Ukiona wenzako wanavyofanya ufugaji wa kuku, Mabanda yao walivyojenga, kwa hakika hutaacha kufuga

Ukiona wenzako wanavyofanya ufugaji wa kuku, Mabanda yao walivyojenga, kwa hakika hutaacha kufuga

Mkuu nakuaminia broiler wako wazuri sana. Hawa vijogoo wanapanda I mean wanafaa kwa mbegu au ndo kula tu? Max uzito wao kiasi gani? Na umri gani wanauzwa?

Jogoo yeyote anapanda,hawa pia wanapanda kama kawaida,kuuzwa as kama utawafuga kienyeji ni kuanzia 13 weeks,but wanakuwa majogoo makubwa sanaaaaaaaa
 
Thanks nimekupata mkuu nitakutafuta mie napenda vitu unique ili kuwa na brand tofauti. Nitakujulisha lini nikiwa tayari

Jembe langu mama Joe aminia sana,kwanza napenda tunavyofanya business though hatujawahi onana,hope soon wale broiler utauza,kama wakifikisha kilo 1.4,nitakuja kuwanunua if possible.
 
Ufugaji wa kuku Tanzania kwa sasa umeshika kasi, watu wameelimishwa wakaufahamu ufugaji huo. Ufugaji wa kuku unaofanywa ni wa aina mbalimbali kuna wanaofuga kuku wa nyama broilers, kuku wa mayai wa kisasa layers, machotara crossbreeds na hata wale wanaofuga kuku wa kienyeji kwa ajili ya mayai na nyama. Kuna wengine pia wanajihusisha na miradi ya utotoreshaji wa vifaranga wakati wengine wakiwa wanafuga kware, Bata mzinga, Kanga nk ili mradi tu kila mtu anafuga kile anachotaka.

Katika mjadala huu nimeona niwatembeze katika miradi mbalimbali ya wafugaji, tuone ufugaji wao mabanda yao, mifugo yao nk ili kupitia kuona huko, naamini kuna kitu tunaweza kujifunza lakini pia kupata hamasa ya kufuga na hivyo kujikwamua kiichumi na kuweza kuondokana na dhana ya kutegemea kuajiriwa.


Lakini pia kupitia mada hii kama utahitaji kuku wa aina yoyote au mazao yake kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kijamii, mahoteli, migahawa nk utapata kwa bei nafuu kabisa. Vilevile tunauza vifaranga wa kware na mayai yake kwa idadi yoyote utakayoihitaji. Kwa mahitaji yako basi usisite kuwasiliana nami na kama ukihitaji namba yangu nitakupm tafadhali. Kwanini tulalamike hakuna kazi wakati kuna fursa za kutosha nchini. Tafakari chukua hatua, umasikini haukubaliki.

Picha chini ni kuku wa nyama aina ya Kenbro wakiwa tayari kwenda sokoni.

View attachment 217763 View attachment 217766 View attachment 217767 View attachment 217769 View attachment 217770

mkuu mi nahitaji kware, tafadhali ni Pm namba yako.
 
Hahaaa kweli hatukuonana usijali karibu wana wiki ya tatu wakubwa, nafikiri wiki nne na nusu watapita kg 1 nitakushtua. Karibu sana
Jembe langu mama Joe aminia sana,kwanza napenda tunavyofanya business though hatujawahi onana,hope soon wale broiler utauza,kama wakifikisha kilo 1.4,nitakuja kuwanunua if possible.
 
Mkuu Aman Ng'oma, hizo picha za vifaranga mimi sijaweza kuziona kwa sababu hazifungi. Tafadhali mkuu hebu zifanyie utaratibu ili nazo tuweze kuziona.
 
Last edited by a moderator:
kuku 2.jpg Picha za kuku.jpg

Hii ndiyo kosaafu nzuri ya kuku wa kienyeji, wakubwa kwa umbo, warefu na wenye afya njema kwa mwonekano.

Hawa ni kuku wa aina ya Kuchi ni maarufu sana katika mikoa ya Dodoma, Singida na Tabora.
 
Huu ni uwekezaji katika miradi ya ufugaji wa kuku. Ni fursa kwa matajiri kugeukia katika sekta hii ya ufugaji wa kuku, badala ya kujenga nyumba za kupangisha watu. Ujenzi wa mabanda ya kuku kama ambavyo yaonekanavyo katika picha hapo chini una gharama kubwa ni vigumu kumudu kwa mtu wa kawaida. Unashauriwa, ili kujenga banda bora na vipimo sahihi kutana na mtaalam wa mifugo kwa msaada zaidi.

Serikali pia nadhani inaweza ikawezesha vijana kwa kuwajengea mambanda ya kufugia kisha wakapangishiwa, maana kijana unaweza kufikiria kufuga na mtaji wako mdogo lakini kikwazo kikawa kwenye pesa ya uwekezaji katika ujenzi wa mabanda.

Banda la kuku 14.jpg Banda la kuku 14.jpg Banda la kuku 15.jpg
 
Nimevutiwa sana na haya mabanda...niko ktk mkakati wa kuanza kilimo cha mifugo...ningependa kupata ushauri zaidi juu ya ujenzi wa mabanda bora ya kuku...eneo ninalo la kutosha.
 
Nayaona mabanda yangu katika hatua za awali.. sasa yameongezeka.. hakuna kitu kizuri kulisha nchi tena si bure unalipwa
 
Samahani dada mim namewapenda sana je wanahitaji nafasi gani kuwafuga?Pili unaweza ukaanza na mtaji wa kiasi gn nimetamani sana.
 
Dada nimefurahia sana sasa nitakupataje?Nataka maelezo zaidi je hawo kuku kwa huku Dar wanapatikan wapi?Na je wauzwa bei gn?lingine chakula chao ni kipi?
 
Inapendeza. Mi ningependa kujua kutoka kwa wazoefu, soko la kuku na mayai linapatikana vipi kwa mtu atayejitosa ktk ufugaji kuku? Natanguliza shukrani.
 
Kwa wanaohitaji ushauri wa ufugaji bora wenye tija wa kuku tuwasiliane kwa namba 0767989713, 0715989713 na 0786989713. Ujenzi wa mabanda bora ya kuku, idadi ya kuku kwa eneo/banda, utambuzi na udhibiti wa magonjwa mbalimbali ya kuku, upatikanaji wa kware na ufugaji wake, upatikanaji wa masoko Tanzania na nje ya nchi karibuni sana kwenye fursa ya uwekezaji katika miradi ya mifugo, kwanini ushindwe wakati wenzako wanaweza?

Njoo tuongee ofisini kwetu Dodoma, maneo ya Chamwino Bonanza mbele kidogo ya soko la maisha plus.
 
Inapendeza. Mi ningependa kujua kutoka kwa wazoefu, soko la kuku na mayai linapatikana vipi kwa mtu atayejitosa ktk ufugaji kuku? Natanguliza shukrani.

Kwa uzoefu wangu ni kwamba Soko la kuku Tanzania ni kubwa lakini changamoto iliyopo ni kuwa chakula cha kuku ni ghali sana ukilinginisha na bei ya mayai. Ushauri wangu kwa wafugaji wa kuku hasa wa mayai kuhakikisha kuwa chakula utakachotengeneza kitengenezwa kwa gharama nafuu ili kupunguza gharama na kujiongezea faida.

Namna ya kupunguza gharama ni pamoja na kununua mahitaji ya kutengenezea chakula cha kuku wakati wa msimu wa mavuno ambapo bei zake huwa ni ndogo.
 
Inapendeza. Mi ningependa kujua kutoka kwa wazoefu, soko la kuku na mayai linapatikana vipi kwa mtu atayejitosa ktk ufugaji kuku? Natanguliza shukrani.

Soko ni kubwa sanaa,though juzi kati lilishuka kidogo,price drop by 35%.But somo is realistic sanaa,usijitose just plan and weka mikakati utafanikiwa tu mkuu
 
Kwa uzoefu wangu ni kwamba Soko la kuku Tanzania ni kubwa lakini changamoto iliyopo ni kuwa chakula cha kuku ni ghali sana ukilinginisha na bei ya mayai. Ushauri wangu kwa wafugaji wa kuku hasa wa mayai kuhakikisha kuwa chakula utakachotengeneza kitengenezwa kwa gharama nafuu ili kupunguza gharama na kujiongezea faida.

Namna ya kupunguza gharama ni pamoja na kununua mahitaji ya kutengenezea chakula cha kuku wakati wa msimu wa mavuno ambapo bei zake huwa ni ndogo.

Mkuu mfano wanaojitengenezea chakula kwa kuku 500,unaweza pata faida kiasi gani,coz my experience ninayo kwenye vyakula vya CP or FALCON .Still napata enough profit
 
Back
Top Bottom