Ukiona daktari wakati wa kukutibu anababaika babaika na anatumia google, mheshimu sana

Field ya afya/medicine ni pana saana.
Huwezi kuweka kila kitu kichwani kwako. Ni kweli kufanya reference ni kitu cha busara sana, ingawa wagonjwa wengi huona kama daktari ni mbabaifu.

Katika kujua tatizo la mgonjwa kuna hatia nyingi:
1: Historia
2: Ukaguzi/kuona na kushika
3: Mtizamo/mwelekeo wa daktari kuhusu aina ya ugonjwa.
3: Vipimo
4: Ugonjwa kubainika au hitaji la bipimo zaidi.
5: Dawa au rufaa ya vipimo zaidi au tiba ya hali ya juu zaidi.
6: Ushauri wa tiba husika

Kwa magonjwa mengi, ukimaliza namba mbili ni muhimu kuwa na uelekeo wa ni kinachomsibu mgonjwa(75%). Ingawa wakati mwingine matatizo hujulikana kwenye namba moja (kulingana na aina ya tatizo).

Hivyo kupima au kutokupima hutokana na asili ya tatizo au kama matatizo yanayofanana yanaelekea kuwepo au tatizo husika ni la lazima kuthibitishwa kwa kipimo, si lazima mtu kupimwa.

Pia, kufanya reference hutegemea na ni nini hasa mtu anakitafuta. Huwezi kumhukumu bila kujua anatafuta nini hasa na kwenye hatua gani katika zile sita.

NB: Referencing ni moja ya njia ya kupunguza errors/makosa kama aina ya dawa, dozi, athari ya dawa, muingiliano wa madhira ya dawa etc.
 
You might be right anyway but not always!
 
Mwanzo nami nilikua naona ni ubabaifu, lakini kimsingi ni sawa kwa sababu tiba zinabadilika, kila uchwao mambo yanabadilika. Na ukizangatia sisi hatuna medical scientists.
Changamoto tu nyingine ni kwamba madaktari wetu hawasomi. Mtu akimaliza amemaliza. Kuna fani kusoma ni endelevu sio option, ni lazima until they day you are buried.
 
Bora akuambie ukapime kuliko ku-google kila kitu,

Ndugu yangu kwa ujinga Kama huu wamemsabibishia Matatizo Makubwa Sana mpaka leo he can't walk anymore
Hakuna mtaalamu wa kugoogle kila kitu. Huo ni uongo bana.
 
Sioni umuhimu wa daktari ili Hali kila ukienda kumuona tuu unalipia alaf anakuelekeza uende maabara , nafkr watu wa maabara wanatakiwa waheshimiwe zaid, unaweza enda Kwa mtaalamu wa maabara ukamwelezea dalili na yeye akakupima mkaona ugonjwa ukasepa Kwa Kwa mtu wa pharmacy ukachora home ..... Madaktari wawe ambao ni specialized, Kwa magonjwa complicated
 
Na kama darasan alikuw kunjanja anaweza google na bado akaenda chaka. Google n pana sana na inakupa unachotaka wew sio kinachostahili over
 
Napinga unaposema ," Daktari mwenye kubabaika ndie mwenye shule"/Elimu kuzidi yule anaejiamini.

Kawaida kabisa mtu anapopata elimu zaidi ndiyo anazidi kujiamini. Na anapunguza kubabaika/Wasiwasi.
 
Madaktari wanafunzi wako bize wanabet na kucheza pc,pepa zikianza wanatafuta vijiji.
 
Mkuu naona upo sahihi,hata uko kuingia google ni ishara ya uelewa,maana anajua nini anakitafuta.
Kuna dokta mmoja alinisaidia pale tumbi kibaha nilipeleka mdogo wangu alikuwa anaumwa kidole,
alifanya hivyo unavyosema,mpaka akamwita na mwenzake,wakajadili wakashauri tofauti na daktari aliyetupeleka kule kwamba afanyiwe operation. Wakatuandikia dawa,na baada ya mdogo wangu kutumia hiyo dawa akaendelea vizuri.
Heshima kwako daktari kama upo humu na umesoma ujumbe huu.
 
Tatizo tunaloweza kuwa bado tunalo sasa hivi labda ni uhaba wa madakatari ila si ujuzi wa madaktari.

Sasa hivi tunao madaktari ambao baadhi ya kazi wanazofanya hadi zinatia shaka kama zimefanywa kwa mkono wa mwanadamu; mtu unaweza ukadhani labda ni malaika walishuka kutoka mbinguni wakafanya kazi hizo
 
Na maabara kazi yake nini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…