Ukioa Kilimanjaro unakuwa ni sawa na umeolewa wewe, kila mwisho wa mwaka unatakiwa kwenda Moshi sherehe za mwisho wa mwaka

Ukioa Kilimanjaro unakuwa ni sawa na umeolewa wewe, kila mwisho wa mwaka unatakiwa kwenda Moshi sherehe za mwisho wa mwaka

Mchaga yupi? Kuna wamachame, warombo, wamarangu, wauru, wakibosho, waoldmoshi na wote hao wanalugha zao hawasikilizani kabisa. Ndugu zangu wameoa wamachame na wamarangu na bado wanaenda huko na kulala kwa wakwe! Au wewe unasema mambo ya mwaka 47?

Ndio maana nimesema "jamii nyingi za wachaga" nikimaanisha huenda sio wote. Ukiona mwanamke anabeba familia pamoja na mume kuwapeleka uchagani ujue hapo kuna mawili
1. Kuna tukio labda wameandaa kama vile ubarikio wa watoto na wamekubaliana wakafanyie huko. Wengi wanaofanya hivi hua wamewekeza kule kwa maana ya kujenga nyumba ya kufikia kipindi cha sikukuu maana hawawezi kulala kwenye nyumba ya baba mkwe.
2. Labda mwanaume mwenyewe aamue kwenda kule katika hali ya kubadilisha mazingira na kupumzika. Watu wengi hata wasio wachaga hua wanaenda kilimanjaro kipindi hiki kupumzika tu na kula bata kwani kunakuaga na "vibe" kama lote, hali ya hewa nzuri nk
3. Sikatai kwamba inawezekana kuna wanaume wanaoburuzwa kupelekwa kule bila ridhaa yao hasa pale unapokuta mama ndio ana sauti kwenye nyumba.
 
Ndoa ndoano wacha waende kutambika na wake zao, wakabadilishe mizimu
 
Mleta mada unaonekana hujui chochote kuhusu mila za wachaga. Katika jamii nyingi za wachaga, mwanamke akishaolewa haruhusiwi tena kurudi na kulala nyumbani kwao unless kuwe na tatizo kubwa kama msiba ndio ataweza kulala. Mwanamke anaeweza kurudi uchagani na kulala ni yule ambae hajaolewa. Kwahiyo hao unaoona wakienda uchagani ni wanaume wa kichaga ambao aidha wameoa wachaga wenzao au wameoa makabila mengine. Kamwe mwanamke wa kichaga hawezi kumchukua mume wake halafu akamlaze kwa baba mkwe uchagani maana yeye mwanamke haruhusiwi kulala huko!
Sio kweli mwanamke aliyeolewa asielala kwao ni yule aliyeolewa maeneo ya jirani na kwao ila kama umeolewa mbali na hapo waweza lala hata mwezi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mara nyingine vizuri ukaficha ulicho nacho kichwani, pita hivi. Unakichwa kigumu huelewi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unajisema au? Kuna neno kuapa unamweleza mtu apa! Kuna neno watu hutamka apa wakati neno sahihi ni hapa (hapa mahala ni kuchafu). Nakereka na mtu kuondoa h katika baadhi ya maneno siku hizi mfano ivo baadala ya hivyo, ivi baadala ya hivi etc
 
Mwanaume ukioa Moshi/Kilimanjaro unakua tu ni sawa umeolewa maana kila mwisho wa mwaka wakwe na mashemeji wanaporudi kwao kwa ajili ya sikukuu na wewe utakua unalazimishwa kwenda.

Nina ndugu zangu 4 wameoa Kilimanjaro, wafanyakazi wenzangu na marafiki zangu na watu wengine ninaowafahamu ambao sio wenyeji wa Kilimanjaro ila kila inapofika mwisho wa mwaka lazima waende huko.

Hata Pascal Mayala amesema yeye kila mwisho wa mwaka huenda Moshi wakati ni Msukuma wa Kanda ya Ziwa.

Ukioa Moshi ni kama umeolewa wewe maana utapelekeshwa kama mbuzi.

Anyway, haya ni maoni yangu na mtazamo wangu, sio lazima uyapende.
Hayo ni mawazo yako potofu mbona mimi nimealika wafanyakazi wenzangu niko nao huku saa hivi tunakula bata ina maana nimewaoa?
 
Mwanaume ukioa Moshi/Kilimanjaro unakua tu ni sawa umeolewa maana kila mwisho wa mwaka wakwe na mashemeji wanaporudi kwao kwa ajili ya sikukuu na wewe utakua unalazimishwa kwenda.

Nina ndugu zangu 4 wameoa Kilimanjaro, wafanyakazi wenzangu na marafiki zangu na watu wengine ninaowafahamu ambao sio wenyeji wa Kilimanjaro ila kila inapofika mwisho wa mwaka lazima waende huko.

Hata Pascal Mayala amesema yeye kila mwisho wa mwaka huenda Moshi wakati ni Msukuma wa Kanda ya Ziwa.

Ukioa Moshi ni kama umeolewa wewe maana utapelekeshwa kama mbuzi.

Anyway, haya ni maoni yangu na mtazamo wangu, sio lazima uyapende.
Kwahiyo naww unahesabiwa au

Sent using Jamii Forums mobile app
 
we n mchaga au upo tu uchagani
Mleta mada unaonekana hujui chochote kuhusu mila za wachaga. Katika jamii nyingi za wachaga, mwanamke akishaolewa haruhusiwi tena kurudi na kulala nyumbani kwao unless kuwe na tatizo kubwa kama msiba ndio ataweza kulala. Mwanamke anaeweza kurudi uchagani na kulala ni yule ambae hajaolewa. Kwahiyo hao unaoona wakienda uchagani ni wanaume wa kichaga ambao aidha wameoa wachaga wenzao au wameoa makabila mengine. Kamwe mwanamke wa kichaga hawezi kumchukua mume wake halafu akamlaze kwa baba mkwe uchagani maana yeye mwanamke haruhusiwi kulala huko!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nna ndoa ya 14yrs na mtoto mzuri wa kichaga lkn sijawahi kwenda huko. Ni uamuzi binafsi na si kulazimishwa
 
Back
Top Bottom