Ukienda kutafuta maisha kwenye mikoa hii ni ngumu sana kutoboa

Mikoa hiyo inategemea unataka kufanya shughuli gani. Mikoa alioacha mleta mada ambayo ni Mikoa ya kusini basi ameangalia fursa ya kilimo tu. Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro ina base ya consumers ukiamua kufanya biashara ya consumer goods. Ni kanda inayofuata baada ya Dar Es Salaam. Sio ni sababu ya kusema hutoki kimaisha wakati takwimu mbali mbali za NBS na TRA zinaonyesha tofauti na dhanio la mleta mada.
 
Achaa uree mnapenda kuwaonea wachagga kila kitu mnatuonea sasa acha uendelee kunifanya kuwachukia tu.
 
Kama hujaweka Tanga hujafanya kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona wewe ulienda Bukoba kama mpenz mtazamaji[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Blaza hivi tunavyoongea mimi nipo Kampaka nimekuja kuchukua mzigo wa nguo. Huku bei ni za kuokota. Unachukua nguo kwa sh. 11,000 ya Uganda ambayo ni kama 6,500 ya Tz unakuja Bukoba unaiuza 15,000 ya TZ!

Kama unataka kufanya nicheki Pm nikupe full plan. Sio mnaongea vitu mnavyovisikia bila kuvifanya. Bukoba ina fursa kubwa sana ya biashara na watu wengi wanatoboa.

Kuhusu vanilla sio lazima ununue. Tunapoongelea fursa za kutoboa ni kutumia fursa zilizopo. Unaweza kulima vanilla pia ukatoboa. Kilo moja mbichi sasa hivi ni 120,000/= na watu tumetoka Dar na degree zetu tumerudi vijijini kuzilima.

Tatizo lenu wakisema fursa za kutoboa mnakimbilia kuwaza kununua Kariakoo na kuuza tu. Kingine Bukoba gharama za maisha ziko chini sana, kama upo makini na hesabu zako kutoboa ni rahisi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We jamaa sometimes unaniboa sana na sifa zako za kipuuzi

Kagera ni kugumu sana baada ya biashara ya kahawa kudorora

Sent using Jamii Forums mobile app
@kapeace hivi kweli dada kijana wa kawaida alikuwa anafanya biashara ya kahawa Kagera??

Au unazungumzia maisha ya wanakijiji wakulima kuwa magumu baada ya kahawa kushuka bei??

Kwanza kahawa haipo kwenye mawazo ya vijana. Hivi unaweza kutoka Dar useme unaenda Kagera kufanya biashara ya kahawa?? Tunazungumzia sehem yenye fursa za mtu mtafutaji kutoboa kimaisha. Nindenga wampelewa kitonsa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeona nimpite tuu....yaan yy kila kitu kusifia kagera!

Mwaka Jana likizo yangu, nimeenda na biashara fulani ya wadada loooh!

Yaan hata elfu mbili ni ishu kwao[emoji848][emoji849]...

Mkoa mgumu sana ule kihela!

Sent using Jamii Forums mobile app
Unapelekaje biashara sehem bila kufanya research kujua ni biashara gani inaenda kwa eneo husika?

Biashara flani inaweza ikawa nzuri kwa mkoa flani lakini ikawa haiendi kabisa kwa mkoa mwingine, alafu kukawa na biashara nyingine inayoenda sana wakati huko ulipotoka mnaiona biashara ya kipimbi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna mkoa wa bukoba hapa duniani
 
Wewe unazungumzia wenyeji. Sisi tunazungumzia mtafutaji anayejielewa akiamua kwenda mahali kutafuta maisha uwezekano wake wa kutoboa. Nadhani sasa umenielewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mhaya amlimie mtu shamba? Asubutuuuu [emoji28].....halafu wamekuwa walevi balaa!

Yaan huko vijijini mmh!

Sent using Jamii Forums mobile app
Achaneni na wachaga au wahaya, tunajadili uwezo wa kutoboa. Wewe na kabila lako zuri au baya ukienda eneo husika kulingana na mazingira yaliyopo utatoboa. Tusichanhanye madawa jamani. Au mimi nimeelewa vibaya mada??

Maana tukijichanganya hapa tunarudi kwenye makabila tu. Na tukirudi kwenye makabila uzi unageuka kuwa wa Haya vs Chagga. Natoa angalizo mapema. Baadae msiseme sikuwaambia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikaa wiki mbili pale niliisoma namba,na sasa nipo kikazi nna mwezi mmoja,hatari sana dom,hela inapukutika kama upepo,nimezoea moro ukienda sokoni na 5000 unapata mahitaji ya siku moja na nusu.huku maisha ya bachela 10k per day.aisee
Umesahau dodoma Ukipata 10k kwa siku yote inaishia sokoni

CC Zero IQ
 
inshu sio gharama ya maisha kuwa chini,kwenye uchumi kuna vitu vingi sana za kuangalia ,nyama kilo 5000,mchele ni 15000-2000,maharage kilo ni 2000,,samaki na dagaa bei ipo juu,ndizi kumi 1000!!!kodi ya nyumba ndio hizo kidogo kuna afadhari tena kwa wale wanao panga nyumba nzima!!huo una fuu wa maisha upo wapi kulinganisha na mzunguko wa pesa uliopo hapo?!!sema mkoa mwingine lakini bukoba hapana!!!!kwanza muingiliano wa watu ni mdogo sana kutokana na jiografia yake!!!hiyo vanilla kuilima unadhania ni kazi rahisi?mkuu tena biashara hiyo ya nguo watu wengi siku hizi wanafuata katoro kwanini?kama hujui siri hiyo fanya uchunguzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…