Wanabodi,
Hili ni bandiko la swali la kuzungumzia uwezo wa wanawake kwenye lile "jambo letu lile", (naomba nisiliseme), ukimuondoa Rais Samia, kama ni lazima awe ni mwanamke, then mwanamke mwingine ni Dr.
Tulia Akson Mwansasu, ameonyesha uwezo, analiweza lile "jambo letu" hivyo kwenye bandiko hili nauliza, je tumchagize kwenye lile "jambo letu", kwasababu ambazo ziko obviously au tuache tuu mambo yaende hivyo hivyo yanavyopaswa kwenda, kama maji kufuata mkondo, kwa kuachia ule utaratibu wa kawaida wa mserereko hata kama ni bora liende, liende tuu?.
Angalizo: JF ni ukumbi wa wote, watoto, vijana, wakubwa na wazee, mimi ni mwandishi wa habari wa wote, nawaandikia watoto, vijana, wakubwa na wazee, ila pia kuna baadhi ya hoja ni za kikubwa, kwanza huwa zinapanda muda watoto wamelala hivyo huwa nawaandikia , wakubwa tuu na sio watoto, hivyo hili sio bandiko la watoto.
Namna ya kujipima kama wewe ni.mkubwa ama mtoto, ni ukijiona umesoma pale nilipoandika "jambo letu" ukijiona wewe unajiuliza hilo "jambo letu" ni jambo gani, basi ujijue tuu hili bandiko sio zaizi yako, okoa tuu muda wako, jiendee mabandiko mengine ya saizi yako.
Hapa ninauzungumzia huo uwezo mkubwa wa Dr. Tulia alionao na aliouonyesha hapo juzi kati, ni upi, kauonyeshea wapi na ana fiti vipi kwa lile "jambo letu lile"?.
Kwanini Dr. Tulia auonyeshee uwezo wake huo kule badala ya hapa nyumbani wakati ni jukumu la mhimili wake kuisimamia serikali yetu!, Je tumshinikize kwa Bunge letu kwanza li do the right thing, kuitekeleza ile hukumu ya Mahakama ya Rufaa, kuhusu ubatili wa katiba yetu na ubatili wa sheria zetu?, kwanini Bunge letu liendelee kututungia sheria batili zinazokwenda kinyume na katiba?.
Kitendo cha kumpa Rais wetu kuzisaini sheria batili kinyume cha katiba, kutakuja kutokea wabunge makini ambao watahitaji Ibara ya 46A ya katiba yetu itekelezwe, kwanini huu mhimili wetu wa Bunge utufanyie hivi wakati mhimili huu uko chini ya Mwanasheria nguli, mbobezi na mbobevu?.
Endelea kufuatana nami mdogo mdogo. ambapo Rais Samia japo anaitwa Mama, kwa umri wangu mimi ni Dada (mimi ni wa 60s) na Dr. Tulia, ni mdogo kwangu, hivyo mimi nawaita ni madada wawili, mtu na dada mtu, au mtu na dada yake, mmoja ni Dada Mkubwa , mwingine ni Dada Mdogo.
Mhimili Mkuu kabisa ni Serikali unaongozwa na Dada Mkubwa, mhimili wa pili kwa ukubwa ni Bunge, unaongozwa na Dada mdogo, tena almanusa na ule mhimili wa tatu, kama tusingepindisha katiba, CJ aendelee kinyume cha katiba, kwenye hierarchy ya mhimili ile, the most senior ilikuwa aingie Mwanamke!, hivyo tungekuwa chini ya madada watatu, "Three Sisters".
Kuhusu jambo letu, kwa vile mada ni kumhusu Dada Mdogo na uwezo wake kwenye lile jambo letu, sio vibaya nikiendelea kusisitiza kuwa hakuna ubishi kuhusu uwezo wa Dada Mkubwa, tena wengi walimjua baada ya kukabidhiwa lile jambo baada ya lile tukio, lakini angalia akina sisi, tulianza nae wapi, au tulianza nae lini.
Dada Mkubwa tulimspoti tangu 2010
New Cabinet: Baadhi ya Majina ni Haya Hapa!
Kuna wengi wamemjua Dada Mkubwa baada ya kuwa..., hapa najikumbusha watu walimpoti lini na wakasema nini kuhusu 2025, tangu 2010, fifteen years back!.
Mtu kama huyu, leo anapomsifia Dada Mkubwa, mtu kumuita, chawa sio kumtendea haki!, ni sawa tuu na kama kumtukana!.
Wanabodi, hili ni bandiko la 2015, 9 years back, watu tulizungumzia jambo letu kumhusu Dada Mkubwa na tulisema kitu kuhusu 2025 ambacho ni cha kweli na huo ndio ukweli wenyewe.
Tulipoanza kulizungumzia jambo letu enzi zile na kujadili possibility ya mwanamke kuwa, aliyeibuka kinana ni Dada Mkubwa
Siku ya Wanawake Duniani: Je, tuna Wanawake wenye sifa za Presidential Material? tulisema
Wanabodi, hili ni bandiko la 2015, 9 years back, watu tulizungumzia jambo letu kumhusu Dada Mkubwa na tulisema kitu kuhusu 2025 ambacho ni cha kweli na huo ndio ukweli wenyewe.
Yule Mwamba alipoingia (Blaza Wangu), tulimlaumu kuteua wanaume zaidi kwa hoja kuwa wanawake hawatoshi
Tuacheni Kumlaumu Rais Kuteua Wanaume, TZ Hatuna Wanawake Wenye Sifa na Vigezo vya Kuteuliwa! ila ukweli sio kweli kuwa wanawake hawatoshi, bali ni tatizo la mfumo dume ulioota mizizi kwenye jamii nyingi za kiasili za Kiafrika.
Paskali.