Ukiachana na dunia kulizunguka jua na kujizungusha kwenye muhimili wake nadhani kuna mzunguko mwingine ambao wanasayansi hawajaugundua

Ukiachana na dunia kulizunguka jua na kujizungusha kwenye muhimili wake nadhani kuna mzunguko mwingine ambao wanasayansi hawajaugundua

Mkuu,

Haya mazungumzo mazuri na muhimu sana. Ni muhimu kwenda na data, but you are definitely on to something here.

Definitely kuna mizunguko mingi zaidi ya uliyotaja ambayo wanasayansi wameigundua na imeandikwa, kwa hivyo tujielimishe kwanza kuhusu hiyo iliyogunduliwa na iliyoandikwa kabla ya kuongelea sana ambayo haijagunduliwa, ambayo nayo inawezekana ipo.

Kuna mizunguko kama ya solar system kuzunguka kitovu cha galaxy hujaitaja, ingawa sifikirii kwamba hii inaweza kuwa na impact kwenye hali ya hewa.

Sijaona ukitaja mambo kama ice ages. Kama hujazisoma hizi, anza kusoma zaidi hapa Ice age - Wikipedia

Kuna mambo mengine hata si mizunguko per se, ila mambo kama sunspots, yani, maeneo ya jua ambayo yanakuwa na joto la chini na kusababisha imbalance katika nishati ya jua tunayoipokea, na hivyo kuweza kusababisha baridi sehemu ambazo hatujazoea.

Kama hujasoma zaidi kuhusu sunspots ona hapa .

Kwa hivyo kuna mambo mengi ya kujifunza.

Ila, kuna mjadala mkubwa kuhusu climate change na jinsi gani inasababishwa na shughuli za watu kama vile kukata miti, kuongeza hewa za Carbon kwenye hewa yetu, na mambo mengine mengi kama hayo. Kuna watu wanasema mabadiliko haya ya hali ya hewa kwa kiasi kikubwa yanatokana na shughuli za watu, na watu wanaweza kubadili muelekeo huu kwa kubadili maisha yao, kuacha kukata miti na kupanda miti zaidi, kuacha kutumia vibaya nishati na kupunguza utoaji wa Carbon kuipeleka kwenye hewa yetu. Na kuna wanaosema kuwa mabadiliko haya yanatokana na mabadiliko ya asili zaidi kama hizo ice ages na sunspots, mambo ambayo yako nje ya uwezo wetu kuyabadilisha.

Kwa sasa, ushahidi mwingi wa kisayansi, pamoja na wanasayansi wengi wasomi, wanakubali kwamba mabadiliko ya hali ya hewa yanasababishwa na maisha ya watu, si mambo ya kiasili, na tuna muda mchache sana wa kuzuia na kusahihisha mabaya haya yanatotokana na matumizi mabaya ya nishati. Wanasayansi wasomi wa mambo haya wanaokubali hivi ni wengi kuliko wanaokubali kwamba haya ni matokeo ya mizunguko na mambo ya kiasili tu.

Labda kwa sasa niseme hivi kama sehemu ya kuanzia tu, halafu, tuweze kupata chachu zaidi ya kuendeleza mjadala kuanzia hapa.

Shukurani The Monk kwa heshima kubwa ya mualiko hapa.
Nimepitia hii kitu ice age inaongelea kuhusu kupunguza joto duniani. Anyway hii ni elimu ambayo inahitaji muda kuielewa. Kuna concepts nyingi tu inaongelea ambazo inakuwa ngumu to make sense of it. Kiufupi nimetoka kapa. Sunspot ndio kabisa hata sielewi wanaongelea kitu gani. There are lot of scientific concepts that a layman is hard to grasp.
 
Dar es salaam haijawahi kuwa na majira ya baridi kwa muda mrefu hivi. Biharamulo nimeona clip kuna hadi barafu inadondoka kitu ambacho hakijawahi kushuhudiwa. Ulaya wanateseka na joto.

Nadhani haya hayatokei kwa bahati mbaya bali kuna universal system ambayo wanasayansi hawajaigundua kama walivyoigundua solar system inayoleta majira ya mwaka au dunia kujizungusha kwenye muhimili wake kunakosababisha kuwepo kwa usiku na mchana.

Nadhani miaka michache ijayo africa tutaanza kushuhudia majira ya baridi kama ilivyo ulaya na Marekani na huenda huko Marekani na Ulaya wakawa na majira kama tuliyo nayo huku Afrika.

Nadhani huu mfumo ambao ushaanza kuleta baridi hii Afrika upo kwenye stages za mwanzo kabisa, nikimaanisha kwamba stages za mwanzo kwenye huu mzunguko huenda ikawa miongo 2 au 3 depending how long the system is. Maybe this is just the tip of the iceberg.

If the system let's say takes 22 centuries to complete that means the world has never experienced such a system hence there is no such a discovery as it has been for a Solar system.

Kwa hiyo hii baridi ya muda mrefu tunayoiona Dar na barafu kudondoka huko Biharamulo ndio mwanzo wa majira ya huu mfumo ambao dunia haijawahi kuushuhudia. Tutegemee miaka ijayo Africa itakuwa na majira kama ya Ulaya na Ulaya itakuwa na majira kama ya Africa.
Mkuu hata bara la antarctica halikuwa limefinikwa na barafu. Lilikuwa na mito na wanyama.
Pia sahara ilikuwa imefunikwa na vegetation.
Ndiyo maana kuna watu wana argue kwamba mabadiliko ya hali ya hewa hayasababishwi na shughuli za kibinadamu
 
Nawaza waTz wengi ambavyo kipato chetu ni kidogo sijui tutawezaje kuafford masweta mazuri, skaf, buti n.k kujikinga na baridi la namna hyo! Kama hali ya hewa itakuwa hvyo kwa maeneo mengi hapa [emoji848][emoji848][emoji848][emoji848][emoji848].
Usijali mkuu,kama itakuwa kama anavyosema mtoa mada kuwa huko ulaya hali itabadilika na kuwa kama yetu basi wao hawatahitaji hayo makoti ya sufi na boot za manyoya,hivyo watatupa sisi masikini tunaoyahitaji,kumbuka hata sasa hayo mavitu yapo tele kwenye mikokoteni mitaani,tena yanauzwa buku moja hadi kumi tu,ondoa shaka mkuu.
 
Mkuu hata bara la antarctica halikuwa limefinikwa na barafu. Lilikuwa na mito na wanyama.
Pia sahara ilikuwa imefunikwa na vegetation.
Ndiyo maana kuna watu wana argue kwamba mabadiliko ya hali ya hewa hayasababishwi na shughuli za kibinadamu
Mkuu ya kweli haya? Ni miaka gani antarctica haikuwa imefunikwa na barafu mkuu? Kama ni kweli basi tujiandae kuwa na maisha kama ya ulaya.
 
Mkuu ya kweli haya? Ni miaka gani antarctica haikuwa imefunikwa na barafu mkuu?
Mamilioni ya miaka iliyopita. Kuna hadi ramani ya zamani ya aliyekuwa admiral wa jeshi ya Ottoman, linaonyesha mito, milima na topography ya anatarctica bila barafu na imekuja kugundulika iko accurate sana. Hiyo ramani ni ya mwaka 1530.
 
Mamilioni ya miaka iliyopita. Kuna hadi ramani ya zamani ya aliyekuwa admiral wa jeshi ya Ottoman, linaonyesha mito, milima na topography ya anatarctica bila barafu na imekuja kugundulika iko accurate sana. Hiyo ramani ni ya mwaka 1530.
Kwa hiyo tujiandae kuishi kama ulaya mkuu?
 
Inachukua muda si unajua kuwa hata magnetic north inashift
Yeah hata mimi nimeliongelea hilo kwenye thread mama. Maybe what we see now is just a tip of the iceberg. Huenda inakuchukua zaidi ya karne kukamilisha hii cycle.
 
Yeah hata mimi nimeliongelea hilo kwenye thread mama. Maybe what we see now is just a tip of the iceberg. Huenda inakuchukua zaidi ya karne kukamilisha hii cycle.
Nimekuwa nikisoma Hindu scriptures na mambo mengine, it seems kila kitu ni cycle yani mambo yanaenda yanafika tamati yanaanza upya.
Ukisoma maandiko ya wahindu yanazungumzia vitu ambavyo ni advanced zaidi ya science tuliyonayo.
Huenda dunia inapitia vipindi kadhaa na kuanza upya tena
 
Nimekuwa nikisoma Hindu scriptures na mambo mengine, it seems kila kitu ni cycle yani mambo yanaenda yanafika tamati yanaanza upya.
Ukisoma maandiko ya wahindu yanazungumzia vitu ambavyo ni advanced zaidi ya science tuliyonayo.
Huenda dunia inapitia vipindi kadhaa na kuanza upya tena
Uko sahihi mkuu. Kuna kitu kinaitwa "the universe". Watu wengi hudhani the universe ni dunia tu, hapana. The universe ni dunia, nyota na sayari zingine ambazo hatuzijui. So, the universe has a lot in store for creatures. Creatures are not only human beings. Kuna viumbe zaidi ya hawa tunaowajua ambao ni wakazi wa hii universe and when the time goes by tutakuja kugundua kuwa kumbe kuna viumbe wengine ambao wana akili zaidi hata ya binadamu wanaishi kwenye hii universe. Na undoubtedly kuna mabadiriko makubwa sana ya hali ya hewa yatatokea yatakayosababishwa na cycles tusizozijua so far. Naomba pia nikubaliane na wewe kuhusu bara la antarctica.
 
Nimekuwa nikisoma Hindu scriptures na mambo mengine, it seems kila kitu ni cycle yani mambo yanaenda yanafika tamati yanaanza upya.
Ukisoma maandiko ya wahindu yanazungumzia vitu ambavyo ni advanced zaidi ya science tuliyonayo.
Huenda dunia inapitia vipindi kadhaa na kuanza upya tena
Na huenda labda kuna cycles zingine bado hazijafikia mwisho.
 
Dar es salaam haijawahi kuwa na majira ya baridi kwa muda mrefu hivi. Biharamulo nimeona clip kuna hadi barafu inadondoka kitu ambacho hakijawahi kushuhudiwa. Ulaya wanateseka na joto.

Nadhani haya hayatokei kwa bahati mbaya bali kuna universal system ambayo wanasayansi hawajaigundua kama walivyoigundua solar system inayoleta majira ya mwaka au dunia kujizungusha kwenye muhimili wake kunakosababisha kuwepo kwa usiku na mchana.

Nadhani miaka michache ijayo africa tutaanza kushuhudia majira ya baridi kama ilivyo ulaya na Marekani na huenda huko Marekani na Ulaya wakawa na majira kama tuliyo nayo huku Afrika.

Nadhani huu mfumo ambao ushaanza kuleta baridi hii Afrika upo kwenye stages za mwanzo kabisa, nikimaanisha kwamba stages za mwanzo kwenye huu mzunguko huenda ikawa miongo 2 au 3 depending how long the system is. Maybe this is just the tip of the iceberg.

If the system let's say takes 22 centuries to complete that means the world has never experienced such a system hence there is no such a discovery as it has been for a Solar system.

Kwa hiyo hii baridi ya muda mrefu tunayoiona Dar na barafu kudondoka huko Biharamulo ndio mwanzo wa majira ya huu mfumo ambao dunia haijawahi kuushuhudia. Tutegemee miaka ijayo Africa itakuwa na majira kama ya Ulaya na Ulaya itakuwa na majira kama ya Africa.
Mkuu,
ukiwa na muda, basi pitia hii Film chini. Inahusiana sana na SPHINX ya Egypt iliyo pembeni na Pyramid of Giza.

 
Jua nalo Lina sogea kutoka kusini kuja kaskazini(movement of the Sun) hii ndio inapelekea vitu kama hivyo.

Nitakuletea baadhi ya evidence za ma navigator waliofanya tafiti na kuthibitisha.
 
Back
Top Bottom