Ukiondoa Ukakasi wa Kauli za RC Chalamila Mnyonge Mnyongeni Ila Haki Yake Mpeni, Waafrika Tunapenda Kulelewa Mpaka Imekuwa Ulemavu

Ukiondoa Ukakasi wa Kauli za RC Chalamila Mnyonge Mnyongeni Ila Haki Yake Mpeni, Waafrika Tunapenda Kulelewa Mpaka Imekuwa Ulemavu

Rorscharch

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
878
Reaction score
2,014
NCHI INAZAMA KWA KUKUMBATIA UJINGA

Je, umewahi kujiuliza kwa nini nchi hii haipigi hatua licha ya kuwa na rasilimali, amani, na nafasi za kujikwamua? Sababu iko wazi: tunakumbatia ujinga na kusambaza mzigo wa maamuzi yetu mabaya kwa wengine.

Mtu anataka kondomu afadhiliwe, akishindwa kuitumia na kupata VVU, anataka dawa za kufubaza ugonjwa zitolewe bure. Akimpa mwanamke mimba, anataka mtoto azaliwe kwa ufadhili wa serikali. Watu hawa ndio wale wale ambao wakifika hospitali kujifungua, hawana hata shilingi 5,000 ya kununua glovu za daktari, lakini wanaamini ni haki yao kupata kila kitu bure. Kwa nini? Kwa sababu wameshawishika kuwa serikali inapaswa kuwajibika kwa kila uamuzi wao mbovu maishani.

Hili suala linafanana kabisa na chuki dhidi ya kauli za RC Chalamila. Yaani mtu amebeba ujauzito bila kuwa na uhakika wa hata shilingi elfu tano ya vifaa vya kujifungulia, halafu anakuja hospitali akiamini kila kitu kitaangukia bure kutoka kwa serikali. Hebu fikiria—ikiwa hata hela ya kondomu siku hiyo haikuwepo, serikali ndiyo ije kubeba mzigo wa mtoto wako? Na kama kweli huna uwezo hata wa kununua glovu, unadhani kweli utakuwa na uwezo wa kumlea huyo mtoto?

Ni mentality hii hii tunayoiona kwa ARV. Mtu anaamua kufanya zinaa bila kinga, akipata UKIMWI anataka matibabu yatolewe bure. Ndio maana mpaka misaada ya Wamarekani inahitajika kulisha taifa linalozaliana bila mpango. Watu milioni 60, lakini wanaochangia mfuko wa bima hawafiki hata milioni 5. Hao wachache ndio wanapaswa kubeba mzigo wa wengine wote? Na bado tunajiita taifa huru!

Tuache unafiki. Hii siyo tena hoja ya CCM au CHADEMA. Ukifukuza CCM na kuleta upinzani, hakuna miujiza itakayofanyika. Historia imetufundisha kuwa mabadiliko hayaji kwa kubadilisha majina ya viongozi, bali kwa kubadili tabia na mtazamo wa jamii. Tanzania ina watu milioni 60, lakini wenye mchango wa moja kwa moja kwenye pato la taifa hawazidi milioni 10. Unadhani nchi yoyote inaweza kuendelea ikiwa idadi kubwa ya watu wake ni mizigo?

Tazama tofauti kati ya Kenya na Switzerland. Miaka ya 1960, nchi hizi zilikuwa na idadi sawa ya watu, lakini leo Kenya ina watu zaidi ya milioni 50, wengi wao wakiishi kwenye umasikini, huku Switzerland ikiwa na milioni 7 wanaoishi maisha mazuri. Unadhani ni kwa bahati mbaya? Hapana. Ni kwa sababu kule watu walitumia akili, huku kwetu wengi wanaamini "Mungu atajalia" huku wakizaliana bila mpango na kutegemea serikali iwahudumie.

Kama hatutabadilika, tusitarajie maendeleo. Tusipokuwa wakweli kwa nafsi zetu, tutaendelea kulalamika huku tukizidi kuzama kwenye lindi la umasikini wa kujitakia.
 
Ndio maana tunalaani uamuzi wa amerika kuwafungia vioo omba omba wenye nguvu akili na mali.
 
Rc Chalamila hajakosea kitu chochote.
Mke wako unampa mimba, anakuwa mja mzito since day one ujue umeingia kwenye majukumu.
Ukienda Clinic siku ya kwanza wanakuhasa kufanya maandalizi pamoja na kuweka hakiba.
Sasa inakuwaje inafika hadi miezi tisa bado mtu analialia eti ameombwa 50000 ya gloves?
Sisi watanzania tunapenda vitu vya bure na kudanganywa danganywa na watawala.
Hakuna kitu cha bure katika mfumo wa ubepari.
Tumeambiwa elimu bure lakini sasa kwa kuwa ni bure amka asubuhi umpeleke mwanao shuleni kawambie amekuja kusoma tu bila vitu vya msingi uone kama utatoboa.
Sisi kama wananchi tufike wakati tuwe na fikra huru, mtu akikwambia hiki ni bure uwaze mara mbili na ujiongeze.
Mimba na mtoto atakayezaliwa ni wako wala siyo wa RC Chalamila.
Kama kakosea ni katika ile hali ya kushindwa kujenga hoja lakini alitaka kuwambia kuwa there's no free lunch.
 
Nimesoma paragraphs 3 tu. Umeandika US3NGE, samahani.

Kodi tunazolipa zina msaada gani? Kuna nchi hapahapa Africa zina free healthcare. Ghana tu wana free maternal healthcare.
 
Rc Chalamila hajakosea kitu chochote.
Mke wako unampa mimba, anakuwa mja mzito since day one ujue umeingia kwenye majukumu.
Ukienda Clinic siku ya kwanza wanakuhasa kufanya maandalizi pamoja na kuweka hakiba.
Sasa inakuwaje inafika hadi miezi tisa bado mtu analialia eti ameombwa 50000 ya gloves?
Sisi watanzania tunapenda vitu vya bure na kudanganywa danganywa na watawala.
Hakuna kitu cha bure katika mfumo wa ubepari.
Tumeambiwa elimu bure lakini sasa kwa kuwa ni bure amka asubuhi umpeleke mwanao shuleni kawambie amekuja kusoma tu bila vitu vya msingi uone kama utatoboa.
Sisi kama wananchi tufike wakati tuwe na fikra huru, mtu akikwambia hiki ni bure uwaze mara mbili na ujiongeze.
Mimba na mtoto atakayezaliwa ni wako wala siyo wa RC Chalamila.
Kama kakosea ni katika ile hali ya kushindwa kujenga hoja lakini alitaka kuwambia kuwa there's no free lunch.
Haswaa
 
You mean unataka tuwajibike na sio kulalamikia wengine for our shortcomings? Hatukubali.

On the other end, watu lazima walalamike wanapoona wanalipa kodi zinaenda kununua V8 kila siku wakati vifaa tiba vya bei ndogo kabisa vinakosekana. Kulikua na ulazima gani wa ku update gari zote za serikali wakati za zamani bado zinafanya kazi? Vipaumbele vimekua vipaunyuma. Wananchi wana haki ya kuhoji matumizi ya kodi zao.
 
So long as tunafanya kazi na kulipa kodi, we deserve health care benefits, mbona wengine wanafanya, au kodi zetu zinaenda wapi?
 
Nimesoma paragraphs 3 tu. Umeandika US3NGE, samahani.

Kodi tunazolipa zina msaada gani, kuna nchi hapahapa Africa zina free healthcare. Ghana tu wana free maternal healthcare.
Nyepesi kwa Ghana kwasababu ina idadi ya Watu wachache zaidi yetu (50% less) na pato la taifa kwa kila mtu (GDP per Capita) ni mara mbili yetu
Kodi mnazokusanya mnauliza zinaenda kufanya nini? Madeni ya mikopo ya kimataifa hayajilipi yenyewe; wote milioni 66 tunahitaji barabara, maji, hospitali, shule, umeme, ajira na kadhalika ila tunachozalisha kwa mkupuo kujustify matumizi hayo yote hakiakisi uhalisia yaani hata tukiondoa ufisadi katika mahesabu bado changamoto bado kubwa sana
 
You mean unataka tuwajibike na sio kulalamikia wengine for our shortcomings? Hatukubali.

On the other end, watu lazima walalamike wanapoona wanalipa kodi zinaenda kununua V8 kila siku wakati vifaa tiba vya bei ndogo kabisa vinakosekana. Kulikua na ulazima gani wa ku update gari zote za serikali wakati za zamani bado zinafanya kazi? Vipaumbele vimekua vipaunyuma. Wananchi wana haki ya kuhoji matumizi ya kodi zao.
Sikatai kwenye hili
 
NCHI INAZAMA KWA KUKUMBATIA UJINGA

Je, umewahi kujiuliza kwa nini nchi hii haipigi hatua licha ya kuwa na rasilimali, amani, na nafasi za kujikwamua? Sababu iko wazi: tunakumbatia ujinga na kusambaza mzigo wa maamuzi yetu mabaya kwa wengine.

Mtu anataka kondomu afadhiliwe, akishindwa kuitumia na kupata VVU, anataka dawa za kufubaza ugonjwa zitolewe bure. Akimpa mwanamke mimba, anataka mtoto azaliwe kwa ufadhili wa serikali. Watu hawa ndio wale wale ambao wakifika hospitali kujifungua, hawana hata shilingi 5,000 ya kununua glovu za daktari, lakini wanaamini ni haki yao kupata kila kitu bure. Kwa nini? Kwa sababu wameshawishika kuwa serikali inapaswa kuwajibika kwa kila uamuzi wao mbovu maishani.

Hili suala linafanana kabisa na chuki dhidi ya kauli za RC Chalamila. Yaani mtu amebeba ujauzito bila kuwa na uhakika wa hata shilingi elfu tano ya vifaa vya kujifungulia, halafu anakuja hospitali akiamini kila kitu kitaangukia bure kutoka kwa serikali. Hebu fikiria—ikiwa hata hela ya kondomu siku hiyo haikuwepo, serikali ndiyo ije kubeba mzigo wa mtoto wako? Na kama kweli huna uwezo hata wa kununua glovu, unadhani kweli utakuwa na uwezo wa kumlea huyo mtoto?

Ni mentality hii hii tunayoiona kwa ARV. Mtu anaamua kufanya zinaa bila kinga, akipata UKIMWI anataka matibabu yatolewe bure. Ndio maana mpaka misaada ya Wamarekani inahitajika kulisha taifa linalozaliana bila mpango. Watu milioni 60, lakini wanaochangia mfuko wa bima hawafiki hata milioni 5. Hao wachache ndio wanapaswa kubeba mzigo wa wengine wote? Na bado tunajiita taifa huru!

Tuache unafiki. Hii siyo tena hoja ya CCM au CHADEMA. Ukifukuza CCM na kuleta upinzani, hakuna miujiza itakayofanyika. Historia imetufundisha kuwa mabadiliko hayaji kwa kubadilisha majina ya viongozi, bali kwa kubadili tabia na mtazamo wa jamii. Tanzania ina watu milioni 60, lakini wenye mchango wa moja kwa moja kwenye pato la taifa hawazidi milioni 10. Unadhani nchi yoyote inaweza kuendelea ikiwa idadi kubwa ya watu wake ni mizigo?

Tazama tofauti kati ya Kenya na Switzerland. Miaka ya 1960, nchi hizi zilikuwa na idadi sawa ya watu, lakini leo Kenya ina watu zaidi ya milioni 50, wengi wao wakiishi kwenye umasikini, huku Switzerland ikiwa na milioni 7 wanaoishi maisha mazuri. Unadhani ni kwa bahati mbaya? Hapana. Ni kwa sababu kule watu walitumia akili, huku kwetu wengi wanaamini "Mungu atajalia" huku wakizaliana bila mpango na kutegemea serikali iwahudumie.

Kama hatutabadilika, tusitarajie maendeleo. Tusipokuwa wakweli kwa nafsi zetu, tutaendelea kulalamika huku tukizidi kuzama kwenye lindi la umasikini wa kujitakia.
Inawezekana kabisa viongozi na wananchi, wote wakawa na makosa.
 
So long as tunafanya kazi na kulipa kodi, we deserve health care benefits, mbona wengine wanafanya, au kodi zetu zinaenda wapi?
Healthcare benefits wanapata waliojiunga na huduma za NHIF, we kodi unayolipa imefanikisha jengo la hospitali na miundombinu yote jumuishi iwepo hapo ilipo; wamekuachia tu mzigo wa kugharamia matibabu yenyewe
 
Nimesoma paragraphs 3 tu. Umeandika US3NGE, samahani.

Kodi tunazolipa zina msaada gani? Kuna nchi hapahapa Africa zina free healthcare. Ghana tu wana free maternal healthcare.
Kodi zinazolipwa bado hazijafikia kiwango cha kutosha cha kutoa kila huduma bure.
 
NCHI INAZAMA KWA KUKUMBATIA UJINGA

Je, umewahi kujiuliza kwa nini nchi hii haipigi hatua licha ya kuwa na rasilimali, amani, na nafasi za kujikwamua? Sababu iko wazi: tunakumbatia ujinga na kusambaza mzigo wa maamuzi yetu mabaya kwa wengine.

Mtu anataka kondomu afadhiliwe, akishindwa kuitumia na kupata VVU, anataka dawa za kufubaza ugonjwa zitolewe bure. Akimpa mwanamke mimba, anataka mtoto azaliwe kwa ufadhili wa serikali. Watu hawa ndio wale wale ambao wakifika hospitali kujifungua, hawana hata shilingi 5,000 ya kununua glovu za daktari, lakini wanaamini ni haki yao kupata kila kitu bure. Kwa nini? Kwa sababu wameshawishika kuwa serikali inapaswa kuwajibika kwa kila uamuzi wao mbovu maishani.

Hili suala linafanana kabisa na chuki dhidi ya kauli za RC Chalamila. Yaani mtu amebeba ujauzito bila kuwa na uhakika wa hata shilingi elfu tano ya vifaa vya kujifungulia, halafu anakuja hospitali akiamini kila kitu kitaangukia bure kutoka kwa serikali. Hebu fikiria—ikiwa hata hela ya kondomu siku hiyo haikuwepo, serikali ndiyo ije kubeba mzigo wa mtoto wako? Na kama kweli huna uwezo hata wa kununua glovu, unadhani kweli utakuwa na uwezo wa kumlea huyo mtoto?

Ni mentality hii hii tunayoiona kwa ARV. Mtu anaamua kufanya zinaa bila kinga, akipata UKIMWI anataka matibabu yatolewe bure. Ndio maana mpaka misaada ya Wamarekani inahitajika kulisha taifa linalozaliana bila mpango. Watu milioni 60, lakini wanaochangia mfuko wa bima hawafiki hata milioni 5. Hao wachache ndio wanapaswa kubeba mzigo wa wengine wote? Na bado tunajiita taifa huru!

Tuache unafiki. Hii siyo tena hoja ya CCM au CHADEMA. Ukifukuza CCM na kuleta upinzani, hakuna miujiza itakayofanyika. Historia imetufundisha kuwa mabadiliko hayaji kwa kubadilisha majina ya viongozi, bali kwa kubadili tabia na mtazamo wa jamii. Tanzania ina watu milioni 60, lakini wenye mchango wa moja kwa moja kwenye pato la taifa hawazidi milioni 10. Unadhani nchi yoyote inaweza kuendelea ikiwa idadi kubwa ya watu wake ni mizigo?

Tazama tofauti kati ya Kenya na Switzerland. Miaka ya 1960, nchi hizi zilikuwa na idadi sawa ya watu, lakini leo Kenya ina watu zaidi ya milioni 50, wengi wao wakiishi kwenye umasikini, huku Switzerland ikiwa na milioni 7 wanaoishi maisha mazuri. Unadhani ni kwa bahati mbaya? Hapana. Ni kwa sababu kule watu walitumia akili, huku kwetu wengi wanaamini "Mungu atajalia" huku wakizaliana bila mpango na kutegemea serikali iwahudumie.

Kama hatutabadilika, tusitarajie maendeleo. Tusipokuwa wakweli kwa nafsi zetu, tutaendelea kulalamika huku tukizidi kuzama kwenye lindi la umasikini wa kujitakia.
Yaani mtu unabeba mimba ukitegemea uhudumiwe bure. Serikali itahudumia watu wangapi? Lazima kuwepo bima za afya ziweze kuwahudumia siyo kupiga simu kwa RC ili akulipie pesa ya kuzaa. Wakati mnaingiza mimba hamkumshirikisha, ila kuzaa ndo mmshirikishe awalipie. Hili jambo la ajabu sana
 
Kati yetu wananchi na viongozi wa umma ni wapi wanapenda kulelewa zaidi...!?

Kodi zinazilpwa na wanajamii zinapaswa kuleta unafuu kwenye maisha wa wananchi badala ya kuimarisha na kuboresha maisha ya viongozi.
 
Ninaunga mkono hoja ya mpagani Kiranga. Serikali na wananchi kwa pamoja wana makosa. Makosa ya serikali ni kutumia pesa nyingi kwenye baadhi ya vitu visivyo vya lazima kama vile kuwabadilishia viongozi magari. Upande wa wananchi ni kama ulivyoelezea.
 
NCHI INAZAMA KWA KUKUMBATIA UJINGA

Je, umewahi kujiuliza kwa nini nchi hii haipigi hatua licha ya kuwa na rasilimali, amani, na nafasi za kujikwamua? Sababu iko wazi: tunakumbatia ujinga na kusambaza mzigo wa maamuzi yetu mabaya kwa wengine.

Mtu anataka kondomu afadhiliwe, akishindwa kuitumia na kupata VVU, anataka dawa za kufubaza ugonjwa zitolewe bure. Akimpa mwanamke mimba, anataka mtoto azaliwe kwa ufadhili wa serikali. Watu hawa ndio wale wale ambao wakifika hospitali kujifungua, hawana hata shilingi 5,000 ya kununua glovu za daktari, lakini wanaamini ni haki yao kupata kila kitu bure. Kwa nini? Kwa sababu wameshawishika kuwa serikali inapaswa kuwajibika kwa kila uamuzi wao mbovu maishani.

Hili suala linafanana kabisa na chuki dhidi ya kauli za RC Chalamila. Yaani mtu amebeba ujauzito bila kuwa na uhakika wa hata shilingi elfu tano ya vifaa vya kujifungulia, halafu anakuja hospitali akiamini kila kitu kitaangukia bure kutoka kwa serikali. Hebu fikiria—ikiwa hata hela ya kondomu siku hiyo haikuwepo, serikali ndiyo ije kubeba mzigo wa mtoto wako? Na kama kweli huna uwezo hata wa kununua glovu, unadhani kweli utakuwa na uwezo wa kumlea huyo mtoto?

Ni mentality hii hii tunayoiona kwa ARV. Mtu anaamua kufanya zinaa bila kinga, akipata UKIMWI anataka matibabu yatolewe bure. Ndio maana mpaka misaada ya Wamarekani inahitajika kulisha taifa linalozaliana bila mpango. Watu milioni 60, lakini wanaochangia mfuko wa bima hawafiki hata milioni 5. Hao wachache ndio wanapaswa kubeba mzigo wa wengine wote? Na bado tunajiita taifa huru!

Tuache unafiki. Hii siyo tena hoja ya CCM au CHADEMA. Ukifukuza CCM na kuleta upinzani, hakuna miujiza itakayofanyika. Historia imetufundisha kuwa mabadiliko hayaji kwa kubadilisha majina ya viongozi, bali kwa kubadili tabia na mtazamo wa jamii. Tanzania ina watu milioni 60, lakini wenye mchango wa moja kwa moja kwenye pato la taifa hawazidi milioni 10. Unadhani nchi yoyote inaweza kuendelea ikiwa idadi kubwa ya watu wake ni mizigo?

Tazama tofauti kati ya Kenya na Switzerland. Miaka ya 1960, nchi hizi zilikuwa na idadi sawa ya watu, lakini leo Kenya ina watu zaidi ya milioni 50, wengi wao wakiishi kwenye umasikini, huku Switzerland ikiwa na milioni 7 wanaoishi maisha mazuri. Unadhani ni kwa bahati mbaya? Hapana. Ni kwa sababu kule watu walitumia akili, huku kwetu wengi wanaamini "Mungu atajalia" huku wakizaliana bila mpango na kutegemea serikali iwahudumie.

Kama hatutabadilika, tusitarajie maendeleo. Tusipokuwa wakweli kwa nafsi zetu, tutaendelea kulalamika huku tukizidi kuzama kwenye lindi la umasikini wa kujitakia.
Me nadhani serikali ndo inawadanganya kuwa huduma ni bure lakini katika uhalisia siyo kweli. Kile kinachotakiwa ni tamko la serikali kuwa hakuna huduma ya bure.
 
Back
Top Bottom