ni kitu cha ajabu, kwamba mwanamke akikamatika kwenye shida kabisa, hata kama ni mke wa mtu, huwa yupo tayari kutoa mwili wake alimradi tu apate, iwe pesa, cheo au kazi. kuna mdada mfanyakazi, na tulimchangia pesa za arusi miezi minne iliyopita (though walikuwa wanabariki), leo kaja kwangu akapiga story akaondoka. baada ya dakika kama 10 ananiandikia msg anasema anaomba pesa akasukie. of course alipokuwa ofisini kwangu, nilikuwa najisikia vibaya kwasababu alikuwa anapoteza muda tu hana la maana alilokujia, na nikajua shetani anataka kuweka mtego kwangu.
kwanza nimejiuliza, nifanyeje, nikajua huyu ana shida ya pesa na amekamatika kwelikweli, pesa ya kusukia tu ninayo, ningeweza kumpa, lakini ana mume, mumewe akimuuliza umetoa wapi pesa ya kusukia atasema katoa wapi? na je, mimi ningekubali mwanaume mwingine ampe mke wangu pesa akasukie? Inawezekana mume wake hana hiyo pesa wiki hii na nywele zake anaona zinahitaji kusukwa ila je? nisemne hiyo ni necessary service kwenye maisha kwamba akikosa kusuka wakati anajipanga kutafuta maisha ataathirika? na ni mdada mzuri tu hata akinyoa atapendeza tu? nikafikia muafaka kwamba, sitampa pesa na nitampiga marufuku kuniomba pesa au kuwa karibu na mimi.
maishani, kabla sijamjua Mungu, nilikuwa dhaifu sana kwa wanawake. nilijifunza na kuhakikisha kwamba ni kweli, dawa ya uzinzi ni kufukia mashimo yote yanayoweza kupitisha uwezekano wa kuzini, hata ikibidi kimbia kwa miguu au kubali kugombana na mtu akuone humtaki alimradi tu usizini, kwasababu ukikaribia shina la uzinzi, utazini kweli na hakuna uzinzi ambao haujawahi kumsababishia mtu madhara, iwe kiroho au kimwili. hata ukiona kimwili upo safi tu jua kiroho kuna kitu kikubwa umepoteza. Mungu atusaidie sote.