Ukimiliki laini zaidi ya moja ya mtandao mmoja utalipa faini Tsh 5M au kufungwa gerezani kwa miezi 12 au vyote kwa pamoja kuanzia 1 Julai, 2020

πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½πŸ‘ŠπŸ½πŸ‘ŠπŸ½πŸ‘ŠπŸ½

 
Wakuu heshima kwenu, kuna wakati nlisikia kuna sheria TCRA inatulazimu kuwa na ulazima wa kumiliki line moja kwa kila mtandao na mwisho ni tareh 30 Juni, 2020, hii imekaaje? Tutafungiwa laini leo?

Kampuni za simu wanasema mwisho laini nne na wewe unasema mwisho laini moja huku CCM wanataka pesa za kodi laini zitanunuliwa na nani?
 
Kabisa Mkuu sheria za KIPUUZI SANA ambazo zinapunguza mapato ya hayo makampuni na pia kodi ya mapato. Nchi nyingi duniani hazina sheria za KIJINGA kama hizi.
South Africa anayesajili laini ni Mgeni tu mwenyeji hana limiti ya kuwa laini hata akitaka line 100 wao wanaangalia mapato tu Serikali ikusanye kodi
 
Hata kama ni njia ya ku boost wateja "NYUMBANI KUMENOGA" sio kwa njia hii walahi.
Serikali ya CCM imejaa washauri wasiojua umuhimu wa pato la Taifa wanakosa pesa nyingi kwenye ununuzi wa line, kwani line nyingi huongeza mapato na pia wenye photocopy hupata pesa wenye viwanda vya karatasi huuza zaidi na Serikali kujipatia kodi
 
Mshauri mkuu wa mtukufu ni NΓ‘ibu Rais ndugu Daud Bashite asiye na vyeti anzia hapo ndipo uendelee
 
Hivi hawa TCRA hawajaona changamoto za kutatua katika sekta ya mawasiliano mpaka wanakuja sheria zisizo na mantiki,sehemu kubwa ya nchi mawasiliano ya simu bado ni dhaifu Sana au hakuna kabisa.
Hayo Ndio mambo ya kushughulikia.

Hii sheria ni ya kisoshalist na kiimla zaidi,ni sawa na kuniambia nisimiliki magari mawili aina ya Toyota.
 
Serikali ya CCM imejaa washauri wasiojua umuhimu wa pato la Taifa wanakosa pesa nyingi kwenye ununuzi wa line, kwani line nyingi huongeza mapato na pia wenye photocopy hupata pesa wenye viwanda vya karatasi huuza zaidi na Serikali kujipatia kodi
Kabisa washauri wazuri hawahitajiki serikalini maana utaambiwa kwamba umetumwa na mabeberu,wao kila kitu wanachukulia kisiasa tu,sioni tatizo la mtu kumiliki line zaidi ya moja kwenye mtandao mmoja wakati amesajili kihalali kabisa kwa NIDA ID.
 
mi nimetoka kupunguza mzigo wa adhabu kwa kupunguza zile za mitandao ninazo zikumbuka...nyingine nimezifungia huku roho inaniuma ......huu utaratibu unaumiza mnooo
 
kama nisingeona huu uzi ningekuwa nang'aa amcho tu..halafu mwishowe naletewa fine milioni 20...nakufa kwa pressure...nazikwa na manispaa bureeeeeeee
 
Tatizo tu mitanzania ni mitahaira Fulani hivi.kwanini tusiamue wote kuwa na laini moja ya mtandao mmoja tu tutakaouchagua ili mitandao mingine ife ili hao tcra wapate furaha zaidi.
 
Mimi nataka nijaribu sumu kwa kuionja. Nina laini zaidi ya moja kwa tigo na airtel na nimeshindwa kuiacha moja bila shuruti.
Mkiona sionekani jukwaani mjue tayari.
[emoji1787][emoji28][emoji38][emoji16] nami nafuata nyayo zako.
 
Hebu Wakuu watumie common sense, mimi nina laini mbili za airtel, Voda na tigo...laini moja natumia kwenye simu na moja ya kutumia kwenye modem...itawezekana vipi nikitaka kutumia modem nitoe laini kwenye simu na isababishe nisiwepo hewani siku nzima?.

Wakumbuke hii mitandao haiko stable kwenye suala la network, kuna wakati unanunua bando la airtel unakuta network iipo slow inabidi ujaribu tigo au voda...kwa maana hiyo ni kwamba Mtu unalazimika kuwa na laini mbili walau kwa kila mtandao ili usikwamishwe shughuli zako kwa kutegemea network ya mtandao mmoja.

Kwa nini TCRA wasianze kuziwajibisha kampuni hizi za huduma iwapo nitanunua kifurushi na sijakitumia basi nirudishiwe pesa zangu...maana nalazimika kununua tena kifurushi kwenye mtandao mwingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…