudia kama ule Muungano wa kwanza wa kina Mwai Kibaki na wengine walipojaribu kuiondoa KANU ambapo walionekana wameungana mwaka 2002; na kwa kweli waliweza kuiondoa KANU madarakani. Lakini sote tunajua matokeo yake yalikuwa nini ilipofika 2007.

Binafsi sijaona kama muungano huu ulifikiriwa sana kabla ya kufanyika (hatukuona wamejiorganize kabla ya Bunge la Katiba wakati wa kura za maoni n.k) ni kama more reactionary than anything. Na kinachowaunganisha ni suala la Tanganyika na Zanzibar hatujui itakuwaje watakapofika kwenye mambo mengine yaliyomo kwenye rasimu kama wataweza kuwa pamoja hasa kama mitazamo ya kivyama itapishana.
Bora wewe mkuu umeliona hilo na wala usidhanie vinginevyo maana kinachofanyika hapa ni Political mind game! inaudhi hasa ukizingatia hawa watu wamepewa dhamana hii kuandika Katiba Mpya.

Sasa tazama basi, CCM wanajua kwa nini hawataki serikali 3 na nakuhakikishia sii kama tunavyofikiria sisi ila wanajua fika karata walonazo CUF na mbinu wanyoitumia hasa kwa kuitaka Zanzibar huru, maana wameisha walisha sumu Wazanzibar wengi kwa Udini na utengano na bara kiasi kwamba Nyerere anaitwa LaatuLLah na mijinga ilowekwa utumwa wa kufikiri. Kisha unakuta mijitu mingine inafikiri sauti ya CUF na wafuasi wake ndio sauti ya Wazanzibar wote kama wao Waznz wanavyofikiri kuwa sauti ya CCM ndio sauti ya bara na Ukristu. Lukuvi alifanya makosa makubwa Kisiasa lakini kuna ukweli ndani ya maelezo yake na hivyo kuchochea wazi wazi Udini. Tundu Lissu kalishwa matapishi na CUF akifikiri kapewa bokoboko.

Tukiendekeza fikra hizi hapa hapatakuwa na Muungano kabisa na mtakuja nambia maana nashukuru Mungu kanijaalia kuona mbali. Na hizi mbinu za UKAWA ni kupingana na CCM tu, kwa sababu wanakisia CCM wanalao jambo na kwa nini wanaibembeleza Zanzibar kumbei vijana hawa hawaelewi uzito na nini hasa maana ya Muungano wa nchi. Watazame Ukraine na Urusi kinavyowaka, Watazame kilichofuatia Ethiopia na Eritrea na majuzi Egypt. Hii yote inatokana na wanasiasa wachache kuchochea moto wa Kisiasa hasa kwa kutumia katiba ya nchi.

Hakuna hatari kubwa ya kuvunja muungano nahata kusababisha vita ikiwa swala la Muungano litakuwa sehemu ya Katiba kwa sababu katiba huundwa baada ya kupatikana NCHI ama TAIFA. hivyo mwongozo huo unasimamia haki za wananchi wake, unaweka shera dhidi ya wahalifu, wahaini, miiko na maadili sii kwa viongozi tu hadi wananchi kulingana na mila na tamaduni zao.

Kilichonichosha zaidi ni pale wajumbe wengi wa UKAWA wanapofikiri kwamba dhamana walopewa ni kutoa mawazo yao japo wamechaguliwa toka ktk vikundi vya kijamii. Hawajui kama wapo pale kutetea haki za vikundio vyao, kusimamia mawazo ya wengi toka ktk makundi yao bali wanachojua wao ni MAWAZO BINAFSI yaani kila mtu aseme anavyoona yeye.

Hii Katiba ama tunatunga kitabu cha hadithi za Alinacha! Hivi kweli watu 300 wenye mawazo yao binafsi wanaweza kfikia muafaka? ukiwauliza ni kipi hasa wanachokitetea dhidi ya serikali 2 utasikia ati muundo huo umepitwa na Wakati wakati gani? mbona Muungano wa Marekani una miaka zaidi ya 200 na wameendelea kutushinda sisi kwa kila kitu..Hadi sasa hivi sijaona hoja ya maana kabisa zaidi ya wajumbe wote kupingana kwa jina la chama.

Utasikia hata kutoka wajumbe wa makundi ya kijamii wakidai Hao CCM wanachakachua, hao Chadema au hao CUF hivi na vile as if wanaandika sera kila mtu anakuja na imani yake ya kiitikadi. Katiba haitungwi kwa kufikiria Maria Sarungi anataka nini, Zitto anataka serikali gani ama Jussa anataka muungano gani. Na kibaya zaidi ati rasimu ya Warioba inaitwa maoni ya wananchi? hii wameipata wapi? hivi kweli tuna Watanzania wangapi wanaotaka muungano wetu uwe wa SHIIRIKISHO kama ilivyo EAC! halafu wanahakika Muungano utaimarika zaidi wakati wanaijua historia ya EAC. Yaani tutoke ktk Muungano wa nchi mbili kuunda Taifa 1 kwenda Mataifa mawili yenye ushirika ndio Muungano unaokwenda na wakati?

Hivi kweli tunaweza kuwa na shirikisho lakini kiti kimoja UN, ama itabidi kila nchi iwe na kitu chake kama ilivyo Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi. Na hata kama tutakuwa na kiti kimoja hawaoni kama kitakachofuatia ni madai ya kila nchi kuwa na kiti UN maana tayari nchi hizo zina shirikisho tu? na wasivyo elewa umuhimu wa Muungano wanazungumzia mifano ya EU kama mfano bora! nani kawaambia muungano wetu ni sawa na ule wa EU ama tukiwa na shirikisho kama hilo tutakuwa wamoja zaidi..

Na sijui kama hawa watu wamewahi kutembelea nchi za EU hasa zilizoendelea na uchumi mzuri wajue jinsi gani wananchi wanavyobaguana na kuchukiana na wageni kufuatia sheria tu ya Uhamiaji toka nchi jirani ambao zamani hawakuwa na fursa hiyo. Ati wananchi wengi wanaunga mkono shirikisho! wananchi hao ni kina nani kama sii kina Jussa na Hizbu yao! mimi sikubaliani kwa mengi na utawala wa CCM lakini ktk hili sintowaunga mkono UKAWA hata kwa mijeledi!
 
Back
Top Bottom