Aman Ng'oma
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 961
- 533
Ufugaji wa kuku Tanzania kwa sasa umeshika kasi, watu wameelimishwa wakaufahamu ufugaji huo. Ufugaji wa kuku unaofanywa ni wa aina mbalimbali kuna wanaofuga kuku wa nyama broilers, kuku wa mayai wa kisasa layers, machotara crossbreeds na hata wale wanaofuga kuku wa kienyeji kwa ajili ya mayai na nyama. Kuna wengine pia wanajihusisha na miradi ya utotoreshaji wa vifaranga wakati wengine wakiwa wanafuga kware, Bata mzinga, Kanga nk ili mradi tu kila mtu anafuga kile anachotaka.
Katika mjadala huu nimeona niwatembeze katika miradi mbalimbali ya wafugaji, tuone ufugaji wao mabanda yao, mifugo yao nk ili kupitia kuona huko, naamini kuna kitu tunaweza kujifunza lakini pia kupata hamasa ya kufuga na hivyo kujikwamua kiichumi na kuweza kuondokana na dhana ya kutegemea kuajiriwa.
Lakini pia kupitia mada hii kama utahitaji kuku wa aina yoyote au mazao yake kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii, mahoteli, migahawa nk utapata kwa bei nafuu kabisa. Vilevile tunauza vifaranga wa kware na mayai yake kwa idadi yoyote utakayoihitaji. Kwa mahitaji yako basi usisite kuwasiliana nami na kama ukihitaji namba yangu nitakupm tafadhali. Kwanini tulalamike hakuna kazi wakati kuna fursa za kutosha nchini. Tafakari chukua hatua, umasikini haukubaliki.
Picha chini ni kuku wa nyama aina ya Kenbro wakiwa tayari kwenda sokoni.

Katika mjadala huu nimeona niwatembeze katika miradi mbalimbali ya wafugaji, tuone ufugaji wao mabanda yao, mifugo yao nk ili kupitia kuona huko, naamini kuna kitu tunaweza kujifunza lakini pia kupata hamasa ya kufuga na hivyo kujikwamua kiichumi na kuweza kuondokana na dhana ya kutegemea kuajiriwa.
Lakini pia kupitia mada hii kama utahitaji kuku wa aina yoyote au mazao yake kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii, mahoteli, migahawa nk utapata kwa bei nafuu kabisa. Vilevile tunauza vifaranga wa kware na mayai yake kwa idadi yoyote utakayoihitaji. Kwa mahitaji yako basi usisite kuwasiliana nami na kama ukihitaji namba yangu nitakupm tafadhali. Kwanini tulalamike hakuna kazi wakati kuna fursa za kutosha nchini. Tafakari chukua hatua, umasikini haukubaliki.
Picha chini ni kuku wa nyama aina ya Kenbro wakiwa tayari kwenda sokoni.




