Ukiacha Dar es Salaam, mikoa iliyobaki ujanja wao ni mchana tu, ikifika saa tatu usiku kila mtu yupo kwake

Ukiacha Dar es Salaam, mikoa iliyobaki ujanja wao ni mchana tu, ikifika saa tatu usiku kila mtu yupo kwake

Kama ni kweli supu ya pweza, biashara ya malaya, bias, chapati na maharage, supu ya kongoro
Chapati za wapemba saa moja usiku ndio anawasha moto,huko kijijini kwetu ndio wanafunga milango walale
 
😀 Mnafanya watu waliopo nje ya Dar na hawajakaa Dar wahisi ukiamka unakunywa chai Serena au Hyatt, wanazoziona katika movie. Kwako una furniture za ulaya, bafu kubwa lina jaccuzzi na sehemu ya steaming,ki shower amazing. Ukienda beach unakodi yatch, unakunywa beer saafi imported,sehemu nzuri

Kumbe UHALISIA bana asubuhi vitumbua au mihogo ya mia mia kwa mama Mwaju, chai ya rangi. Kuoga unatoka na kopo lako la sabuni maji katika ndoo, mavi unayamwagia maji system ya kuflash haipo au maji hayaendi katika system. Mtu anaweza hisi pisi kali unaimiliki kumbe ni mjasiriamwili unapiga,na wengine wanapiga ila una picha yake.


Huyu sio wewe, ila ndio 80% ya life hapa Dar.

Kuhusu night life ni kweli kuna tofauti, ila nimezurura mikoa kadhaa, naijua nightlife ya Mwanza,Arusha,Mbeya na sehemu kadhaa inategemea na mapendeleo yako na hadhi yako.

Hii mada ni aidha ya mtu ambae ni mdogo, au ana experience ndogo katika mambo ya starehe na kuzunguka nchi hii. Nimeenda mpaka vijijini iringa nakuta sehemu unakesha na watu wanakula monde, na ukitaka kuichapa unauliza wakulungwa😀

Jamaa alietoa mada sio mtu wa night life bana, au alienda sehemu muda mfupi. Akataka kwenda kula bata jumatatu au jumanne usiku.

Hata Dar ukiona mtu anakesha mpaka asubuhi katika starehe, mara nyingi ni fala, mwizi au anatumia fedha za kupewa (baba,mama e.t.). Mjanja akienda club saa tano au sita saa 9 au kumi anasepa niamini, waliobaki ni aidha kuna issue maalum ni wachache wengi ni mafala, waomba bia,machawachawa,wezi, malaya(wabovu). wale smart,visu wanakuwa walishachukuliwa 😀

Mitandaoni watu wana mikwara sana, hawaulizi kujua. Inaweza isifikie Dar kwa sababu ya population na infrastructure ila kila sehemu ina night life yake. Night life issue kubwa ni ku refresh tu vinywaji,chakula n.k

Mkoa gani ulitafuta chakula kwa tochi? Au unaongelea aina ya chakula,ulikosa chips kavu? Kama ulikuwa Arusha ungeenda Granmelia ipo pale mkuu ina hadhi ya nyota tano kama Serena unapokunywa chai. Au kama ni masikini masikini ungeenda maeneo Shivers/Mrina ungepata nyama choma na mad* wa kununua.

Tabora ungeenda hata Tabora Belmonte ni nyota tatu haifikii Hyatt unapokula mchana ila ingefidia kidogo, wazungu weusi wenzako huwa wanalala pale pia, kama ni masikini masikini unataka wa kununu ukachakate ungeenda Oxygen Lounge/Club nadhani bado ipo nilipita muda kidogo.

Mwanza zipo sehemu kibao, Iringa zipo.....Mbeya pia nimeshacheki night life yao.

Issue ni hela hamna, au nyie ni madogo na night life mnaigiza mnataka mkute watu weengiii muanze ukenge ukenge 😀 sababu mmeshazoea kufuata mikumbo ya msafara wa mamba.

Halafu watu wa hivi na mitazamo hii hata hapa Dar ndio nyie tunawakimbia club kubwa tunaenda katika vi bar vya nje sababu brother brother nyiiingiii ni bia ya saba zote za mizinga,na kusimulia historia za zamani, ulegend wa kibwege oooh hapa Kino mi legend, babu yangu sijui hivi, wakati watu wanataka kula life kwa kidogo kilichopatikana.

Ukiwasha sigara, haujafika hata katikati anaitaka, unampa nzima anaiweka mfukoni anasubiri unayovuta. Mwishowe unambwatukia dogo kuwa na adabu, kwanza nani kakuita hapa....umeshapata bia na sigara. Ondoka

NB SIO LAZIMA UWE WEWE NDIO WATU KIBAO WALIVYO
Aiseeee
Wewe wa mikoani unatufasiria mji wetu sisi tuliozaliwa, kuuishi na pia kutoka na kuzunguka dunia sio mikoani namaanisha miji mingine duniani, ikiwepo ya US, Europe, Asia na miji mikubwa hata hapa Africa
Halafu unalinganisha Dar na vijiji vilivyochangamka
 
Usingizi ni Afya, ni Muhimu sana Mtu kupumzika vizuri kwa masaa at least 7 au 8, usijisifie kutokulala na kujiona mjanja🫠

wengi wanaopumzika vizuri wana pesa au hali nzuri kiuchumi, sio Hohehahe

Dsm ina hali mbaya sana kimazingira, inanuka sana, inanuka vinyesi, shombo na jalala kila kona

Joto pia ni kali sana

Kutokana na kero hizo utawezaje kupata utulivu na kulala vizuri kwa wakati? Labda kama wewe ni Funza au Inzi
Tatizo ni hivi
Huko mnakokaa kwenye vijiji vilivyochangamka hakuna maisha ya Night Shift
Sio kwamba watu hawalali, Dar kuna Viwanda na kazi zinafanywa kwa shift, yaani watu wanalala mchana na usiku wanaingia kazi, kwa hiyo mji unakuwa unajipanga kuwahudumia kama sehemu ya kula, usafiri na mengineyo
Huko kwenu kwenye vijiji vilivyochangamka, maisha ni mchan tu............
 
Tatizo ni hivi
Huko mnakokaa kwenye vijiji vilivyochangamka hakuna maisha ya Night Shift
Sio kwamba watu hawalali, Dar kuna Viwanda na kazi zinafanywa kwa shift, yaani watu wanalala mchana na usiku wanaingia kazi, kwa hiyo mji unakuwa unajipanga kuwahudumia kama sehemu ya kula, usafiri na mengineyo
Huko kwenu kwenye vijiji vilivyochangamka, maisha ni mchan tu............
Sasa kumbe Dar wanalala Mchana ili usiku eapige kazi, sasa Mkoani watu hawalali mchana zaidi ya kupambana na kazi ma usiki wanalala.....kumbe mwalala mchana 🤣🤣🤣🤣

Hapo tofauti ni Wakati tu wa kufanya kazi
 
Dar unatoka kuamka mwenzio ndo anaingia kulala yani hakuna kupoa
 
Aisee ila jamii forum kuna matapeli wengi sana..mtu.wa.simiyu.akiona hayo mapicha anaweza kuuza ng'ombe zake aje huko kumbe ni wizi.mtu hakuna la maana watu.wanaishi.maisha ya taabu kama watumwa
Pita hayo maeneo muda wa mchana ujionee uhalisia wake, picha zinadanganya sana aiseee, hayo maeneo ni machafu sana ata mpangilio wake uko ovyo tofauti na hizo picha
 
kumbe ujanja ni kukesha usiku kucha .ndio maana mungu aliumba usiku na mchana .je wewe unayekesha usiku kucha unawazidi kitu gani wanaopata muda wa kupumzika
 
Back
Top Bottom