Ukimsikiliza vizuri Lt Urio hii kesi ya Mbowe ilipaswa kuwa ya Uhaini siyo Ugaidi. Urio aliombwa kusaidia CHADEMA kutwaa madaraka Wananchi wasiteseke

Ukimsikiliza vizuri Lt Urio hii kesi ya Mbowe ilipaswa kuwa ya Uhaini siyo Ugaidi. Urio aliombwa kusaidia CHADEMA kutwaa madaraka Wananchi wasiteseke

... hizo ni hadithi za Kingai na wajinga wenzie; doen't reflect reality. Kama vipi baada ya kesi kutupwa (maana inaenda kutupwa), wawakamate tena hapo hapo nje ya mahakama na kuwafungulia hiyo ya uhaini.
Labda wamkamate Urio maana Mbowe ushahidi unagoma!
 
Kwa hiyo Mbowe, alitaka kuipindua Nchi hii, kwa kusaidiwa na huyo Urio?

Hivi, hata Mzee Mgaya anaamini hivyo? Ndugu zangu, tusiwe tunajiumiza vichwa kwa kuwaza mambo ambayo, hata nafsini mwetu hatuamini kuwa yanawezekana!
Alitaka kupindua nchi kwa kukata miti na kulipua vituo vya mafuta 😆
 
Kama utafuatilia kwa makini maelezo ya lt Urio utagundua kesi hii ya Mbowe na makomandoo wa JWTZ ( wastaafu) ilipaswa kuwa ya Uhaini siyo Ugaidi.

Kutwaa madaraka kinyume cha katiba ya JMT kwa kutumia wanajeshi ni uhaini.

Urio anakiri Mbowe aliomba msaada wake ili CHADEMA itwae madaraka wananchi wasiendelee kuishi kwa mateso na unyonge.

Mungu wa mbinguni awabariki sana!

Mwambie bosi wako kuwa hii movie alitakiwa kuajiri Director kutoka CIA au MIG16 au MOSSAD. Watu waliotumika hawana uwezo wa kutengeneza script zilizo karibu na ukweli. Actor aliyeandaliwa hana uwezo wa kukariri script wala kupresent sura ya huruma.


1. Hakuna mfano wa nchi duniani iliyopinduliwa kwa kukata miti na kuchoma vituo vya mafuta.

2. Tanzania kabla ya 2020 imewahi kushuhudia haya yafuatayo
A. Miaka 5 bila ongezeko la mishahara kwa wafanyakazi.
B. Mauaji holela, maiti zilikuwa zinaokotwa coco beach, watu walikuwa wanatekwa na wengine kupotea, watu wamepigwa risasi
C.Watu walibomolewa nyumba zao bila fidia
D. Watu walifukuzwa kazini bila utaratibu wala kufuata sheria
E.Watu walinyanganywa fedha zao hata ambazo zilikuwa benki na biashara zao zikafanyiwa robbing hasa wale wa bureau de change
F.TRA walibambikia watu kodi zisizo lipika
G.Chaguzi ziliibiwa
H.Watu walishushwa mishahara kiholela
I. Masoko yalichomwa moto na biashara kuvunjwa
J.Milipuko ya mabomu

Kama vyote hivyo hapo juu havikuwahi kusababisha hata maandamano ni muujiza gani ungetokea ili kuchoma vituo vya mafuta na kukata miti kusababishe nchi kutokutawalika?

3. Tanzania kwa ukubwa wake ili kuuleta taharuki inakuhitaji kufanya jambo litakalo chukua karibu mikoa 16-20 kwa wakati mmoja? Je watu wanne wangeweza vipi kuratibu matukio katika ukubwa huo.

4. Kama kweli Mbowe alitaka kupindua nchi basi watu sahii wa kuwatumia walikuwa wanajeshi waliopo kazini sio wastaafu au waliofukuzwa.

5. Kama Mbowe angelitaka kuchukua nchi asingelimshikisha mtu kama Urio wakati ana ndugu jeshini

6. Kama Mbowe angelitaka kupindua nchi kama unavyosema basi mtu sahii wa kumzuru alikuwa Magu na sio Sabaya sababu Sabaya ni sisiminzi mbugani hana effect yeyote kwenye uongozi au Selikari ya nchi hii. Hivyo kumzuru Sabaya kusengeleta taaruki yeyote ile sio tu nchi bali hata Hai kwenyewe.

Kihistoria mapinduzi yote Afrika yanatokana na jeshi kuchukua madaraka na sio raia.

Kinachoendelea ni kama Selikari wanawafundisha jeshi mbinu za kuchukua nchi. Siku ataingia General mwenye tamaa atatengeneza mapinduzi, yakifaulu anachukua nchi yakishindwa anasingizia upinzani ulitaka kuleta taharuki na kutaka kuchukua nchi.

Mungu atupe uhai wa kuyaona haya yanayopandwa leo yakiota na kuzaa matunda.

Niliwahi kuwaambia hapa kipindi kile watu wanatekwa na kupotea kwamba mbegu hii itaota na mtapata shida sana na kipindi kile aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani kama sikosei alikuwa Mwingulu Nchemba alikuwa anatoa majibu simple kwamba hao watu wapo kwa wapenzi wao au ni wahamiaji haramu toka Ethiopia.

Leo yule aliyemtishia Nape bastola ambaye Waziri alisema sio askari ni mmoja wa ma askari wanaotuhumiwa kwa mauaji na Mwingulu yupo ofisini hajajiuzuru.
 
Urio anapata intelligence informations kuwa Mh.Mbowe anataka kupindua nchi na urio (mwanajeshi wa TPDF)akiwa ni Lt.(officer)anakimbilia kwa DCI(Director of crime investigations)kutoa taarifa hii bila ya urio kupeleka kwa CO wake au MI!!hii kwangu ni kama igizo la tamthiria ,na middle class wa JF wanaona kabisa urio alikua yupo right kufanya alichokifanya!mimi ningekua ni Chief of Staff wa TPDF leo hii urio angekua ameshavuliwa cheo kile na angekua yupo mahakama ya kijeshi kujibia hili kwanza.
Kuna swali aliulizwa kuwa anajua jeshini kipo kitengo cha Military Intelligence akasema hajui.

Jamaa ni very incompetent and inept.

Kama Mbowe angekua na plan hizo sidhani kwa utawala ule wa kishenzi angekua yuko hai hadi sasa !
 
Kama utafuatilia kwa makini maelezo ya lt Urio utagundua kesi hii ya Mbowe na makomandoo wa JWTZ ( wastaafu) ilipaswa kuwa ya Uhaini siyo Ugaidi.

Kutwaa madaraka kinyume cha katiba ya JMT kwa kutumia wanajeshi ni uhaini.

Urio anakiri Mbowe aliomba msaada wake ili CHADEMA itwae madaraka wananchi wasiendelee kuishi kwa mateso na unyonge.

Mungu wa mbinguni awabariki sana!
Kabla ya informer Luteni Urio kupeleka taarifa za ugaidi tarehe 18/7/2020, tayari Kingai na kundi lake wameshafungua kesi ya ugaidi mapema tarehe 18/7/2020. Nadhani walioteshwa kutakuwa na taarifa za ugaidi kabla Luteni Urio hajapeleka taarifa zake!

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kabla ya informer Luteni Urio kupeleka taarifa za ugaidi tarehe 18/7/2020, tayari Kingai na kundi lake wameshafungua kesi ya ugaidi mapema tarehe 18/7/2020. Nadhani walioteshwa kutakuwa na taarifa za ugaidi kabla Luteni Urio hajapeleka taarifa zake!

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Nimekuelewa bwashee!
 
Hawa sio Wana CCM, watakuwa ni police hao.

Wawakili jihadharini
20220130_101433.jpg
 
Najikuta nashikwa na hasira eti makomandoo 3 au 4 dhidi ya maelfu ya askari mahiri wa JWTZ na wengine ... Halafu dunia nzima iamini
Kwani ugaidi haiwezi kufanywa na makomandoo wa 3 au 4? Hao ni wengi Sana hata gaidi mmoja anaweza kuleta madhara makubwa Sana kwa jamii.
Ndo maana mbowe kashitakiwa kwa ugaidi na siyo uhaini.
 
Kama umewasikiliza kwa makini mashahidi wawili muhimu sana kwenye kesi ya Freeman Mbowe na makomandoo ambao ni Urio na Swilla utagundua makomandoo hawana makosa wala hawajatenda kosa lolote

Na hata Freeman Mbowe haonekani kama aliwatumia makomandoo kutaka kuvunja sheria za nchi zaidi ya kupatiwa ulinzi.

Tulipofikia ni pagumu sana kuamua Mbowe ana kesi ya kujibu kwa sababu connection kwa watuhumiwa wote wanne kuwa na mpango mmoja imeshindikana kujithibitisha.

Maendeleo hayana vyama.

Mungu wa mbinguni awabariki nyote!

RIP wakili msomi Sengodo Mvungi PhD.
 
Kama umewasikiliza kwa makini mashahidi wawili muhimu sana kwenye kesi ya Freeman Mbowe na makomandoo ambao ni Urio na Swilla utagundua makomandoo hawana makosa wala hawajatenda kosa lolote...
Bado unaendelea kusikiliza hayo maigizo

Aliyepanga Script hajasomea Sanaa ya uigizaji

Pale udsm kuna watu wanasoma haya mambo ya uigizaji lakini bado wakitengeneza movie utashangaa jambazi anavua viatu mlangoni na kujifuta vumbi ili aingie ndani

Mashahidi wote kila kitu wanasema sijui mara aulizwe Afande Kingai

Kila shahidi anasema Yeye aliambiwa tu acheze movie lakini aulizwe Afande kingai

Sasa kama kila mcheza movie anakili kuwa hakusoma script vizuri bali aulizwe aliyeandaa script kuna mafanikio hapo

Mashahidi wamejichanganya sana mpaka unaona aibu

Denis Urio aliamua kuanza kucheka cheka mwenyewe

Na Afande Swill akaamua kila wakati kwenda kusoma script chooni na baadae akaanza kuongea peke yake maneno yasiyoeleweka kama mchawi hivi

Ilifika sehemu wakili wa serikali anamuambia shahidi ajilegeze ajifanye anaumwa ili kukimbia maswali anayoulizwa kizimbani

Mahakama imejishushia heshima sana,

Hao wanaosoma sheria Vyuoni si Waache kusoma tu maana wakubwa zao wanashiriki kuandaa script Halafu waigizaji wanaenda tofauti na walichoambiwa mazoezini

Mtu anajifanya anaumwa huyo shahidi mkuu Afande Swilla mnapata weekend nzima ya ku edit script lakini bado anajichanganya

Tanzania sasa watu wamegawanyika sana kuna kundi linalofurahia vifo vya viongozi na ni kundi kubwa sana na kuna kundi ambalo ni la wanafiki wao wanasifia viongozi kwa ajili ya kupata shibe na vyeo lakini nao wakubwa wao wakifariki hufurahia na kuungana na kundi la awali
 
Bwashee kama baraka zikitoka ktk ule mhimili uliojichimbia chin zaid,kila kitu kinawezekana kutokea
Kama umewasikiliza kwa makini mashahidi wawili muhimu sana kwenye kesi ya Freeman Mbowe na makomandoo ambao ni Urio na Swilla utagundua makomandoo hawana makosa wala hawajatenda kosa lolote..
 
Kama umewasikiliza kwa makini mashahidi wawili muhimu sana kwenye kesi ya Freeman Mbowe na makomandoo ambao ni Urio na Swilla utagundua makomandoo hawana makosa wala hawajatenda kosa lolote...
Kada wa lumumba leo utakua umepata kifafa cha kula mdudu roast,sio maneno yng ni yule dk wa kihindi nilimsikia anasema[emoji16]
 
Lakini Tangu Mwanzo si walielezwa kwamba wawaachie bila masharti ? Tatizo lilikuwa wapi kuwakamata bila kujiridhisha huku wakijipambanua kwamba wanaushahidi wa uhakika na safari hii hachomoki?
 
Chifu Hangaya na Sirro wanajisikiaje kwa ushahidi huu uliowasilishwa mahakamani
 
Tutakochoduwaa ni kwamba watuhumiwa wote watakuwa na kesi ya kujibu..
 
Back
Top Bottom